< Mambo ya Walawi 13 >

1 Yahweh akazungumza na Musa na Aroni, akasema,
Yahweh said this to Aaron and Moses/me:
2 Mtu yeyote anayeonekana na uvimbe au pele au doa ling'aalo juu ya ngozi ya mwili wake, na likawa limeambukizwa ugonjwa wa ngozi mwilini mwake, ni lazima aletwe kwa Aroni kuhani mkuu au kwa mmoja wa wanawe makuhani.
“When someone has on his skin a swelling or a rash or a shiny/bright spot that may become (contagious/a dreaded skin disease), he must be brought to Aaron or to one of his sons who are also priests.
3 Naye kuhanai atachunguza ugonjwa huo kwenye ngozi ya mwili wake. Iwapo malaika zilizopo eneo lenye ugonjwa zimegeuka kuwa nyeupe, na iwapo ugonjwa umejitokeza juu ya ngozi, huo ni ugonjwa wa kuambukiza. Baada cha kuhani kumchunguza, atamtangaza kuwa ni najisi.
The priest must examine that part of the person’s skin. If the hair in that area has become white and it appears that the sore is deeper than just on the skin, it is a contagious skin disease. When the priest sees that, he must declare that the person must stay away from other people [MTY].
4 Iwapo lile doa ling'aalo katika ngozi yake ni jeupe, na kuonekana kwake halikwenda chini zaidi ya ngozi, na iwapo malaika za eneo lenye ugonjwa hazijabadilika kuwa nyeupe, naye kuhani atamtenga mgonjwa kwa siku saba.
If the spot on the person’s skin is white but it does not appear that the sore is deeper than just on the skin, the priest must tell him to stay away from other people for seven days.
5 Katika siku ya saba, huyo kuhani itambidi kumchunguza tena ili kuona kama katika maamzi yake huo ugonjwa siyo mbaya, na kama haujaenea kwenye ngozi. Iwapo haujaenea, basi, kuhani atamtenga kwa siku saba zaidi.
Then the priest must examine the person again. If the priest sees that the sore has not changed and has not spread, he must tell the person to stay away from people for seven more days.
6 Naye kuhani atamchunga tena katika siku ya saba ili kuona kama ugonjwa ubepona na haujasambaa zaidi kwenye ngozi. kama haujasambaa, basi, kuhani atamtangaza kuwa yeye ni safi. Ni upele tu. Naye atafua nguo zake, na kisha yeye yu safi.
Then the priest must examine him again. If the sore has faded and has not spread, the priest will allow him to be with other people again; it is only a rash. After the person washes his clothes, he will be allowed to be with other people again.
7 Lakini endapo ule upele utakuwa umishasambaa kwenye ngozi baada ya kuwa amejionyesha kwa kuhani kwa ajili kusafishwa kwake, itambidi kujionyesha tena kwa kuhani.
But if the sore spreads after the priest has examined him, he must go to the priest again.
8 Naye kuhani atamchunguza ilikuona kama huo upele umsambaa zaidi ndani ya ngozi. Na endapo utakuwa umesambaa, kisha kuhani atamtangaza kuwa najisi. Huo ni ugonjwa wa kuambukiza.
The priest will examine him; and if the sore has spread to more of the skin, it is a contagious skin disease, and the priest will declare that he must stay away from other people.
9 Iwapo ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza umo kwa mtu fulani, naye mtu huyo yapasa aletwe kwa kuhan.
When anyone has a contagious skin disease, he must be brought to the priest.
10 Kuhani atamchunguza ili kuona kama kunauvimbe mweupe katika ngozi yake, endapo malaika zitakuwa zimebadilika kuwa nyeupe, au kumekuwa na nyama mbichi kwenye uvimbe.
The priest must examine him. And if there is a white swelling in the skin that has caused the hair in that swelling to become white, and if the flesh in that area is painful/sensitive,
11 Kama ipo, basi, huo ni ugonjwa sugu wa ngozi, naye kuhani atamtangaza kuwa najisi. Hatamtenga kwa kuwa yeye tayari ni najisi.
it is a permanent skin disease, and the priest will declare that he must stay away from other people. The priest does not need to tell that person that he must avoid other people, because other people already are wanting to stay away from him.
