< Zaburi 116 >

1 Nampenda Yahwe kwa kuwa anasikia sauti yangu na kuomba kwangu kwa ajili ya huruma.
われヱホバを愛しむ そはわが聲とわが願望とをききたまへばなり
2 Kwa sababu alinisikiliza, nitamuita yeye ningali ninaishi.
ヱホバみみを我にかたぶけたまひしが故に われ世にあらんかぎりヱホバを呼まつらむ
3 Kamba za mauti zilinizunguka, na mitego ya kuzimu ilinikabili; niliona dhiki na huzuni. (Sheol h7585)
死の繩われをまとひ陰府のくるしみ我にのぞめり われは患難とうれへとにあへり (Sheol h7585)
4 Kisha niliita kwa jina la Yahwe: “Tafadhali Yahwe, uiokoe nafsi yangu.”
その時われヱホバの名をよべり ヱホバよ願くはわが霊魂をすくひたまへと
5 Yahwe ni mwenye neema na haki; Mungu wetu ni mwenye huruma.
ヱホバは恩惠ゆたかにして公義ましませり われらの神はあはれみ深し
6 Yahwe huwalinda wasio na hila; nilishushwa chini akaniokoa.
ヱホバは愚かなるものを護りたまふ われ卑くせられしがヱホバ我をすくひたまへり
7 Nafsi yangu inaweza kurudi mahali pake pa kupumzika, kwa kuwa Yahwe amekuwa mwema kwangu.
わが霊魂よなんぢの平安にかへれ ヱホバは豊かになんぢを待ひたまへばなり
8 Kwa maana uliokoa uhai wangu dhidi ya kifo, mcho yangu dhidi ya machozi, na miguu yangu dhidi ya kujikwaa.
汝はわがたましひを死より わが目をなみだより わが足を顛蹶よりたすけいだしたまひき
9 Nitamtumikia Yahwe katika nchi ya walio hai.
われは活るものの國にてヱホバの前にあゆまん
10 Nilimwamini yeye, hata niliposema, “nimeteswa sana.”
われ大になやめりといひつつもなほ信じたり
11 Kwa haraka nilisema, “Watu wote ni waongo.”
われ惶てしときに云らく すべての人はいつはりなりと
12 Nimlipeje Yahwe kwa wema wake wote kwangu?
我いかにしてその賜へるもろもろの恩惠をヱホバにむくいんや
13 Nitakiinua kikombe cha wokovu, na kuliitia jina la Yahwe.
われ救のさかづきをとりてヱホバの名をよびまつらむ
14 Nitatimiza viapo vyangu kwa Yahwe katika uwepo wa watu wake wote.
我すべての民のまへにてヱホバにわが誓をつくのはん
15 Mauti ya wacha Mungu ina thamani machoni pa Mungu.
ヱホバの聖徒の死はそのみまへにて貴とし
16 Ee Yahwe, hakika, mimi ni mtumishi wako; mimi ni mtumishi wako, mwana wa mjakazi wako; umefungua vifungo vyangu.
ヱホバよ誠にわれはなんぢの僕なり われはなんぢの婢女の子にして汝のしもべなり なんぢわが縲絏をときたまへり
17 Nitakutolea dhabihu ya shukrani na nitaliitia jina la Yahwe.
われ感謝をそなへものとして汝にささげん われヱホバの名をよばん
18 Nitatimiza viapo vyangu kwa Yahwe katika uwepo wa watu wake wote,
我すべての民のまへにてヱホバにわがちかひを償はん
19 katika nyua za nyumba ya Yahwe, katikati yako, Yerusalemu. Msifuni Yahwe.
ヱルサレムよ汝のなかにてヱホバのいへの大庭のなかにて此をつくのふべし ヱホバを讃まつれ

< Zaburi 116 >