< Hesabu 10 >

1 BWANA alinena na Musa, akasema,
And he spoke Yahweh to Moses saying.
2 “tengenza tarumbeta mbili za fedha. Uzitengeneze kwa kufua hizo fedha. Utazitumia hizo tarumbeta kwa kuwaita watu waje pamoja na kwa kuwaita watu wote wakati wa kuondoka kwenye kambi zao.
Make for yourself two trumpets of silver hammered work you will make them and they will be for you for [the] convocation of the congregation and for breaking the camps.
3 Makuhani watapiga tarumbeta kwa ajili ya kuwaita watu wote mbele yako kwenye lango la hema ya kukutania.
And they will give a blast on them and they will gather together to you all the congregation to [the] entrance of [the] tent of meeting.
4 Kama makuhani watapiga tarumbeta moja tu, basi viongozi, vichwa koo za Israeli ndipo watakapokutana kwako.
And if on one [trumpet] they will give a blast and they will gather together to you the leaders [the] heads of [the] families of Israel.
5 Utakapopiga tarumbeta ya sauti kuu, ile kambi ya upande wa mashariki itaanza kusafiri.
And you will give a blast an alarm and they will set out the camps which encamp east-ward.
6 Nawe utakapopiga tarumeta kwa sauti kuu mara ya pili, ile kambi ya upande wa kusini wataanza kusafiri. Watapiga tarumbeta kwa sauti kuu ili kuanza safari yao.
And you will give a blast an alarm second and they will set out the camps which encamp south-ward an alarm they will give a blast for settings out their.
7 Watu wote watakapokutana pamoja, piga hizo tarumbeta lakini si kwa sauti kuu.
And when summon the assembly you will give a blast and not you will give an alarm.
8 Wana wa Haruni, makuhani, watapiga hizo tarumbeta. Huu ndio utakaokuwa utaratibu wa watu wako kwa vizazi vyote.
And [the] sons of Aaron the priests they will give a blast on trumpets and they will become for you a statute of perpetuity to generations your.
9 Nanyi mtakapoenda vitani katika ardhi yenu dhidi ya maadui wenu wanaowakandamiza, ndipo mtakapotoa ishara ya sauti ya tarumbeta. Mimi, BWANA Mungu wako nitawaita kuwakumbuka na kuwaokoa kutoka kwa maadui wenu.
And if you will go war in land your on the foe who opposes you and you will give an alarm on trumpets and you will be remembered before Yahweh God your and you will be delivered from enemies your.
10 Pia, wakati wa kusherehekea, sikukuu zenu za kawaida na katika miandamo ya miezi, mtapiga tarumbeta zenu kwa heshima ya sadaka zenu za kuteketezwa na kwa sadaka zenu za amani. Huu utakuwa ukumbusho wenu kwangu, Mungu wenu. Mimi ndimi BWANA Mungu wenu.”
And on [the] day of rejoicing your and at appointed feasts your and at [the] beginnings of months your and you will give a blast on trumpets over burnt offerings your and over [the] sacrifices of peace offerings your and they will become for you a memorial before God your I [am] Yahweh God your.
11 Katika siku ya ishrini, mwezi wa pili, mwaka wa pili, Lile wingu liliinuliwa toka masikani ya amri za maagano.
And it was in the year second in the month second on [day] twenty in the month it was taken up the cloud from over [the] tabernacle of the testimony.
12 Wana wa Israeli wakaendelea na safari yao toka jangwa la Sinai. Lile wingu likasimama kwenye jangwa la Parani.
And they set out [the] people of Israel to journeyings their from [the] wilderness of Sinai and it settled down the cloud in [the] wilderness of Paran.
13 Walifanya safari yao ya kwanza, kufuatia amri ya BWANA iliyotolewa kupitia kwa Musa.
And they set out at the first [time] on [the] mouth of Yahweh by [the] hand of Moses.
14 Kambi ya mahali pa uzao wa Yuda iliondoka ya kanza, wakiondoa majeshi yao binafsi. Nashoni mwana wa Aminadabu ndiye aliyeongoza jeshi la Yuda.
And it set out [the] standard of [the] camp of [the] descendants of Judah at the first to military groups their and [was] over military group its Nahshon [the] son of Amminadab.
15 Nethaneli mwana wa Zuari aliongoza jeshi la kabila la uzao wa Isakari.
And [was] over [the] military group of [the] tribe of [the] descendants of Issachar Nethanel [the] son of Zuar.
16 Eliabu mwana wa Heloni aliongoza jeshi la kabila la Zabuloni.
And [was] over [the] military group of [the] tribe of [the] descendants of Zebulun Eliab [the] son of Helon.
17 Uzao wa Gerishoni na Merari, ambao walitunza masikani, na kuanza kusafiri.
And it was taken down the tabernacle and they set out [the] descendants of Gershon and [the] descendants of Merari [the] bearers of the tabernacle.
18 Baadaye Walifuata jeshi la mahali pa kambi ya Reubeni walianza safari yao. Elizuri mwana wa Shedeuri alliongoza jeshi la Reubebni.
