< 2 Wafalme 10 >
1 Basi Ahabu alikuwa na watoto sabini katika Samaria. Yehu akaandika barua na kuzituma kwenda Samaria, kwa watawala wa Yezreeli, pamoja na wazee na walinzi wa wana wa Ahabu akisema,
And [belonged] to Ahab seventy sons in Samaria and he wrote Jehu letters and he sent [them] Samaria to [the] officials of Jezreel the elders and to the guardians Ahab saying.
2 “Wana wa bwana wako wako pamoja na wewe, na wewe pia una magari ya farasi na farasi na kuimarisha mji dhidi ya maadui na silaha. Hivyo basi, haraka iwezekanavyo barua hii ikufikiapo,
And now (when comes *LB(ah)*) the letter this to you and [are] with you [the] sons of master your and [are] with you chariotry and horses and a city of fortification and weaponry.
3 mchagueni aliye bora na anayestahili miongoni mwa mtoto wa bwana wenu na kumuweka kwenye kiti cha kifalme cha baba yake, na kupigania ufalme wa bwana wenu.”
And you will see the good and the right of [the] sons of master your and you will set [him] on [the] throne of father his and fight on [the] house of master your.
4 Lakini waliogopa na kusema miongoni mwao, “Tazama, wafalme wawili hawatasimama mbele ya Yehu. Hivyo tutasimamaje?”
And they were afraid very very and they said there! [the] two the kings not they stood before him and how? will we stand we.
5 Kisha yule mtu ambaye alikuwa kiongozi kwenye nyumba ya mfalme, na wale waliowalea watoto, wakatuma ujumbe kwa Yehu, kusema, “Sisi ni watumishi wako. Tutafanya chochote utakacho tuamuru. Hatutamfanya mtu yeyote kuwa mfalme. Fanya lile lililojema machoni pako.”
And he sent [the one] who [was] over the house and [the one] who [was] over the city and the elders and the guardians to Jehu - saying [are] servants your we and all that you will say to us we will do not we will make king anyone the good in view your do.
6 Kisha Yehu akaandika barua mara ya pili, akisema, “Kama mko upande wangu, na kama mtasikiliza sauti yangu, mtachukua vichwa vya watu wa wana wa mabwana wenu, na mje kwangu Yezreeli kesho mda kama huu.” Ndipo wana wa wafalme, sabini kwa hesabu, waliokuwa watu muhimu huko mjini, ambao walikuwa wakiwaleta.
And he wrote to them a letter - second saying if [belong] to me you and to voice my - you [are] listening take [the] heads of [the] men of [the] sons of master your and come to me about this time tomorrow Jezreel towards and [the] sons of the king seventy man [were] with [the] great [people] of the city [who] were bringing up them.
7 Hivyo barua ilipokuja kwao, waliwachukua wana wa wafalme na kisha kuwaua, watu sabini, wakaweka vichwa vyao kwenye vikapu, na kuivituma kwa Yehu katika Yezreeli.
And it was when came the letter to them and they took [the] sons of the king and they slaughtered seventy man and they put heads their in baskets and they sent [them] to him Jezreel towards.
8 Mjumbe mmoja akaja kwa Yehu, akisema, “Wamevileta vile vichwa vya watoto wa wafalme.” Hivyo akasema, viwekeni kwenye mafungu mawili kwenye lango hadi asubuhi.”
And he came the messenger and he told to him saying they have brought [the] heads of [the] sons of the king and he said make them two heaps [the] entrance of the gate until the morning.
9 Asubuhi Yehu akatoka nje na kusimama, na kusema kwa watu wote, “Ninyi hamna hatia. Tazameni, nimefanya fitina dhidi ya bwana wangu na kumuua, lakini ni nani aliyewaua hawa wote?
And it was in the morning and he went out and he stood and he said to all the people [are] righteous you here! I I conspired on master my and I killed him and who? did he strike down all these.
10 Sasa hakika tafakarini kwamba hakuna sehemu ya neno la Yahwe, lile alilonena Yahwe kuhusu familia ya Ahabu, itaanguka kwenye aridhini, kwa kuwa Yahwe amefanya kile alichokiongea kupitia mtumishi wake Eliya.”
Know then that not it will fall any of [the] word of Yahweh [the] ground towards which he has spoken Yahweh on [the] house of Ahab and Yahweh he has done [that] which he spoke by [the] hand of servant his Elijah.
11 Basi Yehu akawaua wote waliokuwa wamebakia wa familia ya Ahabu katika Yezreeli, na watu wake muhimu wote, marafiki zake wa karibu, na makuhani wake, hakuna hata mmoja wao alisalia.
And he struck down Jehu all those [who] remained of [the] house of Ahab in Jezreel and all great [men] his and acquaintances his and priests his until not he had left to him a survivor.
12 Kisha Yehu akainuka na kuondoka; akaenda Samaria. Kadiri alivyokuwa akikaribia Bethi Ekedi ya wachungaji,
And he arose and he went and he went Samaria he [was at] Beth Eked of [the] Shepherds on [the] way.
