< Hesabu 3 >

1 Sasa hii ndiyo historia ya uzao wa Haruni na Musa wakati BWANA aliposema na Musa kwenye mlima Sinai.
Voici l'histoire des générations d'Aaron et de Moïse, au jour où Yahvé parla à Moïse sur la montagne de Sinaï.
2 Majina ya watoto wa Haruni walikuwa Nadabu ambaye ndiyo mtoto wa kwanza, na Abihu, na Eliezeri, na Ithamari.
Voici les noms des fils d'Aaron: Nadab, premier-né, Abihu, Éléazar et Ithamar.
3 Haya ndiyo majina ya wana wa Haruni, makuhani waliokuwa wamepakwa mafuta na kuwekwa wakfu kutumika kama makuhani.
Voici les noms des fils d'Aaron, les prêtres oints, qu'il consacra pour exercer le sacerdoce.
4 Lakini Nadabu na Abihu walikufa mbele ya BWANA walipomtolea moto usiokubalika walipokuwa katika nyika ya Sinai. Nadabu na Abihu hawakuwa na watoto, kwa hiyo Eliazari na Ithamari walitumika kama makuhani pamoja na baba yao.
Nadab et Abihu moururent devant Yahvé lorsqu'ils offrirent du feu étranger devant Yahvé dans le désert du Sinaï, et ils n'eurent pas d'enfants. Eléazar et Ithamar firent le service du sacerdoce en présence d'Aaron, leur père.
5 BWANA alinena na Musa, akamwambia,
Yahvé parla à Moïse, et dit:
6 “Walete kabila ya Lawi na uwaweke kwa Haruni kuhani ili wamsaidie
Fais approcher la tribu de Lévi, et place-la devant le prêtre Aaron, pour qu'elle soit à son service.
7 Nao lazima wafanye majukumu badala ya Haruni na jumuiya yote mbele ya hema ya kukutania. Lazima watumike hemani.
Ils veilleront sur ses besoins et sur ceux de toute l'assemblée devant la tente d'assignation, pour faire le service du tabernacle.
8 Watayatunza mapambo ya hema ya kukutania, na watawatumikia makabila ya Israel kwa huduma ya hemani.
Ils garderont tout le mobilier de la Tente d'assignation et les obligations des enfants d'Israël, pour assurer le service de la Tente d'assignation.
9 Uwaweke Walawi kwa Haruni na watoto wake. Nimewatoa kikamilifu ili wamsaidie kuwatumikia watu wa Israel.
Tu donneras les Lévites à Aaron et à ses fils. Ils lui seront entièrement remis au nom des enfants d'Israël.
10 Umchague Haruni na watoto wake kuwa makuhani, lakini mgeni yeyote atakayekaribia lazima auawe.”
Tu désigneras Aaron et ses fils, et ils conserveront leur sacerdoce, mais l'étranger qui s'approchera sera mis à mort. »
11 BWANA alinena na Musa. akamwambia,
Yahvé parla à Moïse et dit:
12 “Tazama, nimewachagua Walawi katika watu wa Israel. Nimefanya hivyo badala ya kuchukua mzaliwa wa kwanza wa kiume wa wana wa Israel. Hawa Walawi ni wangu.
« Voici, j'ai pris les Lévites du milieu des enfants d'Israël à la place de tous les premiers-nés qui ouvrent le ventre des enfants d'Israël; et les Lévites seront à moi,
13 Na hata wazaliwa wa kwanza ni mali yangu. Katika siku ambyo niliwavamia wazaliwa wote wa kwanza wa nchi ya Misri, Niliwatenga wazaliwa wa kwanza wa Israeli kwa ajili yangu, watu na wanyama pia. Ni mali yangu. Mimi ndimi BWANA.”
car tous les premiers-nés sont à moi. Le jour où j'ai frappé tous les premiers-nés du pays d'Égypte, j'ai consacré à moi tous les premiers-nés d'Israël, hommes et animaux. Ils seront à moi. Je suis Yahvé. »
14 BWANA alinena na Musa katika nyika ya Sinai. Akasema,
Yahvé parla à Moïse dans le désert de Sinaï, et dit:
15 “Wahesabu uzao wa Lawi katika kila familia, katika nyumba za koo zao. Hesabu kila mume kuanzia mwezi mmoja au zaidi.”
« Compte les enfants de Lévi selon les maisons de leurs pères, selon leurs familles. Tu compteras tous les mâles depuis l'âge d'un mois et au-dessus. »
16 Musa aliwahesabu, kufuata maelekezo ya BWANA, kama alivyoamriwa kufanya.
Moïse les compta selon la parole de Yahvé, comme il en avait reçu l'ordre.
17 Majina ya watoto waLawi yalikuwa Gerishoni, Kohathi, na Merari.
Voici les fils de Lévi, selon leurs noms: Guershon, Kehath et Merari.
18 Ukoo uliotokana na watoto wa Gerishoni walikuwa ni Libni na Shimei.
Voici les noms des fils de Gershon, selon leurs familles: Libni et Shimei.
