< Luka 6 >

1 Sasa ilitokea kwenye Sabato kwamba Yesu alikuwa akipita katika ya shamba la nafaka na wanafunzi wake walikuwa wakichuma masuke, wakayasuguasugua kati ya mikono yao wakala nafaka.
One (Sabbath/Jewish day of rest), while Jesus was walking through some grain fields with his disciples, the disciples picked some of the heads of grain. They rubbed them in their hands [to separate the grains from the husks], and ate the grain. [The law of Moses permitted people to do that if they were hungry].
2 Lakini baadhi ya Mafarisayo wakasema, “Kwa nini mnafanya kitu ambacho si halali kisheria kukifanya siku ya sabato”?
Some Pharisees [who were watching] said to Jesus, “(You should not be doing on our rest day [work] that [our] laws forbid!/Why are you doing on our rest day [work] that our laws forbid?)” [RHQ]
3 Yesu, akawajibu, akisema, “Hamkuwahi kusoma kile Daudi alifanya alipokuwa na njaa, yeye na wanaume waliokuwa pamoja naye?
[Jesus wanted to show them that the record in Scriptures indicated that God permitted people to disobey certain religious laws when they needed food]. [So] he replied, “[It is written in the Scriptures] what [our revered ancestor, King] David did when he and the men with him were hungry. You have read about that, ([but you do not think about what it implies/so why do you not think about what it implies]?) [RHQ]
4 Alikwenda katika nyumba ya Mungu, na akachukuwa mikate mitakatifu na kuila baadhi, na kuitoa baadhi kwa watu aliokuwa nao kuila, hatakama ilikuwa halali kwa makuhani kuila.”
David entered God’s big worship tent [and asked for some food]. [The high priest gave him] the bread that the priests had presented to God. It was permitted [in] one of [Moses’ laws] that only the priests could eat that bread. But [even though David was not a priest], he ate some, and gave some to the men who were with him. [And God did not consider that what David did was wrong]!”
5 Kisha akawaambia, “Mwana wa Adamu ni Bwana wa Sabato.”
Jesus also said to them, “[I am] the one who came from heaven, so [I] have the authority [to determine what is right for my disciples to do on] the day of rest!”
6 Ilitokea katika Sabato nyingine kwamba alikwenda ndani ya sinagogi na kuwafundisha watu huko. Palikuwa na mtu ambaye mkono wake wa kulia ulikuwa umepooza.
Another (Sabbath/Jewish day of rest) Jesus entered a (synagogue/Jewish meeting place) and taught the people. There was a man there whose right hand was shriveled.
7 Waandishi na Mafarisayo walikuwa wanamwangalia kwa makini kuona kama angemponya mtu siku ya Sabato, ili waweze kupata sababu ya kumshtaki kwa kufanya kosa.
The men who taught the [Jewish] laws and the Pharisees [who were there] watched Jesus, to see if he would heal the man (on the Sabbath/on the Jewish rest day). They did this so that, [if he healed the man], they would accuse him [of disobeying their laws by working on the day of rest].
8 Lakini alijua nini walikuwa wanafikiri na akasema kwa mtu aliyekuwa amepooza mkono, “Amka, simama hapa katikati ya kila mmoja.” Hivyo huyo mtu akanyanyuka na kusimama pale.
But Jesus knew what they were thinking. So he said to the man with the shriveled hand, “Come and stand here [in front of everyone]!” So the man got up and stood there.
9 Yesu akasema kwao, “Nawauliza ninyi, ni halali siku ya Sabato kufanya mema au kufanya madhara, kuokoa maisha au kuyaharibu?” Kisha aliwaangalia wote na kumwambia yule mtu,
Then Jesus said to the others, “I ask you this: Do the laws that [God gave Moses] permit [people] to do what is good (on the Sabbath/on the Jewish rest day), or [do they permit people] to harm [others]? [Do they permit us] to save [a person’s] life [on our day of rest] or to let [him] die [HYP] [by refusing to help him]?”
10 “Nyoosha mkono wako.” Akafanya hivyo, na mkono wake ulikuwa umeponywa.
[They refused to answer him. So] after he looked around at them all, he said to the man, “Stretch out your [shriveled] hand!” The man did that, and his hand became all right again!
11 Lakini walijawa na hasira, wakaongeleshana wao kwa wao kuhusu nini wanapaswa wafanye kwa Yesu.
But the men who taught the Jewish laws and the Pharisees were very angry, and they discussed with one another what they could do to [get rid of] Jesus.
