< Luka 7 >
1 Baada ya Yesu kumaliza kila kitu alichokuwa anasema kwa watu waliomsikiliza, akaingia Kapernaumu.
After Jesus finished saying this to the people, he went [with his disciples] to Capernaum [town].
2 Mtumwa fulani wa akida, aliyekuwa wa thamani sana kwake, alikuwa mgonjwa sana na alikuwa karibu ya kufa.
There was a Roman army officer there who had a slave whom he thought highly of. This slave was so sick that he was about to die.
3 Lakini akiwa amesikia kuhusu Yesu, yule Akida alimtuma kiongozi wa kiyahudi, kumwomba aje kumwokoa mtumwa wake ili asife.
When the officer heard about Jesus, he [summoned] some Jewish elders. He told them to go to Jesus and ask him to come and heal his slave.
4 Walipofika karibu na Yesu, walimsihi kwa bidii na kusema, “anastahili kwamba unapaswa kufanya hivi kwa ajili yake,
When they came to where Jesus was, they earnestly asked Jesus [to return with them]. They said, “This officer deserves that you [(sg)] do this [for him],
5 kwa sababu analipenda taifa letu, na ndiye aliyejenga sinagogi kwa ajili yetu”.
because he loves us [Jewish] people, and he [paid the money to] build a synagogue for us.”
6 Yesu akaendelea na safari yake pamoja nao. lakini kabla hajaenda mbali na nyumba, afisa mmoja aliwatuma marafiki zake kuzungumza naye. “Bwana, usijichoshe mwenyewe kwa sababu mimi sistahili wewe kuingia kwenye dari yangu.
So Jesus went with them. When he was near the [officer’s] house, the officer [decided that it was not necessary for Jesus to come to his house. So he] summoned some friends. He [told them to] go to Jesus and tell him this: “Lord/Sir, do not bother to come. [Because I am a non-Jew], I am not worthy for you [(sg)], [a Jew], to come into my house [MTY] [and associate with me].
7 Kwa sababu hii sikufikiria hata mimi mwenyewe kuwa ninafaa kuja kwako, lakini sema neno tu na mtumishi wangu atapona.
I did not feel worthy to come to you, [either]. But [please] command [that] my servant [be healed], and he will become well!
8 Kwani mimi pia ni mtu niliyewekwa kwenye mamlaka na nina askari chini yangu. Husema kwa huyu “Nenda” na huenda, na kwa mwingine, “Njoo” naye huja, na kwa mtumishi wangu 'Fanya hiki', na yeye hufanya”.
[I believe this] because, as for me, there are people who have authority over me [and I obey them]. I also have soldiers under my [authority]. When I say to one of them, ‘Go!’ he goes. When I say to another ‘Come!’ he comes. When I say to my slave, ‘Do this!’ he does it. [And I believe that you speak with a similar kind of authority].”
9 Yesu aliposikia haya alishangaa, na kuwageukia makutano waliokuwa wanamfuata na kusema.”Nawaambia, hata katika Israeli, sijawahi kuona mtu mwenye imani kuu kama huyu.
When [the officer’s friends arrived and] told that to Jesus, he marveled at what [the officer had said]. Then he turned and said to the crowd that was going with him, “I tell you, I have never before found anyone who trusted [in me like this non-Jewish man does]. No one from Israel, [where I would expect people to believe in me], has trusted in me like he has!”
10 Kisha wale waliokuwa wametumwa walirudi nyumbani na kumkuta mtumishi akiwa mzima.
When those men returned to the officer’s house, they found that the slave was well.
11 fulani baada ya haya, ilitokea kuwa Yesu alikuwa anasafiri kwenda mji ulioitwa Naini. wanafunzi wake wakaenda pamoja naye wakiambana na umati wa watu.
Soon after that, Jesus went to a town called Nain. His disciples and a large crowd [of other people] went with him.
12 Alipofika karibu na Lango la jiji tazama, mtu aliyekufa alikuwa amebebwa, na ni mtoto wa pekee kwa mama yake. aliyekuwa mjane, na umati wa wawakilishi kutoka kwenye jiji walikuwa pamoja naye.
As they approached the town gate, the corpse of a young man who had just died was being carried out [on a stretcher] {[people] were carrying out [on a stretcher] the corpse of a young man who had just died}. His mother was a widow, and he was her only son. A large group of people from the town were accompanying them.
