< Waamuzi 16 >

1 Samsoni alikwenda Gaza na akamwona kahaba huko, naye akalala pamoja naye.
Samson, étant allé à Gaza, y remarqua une courtisane et se rendit auprès d’elle.
2 Watu wa Gaza wakaambiwa, “Samsoni amekuja hapa.” Watu wa Gaza wakazunguka mahali hapo kwa siri, wakamngoja usiku wote katika lango la jiji. Walikaa kimya usiku wote. Wakisema, “Hebu tusubiri mpaka mchana, na kisha tumwuue.”
Les gens de Gaza, apprenant que Samson était venu chez eux, passèrent la nuit à faire des rondes et à le guetter aux portes de la ville; ils gardèrent toute la nuit un profond silence, se disant: "D’Ici au point du jour, nous l’aurons tué."
3 Samsoni akalala kitandani mpaka usiku wa manane. Usiku wa manane akaamka na akashika mlango wa jiji na miimo yake miwili. Akavivuta kutoka nje, komeo na vyote, akaviweka kwenye mabega yake, akavichukua hadi juu ya kilima, mbele ya Hebroni.
Samson resta couché jusqu’à minuit; à minuit il se leva, et, saisissant les battants de la porte de la ville avec les deux poteaux, les arracha en même temps que la barre, mit le tout sur ses épaules et le porta au sommet de la montagne qui regarde Hébron.
4 Baada ya hayo, Samsoni alimpenda mwanamke aliyeishi katika bonde la Soreki. Jina lake alikuwa Delila.
Plus tard, il s’éprit d’une femme appelée Dalila, dans la vallée de Sorek.
5 Wale wakuu wa Wafilisti wakamwendea, wakamwambia, “mdanganye Samsoni ili uone mahali zilipo nguvu zake kuu, na kwa namna gani tunaweza kumshinda, ili tumfunge na kumtesa. Fanya hili, na kila mmoja wetu atakupa vipande 1, 100 vya fedha.”
Les princes des Philistins vinrent la trouver et lui dirent: "Tâche, par tes séductions, de découvrir d’où vient sa grande vigueur et comment nous pouvons le vaincre, le lier et le réduire à l’impuissance. Tu recevras alors de chacun de nous onze cents pièces d’argent."
6 Ndipo Delila akamwambia Samsoni, “Tafadhali, niambie ni kwa jinsi gani wewe ni mwenye nguvu sana, na kwa namna gani mtu anaweza kukufunga, ili aweze kukudhibiti?”
Dalila dit à Samson: "Apprends-moi donc pourquoi ta force est si grande, et avec quoi il faudrait te lier pour te dompter."
7 Samsoni akamwambia, “Ikiwa watanifunga na kamba saba safi ambazo hazijakauka, nitakuwa dhaifu na kuwa kama mtu mwingine yeyote.”
Samson lui répondit: "Si on me liait avec sept cordelettes fraîches et encore humides, je perdrais ma force et deviendrais semblable à un autre homme."
8 Basi wakuu wa Wafilisti wakamletea Delila kamba saba ambazo hazijakauka, naye akamfunga Samsoni.
Alors les princes philistins lui procurèrent sept cordelettes humides avec lesquelles elle le lia,
9 Sasa alikuwa na watu waliojificha kwa siri, walikaa katika chumba chake cha ndani. Akamwambia, “Wafilisti wako juu yako, Samsoni!” Lakini akazikata kamba kama uzi wakati unapogusa moto. Na hawakujifunza siri ya nguvu zake.
tandis que des hommes, apostés par elle, attendaient dans la chambre; puis elle lui dit: "Les Philistins viennent te surprendre, Samson!" Et il rompit ses liens, comme se rompent des liens d’étoupe à l’approche du feu. Et le secret de sa force resta encore inconnu.
10 Ndipo Delila akamwambia Samsoni, “Ndivyo ulivyonidanganya mimi na kuniambia uongo. Tafadhali, niambie kwa namna gani unaweza kufungwa.”
Dalila dit à Samson: "Tu t’es joué de moi, tu m’as dit des mensonges! Voyons, fais-moi savoir avec quoi l’on pourrait te lier."
11 Akamwambia, “Ikiwa watanifunga na kamba mpya ambayo haijawahi kutumika kwa kazi, nitakuwa dhaifu na kama mtu mwingine yeyote.”
Il lui répondit: "Eh bien! si l’on m’attachait avec des cordes neuves et n’ayant pas encore servi, je perdrais ma force et deviendrais comme un autre homme."
