< Hesabu 11 >
1 Sasa watu wakanung'unika juu ya matatizo yao wakati BWANA alipokuwa akiwasikiliza. BWANA akawasikia watu naye akakasirika. Moto kutoka kwa BWANA ukashuka na ukawaka kati yao na kuteketeza baadhi ya kambi kwenye pembe zake.
Now the people were saying evil against the Lord; and the Lord, hearing it, was angry and sent fire on them, burning the outer parts of the tent-circle.
2 Ndipo watu wakamwita Musa kwa nguvu, Naye Musa akamwomba BWANA, na ule moto ukazimika.
And the people made an outcry to Moses, and Moses made prayer to the Lord, and the fire was stopped.
3 Mahali pale paliitwa Tabera, kwa sababu moto wa BWANA uliwaka kati yao.
So that place was named Taberah, because of the fire of the Lord which had been burning among them.
4 Baadhi ya wageni wakaanza kuweka kambi zao pamoja na wana wa wa Israeli. Walitaka kula chakula kizuri. Kisha wana wa Israeli walipoanza kulia wakisema, “Ni nani atakayetupatia nyama za kula?
And the mixed band of people who went with them were overcome by desire: and the children of Israel, weeping again, said, Who will give us flesh for our food?
5 Tunakumbuka samaki tulizokula bure kule Misri, yale matango, na matikiti maji, na mboga na vitunguu na vitunguu saumu.
Sweet is the memory of the fish we had in Egypt for nothing, and the fruit and green plants of every sort, sharp and pleasing to the taste:
6 Na sasa hatuna hamu ya kula, kwa sababu tunaona mana tu.
But now our soul is wasted away; there is nothing at all: we have nothing but this manna before our eyes.
7 Mana ilifanana na punje ya mtama. ilionekana kama bedola.
Now the manna was like a seed of grain, like small clear drops.
8 watu wakazunguka kisha wakakusanyika. Wakaisaga, wakaitwanga kwa vinu, wakaitokosa nyunguni, na kuitengeneza mikate. radha yake ilikuwa kama mafuta mapya ya mizeituni.
The people went about taking it up from the earth, crushing it between stones or hammering it to powder, and boiling it in pots, and they made cakes of it: its taste was like the taste of cakes cooked with oil.
9 Na umande ulipoanguka kambini usiku ule, na mana ilianguka pia.
When the dew came down on the tents at night, the manna came down with it.
10 Musa akawasikia watu wakilia katika familia zao, na kila mtu alikuwa kwenye lango la hema yake. BWANA alikasirika sana, na mbele ya macho ya Musa malalamiko yao yalikuwa mabaya.
And at the sound of the people weeping, every man at his tent-door, the wrath of the Lord was great, and Moses was very angry.
11 Musa akasema na BWANA, “Kwa nini umemtendea mtumishi wako vibaya namna hiyo? kwa nini hujapendezwa na mimi? unanifanya kubeba mizigo ya hawa watu.
And Moses said to the Lord, Why have you done me this evil? and why have I not grace in your eyes, that you have put on me the care of all this people?
12 Je, mimi ndiye niliyewatungia mimba hawa watu? Mimi ndiye niliyewazaa kiasi kwamba unaniambia, “wabebe kwa ukaribu vifuani mwako kama baba abebavyo mtoto wake? Je, nitawabeba mpaka kwenye nchi ambayo uliwaahidi mababu zao kuwapa?
Am I the father of all this people? have I given them birth, that you say to me, Take them in your arms, like a child at the breast, to the land which you gave by an oath to their fathers?
13 Naweza kupata wapi nyama za kuwapa watu wote hawa? Wanalia mbele zangu na wanasema, 'tupe nyama tule.'
Where am I to get flesh to give to all this people? For they are weeping to me and saying, Give us flesh for our food.
14 Mimi peke yangu siwezi kuwabeba watu wote hawa. Ni wengi sana kwangu.
I am not able by myself to take the weight of all this people, for it is more than my strength.
15 Kwa vile unanitendea hivi, basi uniue, na kama wewe ni mpole kwangu, basi niondolee mzigo huu.”
If this is to be my fate, put me to death now in answer to my prayer, if I have grace in your eyes; and let me not see my shame.
16 BWANA akamwambia Musa, “Niletee wazee sabini miongoni mwa Waisraeli. Hakikisha ni wazee na viongozi wa watu. Uwalete kwenye hema ya kukutania wasimame pamoja na wewe.
And the Lord said to Moses, Send for seventy of the responsible men of Israel, who are in your opinion men of weight and authority over the people; make them come to the Tent of meeting and be there with you.
17 Nami nitashuka niseme nawe mahali pale. Nitatoa sehemu ya roho iliyo ndani yako na kuwapatia wao. Nao watabeba mzigo wa watu pamoja nawe. na hautaubeba peke yako.
And I will come down and have talk with you there: and I will take some of the spirit which is on you and put it on them, and they will take part of the weight of the people off you, so that you do not have to take it by yourself.
18 Waambie watu, 'Jitakaseni ninyi wenyewe, kwa kuwa kesho mtakuala nyama, kwa kuwa mmelia na BWANA amesikia, “Mlipokuwa mkisema kuwa nani atakayetupa nyama tule? Kule Misri tulikula chakula kizuri!” Kwa hiyo BWANA atawapeni nyama, nanyi mtakula nyama.
