< Ayubu 42 >

1 Kisha Ayubu akamjibu Yahweh na kusema,
و ایوب خداوند را جواب داده، گفت:۱
2 “Ninajua kwamba unaweza kufanya mambo yote, ya kuwa hakuna kusudi lako linaweza kuzuiliwa.
«می‌دانم که به هر چیز قادر هستی، وابدا قصد تو را منع نتوان نمود.۲
3 Ni nani huyo ambaye pasipo maarifa huificha mipango? Kwa kweli nilisema mambo ambayo sikuyaelewa, mambo magumu kwangu kuyafahamu, ambayo juu yake sikujua chochote.
کیست که مشورت را بی‌علم مخفی می‌سازد. لکن من به آنچه نفهمیدم تکلم نمودم. به چیزهایی که فوق ازعقل من بود و نمی دانستم.۳
4 Uliniambia, 'Sikiliza sasa, nami nitasema; nitakuuliza mambo, nawe utaniambia.'
الان بشنو تا من سخن گویم. از تو سوال می‌نمایم مرا تعلیم بده.۴
5 Nimekuwa nikikusikia kwa usikivu wa sikio langu, lakini sasa jicho langu linakuona wewe.
ازشنیدن گوش درباره تو شنیده بودم لیکن الان چشم من تو را می‌بیند.۵
6 Basi ninajidharau mwenyewe; ninatubu kwa mavumbi na majivu.”
از این جهت از خویشتن کراهت دارم و در خاک و خاکستر توبه می‌نمایم.»۶
7 Ilitokea baada ya kuwa amekwisha kusema maneno hata kwa Ayubu, Yahweh alimwambia Elifazi Mtemani, “Ghadhabu yangu imewaka dhidi yako na dhidi ya marafiki zako wawili kwa kuwa hamkusema maneno ya haki juu yangu kama alivyofanya mtumishi wangu Ayubu.
و واقع شد بعد از اینکه خداوند این سخنان را به ایوب گفته بود که خداوند به الیفاز تیمانی فرمود: «خشم من بر تو و بر دو رفیقت افروخته شده، زیرا که درباره من آنچه راست است مثل بنده‌ام ایوب نگفتید.۷
8 Sasa basi, jitwalieni mafahari saba na mabeberu saba, kisha mmwendee mtumishi wangu Ayubu na mtoe sadaka ya kuteketezwa kwa ajili yenu. Ndipo Mtumishi wangu Ayubu atawaombea ninyi, nami nitayapokea maombi yake, ili kwamba nisiwashughulikie sawasawa na upumbavu wenu. Maana hamkusema mambo ya haki juu yangu, kama alivyofanya mtumishi wangu Ayubu.”
پس حال هفت گوساله وهفت قوچ برای خود بگیرید و نزد بنده من ایوب رفته، قربانی سوختنی به جهت خویشتن بگذرانید و بنده‌ام ایوب به جهت شما دعا خواهدنمود، زیرا که او را مستجاب خواهم فرمود، مباداپاداش حماقت شما را به شما برسانم چونکه درباره من آنچه راست است مثل بنده‌ام ایوب نگفتید.»۸
9 Basi Elifazi Mtemani, Bildadi Mshuhi na Zofari Mnaamathi walienda na kufanya kama vile Yahweh alivyowaamuru, na Mungu alimtakabali Ayubu.
پس الیفاز تیمانی و بلدد شوحی و صوفرنعماتی رفته، به نوعی که خداوند به ایشان امر فرموده بود عمل نمودند و خداوند ایوب رامستجاب فرمود.۹
10 Na wakati Ayubu alimpowaombea rafiki zake, Yahweh alirejeza bahati yake. Yahweh alimjalia mara mbili ya kile alichokimiliki hapo awali.
و چون ایوب برای اصحاب خود دعا کرد خداوند مصیبت او را دور ساخت وخداوند به ایوب دو چندان آنچه پیش داشته بودعطا فرمود.۱۰
11 Ndipo ndugu zake na Ayubu, na wale jamaa zake wote walikuwa wanajuana naye hapo mwanzo, walikuja hapo kwake na kula chakula pamoja naye katika nyumba yake. Waliomboleza pamoja naye na walimfariji kwa ajili majanga yote ambayo Yahweh alikuwa ameyaleta juu yake. Kila mtu alimpa Ayubu kipande cha fedha na pete ya dhahabu.
و جمیع برادرانش و همه خواهرانش و تمامی آشنایان قدیمش نزد وی آمده، در خانه‌اش با وی نان خوردند و او را درباره تمامی مصیبتی که خداوند به او رسانیده بودتعزیت گفته، تسلی دادند و هرکس یک قسیطه وهرکس یک حلقه طلا به او داد.۱۱
12 Yahweh aliubarikiwa mwisho wa maisha ya Ayubu kuliko mwanzo wake; alikuwa na kondoo kumi na nne elfu, ngamia elfu sita, jozi elfu moja, na punda jike elfu moja.
و خداوند آخرایوب را بیشتر از اول او مبارک فرمود، چنانکه او را چهارده هزار گوسفند و شش هزار شتر و هزارجفت گاو و هزار الاغ ماده بود.۱۲
13 Pia alikuwa na wana saba na mabinti watatu.
و او را هفت پسر و سه دختر بود.۱۳
14 Binti wa kwanza alimwita Yemima, na wa pili Kezia, na wa tatu Kerenihapuki.
و دختر اول را یمیمه ودوم را قصیعه و سوم را قرن هفوک نام نهاد.۱۴
15 Katika nchi yote hawakupatikana wanawake wazuri kama mabinti wa Ayubu. Baba yao aliwapa urithi miongoni mwa kaka zao.
و در تمامی زمین مثل دختران ایوب زنان نیکوصورت یافت نشدند و پدر ایشان، ایشان رادر میان برادرانشان ارثی داد.۱۵
16 Baada ya haya, Ayubu aliishi miaka 140; aliwaona wana wake na wana wa wanawe, hata kizazi cha nne.
و بعد از آن ایوب صد و چهل سال زندگانی نمود و پسران خود و پسران پسران خود را تا پشت چهارم دید.۱۶
17 Basi Ayubu alifariki, akiwa mzee na akijawa na siku nyingi.
پس ایوب پیر و سالخورده شده، وفات یافت.۱۷

< Ayubu 42 >