< Wagalatia 6 >

1 Ndugu, ikiwa mtu amekamatwa katika uovu, ninyi mlio wa kiroho, mnawiwa kumrejesha huyo ndugu katika roho ya upole. Huku mkijiangalia wenyewe ili msijaribiwe.
Brethren, if a man be overtaken in a fault, ye which are spiritual, restore such an one in the spirit of meekness; considering thyself, lest thou also be tempted.
2 Mchukuliane mizigo, na kwa hiyo mtaikamilisha sheria ya Kristo.
Bear ye one another’s burdens, and so fulfil the law of Christ.
3 Ikiwa mtu yeyote anajiona ni bora wakati si kitu, anajidanganya mwenyewe.
For if a man think himself to be something, when he is nothing, he deceiveth himself.
4 Kila mmoja na aipime kazi yake. Kisha atakuwa na kitu mwenyewe peke yake cha kujisifu, bila kujilinganisha mwenyewe na mtu yeyote.
But let every man prove his own work, and then shall he have rejoicing in himself alone, and not in another.
5 Maana kila mtu atachukua mzigo wake mwenyewe.
For every man shall bear his own burden.
6 Mtu aliyefundishwa neno lazima amshirikishe mazuri yote mwalimu wake.
Let him that is taught in the word communicate unto him that teacheth in all good things.
7 Msidanganyike. Mungu hadhihakiwi. Kila apandacho mtu, ndicho atakachovuna pia.
Be not deceived; God is not mocked: for whatsoever a man soweth, that shall he also reap.
8 Kila apandaye mbegu katika asili yake ya dhambi atavuna uharibifu, lakini yeye apandaye mbegu katika Roho, atavuna uzima wa milele kutoka kwa Roho. (aiōnios g166)
For he that soweth to his flesh shall of the flesh reap corruption; but he that soweth to the Spirit shall of the Spirit reap life everlasting. (aiōnios g166)
9 Tusichoke katika kutenda mema, maana kwa wakati wake tutavuna ikiwa hatutakata tamaa.
And let us not be weary in well doing: for in due season we shall reap, if we faint not.
10 Hivyo basi, wakati tutakapokuwa na nafasi, tutende mema kwa kila mmoja. Tutende mema zaidi hasa kwa walio ndani ya imani.
As we have therefore opportunity, let us do good unto all men, especially unto them who are of the household of faith.
11 Angalieni ukubwa wa barua nilizowaandikia kwa mkono wangu mwenyewe.
Ye see how large a letter I have written unto you with mine own hand.
12 Wale wanaotaka kufanya mema kwa mtazamo wa mwili ndiyo wenye kuwalazimisha mtahiriwe. Wanafanya hivyo kwa sababu wasiingie kwenye mateso ya msalaba wa Kristo.
As many as desire to make a fair shew in the flesh, they constrain you to be circumcised; only lest they should suffer persecution for the cross of Christ.
13 Maana hata hao waliotahiriwa wenyewe hawaishiki sheria. Badala yake wanataka ninyi mtahiriwe ili waweze kujivunia miili yenu.
For neither they themselves who are circumcised keep the law; but desire to have you circumcised, that they may glory in your flesh.
14 Isitokee nikajivuna isipokuwa kwa msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo. Ni katika yeye ulimwengu umesulubiwa kwangu na mimi katika ulimwengu.
But God forbid that I should glory, save in the cross of our Lord Jesus Christ, by whom the world is crucified unto me, and I unto the world.
15 Kwa kuwa haijalishi kutahiriwa au kutokutahiriwa kuwa ni kitu. Badala yake uzao mpya ni muhimu.
For in Christ Jesus neither circumcision availeth any thing, nor uncircumcision, but a new creature.
16 Kwa wote wenye kuishi kwa kanuni hii, wawe na amani na rehema iwe juu yao wote, na juu ya Israel ya Mungu.
And as many as walk according to this rule, peace be on them, and mercy, and upon the Israel of God.
17 Tangu sasa mtu yeyote asinitaabishe, maana nimebeba chapa za Yesu mwilini mwangu.
From henceforth let no man trouble me: for I bear in my body the marks of the Lord Jesus.
18 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe na roho zenu, ndugu. Amina.
Brethren, the grace of our Lord Jesus Christ be with your spirit. Amen. Unto the Galatians written from Rome.

< Wagalatia 6 >