< Yoshua 13 >

1 Sasa Yoshua alikuwa mzee wakati Yahweh alipomwambia, “Umekuwa mzee, lakini bado kuna nchi kubwa ya kuteka.
Torej Józue je bil star in zvrhan v letih in Gospod mu je rekel: »Star si in zvrhan v letih in tam ostaja še zelo veliko dežele, da bi bila posedena.
2 Nchi iliyosalia ndio hii: mikoa yote ya Wafilisti, na mikoa ile ya Wageshuri,
To je dežela, ki je še ostala: vse meje Filistejcev in ves Gešur,
3 (tangu Shihori, iliyoko mashariki mwa Misri, na upande wa kaskazini kuelekea mpaka wa Ekroni, inayofikiriwa kuwa ni mali ya Wakanaani; wafalme watano wa Wafilisti, wale wafalme wa Gaza, Ashidodi, Ashikeloni, Gathi na Ekroni - miliki ya Waavi.
od Šihórja, ki je pred Egiptom, celo do mej severno od Ekróna, ki je štet h Kánaancem; pet filistejskih knezov: Gazejci, Ašdódci, Aškelónci, Gitéjci in Ekrónci; tudi Avéjci;
4 Katika upande wa kusini, kulisalia nchi yote ya Wakanaani, na Meara ambayo ni miliki ya Wasidoni, hadi Afeki, hata mpaka wa Waamori;
od juga, vsa dežela Kánaancev in Mara, ki je poleg Sidóncev, do Aféka, do meja Amoréjcev
5 nchi ya Wagebali, Lebanoni kuelekea upande wa mapambazuko ya jua, kutoka Baali- Gadi chini ya Mlima Hermoni mpaka Lebo Hamathi.
in dežela Gebálcev in ves Libanon proti sončnemu vzhodu, od Báal Gada pod goro Hermon do vstopa v Hamát.
6 Pia, wenyeji wote wa nchi ya milima kutoka Lebanoni hadi Misrefothi - Maimu, pamoja na watu wa Sidoni. Nitawafukuza mbele ya jeshi la Israeli. Uwe na uhakika wa kuwapa Waisraeli nchi kama urithi, kama nilivyokuagiza.
Vse prebivalce hribovite dežele, od Libanona do Misrefót Majima in vse Sidónce bom jaz napodil izpred Izraelovih otrok. Samo razdeli jo z žrebom Izraelcem v dediščino, kakor sem ti zapovedal.
7 Igawanye nchi hii kama urithi kwa makabila tisa na kwa nusu ya kabila la Manase.
Zdaj torej razdeli to deželo za dediščino vsem devetim rodovom in polovici Manásejevega rodu,
8 Pamoja na nusu nyingine ya kabila la Manase, Wareubeni na Wagadi wamekwisha kupokea urithi wao ambao Musa aliwapa katika upande wa mashariki wa Yordani,
s katerimi so Rubenovci in Gádovci prejeli svojo dediščino, ki jim jo je dal Mojzes, onkraj Jordana proti vzhodu, torej kakor jim je dal Gospodov služabnik Mojzes:
9 kutoka Aroeri, iliyo katika ukingo wa bonde la mto Arnoni (kujumuisha na mji ambao uko katikati ya bonde), kwa nyanda zote za Medeba hadi Diboni;
od Aroêrja, ki je na bregu reke Arnón in mesta, ki je na sredi reke in vso ravnino Médebo do Dibóna;
10 miji yote ya Sihoni, mfalme wa Waamori, ambaye alitawala katika Heshiboni, hata mpaka wa Waamori,
in vsa mesta amoréjskega kralja Sihóna, ki je kraljeval v Hešbónu, do meje Amónovih otrok;
11 Gileadi na mkoa wa Wageshuri na Maakathi, mlima wote wa Hermoni, Bashani yote mpaka Saleka;
Gileád in mejo Gešuréjcev in Maahčánov in vse gore Hermona in ves Bašán, do Salhe;
12 ufalme wote wa Ogu katika Bashani, aliyetawala katika Ashitarothi na Edrei - hawa ni wale waliosalia katika Refaimu - ambao Musa aliwapiga na kuwafukuzia mbali.
vse Ogovo kraljestvo v Bašánu, ki je kraljeval v Aštarótu in v Edréi, ki je ostalo od preostanka velikanov, kajti te je Mojzes udaril in jih vrgel ven.«
13 Lakini watu wa Israeli hawakuwafukuza Wageshuri wala Wamakathi. Badala yake, Wageshuri na Wamakathi wanaishi miongoni mwa Waisraeli hadi leo.
Kljub temu Izraelovi otroci niso pregnali Gešuréjcev niti Maahčánov, temveč Gešuréjci in Maahčáni prebivajo med Izraelci do tega dne.
14 Kabila la Lawi pekee halikupewa urithi na Musa. Urithi wao ni sadaka za Yahweh, Mungu wa Israeli, zilizotolewa kwa moto, kama Mungu alivyomwagiza Musa.
Samo Lévijevemu rodu ni dal nobene dediščine. Daritve Gospoda, Izraelovega Boga, narejene z ognjem, so njihova dediščina, kakor jim je rekel.
15 Musa aliwapa urithi kabila la Rubeni, ukoo kwa ukoo.
Mojzes je dal rodu Rubenovih otrok dediščino glede na njihove družine.
16 Miliki yao ilikuwa kutoka Aroeri, juu ya ukingo wa bonde la Mto Arnoni, na mji ulio katikati ya bonde, na nyanda zote za Medeba.