13 akamlaki na ndugu wa Ahazia mfalme wa Yuda. Yehu akawaambia, “Ninyi ni akina nani?” Wakajibu, “Sisi ni ndugu zake na Ahazia, na tunashuka chini kuwasalimia watoto wa mfalme na watoto wa Malkia Yezebeli.”
And Jehu he found [the] brothers of Ahaziah [the] king of Judah and he said who? [are] you and they said [are] [the] brothers of Ahaziah we and we have come down for [the] peace of [the] sons of the king and [the] sons of the queen-mother.
14 Yehu akawaambia watu wake mwenyewe, “Wachukue wakiwa hai.” Hivyo wakawachukua wakiwa hai na kuwaua kwenye kisima cha Bethi Ekedi, watu wote arobaini na mbili. Hakumwacha hata mmoja wao akiwa hai.
And he said seize them alive and they seized them alive and they slaughtered them to [the] pit of Beth Eked forty and two man and not he spared anyone from them.
15 Baada ya Yehu kuondoka huko, akakutana na Yehonadabu mwana wa Rekabu anakuja kukutana naye. Yehu akamsalimia na kisha akamwambia, “Je moyo wako uko na mimi, kama moyo wangu ulivyo pamoja na wako?” Yehonadabu akajibu, Ndio.” Yehu akasema, “kama ni ndio, nipatie mkono wako.” Kisha Yehonadabu akampatia mkono wake, na Yehu akampandisha Yehonadabu juu kwenye magari ya farasi pamoja naye.
And he went from there and he found Jonadab [the] son of Rechab to meet him and he blessed him and he said to him ¿ [is] there with heart your right just as heart my [is] with heart your and he said Jonadab there is and there is give! hand your and he gave hand his and he took up him to himself into the chariot.
16 Yehu akasema, “Fuatana pamoja nami na uone wivu wangu kwa Yahwe.” Hivyo alikuwa na Yehonadabu akiendesha gari la farasi.
And he said come! with me and look on zeal my for Yahweh and they made ride him in chariot his.
17 Wakati alipokuja Samaria, Yehu akawaua wote waliobakia kutoka uzao wa Ahabu katika Samaria, hata akawaangamiza ukoo wa kifalme wa Ahabu, kama walivyokuwa wameambiwa kabla ya neno la Yahwe, ambalo aliloambiwa Eliya.
And he came Samaria and he struck down all those [who] remained of Ahab in Samaria until he had destroyed him according to [the] word of Yahweh which he had spoken to Elijah.
18 Kisha Yehu akawakusanya watu wote akwaambia, “Ahabu alimtumikia Baali kidogo, lakini Yehu atamtumikia sana.
And he gathered Jehu all the people and he said to them Ahab he served Baal a little Jehu he will serve him much.
19 Basi niitieni manabii wote wa Baali, wote wamwabuduo, na makuhani wake wote. Asikosekane mtu hata mmoja, kwa kuwa nina dhabihu kubwa nataka kutoa kwa Baali. Yeyote atakayeshindwa kuja hataishi.” Lakini Yehu alifanya haya kwa udanganyifu, kwa dhamira ya kuwaua wanaomwabudu Baali.
And therefore all [the] prophets of Baal all [those who] serve him and all priests his summon to me anyone may not he be missing for a sacrifice great [belongs] to me to Baal any [one] who he will be missing not he will live and Jehu he acted with guile so as to destroy [those who] serve Baal.
20 Yehu akasema, “Tengeni mda tuwe na mkutano kwa ajili ya Baali.” Hivyo wakalitangaza.
And he said Jehu consecrate an assembly to Baal and they proclaimed [it].
21 Kisha Yehu akatuma Israeli yote na wamwabuduo Baali waje, hivyo basi hakuna mtu hata mmoja ambaye aliacha kuja. Walikuja kwenye hekalu la Baali, na ilijaa kutoka mwanzo hadi mwisho.
And he sent Jehu in all Israel and they came all [those who] serve Baal and not he was left anyone who not he came and they went [the] house of Baal and it was filled [the] house of Baal mouth to mouth.
22 Yehu akamwambia yule mtu aliyekuwa anatunza kabati la nguo za makuhani, “Uwatolee mavazi wote wamwabuduo Baali.” Basi yule mtu akawatolea nguo.
And he said to [the one] who [was] over the wardrobe bring out clothing for all [those who] serve Baal and he brought out for them the clothing.
23 Basi Yehu akaingia pamoja na Yohonadabu mwana wa Rekabu kwenye nyumba ya Baali, na kisha akawaambia wanaomwabudu Baali, “Tafuteni na muhahakishe kwamba hakuna mtu hapa pamoja na ninyi kutoka watumishi wa Yahwe, lakini wamwabuduo Baali peke yao.”