12 Ilitokea siku hizo kwamba alikwenda mlimani kuomba. Aliendelea usiku mzima kumuomba Mungu.
About that time [Jesus] went up into the hills to pray. He prayed to God all night.
13 Ilipokuwa asubuhi, aliwaita wanafunzi wake kwake, na akawachagua kumi na wawili kati yao, ambao pia aliwaita “mitume.”
The next day he summoned all his disciples to come near him. From them he chose twelve men, whom he called apostles.
14 Majina ya wale mitume yalikuwa Simoni (ambaye pia alimwita Petro) na Andrea ndugu yake, Yakobo, Yohana, Filipo, Bartolomayo,
They were Simon, to whom he gave the [new] name, Peter; Andrew, Peter’s [younger] brother; James and [his younger brother], John; Philip; Bartholomew;
15 Mathayo, Tomaso na Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni, ambaye aliitwa Zelote,
Matthew, whose other name was Levi; Thomas; [another] James, the [son] of Alpheus; Simon, who belonged to the party [that encouraged people to] rebel [against the Roman government];
16 Yuda mwana Yakobo na Yuda Iskariote, ambaye alikuwa msaliti msaliti.
Judas, the [son] of [another] James; and Judas Iscariot (OR, Judas, the man from Kerioth [Town]), the one who later (betrayed Jesus./enabled the Jewish leaders to seize Jesus.)
17 Kisha Yesu alitelemka pamoja nao toka mlimani na kusimama mahali tambarare. Idadi kubwa ya wanafunzi wake walikuwa huko, pamoja na idadi kubwa ya watu kutoka Uyahudi na Yerusalemu, na kutoka pwani ya Tiro na Sidoni.
[Jesus] came down from the hills with his disciples and stood on a level area. There was a very big crowd of his disciples there. There was also a large group of people who had come from Jerusalem and from many [other] places [in] Judea [district], and from the coastal areas near Tyre and Sidon [cities].
18 Walikuja kumsikiliza na kuponywa magonjwa yao. Watu waliokuwa wakisumbuliwa na pepo wachafu waliponywa pia.
They came to hear Jesus talk to them and to be healed {and for him to heal them} from their diseases. He also healed those whom evil spirits had troubled.
19 Kila mmoja kwenye hilo kusanyiko alijaribu kumgusa kwa sababu nguvu za uponyaji zilikuwa zikitokea ndani yake, na aliwaponya wote.
Everyone [in the crowd] tried to touch him, because he was healing everyone by [his/God’s] power.
20 Kisha akawaangalia wanafunzi wake, na kusema, “Mmebarikiwa ninyi mlio maskini, kwa maana ufalme wa Mungu ni wenu.
He looked [MTY] at his disciples and said, “[God] is pleased with you [who know] that you lack what [he wants you to have; ] he will allow you to be the people whose lives he rules over.
21 Mmebarikiwa ninyi mlio na njaa sasa, kwa maana mtashibishwa. Mmebarikiwa ninyi mliao sasa, kwa maana mtacheka.
[God] is pleased with you who sincerely desire to receive what [MTY] [he wants you to have]; he will give you what you need, until you are satisfied. [God] is pleased with you that grieve now [because of sin]. Later you will be joyful.
22 Mmebarikiwa ninyi ambao watu watakapowachukia na kuwatenga na kuwashutumu ninyi kwamba ni waovu, kwa ajili ya Mwana Adamu.
[God] is pleased with you when [other] people hate you, when they will not let you join them, when they insult you, when they say that you are evil because [you believe in] me, the one who came from heaven.
23 Furahini katika siku hiyo na kurukaruka kwa furaha, kwa sababu hakika mtakuwa na thawabu kubwa mbinguni, kwa maana baba zao waliwatendea vivyohivyo manabii.
When that happens, rejoice! Jump up and down because you are so happy! [God will give] you a great reward in heaven! [When they do these things to you, it will prove that you are God’s servants]. (OR, [People have always treated God’s servants like that].) Do not forget that these people’s ancestors did the same things to the prophets [who served God faithfully]!
24 Lakini ole wenu mlio matajiri! Kwa maana mmekwisha pata faraja yenu.
But there will be terrible punishment for you that are rich; the happiness you have received [from your riches] is the only happiness that you will get.
25 Ole wenu mlio shiba sasa! Kwa maana mtaona njaa baadaye. Ole wenu mnaocheka sasa! Kwa maana mtaomboleza na kulia baadaye.
There will be terrible punishment for you who [think that you] have all that you need now; you will [realize] that these things will not make you feel satisfied. There will be terrible punishment for you who are joyful now; you will [later] be very sad.
