< Hesabu 3 >

1 Sasa hii ndiyo historia ya uzao wa Haruni na Musa wakati BWANA aliposema na Musa kwenye mlima Sinai.
These ben the generaciouns of Aaron and of Moises, in the dai in which the Lord spak to Moises, in the hil of Synay.
2 Majina ya watoto wa Haruni walikuwa Nadabu ambaye ndiyo mtoto wa kwanza, na Abihu, na Eliezeri, na Ithamari.
And these ben the names of `the sones of Aaron; his first gendrid, Nadab; aftirward, Abyu, and Eleazar, and Ythamar; these ben the names of `Aarons sones,
3 Haya ndiyo majina ya wana wa Haruni, makuhani waliokuwa wamepakwa mafuta na kuwekwa wakfu kutumika kama makuhani.
preestis, that weren anoyntid, and whos hondis weren fillid and halewid, that thei schulden `be set in preesthod.
4 Lakini Nadabu na Abihu walikufa mbele ya BWANA walipomtolea moto usiokubalika walipokuwa katika nyika ya Sinai. Nadabu na Abihu hawakuwa na watoto, kwa hiyo Eliazari na Ithamari walitumika kama makuhani pamoja na baba yao.
Nadab and Abyu, whanne thei offeriden alien fier in the `siyt of the Lord, in the deseert of Synay, weren deed without fre children; and Eleazar and Ythamar `weren set in preesthod bifor Aaron hir fadir.
5 BWANA alinena na Musa, akamwambia,
And the Lord spak to Moises,
6 “Walete kabila ya Lawi na uwaweke kwa Haruni kuhani ili wamsaidie
`and seide, `Presente thou the lynage of Leuy, and make to stonde in the siyt of Aaron, preest, that thei mynystre to hym;
7 Nao lazima wafanye majukumu badala ya Haruni na jumuiya yote mbele ya hema ya kukutania. Lazima watumike hemani.
and wake, and that thei kepe what euer thing perteyneth to the religioun of multitude, bifor the tabernacle of witnessyng;
8 Watayatunza mapambo ya hema ya kukutania, na watawatumikia makabila ya Israel kwa huduma ya hemani.
and that thei kepe the vessels of the tabernacle, and serue in the seruyce therof.
9 Uwaweke Walawi kwa Haruni na watoto wake. Nimewatoa kikamilifu ili wamsaidie kuwatumikia watu wa Israel.
And thou schalt yyue bi fre yifte the Leuytis to Aaron and hise sones, to whiche thei ben youun of the sones of Israel.
10 Umchague Haruni na watoto wake kuwa makuhani, lakini mgeni yeyote atakayekaribia lazima auawe.”
Sotheli thou schalt ordeyne Aaron and hise sones on the religioun of preesthod; a straungere, that neiyeth for to mynystre, and schal die.
11 BWANA alinena na Musa. akamwambia,
And the Lord spak to Moyses, `and seide,
12 “Tazama, nimewachagua Walawi katika watu wa Israel. Nimefanya hivyo badala ya kuchukua mzaliwa wa kwanza wa kiume wa wana wa Israel. Hawa Walawi ni wangu.
Y haue take the Leuytis of the sones of Israel for ech firste gendrid thing that openeth the womb in the sones of Israel; and the Leuytis schulen be myne,
13 Na hata wazaliwa wa kwanza ni mali yangu. Katika siku ambyo niliwavamia wazaliwa wote wa kwanza wa nchi ya Misri, Niliwatenga wazaliwa wa kwanza wa Israeli kwa ajili yangu, watu na wanyama pia. Ni mali yangu. Mimi ndimi BWANA.”
for ech firste gendrid thing is myn; sithen Y smoot the firste gendrid in the lond of Egipt, Y halewide to me what euer thing is borun first in Israel; fro man `til to beest thei ben myne; Y am the Lord.
14 BWANA alinena na Musa katika nyika ya Sinai. Akasema,
And the Lord spak to Moises in the deseert
15 “Wahesabu uzao wa Lawi katika kila familia, katika nyumba za koo zao. Hesabu kila mume kuanzia mwezi mmoja au zaidi.”
of Synay, and seide, Noumbre thou the sones of Leuy bi `the housis of her fadris, and bi meynees, ech male fro o monethe and aboue.
16 Musa aliwahesabu, kufuata maelekezo ya BWANA, kama alivyoamriwa kufanya.
Moises noumbride, as the Lord comaundide.