And say to the people, Make yourselves clean before tomorrow and you will have flesh for your food: for in the ears of the Lord you have been weeping and saying, Who will give us flesh for food? for we were well off in Egypt: and so the Lord will give you flesh, and it will be your food;
19 Hamtakula nyama kwa siku moja tu, au siku mbili, au siku tano, au siku kumi, au siku ishirini,
Not for one day only, or even for five or ten or twenty days;
20 Lakini mtakula nyama kwa mwezi mmoja mpaka zitakapowatokea puani. Mpaka zitawakinai kwa sababu mmemkataa BWANA ambaye yuko kati yenu. Mmelia mbele yake. mmesema, “Kwa nini tulitoka Misri?””
But every day for a month, till you are tired of it, turning from it in disgust: because you have gone against the Lord who is with you, and have been weeping before him saying, Why did we come out of Egypt?
21 Kisha Musa akasema, “Mimi nina watu 600, 000, na wewe umesema, “Nitawapa nyama mle kwa mwezi mmoja,'
Then Moses said, The people, among whom I am, are six hundred thousand men on foot; and you have said, I will give them flesh to be their food for a month.
22 Je, tutayachinja haya makundi ya ng'ombe na kondoo ili kuwatosheleza?”
Are flocks and herds to be put to death for them? or are all the fish in the sea to be got together so that they may be full?
23 BWANA akasema na Musa, “Je mkono wangu ni mfupi? Sasa utaona kama maneno yangu ni ya kweli ama sivyo.
And the Lord said to Moses, Has the Lord's hand become short? Now you will see if my word comes true for you or not.
24 Musa alitoka nje kwenda kuwaambia watu maneno ya BWANA. Aliwakusanya wazee sabini wa watu na kuwaweka kuizunguka hema.
And Moses went out and gave the people the words of the Lord: and he took seventy of the responsible men of the people, placing them round the Tent.
25 BWANA akashuka chini katika wingu akaongea na Musa. BWANA akachukua sehemu ya roho iliyokuwa kwa Musa na kuiweka kwa wale wazee sabini. Roho alipowashukia, wakaanza kutoa unabii, lakini ilitokea kwenye tukio hilo tu na haikujirudia tena.
Then the Lord came down in the cloud and had talk with him, and put on the seventy men some of the spirit which was on him: now when the spirit came to rest on them, they were like prophets, but only at that time.
26 Watu wawili waitwao Elidadi na Medadi walibaki kambini. Lakini Roho aliwashukia pia. Majina yao yalikuwa yameandikwa kwenye orodha lakini walikuwa hawajaenda hemani. Hata hivyo nao walitoa unabii wakiwa kambini.
But two men were still in the tent-circle one of them named Eldad and the other Medad: and the spirit came to rest on them; they were among those who had been sent for, but they had not gone out to the Tent: and the prophet's power came on them in the tent-circle.
27 Kijana mmoja huko kambini alikimbia akaenda kumwambia Musa, “Elidadi na Medadi wanatoa unabii kambini.”
And a young man went running to Moses and said, Eldad and Medad are acting as prophets in the tent-circle.
28 Joshua mwana wa Nuni, msaidizi wa Musa, ambaye ni miongoni mwa wale aliowachagua akamwambia Musa, “Bwana wangu Musa, wazuie.”
Then Joshua, the son of Nun, who had been Moses' servant from the time when he was a child, said, My lord Moses, let them be stopped.
29 Musa akamwambia, “una wivu kwa niaba yangu? Natamani kama watu wote wa BWANA wangekuwa manabii na kwamba angeweka Roho yake juu yao wote!”
And Moses said to him, Are you moved by envy on my account? If only all the Lord's people were prophets, and the Lord might put his spirit on them!
30 Kisha Musa na wale wazee wakarudi kambini.
Then Moses, with the responsible men of Israel, went back to the tent-circle.
31 Kisha upepo ukavuma kutoka kwa BWANA ukaja na kware kutokea baharini. Wakaanguka karibu na kambi, kiasi cha umbali wa safari ya siku moja upande huu na umbali wa siku moja upande mwingine. Wale kware wakaizunguka kambi kiasi cha mita moja toka uso wa dunia.
Then the Lord sent a wind, driving little birds from the sea, so that they came down on the tents, and all round the tent-circle, about a day's journey on this side and on that, in masses about two cubits high over the face of the earth.
32 Watu wakawakusanya hao kware kwa bidii mchana huo wote na usiku huo wote, na mchana wote uliofuatia. Hakuna aliyekusanya pungufu ya mita mbili za uajazo. Wakawaanika kweye ardhi yote hapo kambini.
And all that day and all night and the day after, the people were taking up the birds; the smallest amount which anyone got was ten homers: and they put them out all round the tents.
33 Wakati ile nyama ikiwa bado iko kwenye meno yao, wakiwa bado wanatafuna, BWANA akawakasirikia. Akwapiga watu wale kwa gonjwa kubwa sana.
But while the meat was still between their teeth, before it was tasted, the wrath of the Lord was moved against the people and he sent a great outburst of disease on them.
34 Mahali pale paliitwa Kibroti Hataava, kwa sababu pale walizika watu waliotamani nyama.
So that place was named Kibroth-hattaavah; because there they put in the earth the bodies of the people who had given way to their desires.
35 Kutoka Kibroti Hataava watu wakasafiri hadi Hazeroti, ambapo walipumzika.
From Kibroth-hattaavah the people went on to Hazeroth; and there they put up their tents.