Njihova pokrajina je bila od Aroêrja, ki je na bregu reke Arnón in mesto, ki je na sredi reke in vsa ravnina pri Médebi;
17 Wareubeni walipata pia Heshiboni, na miji yake yote zilizo katika uwanda, Diboni, na Bamathi Baali, na Bethi Baalimeoni,
Hešbón in vsa njegova mesta, ki so na ravnini; Dibón in Bamót Báal in Bet Báal Meón,
18 na Yahazi, na Kedemothi, na Mefaathi,
Jahac, Kedemót, Mefáat,
19 na Kiriathaimu, na Sibuma, na Zerethishahari juu ya kilima cha bonde.
Kirjatájim, Sibmo in Ceret Šahar na gori doline,
20 Wareubeni walipata pia Bethi Peori, miteremko ya Pisiga, Bethi Yeshimothi,
Bet Peór, Ašdód-Pisgo, Bet Ješimót
21 miji yote ya uwanda, na ufalme wote wa Sihoni, mfalme wa Waamori, ambaye alikuwa ametawala katika Heshiboni, ambaye Musa alikuwa amemshinda pamoja na viongozi wa Midiani, Evi, Rekemu, Zuri, Huri na Reba, wana wa mfalme wa Sihoni, ambao walikuwa wameishi katika nchi.
in vsa mesta ravnine in vse kraljestvo amoréjskega kralja Sihóna, ki je kraljeval v Hešbónu, ki ga je Mojzes udaril z midjánskimi princi Evíjem, Rekemom, Curjem, Hurom in Rebom, ki so bili sihónski vojvode, prebivajoči v deželi.
22 Pia, watu wa Israeli walimwua kwa upanga Baalam mwana wa Beori, ambaye alifanya mambo ya uaguzi, miongoni mwa wale waliowaua.
Tudi Beórjevega sina Bileáma, napovedovalca usode, so Izraelovi otroci ubili z mečem med tistimi, ki so jih umorili.
23 Mpaka wa kabila la Rubeni ni Mto Yordani; huu ndio mpaka wao. Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Rubeni, uliotolewa kwa kila ukoo, pamoja na miji na vijiji vyao.
Meja Rubenovih otrok je bil Jordan in njegova meja. To je bila dediščina Rubenovih otrok po njihovih družinah, mestih in njihovih vaseh.
24 Hiki ndicho Musa alilipa kabila la Gadi, ukoo kwa ukoo:
Mojzes je dediščino izročil Gadovemu rodu, torej Gadovim otrokom, glede na njihove družine.
25 Himaya yao ilikuwa Yazeri, miji yote ya Gileadi na nusu ya nchi ya Waamoni, hadi Aroeri, iliyo mashariki mwa Raba,
Njihova pokrajina je bila Jazêr in vsa mesta Gileáda in polovica dežele Amónovih otrok, do Aroêrja, ki je pred Rabo;
26 kutoka Heshiboni hadi Ramathi - Mizipe na Betonimu, kutoka Mahanaimu mpaka himaya ya Debiri.
in od Hešbóna do Ramát Micpéja in Betoníma in od Mahanájima do meje Debírja;
27 Katika bonde, Musa aliwapa Bethi -Haramu, Bethi - Nimra, Sukothi, na Zafoni, ufalme uliobakia wa Sihoni mfalme wa Heshiboni, pamoja na Yordani kama mpaka, katika sehemu za chini za mwisho wa Bahari ya Kinerethi, upande wa mashariki ng'ambo ya Yordani.
v dolini pa Beth–aram, Bet Nimra, Sukót in Cafón, preostanek kraljestva hešbónskega kralja Sihóna, Jordan in njegova meja, celó do roba Kinéretskega morja na drugi strani Jordana proti vzhodu.
28 Huu ni urithi wa kabila la Gadi, ukoo kwa ukoo, pamoja na miji na vijiji vyao.
To je dediščina Gadovih otrok po njihovih družinah, mestih in njihovih vaseh.
29 Musa aliwapa urithi nusu ya kabila la Manase. Urithi uligawiwa kwa nusu ya kabila la watu wa Manase kutokana na kabila zao.
Mojzes je dal dediščino polovici Manásejevega rodu. To je bila posest polovice rodu Manásejevih otrok po njihovih družinah.
30 Miliki yao ilikuwa kutoka Mahanaimu, Bashani yote, ufalme wote wa mfalme Ogu wa Bashani, na miji yote ya Yairi, iliyo katika Bashani, miji sitini;
Njihovo ozemlje je bilo od Mahanájima, ves Bašán, celotno kraljestvo bašánskega kralja Oga in vsa Jaírova mesta, ki so v Bašánu, šestdeset mest.
31 nusu ya Gileadi, na Ashitarothi na Edrei (miji ya kifalme ya Ogu katika Bashani). Miji hii iligawanywa kwa ukoo wa Makiri mwana wa Manase -nusu ya watu wa Makiri, walipewa kwa kila familia zao.
Polovica Gileáda, Aštarót in Edréi, mesta Ogovega kraljestva v Bašánu, so pripadla otrokom Mahírja, Manásejevega sina, celo do polovice Mahírjevih otrok po njihovih družinah.
32 Huu ndio urithi ambao Musa aliowagawia katika nyanda za Moabu, ng'ambo ya Yordani mashariki mwa Yeriko.
To so dežele, ki jih je Mojzes razdelil v dediščino na moábskih planjavah, na drugi strani Jordana, pri Jerihi, proti vzhodu.
33 Musa hakulipa urithi kabila la Lawi. kwa kuwa Yahweh, Mungu wa israeli, ni urithi wao, kama vile alivyowaambia.
Toda Lévijevemu rodu Mojzes ni dal nobene dediščine. Gospod, Izraelov Bog, je bil njihova dediščina, kakor jim je rekel.

< Yoshua 13 >