< Mambo ya Walawi 8 >
1 Yahweh akazungumza na Musa, akisema,
Gospod je spregovoril Mojzesu, rekoč:
2 “Walete Aroni na wanawe pamoja naye, mavazi na mafuta ya upako, fahali kwa ajili ya sadaka ya dhambi, kondoo dume wawili, na kikapu cha mkate usio na hamira.
»Vzemi Arona in z njim njegove sinove, obleke, mazilno olje, bikca za daritev za greh, dva ovna in košaro nekvašenega kruha,
3 Ita kusanyiko lote kwenye ingilio la hema la kukutania.”
in zberi skupaj ves zbor k vratom šotorskega svetišča skupnosti.«
4 Kwa hiyo Musa akafanya kama Yahweh alivyomwamru, nalo kusanyiko lilikuja pamoja mbele ya ingilio la hema la kukutania. Kisha Musa akaliambia kusanyiko,
Mojzes je storil, kakor mu je Gospod zapovedal in zbor je bil zbran skupaj k vratom šotorskega svetišča skupnosti.
5 “Hivi ndivyo alivyotuamru Yahweh tutende.”
Mojzes je rekel skupnosti: »To je stvar, ki jo je Gospod zapovedal, da se stori.«
6 Musa akamleta Aroni na wanawe na kuwaosha kwa maji.
Mojzes je privedel Arona in njegove sinove ter jih umil z vodo.
7 Akamvika Aroni kanzu ya ndani yenye urefu wa kufika magotini na kumfunga ukumbuu kiunoni mwake, akamvika joho la nje lenye mikono mirefu na kumvika kile kizibao chenye vipande viwili tumboni na mgongoni na kukifunga kuzunguka kiunoni mwake kwa mshipi uliosokotwa kwa ustadi na kukikaza mwilini mwake.
Nadel mu je plašč, ga opasal s pasom, ga ogrnil s svečanim oblačilom, nanj položil efód in ga opasal s skrbno narejenim pasom efóda in ga s tem prevezal.
8 Kisha Musa akaweka kifuko kifuani mwa Aroni, na ndani ya kifuko hicho akaweka Urimu na Thumimu.
Nanj je dal naprsnik. V naprsnik je položil tudi Urím in Tumím.
9 Na kisha akamfunga kiremba kichwani, na juu ya kiremba kwa mbele, akaweka bamba la dhahabu; liwe taji takatifu, kama Yahweh alivyomwamru yeye.
Turban je položil na njegovo glavo; tudi na turban, torej na njegov sprednji del, je položil zlato ploščico, sveto krono; kakor je Gospod zapovedal Mojzesu.
10 Musa akayatwaa hayo mafuta ya upako, akalipaka lile hema la kukutania na kila kitu kilichokuwamo ndani yake na kuvitenga kwa ajili ya Yahweh.
Mojzes je vzel mazilno olje in mazilil šotorsko svetišče in vse, kar je bilo v njem in to posvetil.
11 Akayanyunyiza hayo mafuta juu ya madhabahu mara saba, na kisha akaipaka mafuta hiyo madhabahu na vyombo vyake vyote, na sinia la kunawia na kitako chake ili kuvitenga wa ajili ya Yahweh.
Od tega je sedemkrat poškropil po oltarju in mazilil oltar ter vse njegove posode, tako [okrogel] umivalnik kot njegovo vznožje, da jih posvéti.
12 Akamimina sehemu ya mafuta ya upako juu ya kichwa cha Aroni na kisha akampaka mafuta ili kumtenga.
Na Aronovo glavo je izlil mazilno olje in ga mazilil, da ga posvéti.
13 Musa akawaleta wana wa Aroni na kuwavika kila mmoja kanzu ya ndani yenye urefu wa kufika magotini. Kila mmoja wao akamfunga kwa ukumbuu kiunoni mwake na kuwafunga vitambaa vya kitani kichwani pao, kama vile Yahweh alivyokuwa amemru Musa.
Mojzes je privedel Aronove sinove, nanje položil plašče, jih opasal s pasovi in nanje položil klobučke; kakor je Gospod zapovedal Mojzesu.
14 Musa akamleta huyo fahali kwa ajili ya sadaka ya dhambi, naye Aroni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha fahali ambaye wamemelete kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
Privedel je bikca za daritev za greh. Aron in njegovi sinovi so svoje roke položili na glavo bikca daritve za greh.
