< Hesabu 7 >

1 Siku ambayo Musa alikamilsha masikani, alitia mafuta na kuiweka wakfu kwa BWANA, pamoja na mapambo yake. Aliifanyia hivyo madhabahu na vyombo vyake. Aliitia mafuta na kuiweka wakfu kwa BWANA.
And it came to pass in the day that Moses had finished the tabernacle, and set it up, and had anointed and sanctified it with all its vessels, the altar likewise and all the vessels thereof,
2 Siku hiyo, viongozi wa Israeli na wale vichwa vya familia za mababu walitoa sadaka. Hawa wanaume walikuwa viongozi wa makabila. Walisaidia kuhesabu watu kwenye ile sensa.
The princes of Israel and the heads of the families, in every tribe, who were the rulers of them who had been numbered, offered
3 Walileta sadaka zao kwa BWANA. Walileta magari sita yaliyofunikwa na mafahari kumi na mbili. Walileta gari moja kwa kila viongozi wawili, kila kiongozi alileta fahari moja. Walileta vitu hivi mbele ya masikani.
Their gifts before the Lord, six wagons covered, and twelve oxen. Two princes offered one wagon, and each one an ox, and they offered them before the tabernacle.
4 Kisha BWANA akanena na Musa, akamwambia,
And the Lord said to Moses:
5 “Uzipokee hizo sadaka kutoka kwao na uzitumie kwa matumizi ya kazi ya hema ya kukutania. Uwape hizo sadaka Walawi, kwa kila mmoja kadri ya uhitaji wa kazi yake.”
Receive them from them to serve in the ministry of the tabernacle, and thou shalt deliver them to the Levites according to the order of their ministry.
6 Musa akayatwaa yale magari na mafahari. na kuwapatia Walawi.
Moses therefore receiving the wagons and the oxen, delivered them to the Levites.
7 Aliwapa magari mawili na mafahari wanne wale wa uzao wa Gerishoni, kwa sababu ndivyo kazi yao ilivyohitaji.
Two wagons and four oxen he gave to the sons of Gerson, according to their necessity.
8 Aliwapatia uzao wa Merari magari manne na mafahari nane, chini ya uangalizi wa Ithamari mwana wa Haruni kuhani. Alifanya hivi kwa sababu ya uhitaji wa kazi yao.
The other four wagons, and eight oxen he gave to the sons of Merari, according to their offices and service, under the hand of Ithamar the son of Aaron the priest.
9 Lakini wale wa uzao wa Kohathi hakuwapa chochote kwa sababu wao waliangalia vitu vtakatifu amabvyo vilipaswa vibebwe mabagani mwao, siyo kwa magari.
But to the sons of Caath he gave no wagons or oxen: because they serve in the sanctuary and carry their burdens upon their own shoulders.
10 Viongozi walitoa bidhaa zo zingine kwa ajili ya kuwekwa wakfu kwa madhabahu katika siku ile ambayo Musa aliitia mafuta madhabahu. Viongozi walitoa sadaka zao mbele ya madhabahu hiyo.
And the princes offered for the dedication of the altar on the day when it was anointed, their oblation before the altar.
11 BWANA akasema na Musa, “kila kiongozi atatoa sadaka kwa siku yake kwa ajili ya kuiweka wakfu madhabahu.”
And the Lord said to Moses: Let each of the princes one day after another offer their gifts for the dedication of the altar.
12 Katika siku ya kwanza, Nashoni mwana wa Aminadabu, wa kabila ya Yuda, alitoa sadaka yake.
The first day Nahasson the son of Aminadab of the tribe of Juda offered his offering:
13 Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 130 na bakuli moja ya fedha ambayo uzito wake ni shekeli sabini, kwa kipimo cha mahali patakatifu. Vyombo vyote hivi vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
And his offering was a silver dish weighing one hundred and thirty sicles, a silver bowl of seventy sicles according to the weight of the sanctuary, both full of flour tempered with oil for a sacrifice:
14 Pia alimpa unga wa dhahabu kiasi cha bakuli moja chenye uzani wa shekeli kumi kilichojaa ubani
A little mortar of ten sides of gold full of incense:
15 Alitoa sadaka ya kuteketezwa fahari mchanga, kondoo dume mmoja na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja.
An ox of the herd, and a ram, and a lamb of a year old for a holocaust:
16 Alitoa beberu kama kama sadaka ya hatia.
And a buck goat for sin:
17 Alitoa makisai mbili, kondoo waume watano, beberu watano na wanakondoo dume watano wenye umri wa mwaka mmoja mmoja, kama sadaka ya amani. Hii ilikuwa sadaka ya Nashoni mwana wa Aminadabu.
