< Ayubu 35 >
1 Aidha, Elihu aliendelea kusema,
S megszólalt Elíhú és mondta:
2 “Je unadhani hii ni sawa unaposema, 'Haki yangu mbele ya Mungu?
Ezt gondolod-e jognak, erről mondod-e: igazságom Isten előtt,
3 Kwa kuwa unauliza, 'Inafaa nini kwangu' na 'Ingekuwa nzuri kwangu kama ningekuwa nimetenda dhambi?'
hogy azt mondod, mi hasznod van, mit érek el többet, mint vétkemmel?
4 Nitakujibu, wewe pamoja na marafiki zako.
Én válaszolok neked szavakkal s barátaidnak veled együtt.
5 Tazama juu angani, na ulione; angalia anga, ambalo liko juu sana kuliko wewe.
Tekints az égre s láss, s nézd a fellegeket, melyek magasabbak nálad!
6 Kama umetenda dhambi, ni madhara gani huwa unayafanya kwa Mungu? Ikiwa makosa yako yameongezeka zaidi, je huwa unafanya nini kwake?
Ha vétkeztél, mit mivelsz ellene, s ha sok a bűntetted, mit teszel neki;
7 Kama wewe ni mwenye haki, unaweza kumpa nini? Je atapokea nini mkononi mwako?
ha igazad van, mit adsz neki, vagy mit fogad el kezedből?
8 Uovu wako waweza kuwaumiza mtu, kama ulivyo wewe ni mtu, na haki yako yaweza kumnufaisha mwana mwingine wa mtu.
A magadféle férfit illeti gonoszságod, és ember fiát igazságod.
9 Watu wanalia kwasababu ya matendo mengi ya unyanyasaji; wanaomba msaada katika mikono ya watu wenye nguvu.
A sok zsarolás miatt kiáltanak, panaszkodnak sokaknak a karja miatt;
10 Lakini hakuna hata mmoja asemaye, ' Mungu Muumba wangu yuko wapi, ambaye hutoa nyimbo wakati wa usiku,
de nem mondják, hol van Isten, teremtőm, a ki adja, hogy énekre keljek éjjel,
11 ambaye hutufundisha sisi zaidi anavyowafundisha wanyama wa dunia, na ambaye hutufanya sisi kuwa wenye hekima kuliko ndege wa angani?
a ki oktat minket a föld barmai által, s az ég madarai által bölcsekké tesz.
12 Huko wanalia, lakini Mungu hawajibu kwasababu ya kibriu ya watu waovu.
Akkor kiáltanak, de nem felel, a rosszak gőgje miatt.
13 Kwa hakika Mungu hatasikia kilio cha kipumbavu; Mwenye nguvu wala hatajali.
Bizony, hamisságot nem hall az Isten, s a Mindenható nem látja meg;
14 Ni kwa namna gani atakujibu ikiwa unasema haumwoni, na ya kwamba hoja yako iko mbele yake, na ya kuwa unamngojea yeye!
hát még midőn mondod, hogy nem látod Őt, előtte van az ügy és to vársz reá.
15 Ni kwa jinsi gani atakujibu kama unasema kwamba hamwadhibu yeyote kwa hasira, na ya kwamba hajishughulishi na kiburi cha watu.
És most azzal, hogy: semmiért büntetett haragja és nem nagyon tudott bűntettről –
16 Basi Ayubu hufumbua kinywa chake tu ili kusema upumbavu; huongeza maneno bila maarifa.”
Jób hiábavalóságra nyitja meg a száját, tudás nélkül szaporít szavakat.