19 Ukoo uliotokana na watoto Kohathi walikuwa ni Amramu na, Izihari, Hebroni, na Uzieli.
Fils de Kehath, selon leurs familles: Amram, Izhar, Hebron et Uzziel.
20 Ukoo uliotokana na watoto wa Merari walikuwa ni Mahili na Mushi. Hizi ndizo koo za Walawi, zilizoorodheshwa ukoo kwa ukoo.
Les fils de Merari, selon leurs familles: Mahli et Mushi. Voici les familles des Lévites, selon les maisons de leurs pères.
21 Koo za Walibini na Washimei zilitokana na Wagerishoni. Hizi ndizo koo za Wagerishoni.
De Guershon, la famille des Libnites et la famille des Shiméites. Ce sont là les familles des Gershonites.
22 Wanaume wote wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi walihesabiwa na kufikia idadi ya 7, 500.
Ceux dont on fit le compte, selon le nombre de tous les mâles depuis l'âge d'un mois et au-dessus, ceux dont on fit le compte furent sept mille cinq cents.
23 Koo za Wagerishoni watapanga upande wa magharibi wa hema.
Les familles des Guershonites camperont derrière le tabernacle, à l'ouest.
24 Eliasafu mwana wa Laeli ataongoza koo za uzao wa Wagerishoni.
Eliasaph, fils de Lael, sera le chef de la maison des pères des Guershonites.
25 Familia ya Gerishoni watalilinda hema la kukutania pamoja na hiyo masikani. Watalilinda hema, kifuniko chake, na lile pazia la lango la hema ya kukutania.
Les fonctions des fils de Gershon dans la Tente d'assignation seront le tabernacle, le chapiteau, sa couverture, le rideau de l'entrée de la Tente d'assignation,
26 Wataulinda ua, lile pazia la kwenye lango—ua unaozunguka mahali patakatifu na madhabahu. Watazilinda kamba za hema ya kukutania na vyote vilivyomo.
les tentures du parvis, le rideau de l'entrée du parvis qui est près du tabernacle et autour de l'autel, et ses cordons pour tout son service.
27 Koo zifuatazo zinatokana na Kohathi: ukoo wa Waamrami, ukoo wa Waizihari ukoo wa Wahebroni, na ukoo wa Wauzieli. Koo hizi zinatokana na Wakohathi.
De Kehath, la famille des Amramites, la famille des Jitseharites, la famille des Hébronites et la famille des Uzzielites. Telles sont les familles des Kehathites.
28 Wanaume 8, 600 wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi walihesabiwa ili kulinda vitu vya BWANA.
D'après le nombre de tous les mâles, depuis l'âge d'un mois et au-dessus, il y en avait huit mille six cents qui observaient les prescriptions du sanctuaire.
29 Familia ya uzao wa Kohathi watapanga upande wa kusini wa Hema.
Les familles des fils de Kehath camperont au sud du tabernacle.
30 Elizafani mwana wa Uzieli ndiye atakayeongoza ukoo wa Wakohathi.
Le chef de la maison des pères des familles des Kehathites sera Elizaphan, fils d'Uzziel.
31 Watalilinda sanduku, meza, vikalishio vya taa, madhabahu, vitu vitakatifu ambvyo hutumika katika huduma yao, pazia, na kazi zote zinazoambatana na hema.
Il sera chargé de l'arche, de la table, du chandelier, des autels, des ustensiles du sanctuaire avec lesquels on fait le service, du rideau et de tout son service.
32 Eliazari mwana wa Haruni kuhani atawaongoza wanaume wanaowaongoza Walawi. Atawasimamia wanaume wanaongoza eneo takatifu.
Éléazar, fils du prêtre Aaron, sera le chef des chefs des lévites, avec la surveillance de ceux qui veillent aux besoins du sanctuaire.
33 Koo mbili zimetoka kwa Merari: Ukoo wa Mahili na ukoo wa Mushi. Koo hizi zimetokana na Merari,
De Merari était la famille des Mahlites et la famille des Mushites. Ce sont là les familles de Merari.
34 Wanaume 6, 200 wenye umri wa mwezi mmoja na zaidi walihesabiwa.
Ceux dont on fit le dénombrement, selon le nombre de tous les mâles depuis l'âge d'un mois et au-dessus, furent six mille deux cents.
35 Zurieli mwana wa Abihaili ataongoza ukoo wa Merari. Hawa watapanga upande wa kaskazini mwa hema.
Le prince de la maison des pères des familles de Merari était Tsuriel, fils d'Abihail. Ils camperont sur le côté nord de la tente.
36 Uzao wa Merari utatunza mbao za hema, mataruma, nguzo, makalishio, viifaa vya ujenzi na vitu vyote vinavyohusika,
Les fils de Merari seront chargés des planches du tabernacle, de ses barres, de ses piliers, de ses socles, de tous ses instruments, de tout son service,
37 na nguzo za ua zinazozunguka hema, makalishio, vigingi na kamba zake.
des piliers du parvis qui l'entourent, de leurs socles, de leurs broches et de leurs cordons.
