< 1 Samweli 10 >

1 Ndipo Samweli akachukua chupa ya mafuta, akayamimina juu ya kichwa cha Sauli, na akambusu. Akasema, “Je, Mungu hajakutia mafuta uwe mtawala juu ya urithi wake?
Forsothe Samuel took `a vessel of oyle, and schedde out on the heed of Saul, and kisside hym, and seide, Lo! the Lord hath anoyntid thee in to prince on hys eritage; and thou schalt delyuere his puple fro the hond of his enemyes, that ben `in his cumpas. And this a tokene to thee, that the Lord hath anoyntid thee in to prince;
2 Utakapoondoka kwangu leo, utawaona wanaume wawili na kaburi la Raheli, katika nchi ya Benyamini hapo Selsa. Watu hao watakuambia, 'Wale punda mliokuwa mkiwatafuta wamepatikana. Sasa, Baba yako ameacha kuwatunza punda, na ana hofu juu yenu, anasema, “Nitafanya nini kuhusu mwanangu?”
whanne thou schalt go fro me to day, thou schalt fynde twei men bisidis `the sepulcre of Rachel, in `the endis of Beniamyn, in myddai, clensynge grete dichis; and thei schulen seie to thee, The femel assis ben foundun, whiche thou yedist to seke; and while the assis ben lefte, thi fadir is bisy for you, and seith, What schal Y do of my sone?
3 Kisha utakwenda mbele kutoka hapo, na utafika katika mwaloni wa Tabori. Utakutana na watu watatu hapo wakienda kwa Mungu huko Betheli, mmoja akibeba wana-mbuzi watatu, mwingine akibeba mikate mitatu, na mwingine akibeba kiriba cha divai.
And whanne thou hast go fro thennus, and hast passid ferthere, and hast come to the ook of Tabor, thre men, stiynge to God in to Bethel, schulen fynde thee there, o man berynge thre kydis, and another man berynge thre kakis of breed, and an other man berynge a galoun of wyn.
4 Watawasalimu na watawapatia mikate miwili, kutoka mikononi mwao.
And whanne thei han gret thee, thei schulen yyue to thee twei loues, and thou schalt take of `the hond of hem.
5 Baada ya hayo, utafika katika mlima wa Mungu, mahali ilipo ngome ya Wafilisti. Utakapofika mjini, utakutana na kundi la manabii wakiteremka chini kutoka mahali pa juu wakiwa na kinanda, tari, kinubi na filimbi mbele yao; na watakuwa wakitabiri.
After these thingis thou schalt come in to the `hil of the Lord, where is the stondyng, that is, forselet, of Filisteis; and whanne thou schalt entre in to the citee, there thou schalt haue metynge thee the flok of prophetis comynge doun fro the hiy place, and a sautree, and tympane, and pipe, and harpe bifor hem, and hem prophesiynge.
6 Roho ya BWANA itakujaza, nawe utatabiri pamoja nao, na utabadilishwa na kuwa mtu tofauti.
And the Spirit of the Lord schal skippe in to thee, and thou schalt prophecie with hem, and thou schalt be chaungid in to another man.
7 Basi, ishara hizi zikikufikia, fanya lolote ambalo mikono yako itaona ifanye, kwa sababu Mungu yu pamoja nawe.
Therfor whanne alle thesse signes bifallen to thee, do thou, what euer thingis thin hond fyndith, `that is, dispose thee to regne comelili and myytily, for the Lord is with thee.
8 Nenda ushuke mbele yangu hadi Gilgali. Kisha nitakufuata huko nitoe dhabihu za kuteketezwa na kutoa dhabihu za amani. Nisubiri kwa muda wa siku saba hadi nije kwako na nikuoneshe unachopaswa kufanya.”
And thou schalt go doun bifor me in to Galgala; for Y schal come doun to thee, that thou offre an offryng, and offre pesible sacrifices; bi seuene daies thou schalt abide, til I come to thee, and shewe to thee what thou schal do.
9 Sauli alipotega mgongo amuache Samweli, Mungu akampa moyo mwingine. Ndipo ishara zote hizi zikatimia siku hiyo.
Therfor whanne Saul hadde turnede awei his schuldre to go fro Samuel, God chaungide another herte to Saul, and alle these signes camen in that dai.
10 Walipofika mlimani, kundi la manabii lilikutana naye, na Roho ya Mungu ikamjilia kwa nguvu ili atabiri pamoja nao.
And thei camen to the forseid hil, and lo! a cumpeny of prophetis metynge hym; and the Spirit of the Lord `scippide on hym, and he propheciede in the myddis of hem.
11 Kila mtu aliyemfahamu kabla hajamwona akitabiri pamoja na manabii, watu waliambizana wao kwa wao:”Kitu gani kimempata mtoto wa Kishi? Hivi Sauli ni mmoja wa manabii siku hizi?”
Sotheli alle men, that knewen hym yisterdai and the thrid dai ago, sien that he was with the prophetis, and that he prophesiede, and thei seiden togidere, What thing bifelde to the sone of Cys? Whether also Saul is among prophetis?
12 Mtu mmoja kutoka eneo hilo akajibu, “Na ni nani baba yao?” Kwa sababu ya jambo hili, ukawapo msemo, “Hivi Sauli naye ni mmoja wa manabii?”
And o man answeride to another man, and seide, And who is `his fadir? Therfor it was turned in to a prouerbe, Whether also Saul is among prophetis?