12 Iwapo huo ugonjwa unajitokeza na kupanuka zaidi kwenye ngozi, na kuifunika ngozi ya mtu kwa ugonjwa tangu kichwani pake hata miguuni, maadamu anajitokeza kwa kuhani,
‘If the disease spreads all over someone’s body, and the priest examines that person and sees that it is covering his skin from his head to his feet,
13 naye kuhani atamchunguza ili kuona kama huo ugonjwa umeshaenea mwili wake wote. Ikiwa imetokeo hivyo, kuhani atamtangaza mtu huyo aliye na ugonjwa kuwa ni safi. Ikiwa amebadilika kuwa mweupe, huyo ni safi.
and it has caused all his skin to become white [which will indicate that the disease has ended], the priest will declare that the person does not have to stay away from other people.
14 Lakini ikiwa nyama mbichi imeonekana juu yake, atakuwa najisi.
But if the person has open sores and they are very painful/sensitive, he has a contagious skin disease,
15 Kuhani ataiangalia hiyo nyama mbichi na kumtanga kuwa najisi kwa sababu hiyo nyama mbichi ni najisi. Huo ni ugonjwa wa kuambukiza.
and when the priest sees that, he will declare that the person must stay away from other people.
16 Lakini endapo hiyo nyama mbichi inageuka kuwa nyeupe tena, naye huyo mtu hana budi kwenda kwa kuhani.
But if the person’s flesh changes and becomes white, he must go to the priest again.
17 Kuhani atamchunguza ili kuona kama hiyo nyama imebadilika kuwa nyeupe. Kama imekuwa hivyo naye kuhani atatangaza kwamba mtu huyo kuwa ni safi.
The priest must examine him again; and if the sores have become white, the priest will declare that the person who had been infected is now permitted to be with other people again.
18 Mtu anapokuwa na jipu juu yangozi yake na limishapona,
‘Then someone has a boil on his skin and it has healed,
19 na mahali pa jipu pamekuwa na uvimbe au doa lenye kung'aa, wekundu unaochanganyikana na weupe, yapasa kuonyeshwa kwa kuhani.
but in the place where the boil was a white swelling or a bright/shiny spot appears, he must go to the priest.
20 Naye kuhani atalichunguza ili kuona kama linaonekana limekwenda chini ya ngozi, na kama hizo malaika zimebadilika kuwa nyeupe, kama ni hivyo, kuhani atamtangaza kuwa najisi. Huo ni ugonjwa wa kuambukiza, endapo utakuwa umezalishwa mahali lilipokuwa jipu hilo.
The priest must examine it. And if it seems to be deeper than just on the skin, and if the hair in that spot has become white, it is a contagious skin disease that has appeared where the boil had been. And the priest will declare that the person must stay away from other people.
21 Lakini endapo kuhani atakuwa amelichunguza na haoni malaika nyeupe ndani yake, na kwamba iliko chini ya ngozi bali limefifia, kisha kuhani atamtenga kwa siku saba.
But when the priest examines it, if there is no white hair in that spot and it is only on the surface of the skin and has become less bright/shiny, then the priest will order him to stay away from other people for seven days.
22 Kama linaenea kwa kupanuka kwenye ngozi, kisha kuhani atamtangaza kuwa najisi. Huo ni ugonjwa wa kuambukiza.
But if it is spreading, it is contagious and the priest will declare that the person must stay away from other people.
23 Lakini kama hilo doa lenye kung'ara linabaki mahali pake na halijasambaa, basi hilo ni kovu la jipu, naye kuhani atamtangaza kuwa safi.
But if that spot is unchanged and has not spread, it is only a scar from the boil, and the priest will declare that the person is permitted to be with other people again.