38 Musa na Haruni na watoto wake watapanga upande wa mashariki wa masikani, mbele ya hema ya kukutania kuelekea mawio ya jua. Wao wataajibika na majukumu ya mahali patakatifu na majukumu ya wana wa Israeli. Mgeni atakayekaribia mahali patakatifu auawe.
Ceux qui campent devant le tabernacle, à l'est, devant la tente d'assignation, vers le lever du soleil, seront Moïse, avec Aaron et ses fils, gardant les exigences du sanctuaire pour le devoir des enfants d'Israël. L'étranger qui s'approchera sera mis à mort.
39 Musa na Haruni wakawahesabu wanaume wote wa ukoo wa Walawi walikuwa na umri wa mwezi mmoja na zaidi, kama vile BWANA alivyokuwa ameagiza. Walihesabu wanaume ishirini na mbili elfu.
Tous les Lévites dont Moïse et Aaron firent le compte sur l'ordre de l'Éternel, selon leurs familles, tous les mâles depuis l'âge d'un mois et au-dessus, furent vingt-deux mille.
40 BWANA alisema na Musa, “Wahesabu wanaume wote ambo ni wazaliwa wa kwanza wa Israeli ambao wana umri wa mwezi mmoja na zaidi. Orodhesha majina yao.
L'Éternel dit à Moïse: « Fais le compte de tous les premiers-nés mâles des enfants d'Israël, depuis l'âge d'un mois et au-dessus, et note le nombre de leurs noms.
41 Unitwalie walawi kwa ajili yangu badala ya wazaliwa wa kwanza wa Israeli, Mimi ndimi BWANA. Na utwae wanyama wa Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wa wanyama wa uzao wa Israeli,”
Tu prendras les Lévites pour moi - je suis Yahvé - à la place de tous les premiers-nés des enfants d'Israël, et le bétail des Lévites à la place de tous les premiers-nés du bétail des enfants d'Israël. »
42 Musa akawahesabu wazaliwa wa kwanza wote wa Israeli kama BWANA alivyomwagiza kufanya.
Moïse compta, comme l'avait ordonné l'Éternel, tous les premiers-nés des enfants d'Israël.
43 Aliwahesabu wazaliwa wote wa kwanza kwa mjina, wenye umri wa mwezi mmoja na zaidi. Alihesabu wanaume 22, 273.
Tous les premiers-nés mâles, selon le nombre des noms, depuis l'âge d'un mois et au-dessus, de ceux qui furent comptés, furent vingt-deux mille deux cent soixante-treize.
44 Tena BWANA alinena na Musa. Akasema,
Yahvé parla à Moïse, et dit:
45 “Watwae Walawi badala ya wazaliwa wote wa kwanza wa wana wa Israeli. Na utwae wanyama wa Walawi badala ya wanyama wa Waisreli wengine. Walawi ni mali yangu. Mimi ndimi BWANA.
« Prends les Lévites à la place de tous les premiers-nés des enfants d'Israël, et le bétail des Lévites à la place de leur bétail; et les Lévites seront à moi. Je suis Yahvé.
46 Unikusanyie shekeli tano za wokovu kwa kila hao 273 za hao wazaliwa wa kwanza wa Israeli za hao wanaozidi idadi ya Walawi.
Pour le rachat des deux cent soixante-treize premiers-nés des enfants d'Israël qui dépassent le nombre des Lévites,
47 Utazitumia hizo shekeli tano kwa kipimo cha mahali patakatifu. Shekeli moja ni sawa na gera ishirini.
tu prendras cinq sicles pour chacun d'eux; tu les prendras selon le sicle du sanctuaire (le sicle est de vingt gérachs);
48 Utawalipa hizo shekeli za wokovu kwa Haruni na wanawe.”
et tu donneras l'argent, avec lequel leur reste est racheté, à Aaron et à ses fils. »
49 Kwa hiyo Musa akakusanya shakeli za wokovu kutoka kwa wale waliozidi idadi ya wale waliookolewa na Walawi.
Moïse prit l'argent du rachat de ceux qui dépassaient le nombre des rachetés par les Lévites;
50 Musa akakusanya zile fedha kutoka kwa hao wazaliwa wa kwanza wa wana wa Israeli. Alikusanya jumla ya shekeli 1, 365, zenye kipimo sawa na mahali patakatifu. Musa akamlipa Haruni na wanawe hizo shekeli za wokovu.
il prit l'argent des premiers-nés des enfants d'Israël, mille trois cent soixante-cinq sicles, selon le sicle du sanctuaire;
51 Musa akafanya kila kitu alichoagizwa na neno la BWANA kama BWANA alivyomwagiza.
et Moïse donna l'argent du rachat à Aaron et à ses fils, selon la parole de Yahvé, comme Yahvé l'avait ordonné à Moïse.

< Hesabu 3 >