And for the sacrifice of peace offerings, two oxen, five rams, five he goats, five lambs of a year old. This was the offering of Nahasson the son of Aminadab.
18 Siku ya pili, Nethanel mwana wa Zuari, kiongozi wa Isakari, alitoa sadaka yake.
The second day Nathanael the son of Suar, prince of the tribe of Issachar, made his offering,
19 Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha ya uzito wa shekeli130 na bakuli moja la fedha lenye uzani wa sheli sabini, kwa kipimo cha mahali patakatifu. Viyombo vyote hivi vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kwa sadaka ya unga.
A silver dish weighing one hundred and thirty sides, a silver bowl of seventy sides, according to the weight of the sanctuary, both full of flour tempered with oil for a sacrifice:
20 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli kumi, iliyojaa ubani.
A little mortar of gold weighing ten sides full of incense:
21 Alitoa sadaka ya kuteketezwa fahari mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo mmoja dume.
An ox of the herd, and a ram, and a lamb of a year old for a holocaust:
22 Alitoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi.
And a buck goat for sin:
23 Alitoa makisai wawili, Kondoo dume watano, beberu watano, na wanakondoo dume watano wa mwaka mmoja mmoja kuwa sadaka ya amani. Hiii likuwa sadaka ya Nethaneli mwana wa Zuari.
And for the sacrifice of peace offerings, two oxen, five rams, five buck goats, five lambs of a year old. This was the offering of Nathanael the son of Suar.
24 Siku ya tatu, Eliabu mwana wa Heloni, kiongozi wa uzao wa Zabuloni alitoa sadaka yake.
The third day the prince of the sons of Zabulon, Eliab the son of Helon,
25 Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha lenye uzito wa shekeli sabini kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. vyombo vyote hivi vilikuwa vimeja unga mwembemba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
Offered a silver dish weighing one hundred and thirty sides, a silver bowl of seventy sides by the weight of the sanctuary, both full of flour tempered with oil for a sacrifice:
26 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzani wa shekeli kumi, kilichojaa ubani.
A little mortar of gold weighing ten sides full of incense:
27 Alitoa sadaka ya fahari mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja.
An ox of the herd, and a ram, and a lamb of a year old for a holocaust:
28 Alitoa beberu mmoja kama sadaka ya dhambi.
And a buck goat for sin:
29 Alitoa makisai wawili, kondoo dume watano, beberu watano, na wanakondoo dume watano wa mwaka mmoja mmoja. kuwa sadaka ya amani. Hii ilikuwa sadaka ya Eliabu mwana Heloni.
And for the sacrifice of peace offerings, two oxen, five rams, five buck goats, five lambs of a year old. This is the oblation of Eliab the son of Helon.
30 Siku ya nne, Elizuri mwana wa shedeuri, kiongozi wa uzao wa Reubeni, alitoa sadaka yake.
The fourth day the prince of the sons of Ruben, Elisur the son of Sedeur,
31 Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzani wa shekeli sabini, kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. Vyombo hivi vyote vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
Offered a silver dish weighing one hundred and thirty sides, a silver bowl of seventy sides according to the weight of the sanctuary, both full of flour tempered with oil for a sacrifice:
32 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzani wa shekeli kumi, kilichoo jaa ubani.
A little mortar of gold weighing ten sides full of incense:
33 Alitoa sadaka ya kuteketezwa fahari mmoja mchanga, mwanakondoo dume mmoja mchanga wa mwaka mmoja.
An ox of the herd, and a ram, and a lamb of a year old, for a holocaust:
34 Alitoa beberu moja kuwa sadaka ya dhambi.
And a buck goat for sin:
35 Alitoa maksai wawili, kondoo dume watano wa mwaka mmoja kuwa sadaka ya amani. Hii ilikuwa sadaka ya Elizuri mwana wa Shedeuri.
And for victims of peace offerings two oxen, five rams, five buck goats. five lambs of a year old. This was the offering of Elisur the son of Sedeur.
36 Siku ya tano, Shelumieli mwana wa Zurishadai, kiongozi wa uzao wa Simeoni, alitoa sadaka yake.
The fifth day the prince of the sons of Simeon, Salamiel the son of Surisaddai,
37 Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shaekali 130 na bakuli mojala fedha lenye uzani wa shekeli sabini kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. Vyombo vyote hivi vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
Offered a silver dish weighing one hundred and thirty sides, a silver bowl of seventy sides after the weight of the sanctuary, both full of flour tempered with oil for a sacrifice:
38 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzani wa shekeli kumi, uliojaa ubani.