24 Ngozi inapoungua na nyama mbichi ya inamekuwa na wekundu uliochanganyika na weupe au doa jeupe,
‘Then someone has a burn on his skin and a bright/shiny or white spot appears, and the flesh in that area is sensitive/painful,
25 kisha kuhani ataichunguza kuona kama malaika zilizoko kwenye doa hilo zimebadilika na kuwa nyeupe, na kama limeonekana kwenda chini zaidi ya ngozi, kama limekuwa hivyo, basi huo ni ugonjwa wa kuambukiza. Umejitokeza kwenye jeraha la moto, naye kuhani atamtangaza kuwa najisi. Huo ni ugonjwa wa kuambukiza.
the priest must examine the spot. If the hair in that spot has turned white and it seems to be deeper than just on the surface of the skin, it is a contagious skin disease that has appeared where the burn was, and that person must stay away from other people.
26 Lakini endapo kuahani analichunguza na naona kwamba hakuna malaika nyeupe kwenye doa, na kwamba halikuenda chini ya ngozi bali linafifia, basi, kuhani atamtenga mtu huyo kwa siku saba.
But when the priest examines it and sees that there is no white hair in that spot and it is only on the surface of the skin, and has faded, the priest will declare that the person must stay away from people for seven days.
27 Kisha yapasa kuahani kumchunguza tena katika siku ya saba. Iwapo litakuwa limesambaa kwa upana kwenye ngozi, naye kuhani atamtangaza kuwa najisi. Huo ni ugojwa wa kuambukiza.
On the seventh day, the priest will examine him again. If the sore is spreading, it is a contagious skin disease, and the priest will declare that the person must stay away from other people.
28 Iwapo hilo doa lisalia mahali pake na halitakuwa limesambaa kwenye ngozi bali limefifia, ni uvimbe tu kutokana na kuungua moto, naye kuhani atamtangaza kuwa safi, kwa kuwa siyo zaidi ya jeraha la kuungua.
However, if the spot is not changed and has not spread but has faded, it is only a scar from the burn, and the priest will declare that the person is permitted to be with other people again.
29 Iwapo mwanaume au mwanamke ana ugonjwa wa kuambukiza kichwani au kidevuni pake,
‘If a man or a woman has a sore on his head or on his chin,
30 kisha kuhani atamchunguza mtu huyo kwa ajili ya ugonjwa wa kuambukiza ili kuona kama unakwenda ndani zaidi ya ngozi, na kama kuna nywele za manjano, nyembamba ndani yake. endapo zinaonekana, kisha kuhani atamtangaza kuwa najisi. Huo ni mwasho, ugonjwa wa kuambukiza kichwani au kidevuni.
the priest must examine it. If it appears to be deeper than [just on the surface of] the skin, and the hair in that spot has thinned out and has become yellowish, it is a contagious skin disease that causes itching. And the priest will declare that the person must stay away from other people.
31 Iwapo kuhani anachunguza ugonjwa wa mwasho na anagundu kuwa hauko chini ya ngozi, na kama hakuna nywele nyeusi ndani yake, kisha kuhani atamtenga mtu huyo mwenye ugonjwa wa mwasho kwa siku saba.
But when the priest examines that kind of sore, if it seems to be only on the surface of the skin and there is no healthy hair in it, the priest will tell the person to stay away from other people for seven days.
32 Katika siku ya saba kuhani atauchunguza tena huo ugonjwa ili kuona kama umesambaa, Endapo hakuna malaika za manjano, na iwapo ugonjwa uko usawa ngozi tu,
On the seventh day, the priest will examine the sore again. If it has not spread and if there is no yellow hair in that spot and if it appears to be only on the surface of the skin,
33 basi, yapasa mtu huyo kunyolewa., lakini sehemu yenye ugonjwa haitanyolewa, naye kuhani atamtenga mtu huyo mwenye ugonjwa wa mwasho kwa siku saba.
the person must shave the hair near the sore but not the hair on the sore. And the priest will tell him to stay away from other people for seven more days.
34 Katika siku ya saba kuhani atauchunguza tena ugonjwa ili kuona kama umacha kusambaa ndani ya ngozi. Iwapo unaonekana kuwa hukwenda chini zaidi ya ngozi, kisha kuhani atamtangaza kuwa safi. Mtu huyo yapasa kufua nguo zake, na kisha atakuwa safi.