And he went Jehu and Jonadab [the] son of Rechab [the] house of Baal and he said to [those who] serve Baal search and see lest there here with you [be] any of [the] servants of Yahweh that except [those who] serve Baal to alone them.
24 Kisha wakaenda kutoa dhabihu na sadaka ya kutekeza. Basi Yehu alichagua watu themanini ambao walikuwa wamesimama nje, na aliwaambia, Kama mtu yeyote miongoni mwa hawa watu ambao nimewaleta kwenye mikono yenu atoroke, yeyote atakayemwacha huyo mtu atoroke, maisha yake yatachukuliwa kwa ajili ya yule aliyeokoka.”
And they went to offer sacrifices and burnt offerings and Jehu he had stationed himself on the outside eighty man and he had said the man who he will escape from the men whom I [am] bringing on hands your life his in place of life his.
25 Hivyo kisha baada ya mda mfupi Yehu alipomaliza kutoa sadaka ya kutekezwa, akamwambia mlinzi na manahodha, “Ingieni na muwaue. Msimwache mtu yeyote atoke.” Basi waliwaua kwa makali ya upanga, na mlinzi na manahodha wakawatupa nje na kwenda kwenye chumba cha ndani cha nyumba ya Baali.
And it was when finished he - to offer the burnt offering and he said Jehu to the runners and to the officers go strike down them anyone may not he come out and they struck down them to [the] mouth of [the] sword and they threw [them] out the runners and the officers and they went to [the] city of [the] house of Baal.
26 Wakazitoa nguzo za mawe ambazo zilikuwa kwenye nyumba ya Baali, na kisha kuzichoma.
And they brought out [the] sacred pillars of [the] house of Baal and they burned it.
27 Kisha wakazivunja zile nguzo za Baali, na kuiharibu nyumba ya Baali na kuifanya choo, ambacho kipo hadi leo.
And they pulled down [the] sacred pillar of Baal and they pulled down [the] house of Baal and they made it (outhouses *Q(K)*) until this day.
28 Hivi ndivyo ambavyo Yehu alivyomharibu muabudu Baali kutoka Israeli.
And he destroyed Jehu Baal from Israel.
29 Lakini Yehu hakuacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambayo ilfanya Israeli kutenda dhambi-ambayo ni, kumwabudu ndama wa dhahabu katika Betheli na Dani.
Only [the] sins of Jeroboam [the] son of Nebat which he caused to sin Israel not he turned aside Jehu from after them [the] calves of gold which [were] Beth-el and which [were] in Dan.
30 Hivyo Yahwe akamwambia Yehu, “Kwa kuwa umefanya vema kwa kufanya yaliyo sahihi kwenye macho yangu, na kumailiza kwenye nyumba ya Ahabu kulingana na yote yaliyokuwa kwenye moyo wangu, uzao wako utakaa kwenye kiti cha Israeli hadi kizazi cha nne.”
And he said Yahweh to Jehu because that you have done well by doing the right in view my according to all that [was] in heart my you have done to [the] house of Ahab descendants of [the] fourth [generation] they will sit of you on [the] throne of Israel.
31 Lakini Yehu hakujali kutembea kwenye sheria ya Yahwe, Mungu wa Israeli, kwa moyo wake wote. Hakugeuka kutoka kwenye dhambi za Yeroboamu, ambayo iliwafanya Israeli kutende dhambi.
And Jehu not he took care to walk in [the] law of Yahweh [the] God of Israel with all heart his not he turned aside from on [the] sins of Jeroboam which he caused to sin Israel.
32 Siku zile Yahwe akaanza kupunguza mikoa ya Israeli, na Hazaeli kuwashinda Waisraeli mipakani mwa Israeli,
In the days those he began Yahweh to cut off in Israel and he struck down them Hazael in all [the] territory of Israel.
33 kutoka Yordani upande wa mashariki, nchi yote ya Gileadi, Wagadi, na Wareubeni, na Wamanase, kutoka Aroeri, alipo karibu na bonde la Arnoni, kupita Geleadi hadi Bashani.
From the Jordan [the] rising of the sun all [the] land of Gilead the Gadite[s] and the Reubenite[s] and the Manassite[s] from Aroer which [is] at [the] wadi of Arnon and Gilead and Bashan.
34 Kama kwa mambo mengine yamhusuyo Yehu, na yote aliyoyafanya, na ushujaa wake, je hayakuandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli?
And [the] rest of [the] matters of Jehu and all that he did and all might his ¿ not [are] they written on [the] scroll of [the] matters of the days of [the] kings of Israel.
35 Yehu akalala na wazee wake, na walimzika katika Samaria. Kisha Yehoahazi mwanaye akawa mfalme katika sehemu yake.
And he lay down Jehu with ancestors his and people buried him in Samaria and he became king Jehoahaz son his in place of him.
36 Mda ambao Yehu alitawala juu ya Israeli katika Samaria ulikuwa miaka ishini na nane.
And the days which he reigned Jehu over Israel [were] twenty and eight year[s] in Samaria.