< Zaburi 110 >
1 Yahwe humwambia bwana wangu, “Kaa mkono wangu wa kuume mpaka nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”
Zaburi ya Daudi. Bwana amwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume, mpaka nitakapowafanya adui zako kuwa mahali pa kuweka miguu yako.”
2 Yahwe atainyosha fimbo ya nguvu yako toka Sayuni; utawale kati ya adui zako.
Bwana ataeneza fimbo yako ya utawala yenye nguvu kutoka Sayuni; utatawala katikati ya adui zako.
3 Siku ile ya uweza wako watu wako watakufuata wakiwa katika mavazi matakatifu ya hiari yao wenyewe; tokea tumbo la alfajiri ujana wako utakuwa kwako kama umande.
Askari wako watajitolea kwa hiari katika siku yako ya vita. Ukiwa umevikwa fahari takatifu, kutoka tumbo la mapambazuko utapokea umande wa ujana wako.
4 Yahwe ameapa, na hatabadilika: “Wewe ni kuhani milele, baada ya namna ya Melkizedeki.”
Bwana ameapa, naye hatabadilisha mawazo yake: “Wewe ni kuhani milele, kwa mfano wa Melkizedeki.”
5 Bwana yuko mkono wako wa kuume. Siku ile ya hasira yake atawaua wafalme.
Bwana yuko mkono wako wa kuume, atawaponda wafalme siku ya ghadhabu yake.
6 Yeye atahukumu matifa; ataujaza uwanja wa vita kwa maiti; atawauwa viongozi kaitka nchi nyingi.
Atawahukumu mataifa, akilundika mizoga na kuwaponda watawala wa dunia nzima.
7 Atakunywa maji ya kijito njiani, kisha baada ya ushindi atainua kichwa chake juu.
Atakunywa maji katika kijito kando ya njia, kwa hiyo atainua kichwa chake juu.