On the seventh day, the priest will examine that spot again. If it has not spread and it appears to be only on the surface of the skin, the priest will declare that the person is permitted to be with people again. The person must wash his clothes, and then he can be with other people.
35 Lakini ikiwa ugonjwa wa mwasho umeenea kwa sehemu kubwa kwenye ngozi baada ya kuhani kutangaza kuwa alikuwa safi,
But if the sore later spreads,
36 naye kuhani itabidi amchunguze tena. Iwapo ugonjwa utakuwa umesambaa katika ngozi, kuhani hahitajiki kutafuta nywele za manjano. Mtu huyo ni najisi.
the priest must examine him again. If the itch/sore has spread, the priest does not need to look for yellow hair, because it is clear that the person has a contagious skin disease.
37 Lakini iwapo katika mtazamo wa kuhani inaonekana kuwa huo ugonjwa wa mwasho umekoma kusambaa, basi huo ugonjwa umekwisha pona. Yeye ni safi, naye kuhani atamtangaza kuwa safi.
However, if the priest thinks that the spot has not changed, and healthy hair is growing in that area, it is clear that the itch has healed, and the priest will declare that the person is permitted to be with other people again.
38 Iwapo mwanume au mwanamke ana madoa juu ya ngozi,
‘Then a man or a woman has white spots on the skin,
39 kisha kuhani atamchunguza mtu huyo ili kuona kama hayo madoa ni meupe kwa kufiifia, ambalo ni kovu tu lililojitokeza kwenye ngozi. Yeye yu safi.
the priest should examine them. But if the spots are dull white, it is only a rash, and [the priest will declare that] the person is permitted to be with other people.
40 Iwapo nywele za mtu zimenyonyoka kichwani, yeye ni kipara lakini yu safi.
‘If a man loses the hair on any part of his head, he does not need to stay away from other people.
41 Na iwapo nywele zake zimenyonyoka upande wa mbele wa kichwa chake, na iwapo paji lake la uso lina kipara, yeye yu safi.
42 Lakini endapo kuna kidonda chenye wekundu uliochanganyika na weupe, juu ya kipara chake au paji lake la uso, huo ni ugonjwa wa kuambukiza uliojitokeza.
But if he gets a bright/shiny sore on his bald head or on his forehead, he has a contagious skin disease.
43 Naye kuhani atamchunguza ili kuona iwapo uvimbe wa eneo linaugua juu ya upara wake au paji lake la uso lina wekundu uliochanganyika na weupe, kama kuonekana kwa ugonjwa wa kuambukiza kwenye ngozi.
The priest must examine him. If the swollen sore is a bright spot like [the spot on someone who has] a contagious skin disease,
44 Ikionekana hivyo, basi huyo ana ugonjwa wa kuambukiza naye ni najisi. Hakika kuhani atamtangaza kuwa najisi kwa sababu ya ugonjwa wake kichwani pake.
the priest will declare that the man has a contagious skin disease and must not be with other people.
45 Mtu aliye na ugojwa wa kuambukiza atavaa nguo zilizochanika, ni lazima nywele zake ziachwe wazi, na yampasa kufunika uso wake mpaka puani na kupiga kelele, 'Najisi, najisi.'
‘Anyone who has a contagious skin disease must wear torn clothes and not comb his hair. [When he is near other people], he must cover the lower part to his face and call out, “Do not come near me! I have a contagious skin disease!”
46 Naye atakuwa najisi siku zote za ugonjwa wake wa kuambukiza. Kwa sababu anao ugonjwa unaosambaa, yapasa kuishi peke yake nje ya kambi.
He is not allowed to be with other people as long as he has the disease. He must live alone, outside the camp.’”
47 Kuna wakati fulani vazi la mtu hupata ukungu juu yake. Laweza kuwa vazi, ama la sufu au kitani,
“Sometimes a person’s clothing gets mildew on it. It may be clothing that is woven from wool or made from linen or from leather.
48 au kitu chochote kilichosukwa au kufumwa kutokana na sufu au kitani, au ngozi au kitu chochote kilichotengenezwa kwa ngozi.
