< Torati 12 >

1 Hizi ni amri na sheria ambazo mtazishika katika nchi ambayo, Yahwe Mungu wa baba zenu, amewapa kumiliki, siku zote mnazoishi kwenye ardhi.
These are the statutes and ordinances, which ye shall take heed to do in the land, which Jehovah the God of thy fathers is giving thee to possess it, all the days that ye live upon the earth.
2 Hakika mtaharibu maeneo yote ambapo mataifa mtakayofukuza miungu yao walioabudu, kwenye milima mirefu, kwenye vilima, na chini ya kila mti wa kijani.
Ye shall utterly destroy all the places wherein the nations which ye shall dispossess have served their gods, upon the high mountains, and upon the hills, and under every green tree;
3 Na mtazivunja madhabahu zao chini, mtaharibu kwa vipandepande nguzo zao za mawe, na kuchoma ncha za Asherahi, mtazikata sanaa za kuchongwa za miungu yao na kuangamiza jina lao nje ya eneo hilo.
and ye shall break down their altars, and shatter their statues, and burn their Asherahs with fire; and ye shall hew down the graven images of their gods, and ye shall destroy the names of them out of that place.
4 Hamtamwabudu Yahwe Mungu wenu kama hivyo.
Ye shall not do so unto Jehovah your God;
5 Lakini kwa eneo ambalo Yahwe Mungu wenu atachagua kutoka makabila yenu kuweka jina lake, hapo patakuwa ni eneo analoishi na huko ndiyo mtaenda.
but unto the place which Jehovah your God will choose out of all your tribes to set his name there, his habitation shall ye seek, and thither thou shalt come;
6 Ni huko ndiko mtaleta sadaka ya kutekeketezwa, dhabihu zenu, zaka zenu, na sadaka zinazotolewa kwa mkono wenu, sadaka zenu za viapo, sadaka za utayari na mzao wa kwanza wa mifugo na wanyama.
and thither ye shall bring your burnt-offerings and your sacrifices, and your tithes, and the heave-offering of your hand, and your vows, and your voluntary-offerings, and the firstlings of your kine and of your sheep;
7 Ni huko mtakula mbele za Yahwe Mungu wenu na kufurahi kuhusu kila kitu ambacho mmeweka mkono, nyie na jamaa zenu, ambapo Yahwe Mungu wenu amewabariki.
and ye shall eat there before Jehovah your God, and ye shall rejoice, ye and your households, in all the business of your hand, wherein Jehovah thy God hath blessed thee.
8 Hamtafanya mambo yote ambayo tunafanya hapa leo; sasa kila moja anafanya chochote kile kizuri machoni pake,
Ye shall not do after all that we do here this day, each one whatever is right in his own eyes.
9 kwa kuwa bado hamjapumzika, kwa urithi ambao Yahwe Mungu wenu anawapa.
For ye are not as yet come to the rest and to the inheritance which Jehovah thy God giveth thee.
10 Lakini pindi mnaenda ng'ambo ya pili ya Yordani na kuishi ndani ya nchi ambayo Yahwe Mungu wenu anasababisha ninyi kurithi, na wakati awapa pumziko kutoka kwa maadui zenu wanaowazunga karibu, ili kusudi muishi kwa usalama,
But when ye have gone over the Jordan, and dwell in the land which Jehovah your God causeth you to inherit, and when he hath given you rest from all your enemies round about, and ye dwell in safety,
11 kisha itakuwa eneo ambalo Yahwe Mungu wenu atachagua kusababisha jina lake kuishi, huko mtaleta yote ninayowaamuru; sadaka za kuteketezwa, dhabihu zenu, zaka zenu, sadaka zilizotolewa kwa mkono wenu, na sadaka za chaguo lenu kwa ajili ya nadhiri mtakazotoa kwa Yahwe.
then there shall be a place which Jehovah your God will choose to cause his name to dwell there; thither shall ye bring all that I command you: your burnt-offerings, and your sacrifices, your tithes, and the heave-offering of your hand, and all your choice vows which ye shall vow to Jehovah.