13 Alipomaliza kutabiri, akafika mahali pa juu.
Forsothe Saul ceside to prophesie, and he cam to an hiy place.
14 Ndipo baba yake mdogo na akamuuliza Sauli na mtumishi wake, “Mlienda wapi?” Naye akamjibu, “Kuwatafuta punnda; tulipoona kwamba hatuwezi kuwapata, tukaenda kwa Samweli.”
And the brothir of `the fadir of Saul seide to hym, and to his child, Whidur yeden ye? And thei answeriden, To seke the femal assis; and whanne we founden `not thoo, we camen to Samuel.
15 Baba yake mdogo akasema, “Tafadhali niambie kile alichosema kwako Samweli,”
And the brother of his fadir seide to hym, Schewe thou to me what Samuel seide to thee.
16 Sauli akamjibu baba yake mdogo, “Alituambia waziwazi kwamba punda wamepatikana.” Lakini kuhusu swala la ufalme alilosema Samweli hakumwambia.
And Saul seide to `the brother of hys fadir, He schewide to vs, that the femal assis weren foundun. Sotheli Saul schewide not to hym of the word of rewme, `which word Samuel spak to hym.
17 Basi Samweli aliwaita watu pamoja huko Mispa.
And Samuel clepide togidere the puple to the Lord in Masphat;
18 Akwaambia watu wa Israeli, “Hivi ndivyo BWANA, Mungu wa Israeli asemavyo: 'Niliwatoa Israeli kutoka Misri, na niliwaokoa kutoka nchi ya Wamisri, na kutoka mkono wa falme zote zilizowaonea.'
and he seide to the sones of Israel, The Lord God of Israel seith these thingis, Y ledde Israel out of the lond of Egipt, and Y delyuerede you fro the hond of Egipcians, and fro the hond of alle kyngis that turmentiden you.
19 Lakini leo mmemkataa Mungu wenu, awaokoaye kutoka kwenye majanga na mahangaiko; na mmemwambia, ' Tuwekee mfalme juu yetu; Sasa jihudhurisheni wenyewe mbele za BWANA kwa kabila na jamaa zenu.”
Forsothe to day ye han caste awei youre Lord God, which aloone sauyde you fro alle youre yuelis and tribulaciouns; and ye seiden, Nay, but ordeyne thou a kyng on vs. Now therfor stonde ye bifor the Lord bi youre lynagis, and bi meynees.
20 Kisha Samweli akawaleta kabila zote za Isareli karibu, na kulichagua kabila la Benyamini.
And Samuel settide to gidere alle the lynages of Israel, and lot felde on the lynage of Beniamyn.
21 Akawasogeza karibu kabila la Benyamini kwa kufuata jamaa zao; na jamaa ya Wamatri ikachaguliwa; na Sauli mwana wa Kishi akachaguliwa. Lakini walipokwenda kumtafuta, hakuweza kuonekana.
And he settide togidere the lynage of Beniamyn, and the meynees therof; and lot felde on the meynees of Mathri, and it cam `til to Saul, the son of Cys. Therfor thei souyten hym, and he was not foundun there.
22 Kisha watu walitaka kumuuliza Mungu maswali zaidi, “Bado yupo mtu mwingine ajaye?” BWANA akajibu, “Yeye mwenyewe kajificha kwenye mizigo.”
And aftir these thingis thei counseliden the Lord, whether Saul schulde come thidur. And the Lord answeride, Lo! he is hid at hoom.
23 Wakaenda mbio na kumleta Sauli kutoka humo. Aliposimama kati yao, alikuwa mrefu kuliko watu wote kuanzia mabega yake kwenda juu.
Therfor thei runnen, and token hym fro thennus; and he stood in the myddil of the puple, and was hiyere than al the puple fro the schulder and `aboue.
24 Kisha Samweli akawaambia watu, “Je, mnamuona mtu ambaye BWANA amemchagua? Hakuna mtu kama yeye kati ya watu wote.” Watu wote wakapiga Kelele, “Mfalme na aishi”
And Samuel seide to al the puple, Certis ye seen whom the Lord hath chose; for noon in al the puple is lijk hym. And al the puple cryede, and seide, Lyue the kyng!
25 Ndipo Samweli akawaambia watu desturi na sheria za ufalme, akaziandika katika kitabu, na kuziweke mbele za BWANA. Baadaye Samweli akawaruhusu watu waondoke kila mtu aende nyumbani kwake.
Forsothe Samuel spak to the puple the lawe of rewme, and wroot in a book, and puttide vp bifor the Lord. And Samuel dilyuerede al the puple, ech man in to his hows;
26 Sauli pia alienda nyumbani kwake huko Gibea, akiwa na baadhi ya watu wenye nguvu, wenye mioyo iliyoguswa na Mungu.
but also Saul yede in to his hous in to Gabaath; and the part of the oost yede with hym, whose hertis God hadde touchid.
27 Lakini baadhi ya watu wasiofaa walisema, “Huyu mtu atatuokoaje?” Watu hawa walimdharau Sauli na hawakumletea zawadi zozote. Lakini Sauli alinyamaza kimya.
Forsothe the sones of Belyal seiden, Whether this man may saue vs? And thei dispisiden hym, and brouyten not yiftis, `that is, preisyngis, to him; forsothe he `dissymelide hym to here.

< 1 Samweli 10 >