13 Alipomwona, Bwana akamsogelea kwa huruma kubwa sana juu yake na akamwambia, “Usilie”.
When the Lord saw her, he pitied her. He said to her, “Do not cry!”
14 Kisha akasogea mbele akaligusa jeneza ambalo walibebea mwili, na wale waliobeba wakasimama akasema “Kijana nasema amka”
Then, [ignoring the Jewish laws about not coming near a corpse], he came close and touched the stretcher [on which the body was lying]. So the men carrying it stood still. He said, “Young man, I say to you, get up!”
15 Mfu akainuka na kukaa chini na akaanza kuongea. Kisha Yesu akamkabidhi kwa mama yake.
The man sat up and began to talk! Jesus returned him to his mother [to care for her].
16 Kisha hofu ikawajaa wote. wakaendelea kumtukuza Mungu wakisema “Nabii mkuu ameinuliwa miongoni mwetu” na “Mungu amewaangalia watu wake”
Then everyone [there] was amazed/awestruck. They praised God, saying, “A great prophet has come among us!” They also said, “God has come to help his people!”
17 Hizi habari njema za Yesu zilienea Yudea yote na kwa mikoa yote ya jirani.
[Then they] reported what Jesus [had done] throughout all of Judea [district] and other nearby areas.
18 Wanafunzi wa Yohana walimwamwambia mambo haya yote.
The disciples of John [the Baptizer went to the prison where John was and] told him about those things.
19 Ndipo Yohana akawaita wawili wa wanafunzi wake na kuwatuma kwa Bwana kusema “Wewe ndiye yule ajaye, au kuna mtu mwingine tumtazamie?
So [one day] John summoned two [of his disciples] and [told them] to go to the Lord and ask him: “Are you [the Messiah who the prophets prophesied would come], or is it someone else that we should expect [to come]?”
20 Walipofika karibu na Yesu hawa wakasema, “Yohana mbatizaji ametutuma kwako kusema, 'Wewe ni yule ajaye au kuna mtu mwingine tumtazamie?”
When those two men came to Jesus, they said, “John the Baptizer sent us to ask you [(sg)] this: Are you [the Messiah that] we are expecting [God] to send, or shall we [(exc)] expect someone else?”
21 kwa wakati huo aliowaponya watu wengi kutoka katika magonjwa na mateso, kutoka kwa roho wachafu, na kwa watu wenye upofu aliwapa kuona.
At that very time Jesus was healing many people of their diseases and [other] sicknesses, he was [casting out] evil spirits, and he was causing many blind people to be able to see.
22 Yesu akajibu na kusema kwao. “Baada ya kuwa mmekwenda mlikotoka mtamjulisha Yohana mlichokiona na kukisikia. Wenye upofu wanapokea kuona na viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakasika, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa na kuwa hai tena, masikini wanaambiwa habari njema.
So he answered those two men, “Go back and report to John what you have seen [me doing] and what you have heard [me telling people. I am enabling] blind people to see. [I am enabling] lame people to walk. [I am] healing people who have leprosy. [I am enabling] deaf people to hear. [I am causing] dead people to become alive again, [and I am] telling [God’s] good message to poor people.
23 Na mtu ambaye hataacha kuniamini mimi kwa sababu ya matendo yangu amebarikiwa”.
[Also tell John that God] is pleased with those who do not stop believing in me [because what I do is not what they expect the Messiah to do].”
24 Baada ya wale waliotumwa na Yohana kurudi walikotoka, Yesu akaanza kusema kwa makutano juu ya Yohana, “Mlikwenda nje kuona nini, mwanzi ukiwa unatikiswa na upepo?
When the men whom John had sent left, Jesus began to talk to the crowd of people about John. He said to them, “[Think about] what sort of person you went to see in the desolate area [when you went there to see John] [RHQ]. [You did not go there to listen to a man who constantly changed the nature of his message] [MET], [like] a reed that is blown back and forth by the wind [RHQ].
25 lakini mlikwenda nje kuona nini, mtu aliyevaa vizuri? tazama watu wale wanaovaa mavazi ya kifalme na kuishi maisha ya starehe wako kwenye nafasi za wafalme.
Then what kind of man did you go there to see [RHQ]? Was he [RHQ] a man who wore expensive clothes? No! [You know very well that] people who wear beautiful clothes and live in luxury are in kings’ palaces, [not in the desolate areas]!
26 lakini mnakwenda nje kuona nini, Nabii? Ndiyo, ninasema kwenu na zaidi sana kuliko nabii.