A little mortar of gold weighing ten sides full of incense:
39 Alitoa sadaka ya kuteketezwa fahari mchanga, dume la kondoo, na dume la mwanakondoo la mwaka mmoja.
An ox of the herd, and a ram, and a lamb of a year old for a holocaust:
40 Alitoa beberu moja kuwa sadaka ya dhambi.
And a buck goat for sin:
41 Alitao maksai wawili, dume wawili wa kondoo, beberu watano, na dume watano wa wanakondoo wa mwaka mmoja mmoja kuwa sadaka y amani. Hiindiyo iliyokuwa sadka ya Shelumei mwana wa Zurishadai.
And for sacrifices of peace offerings, two oxen, five rams, five buck goats, five lambs of a year old. This was the offering of Salamiel the son of Surisaddai.
42 Siku ya sita, Eliasafu mwana wa Deuli, kiongozi wa uzao wa Gadi, alitoa sadaka yake.
The sixth day the prince of the sons of Gad, Eliasaph the son of Duel,
43 Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 130 na bakuli la shaba lenye uzani wa shekeli sabini, kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. Vyombo hivi vyote vilikuwa vimejaa unga mwembemba uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya sadaka ya unga.
Offered a silver dish weighing a hundred and thirty sides, a silver bowl of seventy sides by the weight of the sanctuary, both full of flour tempered with oil for a sacrifice:
44 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzani wa shekeli kumi, kilichojaa ubani.
A little mortar of gold weighing ten sides full of incense:
45 Alitoa sadaka ya kuteketezwa ya fahari changa, kondoo dume mmoja, na dume la mwanakondoo mmoja wa mwaka mmoja.
An ox of the herd, and a ram, and a lamb of a year old for a holocaust:
46 Alitoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi.
And a buck goat for sin:
47 Alitoa maksai wawili, dume watano wa kondoo, beberu watano, na wanakondoo dume watano wa mwaka mmoja kuwa sadaka ya amani. Hii ndiyo iliyokuwa sadaka ya Eliasafu mwana wa Deuli.
And for sacrifices of peace offerings, two oxen, five rams, five buck goats, five lambs of a year old. This was the offering of Eliasaph the son of Duel.
48 Siku ya saba, Elishama mwana wa Amihudi, kiongozi wa uzao wa Efraimu, alitoa sadaka yake.
The seventh day the prince of the sons of Ephraim, Elisama the son Ammiud,
49 Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 130 na bakuli la fedha lenye uzani wa shekeli sabini, kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. Vyombo hivi vyote ilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
Offered a silver dish weighing a hundred and thirty sides, a silver bowl of seventy sides according to the weight of the sanctuary, both full of hour tempered with oil for a sacrifice:
50 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu, kilichojaa ubani
A little mortar of gold weighing ten sides full of incense:
51 Alitoa sadaka ya kuteketezwa, fahari mmoja, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja.
An ox of the herd, and a ram, and a lamb of a year old for a holocaust:
52 Alitoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi.
And a buck goat for sin:
53 Alitoa maksai wawili, kondo dume watano, beberu watano, na na wanakondoo dume watano wa mwaka mmoja mmoja kuwa sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sdaka ya Elishama mwana wa Amidu.
And for sacrifices of peace offerings, two oxen, five rams, five buck goats, five lambs of a year old. This was the offering of Elisama the son of Ammiud.
54 Siku y a nane, Gamaliel mwana wa Pedazuri, kiongozi wa uzao wa Manase, alitoa sadaka yake.
The eighth day the prince of the sons of Manasses, Gamaliel the son of Phadassur,
55 Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli130 na bakuli moja la fedha lenye uzani wa shekeli sabini, kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. Vyombo vyote hivi vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
Offered a silver dish weighing a hundred and thirty sicles, a silver bowl of seventy sicles, according to the weight of the sanctuary, both full of flour tempered with oil for a sacrifice:
56 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzani wa shekeli kumi, kilichojaa ubani.