26 Ole wenu, mtakaposifiwa na watu wote! Kwa maana baba zao waliwatendea manabii wa uongo vivyohivyo.
When most [HYP] people speak well about you, trouble is ahead for you; [it will not prove that you are God’s servants, because] your ancestors used to speak well about those who falsely [claimed that they were] prophets.”
27 Lakini nasema kwenu ninyi mnaonisikiliza, wapendeni adui zenu na kufanya mema kwa wanao wachukieni.
“But I say this to each of you [disciples] who are listening [to what I say]: Love your enemies [as well as your friends]. Do good things for those who hate you!
28 Wabarikini wale wanao walaani ninyi na waombeeni wale wanaowaonea.
[Ask God to] bless those who curse you! Pray for those who mistreat you!
29 Kwake yeye akupigaye shavu moja, mgeuzie na la pili. Kama mtu akikunyang'anya joho lako usimzuilie na kanzu.
If someone [insults one of you by] striking you on one of your cheeks, turn your face [so that he can strike] the other cheek [also]. If [a bandit] wants to take away your [(sg)] coat, let him also have your shirt.
30 Mpe kila akuombaye. Kama mtu akikunyang'anya kitu ambacho ni mali yako, usimuombe akurudishie.
Give something to everyone who asks you [(sg) for something]. If someone takes away things that belong to you [(sg)], do not ask him to return them.
31 Kama mpendavyo watu wawatendee, nanyi watendeeni vivyo hivyo.
In whatever way you [(pl)] want others to act toward you, that is the way that you should act toward them.
32 Kama mkiwapenda watu wawapendao ninyi tu, hiyo ni thawabu gani kwenu? Kwamaana hata wenye dhambi huwapenda wale wawapendao.
If you love [only] those who love you, do not [expect God] to praise you for [doing that] [RHQ], [because] even sinners love those who love them.
33 Kama mkiwatendea mema wale wanaowatendea ninyi mema, hiyo ni thawabu gani kwenu? Kwa maana hata wenye dhambi hufanya vivyo hivyo.
If you do good things [only] for those who do good things for you, do not [expect God] to reward you [for doing that] [RHQ], [because] even sinners do that.
34 Kama mkikopesha vitu kwa watu ambao mnategemea watawarudishia, hiyo ni thawabu gani kwenu? Hata wenye dhambi huwakopesha wenye dhambi, na hutegemea kupokea kiasi hicho hicho tena.
If you lend [things or money only] to those who you expect will give something back to you, do not [expect that God] will reward you [RHQ] [for doing that]. Even sinners lend to other sinners, because they expect them to pay everything back.
35 Lakini wapendeni adui zenu na watendeeni mema. Wakopesheni na msihofu kuhusu kurudishiwa, na thawabu yenu itakuwa kubwa. Mtakuwa wana wa Aliye Juu, kwasababu yeye mwenyewe ni mwema kwa watu wasio na shukurani na waovu.
Instead, love your enemies! Do good things for them! Lend to them, and do not expect them to pay anything back! [If you do that, God will give] you a big reward. And you will be [acting like] his children [should]. Remember that God is kind to people who are not grateful and to people who are wicked, [and he expects you to be like that too].
36 Iweni na huruma, kama Baba yenu alivyo na huruma.
Act mercifully toward others, just like your Father [in heaven acts] mercifully [toward you].”
37 Msihukumu, nanyi hamta hukumiwa. Msilaani, nanyi hamtalaaniwa. Sameheni wengine, nanyi mtasamehewa.
“Do not say how sinfully others have acted, and then [God] will not say how sinfully you have acted. Do not condemn others, and then [he] will not condemn you [DOU]. Forgive others [for the evil things that they have done to you], and then [God] will forgive you.
38 Wapeni wengine, nanyi mtapewa. Kiasi cha ukarimu - kilichoshindiliwa, kusukwasukwa na kumwagika - kitamwagika magotini penu. Kwa sababu kwa kipimo chochote mnachotumia kupimia, kipimo hicho hicho kitatumika kuwapimia ninyi.”
Give [good things to others], and then [God] will give [good] things to you. It will be [as though] [MET] [God is putting things in a basket] for you. He will give you a full amount, pressed down in the basket, which he will shake [so that he can put more in], and it will spill over the sides! [Remember that] the way you act [toward others] will be the way that [God] will act toward you!”
39 Kisha akawaambia mfano pia. “Je mtu aliye kipofu aweza kumwongoza mtu mwingine kipofu? Kama alifanya hivyo, basi wote wangalitumbukia shimoni, je wasingetumbukia?
