< Isaya 39 >

1 Katika mda ule Merodaki mtoto wa Baladani, mfalme wa Babeli, alituma zawadi na barua kwa Hezekia; maana alisikia Hezekia alikuwa anaumwa na amepona.
At that time sent Merodach-baladan, the son of Baladan, the king of Babylon, letters and a present to Hezekiah; for he had heard that he had been sick, and was become strong again.
2 Hezekia alifurahishwa na hivi vitu; alimuonyesha mjumbe nyumba ya ghala la vitu vya thamani- vitu kama fedha, dhahabu, viungo, na mafuta ya thamani, ghala la kuwekea silaha zake, na vitu vyote vilivyopatikana kwenye stoo yake. Hapakuwa na kitu katika nyumba yake, wala ufalme wake wote, Hezekia hakuwaonyesha wao.
And Hezekiah was rejoiced on their account, and showed them his treasure-house, the silver, and the gold, and the spices, and the precious oil, and the whole of his armor-house, and all that was found in his treasures: there was nothing that Hezekiah showed them not, in his house, and in all his dominion.
3 Basi Isaya nabii alikuja kwa mfalme Hezekia na kumuuliza, ''Je watu hawa wamekuambia nini? wametoka wapi?, ''Wamekuja kwangu kutoka mbali nchi ya Babeli.''
Then came Isaiah the prophet unto king Hezekiah, and said unto him, What did these men say? and whence did they come unto thee? And Hezekiah said, From a far-off country are they come unto me, from Babylon.
4 Isaya akamuuliza je ni vitu gani walivyoviona katika nyumba yako? Hezekia akajibu, ''Wameona kila kitu katika nyumba nyangu. Hakuna kitu miongoni mwa vitu vyangu vya thamani ambavyo sijawaonyesha.''
And he said, What did they see in thy house? And Hezekiah said, all that is in my house have they seen; there is nothing that I did not show them in my treasures.
5 Basi Isaya akamwambia Hezekia, ''Sikiliza neno la Yahwe wa majeshi:
And Isaiah said to Hezekiah, Hear the word of the Lord of hosts,
6 'Tazama siku inakaribia kuja pale kila kitu katika nyumba yako, vitu ambavyo mababu zako wamevihifadhi mbali mpaka mda huu wa sasa Vitapelekwa Babeli. Hakuna kitakachobakizwa, asema Yahwe.
Behold, days are coming when all that is in thy house, and that which thy fathers have laid up in store until this day, shall be carried to Babylon: nothing shall be left, saith the Lord.
7 Na watoto watazaliwa kutoka kwako, ambao wewe mwenyewe utawazaa- watachukuliwa mbali, na watakuwa matoashi katika jumba la mfalme wa Babeli.''
And of thy sons that will issue from thee, whom thou wilt beget, shall they take; and they shall be court-servants in the palace of the king of Babylon.
8 Basi Hezekia akamwambia Isaya, ''Neno la Yahwe alilolizunumza ni zuri.'' Maana alifikiria, ''Patakuwa na amani na utulivu katika siku zangu.''
Then said Hezekiah to Isaiah, Good is the word of the Lord which thou hast spoken. He said moreover, For there shall be peace and stability in my days.

< Isaya 39 >