< Kutoka 20 >
1 Mungu alisema maneno yote haya:
Le Seigneur dit ensuite toutes ces paroles:
2 Ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewatoa katika ardhi Misri, nje ya nyumba ya utumwa.
Je suis le Seigneur ton Dieu; qui t’ai retiré de la terre d’Egypte, de la maison de servitude.
3 Msiwe na miungu mingine ila mimi tu.
Tu n’auras point de dieux étrangers devant moi.
4 Msijitengenezee sanamu za kuchonga kufananisha na kitu chochote kilichopo juu ya mbingu, chini ya ardhi, au ndani ya maji.
Tu ne te feras point d’image taillée au ciseau, ni aucune représentation de ce qui est en haut dans le ciel, et de ce qui est en bas sur la terre, ni de ce qui est dans les eaux sous la terre.
5 Msipinde na kuabudu sanamu, mimi Yahweh Mungu wenu, ni Mungu mwenye wivu. Nitaadhibu uovu wa mabubu kwa kuleta adhabu juu ya kizazi, cha tatu hadi kizazi cha nne kwa wale wanao nichukia.
Tu ne les adoreras point, ni ne les honoreras: car c’est moi qui suis le Seigneur ton Dieu fort, jaloux, visitant l’iniquité des pères dans les enfants jusqu’à la troisième et la quatrième génération de ceux qui me haïssent,
6 Ila nitaweka agano la uaminifu kwa maelfu watakao nipenda na kushika amri zangu.
Et faisant miséricorde des milliers de fois à ceux qui m’aiment et gardent mes préceptes.
7 Usilitaje bure jina la Yahweh Mungu wako, sitkuwa na hatia kwa yeyote atakaye taja jina langu bure.
Tu ne prendras point le nom du Seigneur ton Dieu en vain; car le Seigneur ne regardera pas comme innocent celui qui aura pris le nom du Seigneur son Dieu en vain.
8 Ikumbuke siku ya Sabato, na kunitengea.
Souviens-toi de sanctifier le jour du sabbat.
9 lazima ufanye kazi zako zote kwa siku sita.
Pendant six jours tu travailleras, et tu feras tous tes ouvrages.
10 Ila siku ya saba ni Sabato kwaajili ya Yahweh Mungu wako. Siku hiyo usifanye kazi yoyote, wewe, au mwana wako, au binti yako, au mtumishi wako wakiume, au mtumishi wako mwanamke, au ng'ombe zako, au mgeni aliye ndani ya malango yako.
Mais au septième jour est le sabbat du Seigneur ton Dieu; tu ne feras aucun ouvrage en ce jour, ni loi, ni ton fils et ta fille, ton serviteur et ta servante, ta bête et l’étranger qui est au-dedans de tes portes.
11 Kwa siku sita Yahweh aliumba mbingu na nchi, bahari, na vitu vyote vilivyomo, na siku ya saba alipumzika. Kwa hiyo Yahweh aliibariki siku ya Sabato na kuitenga.
Car c’est en six jours que le Seigneur a fait le ciel et la terre, et la mer, et tout ce qui est en eux, et il s’est reposé au septième jour; c’est pour cela que le Seigneur a béni le jour du sabbat et l’a sanctifié.
12 Waheshimu baba na mama yako, ili uweze kuishi miaka mingi duniani Yahweh Mungu wako ametoa.
Honore ton père et ta mère afin que tu sois d’une longue vie sur la terre que le Seigneur ton Dieu te donnera.
14 Usifanye uasherati (usizini).
Tu ne commettras point d’adultère.
15 Usiibe kwa mtu yoyote.
Tu ne feras point de vol.
16 Usishuhudie uongo dhidi ya jirani yako.
Tu ne porteras point de faux témoignage contre ton prochain.
17 Usitaman nyumba ya jirani yako; usitamani mke wa jirani yako, wala mtumishi wake wakiume, mtumishi wake mwanamke, ng'ombe wake, punda wake, au chochote cha jirani yako.
Tu ne convoiteras point la maison de ton prochain, et tu ne désireras point sa femme, ni son serviteur, ni sa servante, ni son bœuf, ni son âne, ni aucune des choses qui sont à lui.
18 Watu wote waliona radi na umeme, na kusikia sauti ya mbiu, na mlima ukitoa moshi. Watu walipoona hivo, walitetemeka na kusimama mbali.
Or tout le peuple entendait les tonnerres et le son de la trompette; il voyait les éclairs et la montagne fumante; c’est pourquoi, épouvantés et frappés de terreur, ils se tinrent au loin,
19 Wakamwambia Musa, ongea na sisi, na tutakusikiliza; lakini usiruhusu Mungu kuongea nasi, ama tutakufa.
Disant à Moïse: Parle-nous loi-même, et nous écouterons; mais que le Seigneur ne nous parle point, de peur que nous ne mourions.
20 Musa akawaambia watu, “msiogope, Mungu alikuja kuwajaribu ili heshima yake iwe ndani yenu, kwa hiyo msitende dhambi.”
Et Moïse répondit au peuple: Ne craignez point; car c’est pour vous éprouver que Dieu est venu, et pour que sa crainte soit en vous, et que vous ne péchiez point.
21 hivyo watu walisimama mbali, na Musa alikaribia giza nene Mungu alipokuwa.
Le peuple donc se tint au loin; mais Moïse s’approcha de l’obscurité dans laquelle était Dieu.
22 Yahweh alimwambia Musa, “Ni lazima uwaambie hili Waisraeli: 'Wewe mwenyewe umeona niliongea na wewe kutoka mbinguni.
Outre cela le Seigneur dit à Moïse: Voici ce que tu diras aux enfants d’Israël: Vous avez vu vous-mêmes que du haut du ciel je vous ai parlé.
23 Misjitengenezee miungu mingine pamoja nami, miungu ya fedha au miungu ya dhahabu.
Vous ne vous ferez point de dieux d’argent, et vous ne vous ferez point de dieux d’or.
24 Tengenezeni madhabahu ya udongo kwa ajili yangu, na lazima mtoe sadaka ya kuteketeza, sadaka ya ushirika, kondoo, na ng'ombe. kila sehemu ntakapotaka jina langu liheshimiwe, nitakuja kwenu na kuwabariki.
Vous me ferez un autel de terre, et vous m’offrirez dessus vos holocaustes et vos hosties pacifiques, vos brebis et vos bœufs, dans tout lieu dans lequel sera la mémoire de mon nom; je viendrai à toi et je te bénirai.
25 Kama mtatengeneza madhabahu ya mawe, msijenge na mawe yaiyokatika, na kama mtatumia vyombo vyenu juu yake, mtaweka unajisi.
Que si tu me fais un autel de pierre, tu ne le bâtiras point de pierres taillées; car si tu lèves le couteau dessus, il sera souillé.
26 msije juu ya madhabahu yangu kwa hatua zenu; hii ni ili msioneshe sehemu zenu za siri.”
Tu ne monteras point par des degrés à mon autel, afin que ta nudité ne soit pas découverte.