And it set out [the] standard of [the] camp of Reuben to military groups their and [was] over military group its Elizur [the] son of Shedeur.
19 Shelumieli mwana wa Zurishadai aliliongoza jeshi la kabila la uzao wa Simeoni.
And [was] over [the] military group of [the] tribe of [the] descendants of Simeon Shelumiel [the] son of Zuri-shaddai.
20 Eliasafu mwana Deuli aliliongoza jeshi la kabila la uzao wa Gadi.
And [was] over [the] military group of [the] tribe of [the] descendants of Gad Eliasaph [the] son of Deuel.
21 Kabila la Kohathi nalo lilianza safari. Wao walibebba vyombo vya mahali patakatifu. Wengine waliisimamisha masikani kabla ya Wakohathi kufika kambi inayofuata.
And they set out the Kohathites [the] bearers of the sanctuary and people set up the tabernacle until came they.
22 Majeshi ya kabila la uzao wa Efraimu ndio waliofuata. Elishama mwana wa Amihudi ndiye aliyeongoza jeshi la Efraimu.
And it set out [the] standard of [the] camp of [the] descendants of Ephraim to military groups their and [was] over military group its Elishama [the] son of Ammihud.
23 Gamalieli mwana wa Pedazuri aliongoza jeshi la uzao wa Manase.
And [was] over [the] military group of [the] tribe of [the] descendants of Manasseh Gamaliel [the] son of Pedah-zur.
24 Abidani mwana wa Gidioni aliongoza jeshi la uzao wa kabila la Benjamini.
And [was] over [the] military group of [the] tribe of [the] descendants of Benjamin Abidan [the] son of Gideoni.
25 Lile jeshi lililoweka kambi mahali pa bango la uzao wa Dani lilikuwa la mwisho kuondoka. Ahizeri mwana wa Amishadai ndiye aliyeongoza jeshi la Dani.
And it set out [the] standard of [the] camp of [the] descendants of Dan a rearguard of all the camps to military groups their and [was] over military group its Ahiezer [the] son of Ammishaddai.
26 Pagieli mwana wa Okirani aliongoza jeshi la wana wa uzao wa Asheri.
And [was] over [the] military group of [the] tribe of [the] descendants of Asher Pagiel [the] son of Ocran.
27 Ahira mwana wa Enani aliongoza jeshi la uzao wa kabila ya Naftali.
And [was] over [the] military group of [the] tribe of [the] descendants of Naphtali Ahira [the] son of Enan.
28 Hivi ndivyo majeshi ya wana wa Israeli yalivyosafiri.
These [are] [the] settings out of [the] people of Israel to military groups their and they set out.
29 Musa alinena na Hobibu mwana wa Reueli wa Kabila la Midiani. Reueli alikuwa baba mke wa Musa. Musa akanena na Hobibu akasema, “Tunasafiri kuelekea mahali ambapo BWANA ametuahidi. BWANA alisema kuwa, “Nitawapeni ninyi hilo eneo, 'Njoni pamoja nasi na tutawatendea mema. BWANA ameahidi kuwafanyia mema Waisraeli.”
And he said Moses to Hobab [the] son of Reuel the Midianite [the] father-in-law of Moses [are] about to set out - we to the place which he said Yahweh it I will give to you come! with us and we will do good to you for Yahweh he has spoken good on Israel.
30 Lakini Hobibu akmwambia Musa, “Sitaambatana nanyi.”
And he said to him not I will go that except to own land my and to kindred my I will go.
31 Naye Musa akamjibu, “Tafadhali msituache. Mnajua jinsi ilivyo kuweka kambi jangwani. Tunaomba mtujali.
And he said may not please you leave us for - since you know encamping we in the wilderness and you will become of us eyes.
32 Kama mtaambatana nasi tutawatendea mema sawa na jinsi BWANA anavyotutendea.”
And it will be that you will go with us and it will be - the good that which he will do good Yahweh with us and we will do good to you.
33 Walisafiri kutoka mlima wa BWANA kwa siku tatu. Sanduku la agano la BWANA liliwatangulia kwa siku tatu ili kupata mahali pa kupumzika.
And they set out from [the] mountain of Yahweh a journey of three days and [the] ark of [the] covenant of Yahweh [was] setting out before them a journey of three days to seek out for them a resting place.
34 Wingu la BWANA lilikuwa juu yao muda wote wa mchana walipokuwa safarini.
And [the] cloud of Yahweh [was] over them by day when set out they from (the camp. *LBH(a)*)
35 Kila hilo sanduku liliposafiri kwenda mbele, Musa alisema, “Inuka BWANA, Uwatawanye maadui wako. Uwafanye wale wanaokuchukia kukukimbia.”
And it was when set out the ark and he said Moses rise up! - O Yahweh so they may be scattered enemies your and they may flee [those who] hate you from before you.
36 Na kila lile sanduku liliposimama, Musa alisema, “BWANA uwarudie, hawa Waisraeli makumi elfu.”
And when rested it he said return! O Yahweh [the] ten thousands of [the] families of Israel.

< Hesabu 10 >