< Hesabu 34 >
1 BWANA akanena na Musa akasema,
And Yahweh spake unto Moses, saying:
2 “Waamuru watu wa Israeli na uwaambie, 'Mtakapoingia katika nchi ya Kanaani, nchi ambayo itakuwa mali yenu, nchi ya Kanaani na mipaka yake, mpaka wenu wa kusini utaendelea kutoka nyika ya Sini hadi mpaka wa Edomu.
Command the sons of Israel, and thou shalt say unto them, When, ye, are coming into the land of Canaan, this is the land which shall fall unto you, as an inheritance, even the land of Canaan, by the boundaries thereof.
3 Mwisho wa mpaka wa kusini utakuwa mwisho wa bahari ya chumvi kuelekea mashariki.
Ye shall therefore have a south corner, from the desert of Zin, on the side of Edom, —so shall ye have a south boundary, from the end of the salt sea, eastward:
4 Mpaka wenu utageukia kusini kutoka mlima kuelekea Akrabimu na kupitia nyika ya Sini. na kutokea huko utaelelkea kusini mwa Kadeshi Barinea na kuelekea Hazari Adari mpaka Azimoni.
and the boundary shall go round for you from the south towards the cliffs of Akrabbim, then cross over towards Zin, and the extension thereof shall be from the south to Kadesh-barnea, then shall it reach out to Hazar-addar, and cross over towards Azmon;
5 Kutoka huko, mpaka utageuka kutoka Azimoni kuelekea kijito cha Misri na kukifuata mpaka baharini.
then shall the boundary turn round from Azmon towards the ravine of Egypt, —and the extension thereof shall be towards the sea.
6 Mpaka wa Magharibi utakuwa pwani ya bahari kuu. Huu ndio utakuwa mpaka wenuwa Magharibi.
And, for a west boundary, —ye shall have the great sea, even a boundary, this, shall serve you as west boundary.
7 Mpaka wenu wa kaskazini utaanzia kwenye bahari kuu hadi Mlima Hori,
And, this, shall serve you as a north boundary, —From the great sea, ye shall draw a line for you to Mount Hor:
8 kisha kutoka Mlima Hori hadi Lebo Hamathi, kisha Zedadi.
From Mount Hor, ye shall draw a line to the entering in of Hamath, —and the extension of the boundary shall be towards Zedad:
9 Mpaka utaendelea hadi Zifroni na kuishia Hazari Enani. Huu ndio utakuwa mpaka wenu wa kaskazini.
then shall the boundary reach out towards Ziphron, and the extension thereof, be to Hazar-enan. This, shall serve you as a north, boundary.
10 Kisha mtaweka alama za mpaka wenu wa mashariki ambao utaanzia Hazari Enani kuelekea kusini Shefamu.
Then shall ye draw for yourselves a line, for an east boundary, —from Hazar-enan towards Shepham;
11 Kisha mpaka wa kusini utaendelea kutoka Shefamu hadi Ribla, upande wa masharikia mwa Aini. Mpaka utaedelea upande huo wa mashariki hadi upande wa mashariki wa bahari ya Kinerethi.
and the boundary shall go down from Shepham towards Riblah, on the east of Ain—then shall the boundary go down and strike on the side of the Sea of Chinnereth, eastward:
12 Kisha mpaka utaendelea kuelekea kusini hadi mto Yorodani na hadi bahari ya chumvi. Hii ndiyo itakuwa nchi yenu, kwa kuifuata mipaka yake yote inayozunguka.'”
then shall the boundary go down towards the Jordan, and the extension thereof be to the salt sea. This shall be your land by the boundaries thereof round about.
13 Kisha Musa akawaamuru watu wa Israeli akasema, “Hii ndiyo nchi ambayo mtaipokes kwa kura, ambayo BWANA ameamuru kuwapa wale makabila tisa na nusu.
And Moses commanded the sons of Israel saying, —This, is the land, which ye shall inherit by lot, which Yahweh had commanded to be given to the nine tribes and the half tribe.
14 Kabila ya uzao wa Reubeni, kwa kufuata jinsi walivyopewa urithi kwa jamaa ya kabila yao, na uzao wa kabila la Gadi, kwa kufuata jinsi walivyopewa urithi kwa jamaa ya kabila yao, na nusu ya Manase wamepata ardhi yao.
For the tribe of the sons of the Reubenites by their ancestral house, and the tribe of the sons of Gad, by their ancestral house, have received, and, the half tribe of Manasseh have received, their inheritance:
15 Wale makabila mawili na nusu wameshapata mgawo wao ng'ambo ya mto Yorodani upande wa mashariki, kuelekea kule linakotokea jua.”
the two tribes, and the half tribe, have received their inheritance—on this side Jordan near Jericho, eastwards, towards sunrise.
16 BWANA akanena na Musa akasema,
Then spake Yahweh unto Moses, saying:
17 “Haya ndiyo majinaya watu watakaoigawa ardhi kwa ajili ya urithi wao: Eliazari kuhani na Joshua mwana wa Nuni.
These, are the names of the men who shall receive for you the land, as an inheritance, Eleazar, the priest, and Joshua, son of Nun.
18 Mtachagua kiongozi mmoja toka kila kabila ili kuigawa ardhi kwa koo zao.
Also, one prince from each tribe, shall ye take to receive the land, as an inheritance.
19 Haya ndiyo majina ya wanaume: Kutoka kabila la Yuda, Kalebu mwana wa Yefune.
These, therefore, are the names of the men, —For the tribe of Judah, Caleb son of Jephunneh;
20 Kutoka kwenye kabila la uzao wa Simeoni, Shemueli mwana wa Amihudi.
And, for the tribe of the sons of Simeon, Shemuel son of Ammihud:
21 Kutoka kabila la Benjamini, Elidadi mwana wa Kisloni.
For the tribe of Benjamin, Elidad son of Chislon;
22 Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Dani, Buki mwana wa Jogili.
And, for the tribe of the sons of Dan, a prince—Bukki, son of Jogli:
23 Kiongozi kutoka uzao wa Yusufu, kwenye kabila la Manase, Hannieli mwana wa Efodi.
For the sons of Joseph, For the tribe of the sons of Manasseh, a prince, —Hanniel son of Ephod;
24 Kiongozi kutoka kwenye kabila la uzao wa Efraimu, Kemueli mwana wa Shiftani.
And, for the tribe of the sons of Ephraim, a prince, —Kemuel, son of Shiphtan;
25 Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Zabuloni, Elizafani mwana wa Parinaki.
And, for the tribe of the sons of Zebulun, a prince, —Elizaphan, son of Parnach;
26 Kiongozi kutoka kwenye kabila la uzao wa Isakari, Palitieli mwana wa Azzani.
And, for the tribe of the sons of Issachar, a prince, —Paltiel son of Azzan;
27 Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Asheri, Ahihudi mwana wa Shelomi.
And, for the tribe of the sons of Asher, a prince, —Ahihud son of Shelomi:
28 Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Naftali, Pedaheli mwana wa Amihudi.”
And, for the tribe of the sons of Naphtali, a prince, —Pedahel, son of Ammihud.
29 BWANA aliwaamuru wanaume hawa kuigawa nchi ya Kanaani na kuwapa kila kabla sehemu yao.
These, are they whom Yahweh hath commanded to receive for the sons of Israel their inheritance, in the land of Canaan.