< 1 Timotheo 4 >
1 Sasa Roho anasema waziwazi kwamba katika nyakati zijazo baadhi ya watu wataiacha imani na kuwa makini kusikiliza roho zidanganyazo na mafundisho ya kipepo yatakayofundishwa
NOW the Spirit speaketh expresly, that in the latter days some will apostatise from the faith, giving heed to spirits of delusion, and doctrines of devils;
2 katika uongo na unafiki. Dhamiri zao zitabadilishwa.
men who teach lies with hypocrisy; and have their own consciences cauterised;
3 Watawazuia kuoa na kupokea vyakula ambavyo Mungu aliviumba vitumiwe kwa shukrani miongoni mwao waaminio na wenye kuijua kweli.
prohibiting marriage, and enjoining abstinence from particular meats, which God created to be received with thanksgiving by the faithful, and those who acknowledge the truth.
4 Kwa sababu kila kitu ambacho Mungu amekiumba ni chema. Hakuna ambacho tunapokea kwa shukrani kinastahili kukataliwa.
For every creature of God is good, and none to be rejected, if used with thanksgiving:
5 Kwa sababu kinatakaswa kupitia neno la Mungu na kwa njia ya maombi.
for it is sanctified by the word of God and prayer.
6 Kama utayaweka mambo haya mbele ya ndugu, utakuwa mtumishi mzuri wa Yesu Kristo. Kwa sababu umestawishwa kwa maneno ya imani na kwa mafundisho mazuri ambayo umeyafuata.
If thou suggest these truths to the brethren, thou shalt be a good minister of Jesus Christ, nourished up in the words of faith and sound doctrine, whereunto thou hast attained.
7 Lakini zikatae hadithi za kidunia ambazo zinapendwa na wanawake wazee. Badala yake, jifunze mwenyewe katika utaua.
But profane and antiquated fables reject, but exercise thyself unto godliness.
8 Kwa maana mazoezi ya mwili yafaa kidogo, bali utauwa wafaa sana kwa mambo yote. Hutunza ahadi kwa maisha ya sasa na yale yajayo.
For bodily exercise is of little advantage, but godliness is profitable for all things, having the promise of the life which now is, and of that which is to come.
9 Ujumbe huu ni wakuaminiwa na unastahili kukubaliwa kabisa.
This is a faithful saying, and deserving all acceptance.
10 Kwa kuwa ni kwa sababu hii tunataabika na kufanya kazi kwa bidii sana. Kwa kuwa tunao ujasiri katika Mungu aliye hai, ambaye ni Mwokozi wa watu wote, lakini hasa kwa waaminio.
For therefore do we labour and are exposed to abuse, because we have hoped in the living God, who is the Saviour of all men, especially of the faithful.
11 Uyaseme na kuyafundisha mambo haya.
Announce and teach these things.
12 Mtu yeyote asiudharau ujana wako. Badala yake, uwe mfano kwa wote waaminio, katika usemi, mwenendo, upendo, uaminifu, na usafi.
Let no man despise thy youth; but be a pattern of the faithful, in discourse; in conduct, in love, in spirit, in faith, in purity.
13 Mpaka nitakapokuja, dumu katika kusoma, katika kuonya, na katika kufundisha.
Till I come, apply to reading, to exhortation, to teaching.
14 Usiipuuze karama iliyomo ndani yako, ambayo ulipewa kupitia unabii, kwa kuwekewa mikono na wazee.
Neglect not the gift which is in thee, which was given thee by prophecy, with imposition of the hands of the presbytery.
15 Uyajali mambo haya. Ishi katika hayo ili kukua kwako kuwe dhahiri kwa watu wote. Zingatia sana mwenendo wako na mafundisho.
Let these things be thy care; be wholly devoted to them; that thy progress may be evident to all men.
16 Dumu katika mambo haya. Maana kwa kufanya hivyo utajiokoa mwenyewe na wale wanaokusikiliza.
Take heed unto thyself, and to thy doctrine; abide in them: for so doing thou shalt both save thyself, and those who hear thee.