Then what [kind of person] did you go to see? [Did you] [RHQ] [go there to see John because he was] a prophet? Yes! But I will tell you that [John is] more [important] than an [ordinary] prophet.
27 Huyu ndiye aliyeandikiwa, “Tazama, namtuma mjumbe wangu mbele ya macho yenu, atakeyeandaa njia kwa ajili yangu,
He is the one about whom [these words] that God said to the Messiah have been written {[the prophet Malachi] wrote [these words]} [in the Scriptures]: ‘Listen! I am going to send my messenger ahead of you [(sg)] [SYN]. He will prepare [people] for your coming.’
28 Nasema kwenu, kati ya wale waliozaliwa na mwanamke, hakuna mkuu kama Yohana, lakini mtu asiye muhimu sana atakayeishi na Mungu mahali alipo yeye, atakuwa mkuu kuliko Yohana.”
I tell you that from among all the people who have ever lived, [God considers that] no one is greater than John. However, [God considers] everyone who has let God rule their [lives] [MET] to be greater than [John], [even if they are] insignificant [people].”
29 Na watu wote waliposikia haya pamoja na watoza ushuru, walitangaza kuwa Mungu ni mwenye Haki. Walikuwepo kati yao wale waliobatizwa kwa ubatizo wa Yohana.
When they heard [what Jesus said] (OR, [what John preached]), all the people, including tax collectors, [whom many people despised], agreed that God’s way was right. By being baptized by John {By [letting] John baptize them}, [they had agreed that what God required people to do in order to be saved was right].
30 Lakini mafarisayo na wataalamu wa sheria za kiyahudi, ambao hawakubatizwa na yeye walikataa hekima za Mungu kwa ajili yao wenyewe.
But the Pharisees and the men who taught the [Jewish] laws were not baptized by John {did not [let] John baptize them} because they rejected what God wanted them to do.
31 Tena naweza kuwalinganisha na nini watu wa kizazi hiki? Wakoje hasai?
[Then Jesus also said], “[Many of] you people have heard what [John and I] have taught. (I will illustrate what you are like./Do you know what [many of] you people who have heard what [John and I] have taught are like?) [RHQ]
32 Wanafanana na watoto wanaocheza kwenye eneo la soko, wanaokaa na kuitana mmoja baada wa mwingine wakisema, 'Tumepuliza filimbi kwa ajili yenu, na hamkucheza. tumeomboleza na hamkulia.'
You are like children who are [playing games] in an open area. [Some of them] are calling to [the others], saying, ‘We [(exc)] played happy music for you on the flute, but you did not dance! Then we sang sad funeral songs for you, but you did not cry!’
33 Yohana mbatizaji alikuja hakula mkate wala hakunywa divai, na mkasema “Ana pepo.
[Similarly, you people are dissatisfied with both John the Baptizer and me]! When John came and [preached to you], he did not eat [ordinary] food [SYN] or drink wine, [like most people do]. But you [rejected him], saying, ‘A demon is controlling him!’
34 Mwana wa Mtu amekuja amekula na kunywa na mkasema, “Angali ni mlafi na mlevi, rafiki wa watoza ushuru na wenye dhambi!
In [contrast], [I], the one who came from heaven, eat [the same food] and drink [wine as others do]. But you [reject me], saying, ‘Look! [This man] eats too much food and drinks too much wine, and he associates with tax collectors and [other] sinners!’
35 Lakini hekima imetambulika kuwa ina haki kwa watoto wake wote.”
But those who are [truly God’s] children [PRS] realize that [what John and I do is truly] wise.”
36 Mmoja wa mafarisayo alimwomba Yesu aende kula pamoja naye. Baada ya Yesu kuingia kwenye nyumba ya farisayo, aliegemea kwenye meza ili ale.
[One day] one of the Pharisees [named Simon] invited Jesus to eat a meal with him. So Jesus went to the man’s house and reclined [to eat].
37 Tazama kulikuwa na mwanamke mmoja katika jiji hilo aliyekuwa na dhambi. Akagundua kuwa alikuwa amekaa kwa Farisayo, akaleta chupa ya manukato.
There was a woman in that city [who many people knew had been] a prostitute [EUP]. She heard that Jesus was eating in the Pharisee’s house. So she went there, taking a stone jar that contained perfume.
38 Alisimama nyuma yake karibu na miguu yake huku akilia. Tena alianza kulowanisha miguu yake kwa machozi, na kuifuta kwa nywele za kichwa chake, akiibusu miguu yake na kuipaka manukato.