12 Basi Delila alichukua kamba mpya akamfunga pamoja naye, akamwambia, “Wafilisti wako juu yako Samsoni!” Watu waliokuwa wakisubiri walikuwa ndani ya chumba cha ndani. Lakini Samsoni akaondoa kamba kutoka mikono yake kama kilikuwa kipande cha uzi.
Alors Dalila prit des cordes neuves avec lesquelles elle le lia, tandis qu’on était aux aguets dans la chambre, puis elle lui dit: "Les Philistins viennent te surprendre, Samson!" Mais il arracha les cordes de ses bras comme du fil.
13 Delila akamwambia Samsoni, “Mpaka sasa umenidanganya na kuniambia uongo. Niambie kwa namna gani unaweza kufungwa.” Samsoni akamwambia, 'Ikiwa utavifuma vifungo saba vya nywele zangu na kuvifunga kwenye kitambaa, kisha kufunga kwenye msumari, nitakuwa kama mtu mwingine yeyote.”
Et Dalila dit à Samson: "Jusqu’à présent tu t’es raillé de moi et ne m’as dit que des mensonges. Apprends-moi comment on pourrait te lier!" Il lui répondit: "Tu n’aurais qu’à entre-tisser les sept boucles de ma chevelure avec la chaîne du tissu."
14 Alipokuwa amelala, Dalila akavifuma vifungo saba vya nywele zake akavifunga ndani ya kitambaa na kuzifunga kwenye msumari, akamwambia, “Wafilisti wako juu yako, Samsoni!” Aliamka kutoka usingizini akang'oa kitambaa na pini zilizokuwa zimefungwa.
Lorsqu’elle eut fixé la cheville, elle lui dit: "Les Philistins viennent te surprendre, Samson!" Il se réveilla de son sommeil et arracha du même coup la cheville du métier et le tissu.
15 Akamwambia, “Wawezaje kusema,” Unanipenda, wakati hushiriki siri zako na mimi? Umenidhihaki mara tatu hizi na hukukuambia ni kwa jinsi gani unazo nguvu nyingi.”
"Quoi! lui dit-elle, tu prétends que tu m’aimes, et ton cœur m’est étranger! Trois fois déjà tu t’es joué de moi, en ne me révélant pas la cause de ta force si grande…"
16 Kila siku alisisitiza kwa bidii na maneno yake, naye akamkemea sana kiasi kwamba alitamani kufa.
Tourmenté ainsi chaque jour et harcelé par ses propos, il en fut enfin excédé à la mort,
17 Basi Samsoni alimwambia kila kitu, akamwambia, “Wembe haujawahi kukata nywele juu ya kichwa changu, kwa maana nimekuwa Mnaziri kwa Mungu kutoka tumboni mwa mama yangu. Ikiwa kichwa changu kitanyolewa, basi nguvu zangu zitaniacha, nami nitakuwa dhaifu na kuwa kama kila mtu mwingine. '
et il lui dévoila tout son cœur, en disant: "Jamais rasoir n’a touché ma tête, car je suis voué à Dieu comme Naziréen depuis le sein maternel; si l’on me coupait les cheveux, je perdrais ma force et je deviendrais faible comme tout autre homme."
18 Delila alipoona kwamba amemwambia ukweli juu ya kila kitu, akawatuma na kuwaita watawala wa Wafilisti, akisema, “Njooni tena, kwa maana ameniambia kila kitu.” Ndipo wakuu wa Wafilisti wakamwendea, wakaleta fedha mkononi mwao.
Dalila vit alors qu’il lui avait ouvert son cœur, et elle envoya quérir les princes philistins, avec ces mots: "Venez cette fois, il m’a parlé à cœur ouvert." Et les princes philistins montèrent chez elle, munis de la somme d’argent.
19 Alimfanya alale katika magoti yake. Alimwita mtu avinyoe vifungo saba vya kichwa chake, naye akaanza kumshinda, kwa maana nguvu zake zilikuwa zimemwacha.
Elle l’endormit sur ses genoux, et, ayant mandé un homme, lui fit couper les sept boucles de sa chevelure; dès lors elle put le maîtriser, car sa vigueur l’avait abandonné.
20 Alisema, “Wafilisti wako juu yako, Samsoni!” Aliamka nje ya usingizi wake akasema, “Nitatoka nje kama nyakati nyingine na kujiweka huru.” Lakini hakujua kwamba Bwana amemwacha.
Elle cria: "Les Philistins te menacent, Samson!" Il se réveilla et se dit: "J’En sortirai comme toujours et me débarrasserai", ne sachant pas que l’Eternel l’avait abandonné.
21 Wafilisti walimkamata na kumng'oa macho. Wakampeleka Gaza na kumfunga kwa shaba. Alikuwa akisaga ngano katika gerezani.