A little mortar of gold weighing ten sicles full of incense:
57 Alitoa sadaka ya kuteketezwa ya fahari mmoja, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja.
An ox of the herd, and a ram, and a lamb of a year old for a holocaust:
58 Alitoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi.
And a buck goat for sin:
59 Alitoa maksai wawili, kondoo dume watano, beberu watano, na wanakondoo dume watano wa mwaka mmoja mmoja kuwa sadaka ya amani. Hii ndiyo iliyokuwa sadaka ya Gamaliel mwana wa Pedazuri.
And for sacrifices of peace offerings, two oxen, five rams, five buck goats, five lambs of a year old. This was the offering of Gamaliel the son of Phadassur.
60 Siku ya tisa, Abidani mwana wa Gidioni, kiongozi wa uzao wa Benjamini, alitoa sadaka yake.
The ninth day the prince of the sons of Benjamin, Abidan the son of Gedeon,
61 Sadaka yake ilikuwa sahani moja yafedha yenye uzani wa sheli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzito wa shekeli sabini, kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. Vyombo vyote hivi vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
Offered a silver dish weighing a hundred and thirty sides, a silver bowl of seventy sides by the weight of the sanctuary, both full of flour tempered with oil for a sacrifice:
62 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzani wa shekeli kumi, kilichojaa ubani.
A little mortar of gold weighing ten sides full of incense:
63 Alitoa sadaka ya kuteketezwa fahari mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na mwanakondoo dume mmoja wa mwaka mmoja.
An ox of the herd, and a ram, and a lamb of a year old for a, holocaust:
64 Alitoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi.
And a buck goat for sin:
65 Alitoa makisai wawili, kondoo dume watano, beberu watano, na wanakondoo dume watano kuwa sadaka ya amani. Hii ndiyo iliyokuwa sadaka ya Abidani mwana wa Gidioni.
And for sacrifices of peace offerings, two oxen, five rams, five buck goats, five lambs of a year old. This was the offering of Abidan the son of Gedeon.
66 Siku ya kumi, Ahizeri mwana wa Amishadai kiongozi wa Dani alitoa sadaka yake.
The tenth day the prince of the sons of Dan, Ahiezer the son of Ammisaddai,
67 Alitoa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shaekeli 130 na bakuli moja lenye uzani wa shekeli sabini, kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. Vyombo vyote hivi vilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
Offered a silver dish weighing a hundred and thirty sides, a silver bowl of seventy sides, according to the weight of the sanctuary, both full of flour tempered with oil for a sacrifice:
68 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzito wa shekeli kumi, kilichojaa ubani.
A little mortar of gold weighing ten sides full of incense:
69 Alitoa sadaka ya kuteketezwa fahari mmoja mchanga, dume moja la kondoo, na dume moja la mwanakondoo wa mwaka mmoja.
An ox of the herd, and a ram, and a lamb of a year old for a holocaust:
70 Alitoa beberu moja kuwa sadaka ya dhambi.
And a buck goat for sin:
71 Alitoa maksai wawili, kondoo dume watano, beberu watano, na wanakondoo dume watano wa mwaka mmoja mmoja, kuwa sadaka ya amani. Hii ndiyo iliyokuwa sadaka ya Ahizeri mwana wa Amishadai.
And for sacrifices of peace offerings, two oxen, five rams, five buck goats, five lambs of a year old. This was the offering of Ahiezer the son of Ammisaddai.
72 Siku ya kumi na moja. Pagieli mwana wa Okrani kiongozi wa uzao wa Asheri alaitoa sadaka yake.
The eleventh day the prince of the sons of Aser, Phegiel the son of Ochran,
73 Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzani wa shekeli sabani, kwa kipimo cha shekeli ya mahali patakatifu. Vyombo vyote hivi ilikuwa vimejaa unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
Offered a silver dish weighing a hundred and thirty sides, a silver bowl of seventy sides, according to the weight of the sanctuary, both full of flour tempered with oil for a sacrifice:
74 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzani wa shekeli kumi, kilichojaa ubani.
A little mortar of gold weighing ten sides full of incense:
75 Alitoa sadaka ya kuteketezwa fahari mmoja mchanga. dume la kondoo moja, dume moja la mwanakondoo wa mwaka mmoja.
An ox of the herd, and a ram, and a lamb of a year old for a holocaust:
76 Alitoa beberu moja kuwa sadaka ya dhambi.
And a buck goat for sin:
77 Alitoa maksai wawili, dume watano wa kondoo, na wanakondoo dume watano kuwa sadaka ya amani. Hii ndiyo iliyokuwa sadaka ya Pagieli mwana wa Okrani.
And for sacrifices of peace offerings, two oxen, five rams, five buck goats, five lambs of a year old. This was the offering of Phegiel the son of Ochran.
