< Ayubu 34 >
1 Zaidi ya hayo, Elihu aliendelea kusema:
And Elihu made answer and said,
2 “Sikilizeni maneno yangu, ninyi watu wenye hekima; nisikieni, ninyi mlio na maarifa.
Give ear, you wise, to my words; and you who have knowledge, give attention to me;
3 Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama ambavyo kaakaa huonja chakula.
For words are tested by the ear, as food is tasted by the mouth.
4 Na tujichagulie sisi wenyewe yale yenye adili: na tujigundulie miongoni mwetu yale yaliyo mazuri.
Let us make the decision for ourselves as to what is right; let us have the knowledge among ourselves of what is good.
5 Kwa kuwa Ayubu amesema, 'mimi ni mwenye haki, lakini Mungu ameondoa haki zangu.
For Job has said, I am upright, and it is God who has taken away my right;
6 Pamoja na haki zangu, ninaangaliwa kama mwongo. Kidonda changu hakiponyeki, ingawa mimi sina dhambi.'
Though I am right, still I am in pain; my wound may not be made well, though I have done no wrong.
7 Ni mtu gani aliye kama Ayubu ambaye hunywa dharau kama maji,
What man is like Job, a man who freely makes sport of God,
8 ambaye huzunguka katika ushirika wa watu ambao ni waovu, na ambaye hutembea pamoja na watu waovu?
And goes in the company of evil-doers, walking in the way of sinners?
9 Kwa kuwa anasema, ' Hakuna faida kwa mtu kujifurahisha kwa kufanya mambo ambayo Mungu anayataka.'
For he has said, It is no profit to a man to take delight in God.
10 Basi nisikilizeni mimi, enyi watu wenye ufahamu: na iwe mbali na Mungu kwamba atatenda uovu;
Now then, you wise, take note; you men of knowledge, give ear to me. Let it be far from God to do evil, and from the Ruler of all to do wrong.
11 na iwe mbali na Mwenye enzi kwamba atatenda dhambi. Kwa kuwa humlipa mtu kutokana na kazi yake; na humfanya mtu apate thawabu za njia zake mwenyewe.
For he gives to every man the reward of his work, and sees that he gets the fruit of his ways.
12 Kwa hakika, Mungu hatendi uovu, wala Mwenye nguvu hajaIpotosha haki.
Truly, God does not do evil, and the Ruler of all is not a false judge.
13 Ni nani aliyemweka kuwa mtawala wa dunia? Ni nani aliyeiweka dunia yote chini yake?
Who put the earth into his care, or made him responsible for the world?
14 Ikiwa aliweka makusudio yake juu yake mwenyewe, na kama amejikusanyia mwenyewe nafsi yake na pumzi yake,
If he made his spirit come back to him, taking his breath into himself again,
15 basi miili yote itateketea pamoja; mwanadamu angerudi mavumbini tena.
All flesh would come to an end together, and man would go back to the dust.
16 Kama sasa mna ufahamu, sikilizeni haya; sikilizeni sauti ya maneno yangu.
If you are wise, take note of this; give ear to the voice of my words.
17 Je yeye anayeichukia haki aweza kutawala? Je mtamhukumu Mungu kuwa ni mwenye makosa, ambaye ni mwenye haki na mwenye nguvu?
How may a hater of right be a ruler? and will you say that the upright Ruler of all is evil?
18 Mungu ambaye humwambia mfalme, ' Wewe ni mbaya; au huwaambia wenye kuheshimiwa, 'Ninyi ni waovu'?
He who says to a king, You are an evil-doer; and to rulers, You are sinners;
19 Mungu ambaye haoneshi upendeleo kwa viongozi na ambaye hawakubali zaidi watu matajiri kuliko masikini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake.
Who has no respect for rulers, and who gives no more attention to those who have wealth than to the poor, for they are all the work of his hands.
20 Watakufa kwa muda mfupi; wakati wa usiku watu watatikiswa na watapita; watu wenye nguvu watatwaliwa mbali, lakini si kwa mikono ya wanadamu.
Suddenly they come to an end, even in the middle of the night: the blow comes on the men of wealth, and they are gone, and the strong are taken away without the hand of man.
21 Kwa kuwa macho ya Mungu yako juu ya njia za mtu; anaziona hatua zake zote.
For his eyes are on the ways of a man, and he sees all his steps.
22 Hakuna giza, wala hakuna weusi mzito ambao watenda mabaya wanaweza kujificha wao wenyewe.
There is no dark place, and no thick cloud, in which the workers of evil may take cover.
23 Kwa kuwa Mungu hahitaji kumchunguza mtu zaidi; wala hakuna haja kwa mtu yeyote kwenda mbele zake kwa hukumu.
For he does not give man a fixed time to come before him to be judged.
24 Huwavunja vipande vipande watu wenye nguvu kwa ajili ya njia zao ambazo hazihitaji uchunguzi zaidi; huwaweka watu wengine katika nafasi zao.
He sends the strong to destruction without searching out their cause, and puts others in their place.
25 Kwa namna hii ana maarifa juu ya matendo yao; huwatupa watu hawa wakati wa usiku; nao wameangamizwa.
For he has knowledge of their works, overturning them in the night, so that they are crushed.
26 Huwaua kwa matendo yao mabaya kama wakosaji dhahiri mbele za watu wengine
The evil-doers are broken by his wrath, he puts his hand on them with force before the eyes of all onlookers.
27 kwasababu wamegeuka na kuacha kumfuata yeye na wamekataa kuzisadiki njia zake zozote.
Because they did not go after him, and took no note of his ways,
28 Na kwa namna hii, wamekifanya kilio cha watu masikini kimfikie; amekisikia kilio cha watu walioteswa.
So that the cry of the poor might come up to him, and the prayer of those in need come to his ears.
29 Na wakati akaapo kimya, nani aweza kumhukumu kuwa mkosaji? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumjua? Anatawala sawa sawa juu ya taifa na mtu pia,
30 ili kwamba watu wasiomjua Mungu wasije wakatawala, ili kwamba asiwepo mtu wa kuwanasa watu.
31 Fikiria mtu akimwambia Mungu, ' Mimi ni mwenye hatia kabisa, lakini sitatenda dhambi tena;
32 nifunze kile ambacho siwezi kukiona; nimetenda dhambi, lakini sitafanya tena.'
33 Je unadhani kwamba Mungu ataiadhibu dhambi ya mtu huyo, kwa kuwa unayachukia yale ambayo Mungu huyatenda? Ni lazima uchague, siyo mimi. Basi sema yale ambayo unayajua.
34 Watu wenye ufahamu wataniambia, kwa kweli, kila mtu mwenye hekima ambaye hunisikia atasema,
Men of knowledge, and all wise men, hearing me, will say,
35 Ayubu anazungumza bila maarifa; maneno yake hayana hekima.'
Job's words do not come from knowledge; they are not the fruit of wisdom.
36 Kama Ayubu alijaribiwa kwa kitu kidogo kabisa katika kesi yake kwasababu ya kuongea kwake kama watu waovu.
May Job be tested to the end, because his answers have been like those of evil men.
37 Kwa kuwa anaongeza uasi juu ya dhambi yake; anapiga makofi ya dharau kati yetu; anaweka maneno kinyume na Mungu.”
For in addition to his sin, he is uncontrolled in heart; before our eyes he makes sport of God, increasing his words against him.