12 Mtafurahi mbele za Yahwe Mungu wenu-nyie, watoto wenu, binti zenu, wajakazi wa kiume, wajakazi wa kike, na Walawi walio ndani ya lango lenu, kwa sababu hana sehemu au urithi miongoni mwenu.
And ye shall rejoice before Jehovah your God, ye, and your sons, and your daughters, and your bondmen, and your handmaids, and the Levite that is within your gates; for he hath no portion nor inheritance with you.
13 Uwe makini mwenyewe kwamba usitoe sadaka zako za kuteketezwa kila eneo unaloona;
Take heed to thyself that thou offer not thy burnt-offerings in every place that thou seest;
14 lakini ni katika eneo hilo ambalo Yahwe atawachagua miongoni moja kati ya makabila yenu ambalo litatoa sadaka ya kuteketezwa, na huko mtafanya kila kitu ninachokuamuru.
but in the place which Jehovah will choose in one of thy tribes, there thou shalt offer thy burnt-offerings, and there thou shalt do all that I command thee.
15 Hata hivyo, mtaweza kuua na kula wanyama ndani ya malango yenu, kama mnavyotaka, kupokea baraka ya Yahwe Mungu wenu kwa ajili ya yote amewapa; na watu wasio safi na safi wote wanaweza kula, wanyama kama vile paa na kulungu.
Nevertheless, according to all the desire of thy soul thou mayest slay and eat flesh in all thy gates, according to the blessing of Jehovah thy God which he hath given thee: the unclean and the clean may eat thereof, as of the gazelle, and the hart.
16 Lakini hamtakula damu, mtaimwaga kwenye ardhi kama maji.
Only, ye shall not eat the blood; ye shall pour it upon the earth as water.
17 Mnaweza msile ndani ya malango kutoka kwenye zaka ya nafaka zenu, mvinyo wenu mpya, mafuta yenu au mzao wa kwanza wa mifugo au wanyama; na mnaweza msile nyama yoyote mnayoitoa dhabihu pamoja na viapo vyovyote vyenu mnafanya, wala sadaka yenu ya utayari, wala sadaka mnayotoa kwa mkono wenu.
Thou mayest not eat within thy gates the tithe of thy corn, or of thy new wine, or of thine oil, or the firstlings of thy kine or of thy sheep, nor any of thy vows which thou vowest, nor thy voluntary-offerings, nor the heave-offering of thy hand;
18 Badala yake, mtakula mbele ya Yahwe Mugu wenu katika eneo ambalo Yahwe Mungu atachagua- nyie, mtoto wenu, binti yenu, mjakazi wa kiume, mjakazi wa kike, na Mlawi aliye malangoni mwenu; mtafurahi mbele ya Yahwe Mungu wenu kuhusu kila kitu ambacho mnaweka mkono wenu.
but before Jehovah thy God shalt thou eat them in the place which Jehovah thy God will choose, thou and thy son, and thy daughter, and thy bondman, and thy handmaid, and the Levite that is within thy gates; and thou shalt rejoice before Jehovah thy God in all the business of thy hand.
19 Muwe makini wenyewe ili kwamba msimwache Mlawi maadamu mnaishi kwenye nchi yenu.
Take heed to thyself that thou forsake not the Levite all the days thou shalt be in thy land.
20 Wakati Yahwe Mungu wenu apanua mipaka yenu, kama alivyowaahidi, na kusema, “Nitakula nyama,” kwa sababu ya tamaa zenu mnakula nyama, mnaweza kula nyama, kama tanmaa za roho zenu.
When Jehovah thy God shall enlarge thy border, as he promised thee, and thou say, I will eat flesh, because thy soul longeth to eat flesh, thou mayest eat flesh, according to all the desire of thy soul.
21 Kama eneo ambalo Yahwe Mungu wenu achagua kuliweka jina lake ni mbali kutoka kwenu, basi mtaua baadhi ya mifugo yenu na wanyama wenu ambao Yahwe amewapa, kama nilivyowaamuru: hivyo mnaweza kula ndani ya malango yenu, kama tamaa za roho zenu.