78 Siku ya kumi na mbili., Ahira mwana wa Enani, kiongozi wa uzao wa Naftali, alitoa sadaka yake.
The twelfth day the prince of the sons of Nephtali, Ahira the son of Enan,
79 Sadaka yake ailikuwa sahani moja ya fedha yenye uzani wa shaekeli 130 na bakuli moja la fedha lenye uzani wa shekeli sabini, kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu. Vyombo vyote hivi vilikuwa vimejaa unga mwembamba ulichanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga.
Offered a silver dish weighing a hundred and thirty sides, a silver bowl of seventy sides, according to the weight of the sanctuary, both full of flour tempered with oil for a sacrifice:
80 Pia alitoa kijiko kimoja cha dhahabu chenye uzani wa shekeli kumi, kilichojaa ubani.
A little mortar of gold weighing ten sides full of incense:
81 Alitoa sadaka ya kuteketezwa fahari mmoja mchanga, dume moja la kondoo, na mwanakondoo dume moja wa mwaka mmoja.
An ox of the herd, and a ram, and a lamb of a year old for a holocaust:
82 Alitoa beberu moja kuwa sadaka ya dhambi.
And a buck goat for sin:
83 Alitoa maksai wawili, kondoo dume watano, beberu watano, na wanakondoo dume watano wa mwaka mmoja mmoja kuwa sadaka ya amani. Hii ndiyo iliyokuwa sadaka ya Ahra mwana wa Enani.
And for sacrifices of peace offerings, two oxen, five rams, five buck goats, five lambs of a year old. This was the offering of Ahira the son of Enan.
84 Viongozi wa Israeli waliviweka wakfu hivi vitu vyote siku ambayo Musa alimimina mafuta kwenye madhabahu. Waliziweka wakfu zile sahani kumi na mbili za fedha, Bakuli kumi na mbili za fedha, na vijiko kumi na vili vya dhahabu.
These were the offerings made by the princes of Israel in the dedication of the altar, in the day wherein it was consecrated. Twelve dishes of silver: twelve silver bowls: twelve little mortars of gold:
85 Zile sahani za fedha kila moja ilikuwa na uzani wa shaekeli 130 na kila bakuli ye fedha ilikuwa na uzani wa shekeli sabini. Vyombo vyote vya fedh vilikuwa na ujumla ya uzani wa shekeli 2, 400, kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu.
Each dish weighing a hundred and thirty sides of silver, and each bowl seventy sides: that is, putting all the vessels of silver together, two thousand four hundred sides, by the weight of the sanctuary.
86 Vile vijiko vya dhahabu vilivyokuwa vimejaa ubani, vilikuwa na uzani wa shekeli kumi kila kimoja. Vijiko vyote vya dhahabu vilikuwa na uzani wa shekeli 120.
Twelve little mortars of gold full of incense, weighing ten sides apiece, by the weight of the sanctuary: that is, in all a hundred and twenty sides of gold.
87 Waliwatenga wanyama wote kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, fahari kumi na wawili, kondoo dume kumi na wawili, na wanakondoo dume kumi na wawili wa mwaka mmoja mmoja. Walitoa sadaka yao ya unga. Walitoa beberu kumi na wawili kuwa sadaka ya dhambi.
Twelve oxen out of the herd for a holocaust, twelve rams, twelve lambs of a year old, and their libations: twelve buck goats for sin.
88 Kutokana na ng'ombe zao, walitoa fahari ishirini na nne, kondoo dume sitini beberu sitini, na wanakondoo dume sitini wa mwaka mmoja mmoja kuwa sadaka ya amani. Hii ilikuwa kwa ajiliya kuiweka wafu ile madhabahu baada ya kumiminiwa mafuta.
And for sacrifices of peace offerings, oxen twenty-four, rams sixty, buck goats sixty, lambs of a year old sixty. These things were offered in the dedication of the altar, when it was anointed.
89 Musa alipoingia kwenye hema ya kukutania kusema na BWANA, ndipo alipoisikia sauti yake ikisema naye. BWANA alinena naye kutoka juu ya kiti cha rehema kilichokuwa juu ya sanduku la ushahidi, kutoka katikati ya makerubi. Alinena naye.
And when Moses entered into the tabernacle of the covenant, to consult the oracle, he heard the voice of one speaking to him from the propitiatory, that was over the ark between the two cherubims, and from this place he spoke to him.

< Hesabu 7 >