< Mithali 29 >

1 Mtu aliyepokea makaripio mengi lakini anashupaza shingo yake atavunjika ndani ya muda mfupi na hata pona.
Cualquiera que siga rechazando obstinadamente muchas advertencias, sufrirá destrucción repentina, sin ningún remedio.
2 Watenda mema wanapoongezeka, watu wanafurahi, bali wakati mtu mwovu anapotawala, watu huugua.
Cuando los justos están a cargo, todos celebran; pero cuando los malvados gobiernan, todos gimen.
3 Mwenye kupenda hekima baba yake anafurahi, bali anayeshikamana na makahaba huuharibu utajiri wake.
El hombre que ama la sabiduría, hace feliz a su padre; pero el que visita a las prostitutas, está desperdiciando su dinero.
4 Mfalme huimarisha nchi kwa haki, bali mwenye kudai rushwa huirarua.
El rey que gobierna con justicia hace que el país esté seguro; pero el que pide sobornos, lo destruirá.
5 Mtu anayejipendekeza kwa jirani yake anatandaza wavu kwenye miguu yake.
Los que adulan a sus amigos ponen una trampa para hacerlos caer.
6 Mtu mbaya hunaswa kwenye mtego wa dhambi yake mwenyewe, bali yeye atendaye haki huimba na kufurahi.
Los malvados están atrapados por sus propios pecados; pero los que hacen el bien, cantan y celebran.
7 Atendaye haki hutetea madai ya masikini; mtu mwovu hafahamu maarifa kama hayo.
Los justos se preocupan por trartar a los pobres con justiciar; pero los malvados no piensan en ello.
8 Mwenye dhihaka huutia moto mji, bali wale wenye busara huigeuza ghadhabu.
Los cínicos pueden inflamar toda una ciudad, pero los sabios hacen calmar el furor.
9 Mtu mwenye busara anapojadiliana na mpumbavu, hughadhabika na kucheka, hakutakuwa na utulivu.
Cuando un sabio lleva a un tonto a la corte, habrá rabia y ridículo pero sin soluciones.
10 Mkatili humchukia mwenye ukamilifu na hutafuta maisha ya mwenye haki.
Los asesinos odian a las personas con integridad, pero los que viven rectamente tratarán de ayudarlos.
11 Mpumabavu huonyesha hasira yake, bali mtu mwenye busara huishikilia na kujituliza mwenyewe.
Los tontos dejan salir toda su rabia, pero los sabios la contienen.
12 Kama matawala atazinagatia uongo, maafisa wake wote watakuwa waovu.
El gobernante que escucha la mentira no tendrá nada, sino solo oficiales malvados.
13 Mtu masikini na mkandamizaji wanafanana, maana Yehova huyapa nuru macho yao wote.
Los pobres y sus opresores tienen algo en común: el Señor les da la vida.
14 Kama mfalme atamhukumu masikini kwa uaminifu, kiti chake cha enzi kitaimarishwa milele.
Si un rey juzga con justicia a los pobres, tendrá un largo reinado.
15 Fimbo na maonyo huleta hekima, bali mtoto huru mbali na makaripio humwaibisha mama yake.
La disciplina y la corrección proporcionan sabiduría; pero el hijo que no recibe disciplina es una vergüenza para su madre.
16 Watu waovu wanapotawala, uovu huongezeka, bali wenye kutenda haki wataona anguko la watu waovu.
Cuando los malvados están al poder, el pecado aumenta; pero los justos verán su caída.
17 Mwadibishe mwanao naye atakupa pumziko; ataleta furaha katika maisha yako.
Disciplina a tus hijos, y no te causarán preocupaciones. Te harán muy feliz.
18 Pasipo na maono ya kinabii watu huenda bila utaratibu, bali mwenye kuitunza sheria amebarikiwa.
Sin la revelación de Dios el pueblo se descontrola; pero los que guardan la ley son felices.
19 Mtumwa hawezi kurekebishwa kwa maneno, maana ingawa anaelewa, hakuna mwitikio.
Un siervo no puede ser disciplinado solo con palabras; aunque entienden, no siguen la instrucción.
20 Je unamwona mtu mwenye haraka katika maneno yake? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
¿Has visto a un hombre que habla sin pensar? ¡Hay más esperanza para un tonto que para él!
21 Mwenye kumdekeza mtumwa wake tangu ujana, mwisho wake itakuwa taabu.
El siervo consentido desde la infancia será incontrolable.
22 Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi na bwana mwenye hasira sana hutenda dhambi nyingi.
La gente enojada crea problemas, los irascibles cometerán muchos pecados.
23 Kiburi cha mtu humshusha chini, bali mwenye roho ya unyenyekevu atapewa heshima.
Si eres orgulloso serás humillado; pero si eres humilde, serás honrado.
24 Anayeshirikiana na mwizi huyachukia maisha yake mwenyewe; husikia laana na wala hasemi chochote.
El compañero de un ladrón aborrece su vida; incluso bajo amenaza y maldiciones, no podrá decir la verdad.
25 Kumwogopa binadamu ni mtego, bali mwenye kumtumaini Yehova atalindwa.
El temor a la gente es una trampa. Pero si confías en el Señor estarás a salvo.
26 Wengi huutafuta uso wa mtawala, bali kutoka kwa Yehova huja haki kwa ajili yake.
Muchos procuran el favor de un gobernante; pero la justicia viene del Señor.
27 Mtu dhalimu ni chukizo kwa wenye kutenda haki, bali mwenye njia ya haki ni chukizo kwa watu waovu.
Los justos aborrecen a los injustos; los malvados aborrecen a los que hacen el bien.

< Mithali 29 >