17 Majina ya watoto waLawi yalikuwa Gerishoni, Kohathi, na Merari.
And the sones of Leuy weren foundun, bi her names, Gerson, and Caath, and Merary;
18 Ukoo uliotokana na watoto wa Gerishoni walikuwa ni Libni na Shimei.
the sones of Gerson weren Lebny, and Semey;
19 Ukoo uliotokana na watoto Kohathi walikuwa ni Amramu na, Izihari, Hebroni, na Uzieli.
the sones of Caath weren Amram, and Jessaar, Hebron, and Oziel;
20 Ukoo uliotokana na watoto wa Merari walikuwa ni Mahili na Mushi. Hizi ndizo koo za Walawi, zilizoorodheshwa ukoo kwa ukoo.
and the sones of Merari weren Mooly, and Musi.
21 Koo za Walibini na Washimei zilitokana na Wagerishoni. Hizi ndizo koo za Wagerishoni.
Of Gerson weren twei meynees, of Lebny, and of Semei;
22 Wanaume wote wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi walihesabiwa na kufikia idadi ya 7, 500.
of whiche the puple of male kynde was noumbrid, fro o monethe and aboue, seuene thousynde and fyue hundrid.
23 Koo za Wagerishoni watapanga upande wa magharibi wa hema.
These schulen sette tentis aftir the tabernacle at the west,
24 Eliasafu mwana wa Laeli ataongoza koo za uzao wa Wagerishoni.
vndur the prince Eliasaph, the sone of Jahel.
25 Familia ya Gerishoni watalilinda hema la kukutania pamoja na hiyo masikani. Watalilinda hema, kifuniko chake, na lile pazia la lango la hema ya kukutania.
And thei schulen haue kepyngis in the tabernacle of boond of pees, the tabernacle it silf, and the hilyng therof, the tente which is drawun bifor the yatis of the hilyng of the witnessyng of boond of pees;
26 Wataulinda ua, lile pazia la kwenye lango—ua unaozunguka mahali patakatifu na madhabahu. Watazilinda kamba za hema ya kukutania na vyote vilivyomo.
and the curteyns of the greet street, also the tente which is hangid in the entryng of the greet street of the tabernacle, and what euer thing perteyneth to the custom of the auter, the cordis of the tabernacle, and al the purtenaunce therof.
27 Koo zifuatazo zinatokana na Kohathi: ukoo wa Waamrami, ukoo wa Waizihari ukoo wa Wahebroni, na ukoo wa Wauzieli. Koo hizi zinatokana na Wakohathi.
The kynrede of Caath schal haue the puplis of Amram, and of Jessaar, and of Ebron, and of Oziel;
28 Wanaume 8, 600 wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi walihesabiwa ili kulinda vitu vya BWANA.
these ben the meynees of Caathitis, noumbrid bi her names, alle of male kynde, fro o monethe and aboue, eiyte thousynde and sixe hundrid.
29 Familia ya uzao wa Kohathi watapanga upande wa kusini wa Hema.
Thei schulen haue kepyngis of the seyntuarie, and schulen sette tentis at the south coost;
30 Elizafani mwana wa Uzieli ndiye atakayeongoza ukoo wa Wakohathi.
and `the prince of hem schal be Elisaphan, the sone of Oziel.
31 Watalilinda sanduku, meza, vikalishio vya taa, madhabahu, vitu vitakatifu ambvyo hutumika katika huduma yao, pazia, na kazi zote zinazoambatana na hema.
And thei schulen kepe the arke, and the boord, and the candilstike, the auters, and vesselis of the seyntuarie in whiche it is mynystrid, and the veil, and al sich purtenaunce.
32 Eliazari mwana wa Haruni kuhani atawaongoza wanaume wanaowaongoza Walawi. Atawasimamia wanaume wanaongoza eneo takatifu.
Sotheli the prince of princis of Leuytis schal be Eleazar, the sone of Aaron, preest; and he schal be on the keperis of the kepyng of the seyntuarie.
33 Koo mbili zimetoka kwa Merari: Ukoo wa Mahili na ukoo wa Mushi. Koo hizi zimetokana na Merari,
And sotheli of Merary schulen be the puplis of Mooli, and of Musi,
34 Wanaume 6, 200 wenye umri wa mwezi mmoja na zaidi walihesabiwa.
noumbrid bi her names, alle of male kynde fro o monethe and aboue, sixe thousynde and two hundrid;
35 Zurieli mwana wa Abihaili ataongoza ukoo wa Merari. Hawa watapanga upande wa kaskazini mwa hema.
`the prince of hem schal be Suriel, the sone of Abiahiel; thei schulen sette tentis in the north coost.
36 Uzao wa Merari utatunza mbao za hema, mataruma, nguzo, makalishio, viifaa vya ujenzi na vitu vyote vinavyohusika,
And vndur `the kepyng of hem schulen be the tablis of the tabernacle, and the barris, and the pileris, and `the foundementis of tho, and alle thingis that perteynen to sich ournyng,
37 na nguzo za ua zinazozunguka hema, makalishio, vigingi na kamba zake.
and the pileris of the greet street bi cumpas, with her foundementis, and the stakis with coordis.