He also told [his disciples] this parable [to show them that they should be like him, and not be like the Jewish religious leaders]: “(You certainly would not [expect] a blind man to lead another blind man./Would you [expect] a blind man to lead [another] blind man?) [RHQ] If he tried to do [that], (they would both probably fall into a hole!/wouldn’t they both probably fall into a hole?) [RHQ] [I am your teacher, and you disciples should be like me].
40 Mwanafunzi hawi mkubwa kuliko mwalimu wake, lakini kila mtu akiisha kufundishwa kwa ukamilifu atakuwa kama mwalimu wake.
A disciple should not [expect to be] better known than his teacher. But if a student is fully trained {if someone fully trains a student}, the student can become like his teacher [MET]. [So you should be content to be like me].
41 Na kwa nini basi wakitazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, na boriti lililo ndani ya jicho lako huliangalii?
(Why do you notice [someone else’s small faults]?/None of you should be concerned about [someone else’s small faults] [MET, RHQ].) [That would be like] noticing a speck in that person’s eye. But you should be concerned about [your own big faults. They are like] planks in your own eye, [which you do not notice].
42 Utawezaje kumwambia ndugu yako, 'Ndugu, naomba nikitoe kibanzi kilicho ndani ya jicho lako,' nawe huangalii boriti iliyo katika jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe! Kwanza itoe boriti katika jicho lako mwenyewe, ndipo utaona vizuri kutoa kibanzi katika jicho la ndugu yako.
(You [(sg)] should not say, ‘Friend, let me take out that speck in your eye!’ when you do not notice the log in your own eye!/Why do you say, ‘Friend, let me take out that speck in your eye!’ when you do not notice the log in your own eye?) [RHQ] [If you do that], you are a hypocrite! You should first [stop committing your own sins. That will be like] removing the plank from your own eye. Then, as a result, you will have the spiritual insight you need to help others get rid of the [faults that are like] specks in their eyes.”
43 Kwa sababu hakuna mti mzuri uzaao matunda mabaya, wala hakuna mti mbaya uzaao matunda mazuri.
“[People are like trees] [MET]. Healthy trees do not bear bad fruit (OR, bear only good fruit), and unhealthy trees do not bear good fruit.
44 Kwa sababu kila mti hutambulika kwa matunda yake. Kwa sababu watu hawachumi tini kutoka kwenye miba, wala hawachumi zabibu kutoka kwenye michongoma.
[Just like you] can tell if a tree is good or bad by looking at its fruit, [you can tell which people are good and which are bad by looking at the way they] conduct their lives. [For example, because thornbushes cannot produce figs], no one can pick figs from thornbushes. And [since bramble bushes cannot produce grapes], no one can [pick] grapes from bramble bushes.
45 Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema, na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoa yaliyo maovu. Kwa sababu kinywa chake husema yale yaujazayo moyo wake.
[Similarly], good people will conduct their lives in a good way because they think a lot of good [things], and evil people will live in an evil way because they think a lot of evil [things]. The basic principle is that people speak [and act] according to all that they think.”
46 Kwanini mnaniita, 'Bwana, Bwana', na bado hamyatendi yale nisemayo?
“[Because people should obey what their masters tell them], (it is disgraceful that you say that I am your master but you do not do what I tell you!/why do you say that I am your master but you do not do what I tell you?) [RHQ]
47 Kila mtu ajaye kwangu na kuyasikia maneno yangu na kuyatendea kazi, nitawaonyesha jinsi alivyo.
Some people come to me, and hear my messages and obey them. I will tell you what they are like.
48 Anafanana na mtu ajengae nyumba yake, ambaye huchimba chini sana, na kujenga msingi wa nyumba juu ya mwamba imara. Mafuriko yalipokuja, maporomoko ya maji yaliipiga nyumba, lakini hayakuweza kuitikisa, kwa sababu ilikuwa imejengwa vizuri.
They are like a man who dug deep [into the ground to prepare to build his house]. He made sure that the foundation was on solid ground. Then when there was a flood, the water tried to wash away the house. But the river could not shake the house, because it was built {he built it} on a solid [foundation].
49 Lakini yeyote asikiaye neno langu na hakulitii; mfano wake ni mtu aliyejenga nyumba juu ya ardhi pasipokuwa na msingi, mto ulipoishukia kwa nguvu, nyumba ile ilitopata maangamizi makubwa.
But some people hear my messages but do not obey them. They are like a man who built a house on top of the ground without [digging] a foundation. When the river flooded, the house collapsed immediately and was completely ruined. [So it is important for you to obey what I teach you].”

< Luka 6 >