Les Philistins se saisirent de lui et lui crevèrent les yeux; puis ils l’emmenèrent à Gaza, où il fut chargé de chaînes et forcé de tourner la meule dans la prison.
22 Lakini nywele juu ya kichwa chake zilianza kukua tena baada ya kunyolewa.
Mais sa chevelure, qu’on avait rasée, commença à repousser.
23 Watawala wa Wafilisti walikusanyika ili kutoa dhabihu kubwa kwa Dagoni mungu wao, na kufurahi. Walisema, “mungu wetu amemshinda Samsoni, adui yetu, na kumtia katika ufahamu wetu.”
Or, les princes des Philistins s’assemblèrent pour faire de grands sacrifices à leur dieu Dagon et se livrer à des réjouissances, car, disaient-ils, notre dieu a fait tomber dans nos mains Samson, notre ennemi!
24 Watu walipomwona, walimsifu mungu wao, kwa sababu walisema, “mungu wetu ameshinda adui yetu na kutupa sisi - mharibifu wa nchi yetu, ambaye aliwaua wengi wetu.”
Le peuple aussi, en le voyant, glorifia son dieu et s’écria: "C’Est notre dieu qui nous a livré notre ennemi, le fléau de notre pays, celui qui a tué tant des nôtres!"
25 Walipokuwa wakisherehekea, wakasema, 'Mwite Samsoni, aje kutufurahisha.' Walimwita Samsoni nje ya jela na akawafanya wacheke. Walimsimamisha katikati ya nguzo.
Comme ils étaient en belle humeur, ils dirent: "Faites venir Samson, pour qu’il nous divertisse!" Et on le fit venir de la prison, et il les amusa, et on le plaça entre les colonnes.
26 Samsoni akamwambia yule kijana ambaye alikuwa ameshika mkono wake, 'Niruhusu nishike nguzo zilizoshikilia nyumba hii, ili nipate kuegemea.”
Samson dit au jeune garçon qui le conduisait par la main: "Laisse-moi; fais-moi seulement toucher les colonnes qui soutiennent l’édifice, pour que je m’y appuie."
27 Sasa nyumba ilikuwa imejaa wanaume na wanawake. Watawala wote wa Wafilisti walikuwa huko. Juu ya paa kulikuwa na wanaume na wanawake elfu tatu, ambao walikuwa wakiangalia wakati Samsoni alipokuwa akiwafurahisha.
Or, le temple était rempli d’hommes et de femmes; tous les princes philistins s’y trouvaient, et, sur le toit, environ trois mille personnes, hommes et femmes, qui assistaient au divertissement de Samson.
28 Samsoni akamwita Bwana, akasema, “Bwana MUNGU, nipe nia! Tafadhali niimarishe mara moja tu, Mungu, ili nipate kulipiza kisasi kwa Wafilisti kwa kuchukua macho yangu mawili.
Celui-ci invoqua l’Eternel en disant: "Seigneur Elohim! Daigne te souvenir de moi! daigne me rendre assez fort cette fois seulement, mon Dieu! pour que je fasse payer d’un seul coup mes deux yeux aux Philistins!"
29 Samsoni aliweka nguzo mbili katikati ambzo zinashikilia nyumba hiyo, naye akaegemea juu yake, nguzo moja kwa mkono wake wa kuume, na mwingine kwa kushoto kwake.
Et Samson embrassa, en pesant dessus, les deux colonnes du milieu qui soutenaient le temple, l’une avec le bras droit, l’autre avec le gauche,
30 Samsoni akasema, “Na nife pamoja na Wafilisti!” Alipanda kwa nguvu zake na jengo likaanguka juu ya watawala na juu ya watu wote waliokuwa ndani yake. Hivyo waliouawa wakati alikufa walikuwa zaidi ya wale waliouawa wakati wa maisha yake.
en disant: "Meure ma personne avec les Philistins!" Et d’un vigoureux effort, il fit tomber la maison sur les princes et sur toute la foule qui était là; de sorte qu’il fit périr plus de monde à sa mort qu’il n’en avait tué de son vivant.
31 Kisha ndugu zake na nyumba yote ya baba yake wakashuka. Wakamchukua, wakamrudisha na kumzika kati ya Sora na Eshtaoli katika mahali pa kuzikwa Manoa, baba yake. Samsoni alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka ishirini.
Ses frères et toute sa famille vinrent pour emporter son corps, et remontèrent pour l’ensevelir entre Çorea et Echtaol, dans le sépulcre de Manoah, son père. Il avait gouverné Israël vingt années.

< Waamuzi 16 >