< Hesabu 34 >

1 BWANA akanena na Musa akasema,
Il Signore disse a Mosè:
2 “Waamuru watu wa Israeli na uwaambie, 'Mtakapoingia katika nchi ya Kanaani, nchi ambayo itakuwa mali yenu, nchi ya Kanaani na mipaka yake, mpaka wenu wa kusini utaendelea kutoka nyika ya Sini hadi mpaka wa Edomu.
«Dà questo ordine agli Israeliti e riferisci loro: Quando entrerete nel paese di Canaan, questa sarà la terra che vi toccherà in eredità: il paese di Canaan.
3 Mwisho wa mpaka wa kusini utakuwa mwisho wa bahari ya chumvi kuelekea mashariki.
Il vostro confine meridionale comincerà al deserto di Sin, vicino a Edom; così la vostra frontiera meridionale partirà dall'estremità del Mar Morto, a oriente;
4 Mpaka wenu utageukia kusini kutoka mlima kuelekea Akrabimu na kupitia nyika ya Sini. na kutokea huko utaelelkea kusini mwa Kadeshi Barinea na kuelekea Hazari Adari mpaka Azimoni.
questa frontiera volgerà al sud della salita di Akrabbim, passerà per Sin e si estenderà a mezzogiorno di Kades-Barnea; poi continuerà verso Cazar-Addar e passerà per Asmon.
5 Kutoka huko, mpaka utageuka kutoka Azimoni kuelekea kijito cha Misri na kukifuata mpaka baharini.
Da Asmon la frontiera girerà fino al torrente d'Egitto e finirà al mare.
6 Mpaka wa Magharibi utakuwa pwani ya bahari kuu. Huu ndio utakuwa mpaka wenuwa Magharibi.
La vostra frontiera a occidente sarà il Mar Mediterraneo: quella sarà la vostra frontiera occidentale.
7 Mpaka wenu wa kaskazini utaanzia kwenye bahari kuu hadi Mlima Hori,
Questa sarà la vostra frontiera settentrionale: partendo dal Mar Mediterraneo, traccerete una linea fino al monte Or;
8 kisha kutoka Mlima Hori hadi Lebo Hamathi, kisha Zedadi.
dal monte Or, la traccerete in direzione di Amat e l'estremità della frontiera sarà a Zedad;
9 Mpaka utaendelea hadi Zifroni na kuishia Hazari Enani. Huu ndio utakuwa mpaka wenu wa kaskazini.
la frontiera continuerà fino a Zifron e finirà a Cazar-Enan: questa sarà la vostra frontiera settentrionale.
10 Kisha mtaweka alama za mpaka wenu wa mashariki ambao utaanzia Hazari Enani kuelekea kusini Shefamu.
Traccerete la vostra frontiera orientale da Cazar-Enan a Sefam;
11 Kisha mpaka wa kusini utaendelea kutoka Shefamu hadi Ribla, upande wa masharikia mwa Aini. Mpaka utaedelea upande huo wa mashariki hadi upande wa mashariki wa bahari ya Kinerethi.
la frontiera scenderà da Sefam verso Ribla, a oriente di Ain; poi la frontiera scenderà e si estenderà lungo il mare di Genèsaret, a oriente;
12 Kisha mpaka utaendelea kuelekea kusini hadi mto Yorodani na hadi bahari ya chumvi. Hii ndiyo itakuwa nchi yenu, kwa kuifuata mipaka yake yote inayozunguka.'”
poi la frontiera scenderà lungo il Giordano e finirà al Mar Morto. Questo sarà il vostro paese con le sue frontiere tutt'intorno».
13 Kisha Musa akawaamuru watu wa Israeli akasema, “Hii ndiyo nchi ambayo mtaipokes kwa kura, ambayo BWANA ameamuru kuwapa wale makabila tisa na nusu.
Mosè comunicò quest'ordine agli Israeliti e disse loro: «Questo è il paese che vi distribuirete a sorte e che il Signore ha ordinato di dare a nove tribù e mezza;
14 Kabila ya uzao wa Reubeni, kwa kufuata jinsi walivyopewa urithi kwa jamaa ya kabila yao, na uzao wa kabila la Gadi, kwa kufuata jinsi walivyopewa urithi kwa jamaa ya kabila yao, na nusu ya Manase wamepata ardhi yao.
poiché la tribù dei figli di Ruben, secondo i loro casati paterni, e la tribù dei figli di Gad, secondo i loro casati paterni, e metà della tribù di Manàsse hanno ricevuto la loro porzione.
15 Wale makabila mawili na nusu wameshapata mgawo wao ng'ambo ya mto Yorodani upande wa mashariki, kuelekea kule linakotokea jua.”
Queste due tribù e mezza hanno ricevuto la loro porzione oltre il Giordano di Gerico, dal lato orientale».
16 BWANA akanena na Musa akasema,
Il Signore disse a Mosè:
17 “Haya ndiyo majinaya watu watakaoigawa ardhi kwa ajili ya urithi wao: Eliazari kuhani na Joshua mwana wa Nuni.
«Questi sono i nomi degli uomini che spartiranno il paese fra di voi: il sacerdote Eleazaro e Giosuè, figlio di Nun.
18 Mtachagua kiongozi mmoja toka kila kabila ili kuigawa ardhi kwa koo zao.
Prenderete anche un capo di ogni tribù per fare la spartizione del paese.
19 Haya ndiyo majina ya wanaume: Kutoka kabila la Yuda, Kalebu mwana wa Yefune.
Ecco i nomi di questi uomini. Per la tribù di Giuda, Caleb figlio di Iefunne.
20 Kutoka kwenye kabila la uzao wa Simeoni, Shemueli mwana wa Amihudi.
Per la tribù dei figli di Simeone, Samuele figlio di Ammiud.
21 Kutoka kabila la Benjamini, Elidadi mwana wa Kisloni.
Per la tribù di Beniamino, Elidad figlio di Chislon.
22 Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Dani, Buki mwana wa Jogili.
Per la tribù dei figli di Dan, il capo Bukki figlio di Iogli.
23 Kiongozi kutoka uzao wa Yusufu, kwenye kabila la Manase, Hannieli mwana wa Efodi.
Per i figli di Giuseppe, per la tribù dei figli di Manàsse, il capo Anniel figlio di Efod;
24 Kiongozi kutoka kwenye kabila la uzao wa Efraimu, Kemueli mwana wa Shiftani.
per la tribù dei figli di Efraim, il capo Kemuel figlio di Siptan.
25 Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Zabuloni, Elizafani mwana wa Parinaki.
Per la tribù dei figli di Zàbulon, il capo Elisafan figlio di Parnach.
26 Kiongozi kutoka kwenye kabila la uzao wa Isakari, Palitieli mwana wa Azzani.
Per la tribù dei figli di Issacar, il capo Paltiel figlio di Azzan.
27 Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Asheri, Ahihudi mwana wa Shelomi.
Per la tribù dei figli di Aser, il capo Achiud, figlio di Selomi.
28 Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Naftali, Pedaheli mwana wa Amihudi.”
Per la tribù dei figli di Nèftali, il capo Pedael figlio di Ammiud».
29 BWANA aliwaamuru wanaume hawa kuigawa nchi ya Kanaani na kuwapa kila kabla sehemu yao.
Questi sono coloro ai quali il Signore ordinò di spartire il possesso del paese di Canaan tra gli Israeliti.

< Hesabu 34 >