< Ezekieli 36 >

1 “Na wewe, mwanadamu, itabirie milima ya Israeli na useme, 'Milima ya Israeli, lisikilizeni neno la Yahwe.
Forsothe thou, sone of man, profesie on the hillis of Israel; and thou schalt seie, Hillis of Israel, here ye the word of the Lord.
2 Bwana Yahwe asema hivi: Adui amesema kuhusu ninyi, “Aha!” na “Mahala pa juu pa zamani pamekuwa milki yetu.”'
The Lord God seith these thingis, For that that the enemy seide of you, Wel! euerlastyng hiynessis ben youun to vs in to eritage;
3 Kwa hiyo tabiri na sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: Kwa sababu ya ukiwa wenu na kwa sababu mashambulizi yaliyokuja juu yenu kutoka pande zote, mmekuwa milki ya mataifa mengine; mmeambiwa kwa midomo yao waongeao, na kwa masingizio ya watu.
therefore profesie thou, and seie, The Lord God seith these thingis, For that that ye ben maad desolat, and defoulid bi cumpas, and ben maad in to eritage to othere folkis, and ye stieden on the lippe of tunge, and on the schenschipe of puple;
4 Kwa hiyo, milima ya Israeli, sikilizeni neno la Bwana Yahwe: Bwana Yahwe asema hivi kwa milima na vilima, mifereji ya maji na mabonde, mahali palipoharibika kuwa ukiwa na miji iliyoachwa ambayo imetekwa nyara na kutokuwa huru kwa kutaniwa na mataifa yaliyowazunguka-
therfor, hillis of Israel, here ye the word of the Lord God. The Lord God seith these thingis to the mounteyns, and litle hillis, to strondis, and to valeis, and to peecis of wallis left, and to citees forsakun, that ben maad bare of puplis, and ben scorned of othere folkis bi cumpas;
5 kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi: Hakika nimeongea katika moto wa hasira yangu juu ya mataifa meningine, juu ya Edemu na wote waliochukua nchi yangu kwa ajili yao wenyewe kama milki, dhidi ya wale walikuwa na furaha yote katika mioyo yao na dharau katika roho zao, kama walivyoitwaa nchi yangu kwamba wangeweza kudai nchi za malisho kwa ajili yao.
therfore the Lord God seith these thingis, For in the fier of my feruour Y spak of othere folkis, and of al Idumee, that yauen my lond in to eritage to hem silf with ioie `and al herte, and of entent, and castiden out it, to distrie it; therfor profesie thou on the erthe of Israel,
6 Kwa hiyo, tabiri kwa nchi ya Israeli na sema kwa milima na vilima, hata kwenye mifereji na mabonde, Bwana Yahwe asema hivi: Tazama! Katika ghadhabu yangu na hasira yangu nasema hivi kwa sababu mmechukua fedheha za mataifa.
and thou schalt seie to mounteyns, and litle hillis, to the hiynesse of hillis, and to valeis, The Lord God seith these thingis, For that that ye ben desolat, lo! Y spak in my feruour and in my strong veniaunce. For that that ye suffriden schenschipe of hethene men;
7 Kwa hiyo, Bwana Yahwe asema hivi: Mimi mwenyewe nitainua mkono wangu kuapa kwamba mataifa yanayowazunguka yamkini yatawabebea aibu yao wenyewe.
therfor the Lord God seith these thingis, Lo! Y reiside myn hond ayens hethene men, that ben in youre cumpas, that thei bere her schenschipe.
8 Lakini ninyi, milima ya Israeli, mtachipuza matawi na kuzaa matunda kwa ajili ya watu wangu Israeli, kwa kuwa watarudi kwenu.
Forsothe, ye hillis of Israel, brynge forth youre braunchis, and bringe ye fruit to my puple Israel; for it is niy that it come.
9 Maana tazama, nipo kwa ajili yenu, na kuwachukulia kwa fadhili; mtalimwa na kupandwa mbegu.
For lo! Y to you, and Y schal turne to you, and ye schulen be erid, and schulen take seed.
10 Hivyo nitawaongeza juu ya milima yenu watu katika nyumba ya Israeli, yote. Miji itakaa na palipoharibiwa kujengwa.
And in you I schal multiplie men, and al the hous of Israel; and citees schulen be enhabitid, and ruynouse thingis schulen be reparelid.
11 Nitaongeza mtu na wanyama juu yenu milima ili kwamba itaongezeka na kuzaa. Kisha nitawafanya kuishi kama mlivyokuwa, na nitawafanya kustawi zaidi kuliko mlivyokuwa zamani, kwa kuwa mtajua yakwamba mimi ni Yahwe.
