< 2 Wafalme 20 >

1 Katika siku hizo Hezekia aliugua akawa kwenye hatari ya kufa. Hivyo Isaya mwana wa Amozi, akaja, na kumwambia, “Yahwe asema, 'Weka nyumba yako kwenye mpangilio; kwa kuwa utakufa, na hutapona.'”
About that time, Hezekiah became very ill. [He thought that he] was about to die. Isaiah the prophet came to him and said, “This is what Yahweh says: ‘You should tell the people in your palace what you want them to do after you die, because you are not going to recover from this illness. You are going to die.’”
2 Kisha Ahazi akageuza uso wake kwenye ukuta na kumuomba Yahwe, akisema,
Hezekiah turned his face toward the wall and prayed,
3 “Tafadhali, Yahwe, ukumbuke jinsi nilivyo mwaminifu kutembea mbele yako kwa moyo wangu wote, na jinsi nilivyofanya yaliyo mazuri usoni kwako.” Kisha Hezekia akalia kwa sauti.
“Yahweh, do not forget that I have always served you faithfully, and I have done things that pleased you.” Then Hezekiah started to cry loudly.
4 Kabla ya Isaya hajatoka nje kwenye mji wa kati, neno la Yahwe likamjia, kusema,
Isaiah left the king, but before he had crossed the middle courtyard of the palace, Yahweh gave him a message
5 '“Rudi, na umwambie Hezekia, kiongozi wa watu wangu, 'Hivi ndivyo Yahwe, Mungu wa Daudi babu yako, asemavyo: “Nimesikia maombi yako, na nimeyaona machozi yako. Nitakuponya katika siku ya tatu, na utapanda juu kwenye nyumba ya Yahwe.
which said, “Go back to Hezekiah, the ruler of my people, and say to him, ‘I, Yahweh, the God whom your ancestor King David [worshiped], have heard what you prayed. And I have seen your tears. So, listen: I will heal you. Two days from now you will [be able to] go up to my temple.
6 Nitakuongeza miaka kumi na tano ya maisha yako, na nitakulinda na huu mji kwa ajili yangu na kwa ajili ya mtumishi wangu."”'
I will enable you to live for 15 more years. And I will rescue you and this city again from the power [MTY] of the king of Assyria. I will defend this city for the sake of my own reputation and because of what I promised King David, who served me [well].’”
7 Hivyo Isaya akasema, “Chukueni mkate wa tini.” Walifanya hivyo na kuweka kwenye jipu lake, na akapona.
So Isaiah [returned to the palace and told Hezekiah what Yahweh had said. Then he] [to Hezekiah’s servants], “Bring a paste made of boiled figs. Put some of it on his boil, and he will get well.”
8 Hezekia akamwambia Isaya, “Je kutakuwa na alama gani ambayo Yahwe ataniponya, na kwamba nitapanda juu hadi kwenye hekalu la Yahwe katika siku ya tatu?”
Then Hezekiah replied to Isaiah, “What will Yahweh do to prove that he will heal me and that two days from now I will be able to go up to the temple?”
9 Isaya akajibu, “Hii ndiyo itakuwa ishara kwako kutoka kwa Yahwe, kwamba Yahwe atafanya kitu amacho alichokisema. Je kivuli kitaenda mbele hatua saba, au kurudi nyuma hatua saba?”
Isaiah replied, “Yahweh will do something that will prove to you that he will do what he promised. Do you want him to cause the shadow on the stairway/sundial to go back ten steps/degrees, or to go forward ten steps/degrees?”
10 Hezekia akajibu, “Ni kitu chepesi kwa kivuli kwenda mbele hatua kumi. Hapana, hicho kivuli kirudi nyuma hatua kumi.”
Hezekiah replied, “It is easy to cause the shadow to move forward, [because that is what it always does]. Tell him to cause it to move backward ten steps/degrees.”
11 Hivyo Isaya nabii akamlilia Yahwe, na akaleta kivuli hatua kumi nyuma, kutoka pale ambapo zilikuwa zimevuka kwenye ngazi za Ahazi.
So Isaiah prayed earnestly to Yahweh, and Yahweh caused the shadow to go backward ten steps/degrees on the stairway/sundial that King Ahaz had made (OR, that workers had built for King Ahaz).