15 Musa akamchinja, na kisha akachukua sehemu ya damu yake kwa kidole chake na kuiweka juu ya mpembe za madhabahu, akaitakasa hiyo madhabahu, na kuitenga kwa Mungu, ambapo kwa kufanya hivyo, aliisababisha madhabahu kuwa sehemu ya kufaa kwa kufanyia upatanisho.
Zaklal ga je in Mojzes je vzel kri in jo s svojim prstom dal vsenaokrog na rogove oltarja in očistil oltar in kri izlil ob vznožju oltarja in ga posvetil, da bi na njem opravil pobotanje.
16 Akachukua mafuta yote yaliyokuwa sehemu za ndani, kile kiwambo cha ini, zile figo mbili pamoja na mafuta yake, Musa akaichoma hiyo nyama yote juu ya madhabahu.
Vzel je vso tolščo, ki je bila na drobovju, opno nad jetri, dve ledvici, njuno tolščo in Mojzes je to sežgal na oltarju.
17 Lakini yule fahali, ngozi yake, nyama yake na kinyesi chake, akavichoma nje ya kambi, kama vile Yehweh alivyokuwa amemwamru yeye.
Toda bikca, njegovo kožo, njegovo meso in njegov iztrebek je z ognjem sežgal zunaj tabora; kakor je Gospod zapovedal Mojzesu.
18 Musa akamleta yule konndoo dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, naye Aroni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha huyo kondoo.
In privedel je ovna za žgalno daritev, Aron in njegovi sinovi pa so svoje roke položili ovnu na glavo.
19 Musa akamchinja kondoo na kuinyunyizia damu yake kila upande wa madhabahu.
Zaklal ga je in Mojzes je kri poškropil naokoli po oltarju.
20 Naye akamkatakata kondoo vipande vipande na akakiteketeza kichwa chake pamoja na vile vipande na mafuta.
Ovna je razrezal na koščke in Mojzes je sežgal glavo, koščke in tolščo.
21 Akaziosha kwa maji zile sehemu za ndani pamoja na miguu na akamteketeza kandoo mzima juu ya madhabahu. Ilikuwa ni dhabihu ya kuteketezwa na ilitoa harufu ya kupendeza, sadaka iliyofanywa kwa Yahweh kwa moto kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamru Musa.
Drobovje in noge je opral v vodi in Mojzes je celotnega ovna sežgal na oltarju. To je bila žgalna daritev v prijeten vonj in ognjena daritev Gospodu; kakor je Gospod zapovedal Mojzesu.
22 Kisha Musa akamleta yule kondoo dume mwingine, kondoo wa kuwekwa wakfu, naye Aroni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa cha kondoo.
Privedel je drugega ovna, ovna uméstitve, Aron in njegovi sinovi pa so svoje roke položili ovnu na glavo.
23 Aroni akamchinja, naye Musa akachukua sehemu ya damu na kuiweka kwenye ncha ya sikio la Aroni la kulia, juu ya dole gumba la mkono wake wa kulia, na kwenye kidole kikumbwa cha mguu wake wa kulia.
In on ga je zaklal. Mojzes je vzel od njegove krvi, jo pomazal na konico Aronovega desnega ušesa, na palec njegove desne roke in na palec njegovega desnega stopala.
24 Akawaleta wana wa Aroni, naye akaweka sehemu ya damu ya kondoo yule kwenye ncha ya sikio lao la kulia, kwenye dole gumba lao cha mkono wa kulia na kwenye kidole chao kikubwa cha mguu wa kulia. Kisha Musa akainyunyiza damu ya huyo kila upande wa madhabahu
Privedel je Aronove sinove in Mojzes je dal od krvi na konico njihovih desnih ušes in na palce njihovih desnih rok in na palce njihovih desnih stopal; in Mojzes je kri poškropil naokoli po oltarju.
25 Naye akayatwaa yale mafuta, mafuta ya mkiani, mafuta liyolikuwa sehemu za ndani, na mafuta yafunikayo ini, zile figo mbili pamoja na mafuta yake na paja la kulia.
Vzel je tolščo, tolsti rep, vso tolščo, ki je bila na drobovju, opno nad jetri, dve ledvici in njuno tolščo ter desno pleče.
26 Akachukua mkate mmoja kutoka kwenye kikapu cha mikate isiyo na hamira ambayoo ilikuwa mbele za Yahweh, akatwaa mkate moja usio na hamira, na mkate mmoja ulioandaliwa kwa mafuta, na mkate mwemba wa kaki na akaiweka juu ya mafuta na juu ya paja la kulia la kondoo.