And Y schal fille you with men and beestis, and thei schulen be multiplied, and schulen encreesse; and Y schal make you to dwelle as at the bigynnyng, and Y schal rewarde with more goodis than ye hadden at the bigynnyng; and ye schulen wite, that Y am the Lord.
12 Nitawaleta watu, watu wangu Israeli, kutembea juu yenu. Watakumiliki, na utakuwa urithi wao, na hutasababisha tena watoto wao kufa.
And Y schal brynge men on you, my puple Israel, and bi eritage thei schulen welde thee, and thou schalt be to hem in to eritage; and thou schalt no more leie to, that thou be with out hem.
13 Bwana Yahwe asema hivi: Kwa sababu wanakwambia, “Wewe unakula watu, na watoto wa nchi yako wamekufa,”
The Lord God seith these thingis, For that that thei seien of you, Thou art a deuouresse of men, and stranglist thi folk;
14 kwa hiyo hautawala watu wangu tena, na hutalifanya tena taifa lako kuomboleza vifo vyao. Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
therfor thou schalt no more ete men, and thou schalt no more sle thi folk, seith the Lord God.
15 Wala sintokuruhusu kusikiliza fedhiha za mataifa tena; hautachukua tena aibu ya watu au kufanya taifa lako kuanguka-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”'
And Y schal no more make herd in thee the schenschipe of hethene men, and thou schalt no more bere the schenschipe of puplis, and thou schalt no more leese thi folk, seith the Lord God.
16 Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
And the word of the Lord was maad to me, and he seide, Thou,
17 “Mwanadamu, wakati nyumba ya Israeli walipoikalia nchi yao, waliinajisi kwa njia zao na matendo yao. Njia zao zilikuwa kama uchafu wa hedhi ya mwanamke mbele yangu.
sone of man, the hous of Israel dwelliden in her lond, and thei defouliden it in her weies, and in her studies; bi the vnclennesse of a womman in rotun blood the weie of hem is maad bifor me.
18 Hivyo nilimwaga ghadhabu yangu juu yao kwa ajili ya damu ambayo waliyoimwaga juu ya nchi na kwa ajili ya uchafu wa hiyo kwa sanamu zao.
And Y schedde out myn indignacioun on hem, for blood which thei schedden on the lond, and in her idols thei defouliden it.
19 Nimewatawanya miongoni mwa mataifa; walitawanyika katika nchi nyingi. Nimewahukumu kulingana na njia zao na matendo yao.
And Y scateride hem among hethene men, and thei weren wyndewid to londis; Y demede hem bi the weies and fyndyngis of hem.
20 Kisha wakaenda kati ya mataifa, na popote walipoenda, walilitukana jina langu takatifu wakati watu waliwasema, 'Je! hawa kweli ni watu wa Yahwe? Kwa kuwa wamefukuzwa nje ya nchi yake.
And thei entriden to hethene men, to whiche thei entriden, and defouliden myn hooli name, whanne it was seid of hem, This is the puple of the Lord, and thei yeden out of the lond of hym.
21 Lakini nilikuwa na huruma kwa ajili ya jina langu takatifu ambalo nyumba ya Israeli walilinajisi miongoni mwa mataifa, walipoenda huko.
And Y sparide myn hooli name, which the hous of Israel hadde defoulid among hethene men, to whiche thei entriden.
22 Kwa hiyo waambie nyumba ya Israeli, 'Bwana Yahwe asema hivi: Sifanyi haya kwa ajili yenu, nyumba ya Israeli, lakini jina langu, mlilolitukana miongoni mwa mataifa kila sehemu mlipoenda.
Therfor thou schalt seie to the hous of Israel, The Lord God seith these thingis, O! ye hous of Israel, not for you Y schal do, but for myn hooli name, which ye defouliden among hethene men, to whiche ye entriden.
23 Kwa kuwa nitalifanya jina langu kuu kuwa takatifu, mlilolitukana miongoni mwa mataifa-katikati ya mataifa, mmelitukana. Kisha mataifa watajua kwamba mimi ni Yahwe-hivi ndivyo asemavyo Bwana Yahwe-asemavyo-wakati mtakapoona kwamba mimi ni mtakatifu.
And Y schal halewe my greet name, which is defoulid among hethene men, whiche ye defouliden in the myddis of hem; that hethene men wite, that Y am the Lord, seith the Lord of oostis, whanne Y schal be halewid in you before hem.
24 Nitawachukua kutoka mataifa na kuwakusanya kutoka kila nchi, na nitawaleta hata nchi yenu.
For Y schal take awei you fro hethene men, and Y schal gadere you fro alle londis, and Y schal brynge you in to youre lond.
25 Kisha nitanyunyiza maji masafi juu yenu ili muwe wasafi kutoka kwenye uchafu wote, na nitawasafisha kutoka sanamu zenu zenu.