49 Iwapo sehemu iliyochafuliwa ina rangi ya kijani au nyekundu katika vazi, ngozi, kifaa kilichosukwa au kufumwa, basi huo ni ukungu uanasambaa, ni lazima uonyeshwe kwa kuhani.
If the contaminated/mildewed part is greenish or reddish, it is a spreading mildew, and it must be shown to the priest.
50 Yapasa kuhani akichunguze hicho kifaa kwa ajili ya ukungu; ni lazima akitenge kitu chochote kilicho na ukungu kwa siku saba.
The priest will examine it, and then put it in a separate place by itself for seven days.
51 Naye atauchunguza tena huo ukungu katika siku ya saba. Endapo utakuwa umesambaa katika kifaa hicho, basi ni wazi kwamba huo ni ukungu wenye kuangamiza, na hicho kifaa ni najisi.
On the seventh day he must examine it again. If the mildew has spread, it is clear that it is a type of mildew that destroys clothing, and that clothing must not be worn again.
52 Na mwenye kukimiliki atalazimika kukichoma na kukiteketeza kabisa hicho kifaa kilichoonekana na ukungu ndani yake, haijalishi kiwe ni kifaa cha aina gani, kwani huo ukungu unaweza kusababisha ugonjwa.
The owner must burn completely the item that has the mildew in it, whatever kind of item it is.
53 Iwapo kuhani anakichunguza hicho kifaa na kuona kwamba ukungu haujaenea kwenye vazi au chombo kilichosukwa au kusokotwa kutokana na sufu, kitani au ngozi,
But when the priest examines it, if the mildew has not spread,
54 basi atawaagiza wakisafishe hicho kifaa kilichopatikana na ukungu, naye yampasa kukitenga kwa siku saba zaidi.
he will tell the person [who owns it] to wash it. Then he must put it in a separate place for another seven days.
55 Kisha kuhani atakichunguza tena hicho kifaa chenye ukungu baada ya kuwa kimesafinshwa. Kama ukungu haukubadilika rangi yake, hata kama haukusambaa, kifaa hicho ni najisi. Yapasa kichomwe, haijalishi ni wapi ukungu huo utakuwa umekichafua.
Then the priest will examine it again. If the color of the mildew has not changed, even though it has not spread, that item must not be worn again. It does not matter if the mildew is on the inside of the clothing or on the outside; it must be burned.
56 Iwapo kuhani anakichunguza hicho kifaa, na kama ukungu umefifia baada ya kuwa umeoshwa, basi atakirarua kile kipande kilichochaufuliwa kutoka kwenye vazi au kutoka kwenye ngozi, au kutoka kwenye chombo kilichosukwa au kusokotwa.
But when the priest examines it [after it has been washed], if the mildew has faded, he must tear out that part that had the mildew in it.
57 Ikiwa ukungu unazidi kuonekana katika vazi, ama katika chombo kilichosukwa au kufumwa, au katika kitu chochote kilichotengenezwa kwa ngozi, basi, ukungu utakuwa unasambaa. Kifaa chochote kilicho na ukungu ni lazima kichomwe.
But if the mildew reappears in that item, it is clear that it is spreading, and the whole item must be burned.
58 Vazi au kitu chochote kilichosukwa au kufumwa kutokana na sufu, au kitani, au ngozi au kitu chochote kilichotengenezwa kwa ngozi—iwapo unakisafisha kifaa nao ukungu ukawa umetoka, nacho kifaa lazima kisafishwe mara ya pili, kisha kitakuwa safi.
But after the clothing is washed and the mildew disappears, it must be washed again, and then it can be worn again.
59 Hii ndiyo sheria ihusuyo ukungu katika vazi la sufu au kitani, au kwenye kitu chochote kilichosukwa au kufumwa kutokana na sufu, au kitani, au kitu chochote kilichotengenewa kwa ngozi, ili kwamba mweze kuvitangaza kuwa safi au najisi.
Those are the regulations concerning mildew on things made of wool or linen or leather, for deciding whether those things can continue to be worn or not.”

< Mambo ya Walawi 13 >