38 Musa na Haruni na watoto wake watapanga upande wa mashariki wa masikani, mbele ya hema ya kukutania kuelekea mawio ya jua. Wao wataajibika na majukumu ya mahali patakatifu na majukumu ya wana wa Israeli. Mgeni atakayekaribia mahali patakatifu auawe.
Forsothe Moises and Aaron with hise sones schulen sette tentis bifor the tabernacle of boond of pees, that is, at the eest coost, and schulen haue the keping of the seyntuarie, in the myddis of the sones of Israel; what euer alien neiyeth, he schal die.
39 Musa na Haruni wakawahesabu wanaume wote wa ukoo wa Walawi walikuwa na umri wa mwezi mmoja na zaidi, kama vile BWANA alivyokuwa ameagiza. Walihesabu wanaume ishirini na mbili elfu.
Alle the Leuytis, whiche Moises and Aaron noumbriden, bi comaundement of the Lord, bi her meynees, in male kynde, fro o monethe and aboue, were two and twenti thousynd.
40 BWANA alisema na Musa, “Wahesabu wanaume wote ambo ni wazaliwa wa kwanza wa Israeli ambao wana umri wa mwezi mmoja na zaidi. Orodhesha majina yao.
And the Lord seide to Moises, Noumbre thou the firste gendrid children of male kynde of the sones of Israel, fro o monethe and aboue; and thou schalt haue the summe of hem; and
41 Unitwalie walawi kwa ajili yangu badala ya wazaliwa wa kwanza wa Israeli, Mimi ndimi BWANA. Na utwae wanyama wa Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wa wanyama wa uzao wa Israeli,”
thou schalt take Leuytis to me for alle the firste gendrid of the sones of Israel; Y am the Lord; and thou schalt take `the beestis of hem for alle the firste gendrid of the sones of Israel.
42 Musa akawahesabu wazaliwa wa kwanza wote wa Israeli kama BWANA alivyomwagiza kufanya.
And as the Lord comaundide, Moises noumbride the firste gendrid children of the sones of Israel; and the males weren bi her names,
43 Aliwahesabu wazaliwa wote wa kwanza kwa mjina, wenye umri wa mwezi mmoja na zaidi. Alihesabu wanaume 22, 273.
fro o monethe and aboue, two and twenti thousynde two hundrid and seuenti and thre.
44 Tena BWANA alinena na Musa. Akasema,
And the Lord spak to Moises, and seide,
45 “Watwae Walawi badala ya wazaliwa wote wa kwanza wa wana wa Israeli. Na utwae wanyama wa Walawi badala ya wanyama wa Waisreli wengine. Walawi ni mali yangu. Mimi ndimi BWANA.
Take thou Leuytis for the firste gendrid children of the sones of Israel, and the beestis of Leuytis for the beestis of hem, and the Leuytis schulen be myne; Y am the Lord.
46 Unikusanyie shekeli tano za wokovu kwa kila hao 273 za hao wazaliwa wa kwanza wa Israeli za hao wanaozidi idadi ya Walawi.
Forsothe in the prijs of two hundrid seuenti and thre, that passen the noumbre of `Leuytis, of the firste gendrid children of the sones of Israel,
47 Utazitumia hizo shekeli tano kwa kipimo cha mahali patakatifu. Shekeli moja ni sawa na gera ishirini.
thou schalt take fyue ciclis bi ech heed, at the mesure of seyntuarie; a sicle hath xx. halpens;
48 Utawalipa hizo shekeli za wokovu kwa Haruni na wanawe.”
and thou schalt yyue the money to Aaron and to hise sones, the prijs of hem that ben aboue.
49 Kwa hiyo Musa akakusanya shakeli za wokovu kutoka kwa wale waliozidi idadi ya wale waliookolewa na Walawi.
Therfor Moises took the money of hem that weren aboue, and whiche thei hadden ayenbouyt of the Leuytis, for the firste gendrid of the sones of Israel,
50 Musa akakusanya zile fedha kutoka kwa hao wazaliwa wa kwanza wa wana wa Israeli. Alikusanya jumla ya shekeli 1, 365, zenye kipimo sawa na mahali patakatifu. Musa akamlipa Haruni na wanawe hizo shekeli za wokovu.
a thousand thre hundrid sixti and fyue of siclis, bi the weiyte of seyntuarie;
51 Musa akafanya kila kitu alichoagizwa na neno la BWANA kama BWANA alivyomwagiza.
and he yaf that money to Aaron and to hise sones, bi the word which the Lord comaundide to hym.

< Hesabu 3 >