12 Katika kipindi hicho Merodak Baladani mfalme wa Babeli alituma barua na zawadi kwa Hezekia, kwa kuwa alisikia kwamba Hezekia alikuwa anaumwa.
At that time, King Merodach-Baladan, the son of Baladan the [previous] King of Babylonia, heard a report that King Hezekiah had been very sick. So he wrote some letters and gave them to some messengers to take to Hezekiah, along with a gift.
13 Hezekia akasikiliza hizo barua, na kisha kuwaonyesha wajumbe sehemu zote na sehemu zake za thamani, fedha, dhahabu, manukato na marhamu na nyumba yenye ghala la silaha zake, na yote yaliyokutwa kwenye ghala za nyumba zake. Hapakuwa na kitu kwenye nyumba, wala kwenye ufalme wake wote, ambao Hezekia hakuwaonyesha.
[When the messengers arrived], Hezekiah welcomed them gladly. Then he showed them everything that was in his (treasure houses/places where very valuable things were stored)—the silver and gold, the spices, the nice-smelling olive oil, and all the weapons [for his soldiers]. He showed them all the [valuable] things in his storerooms and everywhere else in his kingdom [HYP]; he showed them everything.
14 Kisha Isaya akaja kwa Hezekia na kumuuliza, “Hawa watu walikuwa wanakwambiaje? Wanatokea wapi?” Hezekia aksema, “Wamekuja kutoka nchi ya mbali ya Babeli.
Then the prophet Isaiah went to Hezekiah and asked him, “Where did those men come from, and what did they say to you?” Hezekiah replied, “They came from a country very far from here. They came from Babylonia.”
15 Isaya akauliza, “Wameona nini kwenye nyumba yako?” Hezekia akajibu, “Wameona kila kitu kwenye nyumba yangu. Hakuna kitu miongoni mwa vitu vyangu vya thamani ambavyo sijawaonyesha.”
Isaiah asked, “What did they see in your palace?” Hezekiah replied, “They saw everything. I showed them absolutely everything that I own—all my valuable things.”
16 Basi Isaya akamwambia Hezekia, “Sikiliza neno la Yahwe:
[Isaiah knew that Hezekiah had done a very foolish thing]. So Isaiah said to him, “Listen to what Yahweh says to you.
17 'Tazama siku zinakuja wakati kila kitu kwenye kwenye nyumba yako ya kifalme, vitu ambavyo babu zako walivitunza huko hadi leo, vitabebwa kwenda Babeli. Hakuna kitakachobakia, Yahwe asema.
There will be a time when everything that is still in your palace, all the valuable things that were put there by you and your ancestors, will be carried away to Babylon. There will be nothing left here! [That is what] Yahweh says [to you]
18 Watoto waliozaliwa na wewe, ambao umewazaa wewe mwenyewe-watawachukua mbali, na watakuwa matowashi kwenye nyumba ya kifalme ya mfalme wa Babeli.'”
Furthermore, some of your own descendants will be forced to go there, and they will be castrated in order that they may become servants in the palace of the King of Babylon.”
19 Hezekia akamwambia Isaya, “neno la Yahwe uliloliongea ni jema.” Kwa kuwa alifikiri, Je sivyo ikiwapo amani na kweli katika siku zangu?”
Then Hezekiah replied to Isaiah, “That message from Yahweh that you have given to me is good.” He said that because he was thinking, “Even if that happens, there will be peace and security [in Israel] all the rest of my life.”
20 Kama kwa mambo mengine yanamuhusu Hezekia, na ushujaa wake wote, na jinsi alivyotengeza bwawa la maji na mfereji, na kuleta maji kwenye mji-hayakuandikwa kwenye kitabu cha ya matukio ya wafalme wa Yuda?
[If you want to know more about] [RHQ] all the other things that Hezekiah did, about his brave deeds in battle, about his ordering a reservoir to be built in the city and a tunnel [to be dug] to bring water into the reservoir, they are all written in the scroll called ‘The History of the Kings of Judah’.
21 Hezekia akalala na babu zake, na Manase mwanae akawa mfalme katika sehemu yake.
Later Hezekiah died [EUP], and his son Manasseh became the king.

< 2 Wafalme 20 >