Iz košare nekvašenega kruha, ki je bila pred Gospodom, je vzel en nekvašen kolač, kolač oljnatega kruha in en vafelj ter jih položil na tolščo in na desno pleče.
27 Akaiweka yote mikoni mwa Aroni na katika mikono ya wanawe na kuitikisa mbele za Yahweh kuwa sadaka ya kutikiswa
Vse to je dal na Aronove roke in na roke Aronovih sinov in jih majal za majalno daritev pred Gospodom.
28 Kisha Musa akaichukua mikate hiyo kutoka mikononi mwao na kuiteketeza juu ya madhabahu kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. Zilikuwa ni sadaka ya kuwekwa wakfu na ilitoa harufu ya kupendeza. Ilikuwa sadaka iliyofanywa kwa Yahweh kwa moto.
Mojzes jih je vzel iz njihovih rok in jih sežgal na oltarju nad žgalno daritvijo. To so bile uméstitvene [daritve] za prijeten vonj. To je ognjena daritev Gospodu.
29 Musa akakichukua kidari na kukitikisa kuwa sadaka ya kutikiswa kwa Yahweh. Ilikuwa ni mgao wa Musa wa kondoo wa kuwekewa mikono kwa makuhani, Kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru yeye.
Mojzes je vzel prsi in jih majal za majalno daritev pred Gospodom, kajti od ovna uméstitve je bil to Mojzesov delež; kakor je Gospod zapovedal Mojzesu.
30 Musa akatwaa sehemu ya mafuta ya upako na damu iliyokuwa juu ya madhabahu; naye akayanyunyiza haya juu ya nguo za Aroni, juu ya nguo zake mwenyewe na juu ya nguo za wana wa Aruni waliokua pamoja naye. Kwa njia hii alimtenga Aroni na nguo zake, na wanawe na nguo zao kwa ajili ya Yahweh.
Mojzes je vzel od mazilnega olja in od krvi, ki je bila na oltarju in to poškropil na Arona, na njegove obleke, na njegove sinove in na obleke njegovih sinov z njim; in posvetil je Arona, njegove obleke, njegove sinove in obleke njegovih sinov z njim.
31 Kwa hiyo Musa akawambia Aruni na wanawe, “Ipikeni nyama mbele ya ingilio la hema la kukutania, na hapo mtaila pamoja na mkate ulio kwenye kikapu cha kuwekwa wakfu, kama ilivyoamriwa, kusema, 'Aroni na wanawe wataila.'
Mojzes je rekel Aronu in njegovim sinovim: »Meso skuhajte pri vratih šotorskega svetišča skupnosti. Tam ga pojejte s kruhom, ki je v košari uméstitvenih [daritev], kakor sem zapovedal, govoreč: ›Aron in njegovi sinovi bodo to jedli.‹
32 Masalio yoyote ya nyama na mikate utayateketeza kwa moto.
To, kar pa ostane od mesa in od kruha, boste sežgali z ognjem.
33 Na hamtatoka kwenye ingilio la hema la kukutania kwa muda wa siku saba, hata zitakapotimia siku za kuwekwa mikono kwenu. Kwa kuwa kwa muda wa siku saba, Yahweh atawaweka wakfu.
Sedem dni ne boste šli od vrat šotorskega svetišča skupnosti, dokler dnevi vaše uméstitve ne bodo končani, kajti sedem dni vas bo uméščal.
34 Kilichotendeka siku hii— Yahweh ndiye amekiamru kitendekeke ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
Kakor je storil ta dan, tako je Gospod zapovedal storiti, da za vas opravi spravo.
35 Mtakaa kwenye ingilio la hema la kukutania mchana na usiku siku saba, nanyi ishikeni amri ya Yahweh ili msije mkafa, kwa sababu hivi ndivyo ilivyoamriwa.
Zato boste sedem dni, dan in noč, ostajali pri vratih šotorskega svetišča skupnosti in se boste držali Gospodovega naročila, da ne umrete, kajti tako mi je bilo zapovedano.«
36 Kwa hiyo Aroni na wanawe wakafanya mambo yote ambayo Yahweh alikuwa amewaamru kwa kinywa cha Musa.
Tako so Aron in njegovi sinovi storili vse stvari, ki jih je Gospod zapovedal po Mojzesovi roki.