[As the people there were reclining to eat], the woman stood behind [Jesus, at his] feet. As she was crying [because she was sorry for her sins, her tears fell on Jesus’ feet]. Then she wiped his feet with her hair, and kissed his feet, and anointed them with the perfume.
39 Na yule farisayo aliyekuwa amemwalika Yesu alipoona hivyo, akawaza mwenyewe akisema, “Kama huyu mtu angekuwa nabii, angejua huyu ni nani na ni aina gani ya mwanamke anayemgusa, ya kuwa ni mwenye dhambi.
When the Pharisee who had invited [Jesus] saw that, he thought, “[Prophets know about other people’s lives], [so] if Jesus were a prophet, he would have known who this woman is who is touching him, and what kind of a person she is. He would have known that she is a prostitute! [EUP]”
40 Yesu akajibu na kumwambia, “Simoni nina kitu cha kukuambia. “Akasema” “Kiseme tu mwalimu!”
Jesus said to him, “Simon, there is something I want to tell you [(sg)].” He replied, “Teacher, what is it?”
41 Yesu akasema “Kulikuwa na wadaiwa wawili kwa mkopeshaji mmoja. Mmoja alikuwa anadaiwa dinari mia tano na wa pili alidaiwa dinari hamsini.
Jesus replied, “Two people owed some money to a man who [earned money by] lending [it to others]. One owed him 500 silver coins, and the other owed him 50 silver coins.
42 Na walipokuwa hawana pesa ya kumlipa aliwasamehe wote. Sasa ni nani atampenda zaidi?
Neither of them was able to pay back [what he owed], so the man [very kindly] said that they did not have to pay back anything. So, which of those two men will love that man more?”
43 Simoni akamjibu na kusema, “Nadhani aliyesamehewa zaidi.”Yesu akamwambia, “Umehukumu kwa usahihi.”
Simon replied, “I think that the one who owed the most money and did not have to pay it back [will love him more].” Jesus said to him, “That is correct.”
44 Yesu akamgeukia mwanamke na kusema kwa Simoni, “Unamwona huyu mwanamke. Nimeingia kwenye Nyumba yako. Hukunipa maji kwa ajili ya miguu yangu, lakini huyu, kwa machozi yake, alilowanisha miguu yangu na kuifuta kwa nywele zake.
Then he turned toward the woman, and said to Simon, “(Think about [what] this woman [has done]!/Do you [(sg)] see [what] this woman [has done]?) [RHQ] When I entered your house, you [did not follow our custom of welcoming guests by] giving me any water [to wash] my feet, but this woman has wet my feet with her tears and then wiped them with her hair!
45 Hukunibusu, lakini yeye, tangu alipoingia humu hakuacha kunibusu miguu yangu.
You did not [follow our custom of greeting by] kissing me, but since I came in, this woman has not stopped kissing my feet!
46 Hukuipaka miguu yangu kwa mafuta, lakini ameipaka miguu yangu kwa manukato.
You did not [follow our custom of welcoming guests by] anointing my head with [olive] oil, but she has anointed my feet with fragrant perfume.
47 Kwa jambo hili, nakwambia kwamba alikuwa na dhambi nyingi na amesamehewa zaidi, na pia alipenda zaidi. Lakini aliyesamehewa kidogo, hupenda kidogo tu.”
So I will tell you that even though this woman has sinned very much, she has been forgiven {[I] have forgiven her}. [By what she has done she has shown that] she loves [me] very much. But a person who has [sinned] just a little bit, but whom [I] have forgiven, will love [me just a little bit].”
48 Baadaye akamwambia mwanamke, “Dhambi zako zimesamehewa”
Then he said to the woman, “You have been forgiven {[I have] forgiven [you]} [for] your sins.”
49 Wale waliokaa mezani pamoja naye wakaanza kusemezana wao kwa wao, “Huyu ni nani mpaka anasamehe dhambi?”
Then those who were eating with him said among themselves, “(This man must [think that he is God]!/Who does this man [think that he] is [RHQ]), saying that he can forgive [people for] their sins?”
50 Na Yesu akamwambia mwanamke, “Imani yako imekuokoa. Enenda kwa amani”
But Jesus said to the woman, “Because you have trusted [PRS] [in me, God] has saved you [from the guilt of your sins]. May [God] give you inner peace as you go!”