If the place which Jehovah thy God will choose to set his name there be too far from thee, then thou shalt slay of thy kine and of thy sheep which Jehovah hath given thee, as I have commanded thee, and thou shalt eat in thy gates according to all the desire of thy soul.
22 Kama paa na Kulungu wanaliwa, hivyo mtakula watu wasio safi na wasafi wanaweze kula kadhalika.
Even as the gazelle and the hart is eaten, so thou shalt eat them: the unclean and the clean alike may eat of them.
23 Lakini muwe na uhakika kwamba hamtumii damu, kwa kuwa damu ni uhai, hamtakula uhai pamoja na nyama.
Only, be sure that thou eat not the blood; for the blood is the life, and thou mayest not eat the life with the flesh;
24 Hamtakula, mtaimwaga nje kwenye ardhi kama maji.
thou shalt not eat it; thou shalt pour it upon the earth as water:
25 Hamtakula, ili kwamba iweze kuwa vizur kwenu, na watoto wenu baada yenu, wakati mtafanya kile kilicho sahihi machoni pa Yahwe.
thou shalt not eat it; that it may go well with thee, and with thy children after thee, when thou shalt do what is right in the eyes of Jehovah.
26 Lakini mambo ambayo ni ya Yahwe ambayo mnayo na sadaka za viapo vyenu-mtachukua hizi na kwenda eneo ambalo Yahwe achagua.
But thy hallowed things which thou hast, and what thou hast vowed, thou shalt take, and come to the place which Jehovah will choose;
27 Hapo mtatoa sadaka ya kuteketekezwa, nyama na damu, kwenye madhabahu ya Yahwe Mungu wenu, damu ya dhabihu zenu itamwangwa nje kwenye madhabahu ya Yahwe Mungu wenu, na mtakula nyama.
and thou shalt offer thy burnt-offerings, the flesh and the blood, upon the altar of Jehovah thy God; and the blood of thy sacrifices shall be poured out upon the altar of Jehovah thy God, and the flesh shalt thou eat.
28 Mchunguze na msikilize haya maneno yote ambayo - ninawaamuru, ili iwe uzuri kwenu na watoto wenu baada yenu milele, wakati mnafanya kile kilicho kizuri na sawa machoni pa Yahwe Mungu wenu.
Take heed to hear all these words which I command thee, that it may be well with thee, and with thy children after thee for ever, when thou doest what is good and right in the eyes of Jehovah thy God.
29 Wakati Yahwe Mungu wenu anapunguza mataifa kutoka kwenu, wakati mnaingia kuwafukuza, na mnawafukuza na kuishi katika nchi yao,
When Jehovah thy God cutteth off from before thee the nations whither thou goest, to take possession of them, and thou hast dispossessed them, and dwellest in their land,
30 muwe makini wenyewe ili kwamba msinaswe kwa kuwafuata, baada ya kuangamizwa kutoka kwenu kunaswa katika kuchunguza miungu yao, katika kuuliza, “Kwa namna gani haya mataifa yanaabudu muingu yao? Nitafanya hivyo hivyo.
take heed to thyself that thou be not ensnared [to follow] after them, after that they are destroyed from before thee; and that thou inquire not after their gods, saying, How did these nations serve their gods? even so will I do likewise.
31 Hautafanya hivyo katika kumheshimu Yahwe Mungu wako, kwa kuwa kila kitu ambacho ni chukizo kwa Yahwe, mambo ambayo anayachukia- wamefanya haya na miungu yao, hata mnateketeza vijana wao na binti zao kwenye moto kwa ajili ya miungu yao.
Thou shalt not do so to Jehovah thy God; for every [thing that is] abomination to Jehovah, which he hateth, have they done unto their gods; for even their sons and their daughters have they burned in the fire to their gods.
32 Chochote ninakuamuru, chunguza. Usiongeze juu yake au kupunguza.
Everything that I command you, ye shall take heed to do it; thou shalt not add thereto, nor take from it.

< Torati 12 >