And Y schal schede out clene watir on you, and ye schulen be clensid fro alle youre filthis; and Y schal clense you fro alle youre idols.
26 Nitawapatia moyo mpya na roho mpya sehemu zenu za ndani, na nitautoa moyo wa jiwe kutoka kwenye nyama zenu. Kwa kuwa nitawapatia moyo wa nyama.
And Y schal yyue to you a newe herte, and Y schal sette a newe spirit in the myddis of you; and Y schal do awei an herte of stoon fro youre fleisch, and Y schal yyue to you an herte of fleisch,
27 Nitaiweka Roho yangu ndani yenu na kuwawezesha kutembea katika sheria zangu na kuziweka hukumu zangu, hivyo mtazitenda.
and Y schal sette my spirit in the myddis of you. And Y schal make that ye go in my comaundementis, and kepe and worche my domes.
28 Kisha mtakaa katika nchi niliyowapa babu zenu; mtakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu.
And ye schulen dwelle in the lond, whiche Y yaf to youre fadris; and ye schulen be in to a puple to me, and Y schal be in to a God to you.
29 Kwa kuwa nitawaokoa kutokana na uchafu wenu wote. Nitaita ngano kuiongeza. Sitaweka tena njaa juu yenu.
And Y schal saue you fro alle youre filthis; and Y schal clepe wheete, and Y schal multiplie it, and Y schal not put hungur on you.
30 Nitaongeza tunda la mti na kuzalisha kwenye mashamba ili kwamba msichukue tena aibu ya njaa juu ya mataifa.
And Y schal multiplie the fruyt of tree, and the seedis of the feeld, that ye bere no more the schenschipe of hungur among hethene men.
31 Kisha mtazikumbuka njia zenu mbaya na matendo yenu ambayo hayakuwa mazuri, na mtaonyesha chuki kwenye nyuso zenu kwa sababu ya dhambi zenu na matendo yenu maovu.
And ye schulen haue mynde on youre worste weies, and on studies not goode; and youre wickidnessis, and youre grete trespassis schulen displese you.
32 Sifanyi hili kwa ajili yenu-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-ijulikane kwenu. Hivyo tahayarikeni na kufadhaika kwa sababu ya njia zenu, nyumba ya Israeli.
Not for you Y schal do, seith the Lord God, be it knowun to you; O! the hous of Israel, be ye schent, and be ye aschamed on youre weies.
33 Bwana Yahwe asema hivi: Katika siku niliyowatakasa kutoka kwenye uovu wenu wote, nitawafanya miji ikaliwe na kuzijenga sehemu zilizoharibiwa.
The Lord God seith these thingis, In the dai in which Y schal clense you fro alle youre wickidnessis, and Y schal make citees to be enhabitid, and Y schal reparele ruynouse thingis,
34 Kwa kuwa mtailima nchi iliyoharibiwa hadi itakapoonekana haijaaharibika mbele za macho ya wote wapitao karibu.
and the desert lond schal be tilid, that was sum tyme desolat, bifor the iyen of ech weiegoere,
35 Kisha watasema, “Hii nchi ilikuwa ukiwa, lakini imekuwa kama bustani ya Edeni; miji ya ukiwa na isiyo na wakaaji iliyo magofu ambayo ilibomolewa sasa inakaliwa.
thei schulen seie, Thilke lond vntilid is maad as a gardyn of likyng, and citees forsakun and destitute and vndur myned saten maad strong; and hethene men,
36 Kisha mataifa mengine waliowazunguka watajua yakwamba mimi ni Yahwe, kwamba nimejenga palipokuwa pameharibiwa na kuipanda mbegu sehemu iliyokuwa ukiwa.
whiche euer ben left in youre cumpas, schulen wite, that Y the Lord haue bildid distried thingis, and Y haue plauntid vntilid thingis; Y the Lord spak, and Y dide.
37 Bwana Yahwe asema hivi: Tena nitaulizwa na nyumba ya Israeli kufanya hivi kwa ajili yao, kuwaongeza kama kundi la watu.
The Lord God seith these thingis, Yit in this thing the hous of Israel schulen fynde me, that Y do to hem; Y schal multiplie hem as the floc of men, as an hooli floc,
38 Kama kundi lililotengwa kwa ajili ya sadaka, kama kundi katika Yerusalimu katika sikukuu yake iliyoteuliwa, hivyo miji itaharibiwa kwa kujazwa na makundi ya watu na watajua kwamba mimi ni Yahwe.”'
as the floc of Jerusalem in the solempnytees therof, so the citees that ben forsakun, schulen be fulle of the flockis of men; and thei schulen wite, that Y am the Lord.

< Ezekieli 36 >