< 1 Wafalme 7 >
1 Ilimchukua Sulemani miaka kumi na tatu kujenga ikulu yake.
Solomon was thirteen years building a house for himself till it was complete.
2 Aliijenga ikulu iliyoitwa mwitu wa Lebanoni. Urefu wake ulikuwa mita 46, na upanawake ulikuwa mita 23, na kimo chake kilikuwa mita 14. Nayo ilikuwa na safu nne ya nguzo za mierezi na mithili ya mwerezi juu ya nguzo.
And he made the house of the Woods of Lebanon, which was a hundred cubits long and fifty cubits wide and thirty cubits high, resting on four lines of cedar-wood pillars with cedar-wood supports on the pillars.
3 Paa la ikulu lilikuwa la mwerezi ambalo lilikaa juu ya mihimili. Mihili hiyo ilikuwa imeshikiliwa na nguzo. Kulikuwa na mihimili arobaini na tano, ambayo ilikuwa katika safu kumi na tano.
And it was covered with cedar over the forty-five supports which were on the pillars, fifteen in a line.
4 Nayo mihimili ilikuwa safu tatu, na kila dirisha lilikabili dirisha lingine katika madaraja matatu.
There were three lines of window-frames, window facing window in every line.
5 Milango yote na miimo ilitengenezwa kwa mraba, na madirisha yalikuwa yakikabiliana katika madaraja matatu
And all the doors and windows had square frames, with the windows facing one another in three lines.
6 Akatengeneza baraza lenye uerfu wa mita 23 na upana wa mita 14. Mbele yake kulikuwa na ukumbi ulioezekwa.
And he made a covered room of pillars, fifty cubits long and thirty cubits wide, and ... with steps before it.
7 Sulemani akajenga baraza yenye kiti cha enzi ambacho alitolea hukumu ya haki. Nayo ilikuwa imeezekwa kwa mwerezi kutoka sakafu moja hadi nyingine.
Then he made a covered room for his high seat when he gave decisions; this was the covered room of judging; it was covered with cedar-wood from floor to roof.
8 Nyumba ya Sulemani ambayo alikusudia kuishi, katika behewa nyingine ndani ya sehemu ya chini ya ikulu, ilitengenezwa kwa kazi hiyo hiyo. Pia alimjengea binti wa Farao nyumba kama hii, ambaye alikuwa mke wake
And the house for his living-place, the other open square in the covered room, was made in the same way. And then he made a house like it for Pharaoh's daughter, whom Solomon had taken as his wife.
9 Majengo haya yalipmbwa kwa vitu vya thamaini, mawe ya thamani, yaliyochongwa na kukatwa kwa msimeno kufuata vipimo sahihi na kulainishwa pande zote. Mawe ya namna hii ndiyo yale yaliyotumika kuanzia kwenye msingi hadi juu, pia na nje hadi kwenye baraza.
All these buildings were made, inside and out, from base to crowning stone, and outside to the great walled square, of highly priced stone, cut to different sizes with cutting-instruments.
10 Msingi ulijengwa kwa mawe makubwa sana na ya thamani yenye urefu wa mita 3. 7 na mengine mita 4. 8.
And the base was of great masses of highly priced stone, some ten cubits and some eight cubits square.
11 Kwa juu ilipambwa kwa, mawe ya thamani yaliyochongwa sawa sawa kwa msimeno na kwa mihimili ya mierezi.
Overhead were highly priced stones cut to measure, and cedar-wood.
12 Na behewa kubwa iliyokuwa ikizunguka ikulu ilikuwa na safu tatu za mawe yaliyokatwa na safu moja ya mihimili ya mierezi kama ilivyo kwenye baraza la ndani la hekalu la BWANA na ule ukumbi wa hekalu.
The great outer square all round was walled with three lines of squared stones and a line of cedar-wood boards, round about the open square inside the house of the Lord and the covered room of the king's house.
13 Mfalme Sulemani alituma watu kumleta Huramu kutoka Tiro.
Then King Solomon sent and got Hiram from Tyre.
14 Huramu alikuwa mwana wa mjane wa kabila ya Naftali; baba yake alikuwa mtu wa Tiro, mfua shaba. Huramu alikuwa mwingi wa hekima na ufahamu na stadi za kufanya kazi kubwa za shaba. Aliletwa kwa mfalme ili kufanya kazi zilizohusiana na shaba kwa mfalme.
He was the son of a widow of the tribe of Naphtali, and his father was a man of Tyre, a worker in brass; he was full of wisdom and knowledge and an expert worker in brass. He came to King Solomon and did all his work for him.
15 Huramu alizilemba zile nguzo mbili za shaba, kila moja ilikuwa na kimo cha mita 8. 3 na mzingo wa mita 5. 5.
He it was who made the two brass pillars; the first pillar was eighteen cubits high, and a line of twelve cubits went round it; and the second was the same.
16 Akatengeneza taji mbili za shaba za kuwekwa juu ya zile nguzo. Kimo cha kila taji ilikuwa mita 2. 3.
And he made the two crowns to be put on the tops of the pillars, of brass made soft in the fire; the crowns were five cubits high.
17 Kulikuwa na nyavu za kuwa kama kazi ya kusuka, na masongo ya mikufu, kwa ajili ya kuvipamba vile vichwa vya nguzo, nayo yailikuwa saba kwa kila kichwa.
There were nets of open-work for the crowns on the tops of the pillars, a net of open-work for one and a net of open-work for the other.
18 Kwa hiyo Huramu akafanya safu mbili za komamanga kuzunguka vile vichwa vya nguzo ili kuvipamba vile vichwa.
And he made ornaments of apples; and two lines of apples all round over the network, covering the crowns of the pillars, the two crowns in the same way.
19 Zile taji kwenye vile vichwa vya nguzo za ukumbi zilikuwa zimepambwa kwa maua, yenye vimo vya mita 1. 8.
The crowns on the tops of the pillars were ornamented with a design of flowers, and were four cubits across.
20 Hizo taji kwenye hizo nguzo mbili kwenye vichwa vyake, karibu yake kulikuwa na makomamanga mia mbili yote yakiwa kwenye safu.
And there were crowns on the two pillars near the round part by the network, and there were two hundred apples in lines round every crown.
21 Alisimamisha nguzo kwenye ukumbi wa hekalu. Ile nguzo ya kuume akaipa jina la Yakini, na ile ya kushoto akaipa jina la Boazi.
He put up the pillars at the doorway of the Temple, naming the one on the right Jachin, and that on the left Boaz.
22 Na juu ya zile nguzo kulikuwa na mapambo kama maua. Hivyo ndivyo zile nguzo zilivyotengenezwa.
The tops of the pillars had a design of flowers; and the work of making the pillars was complete.
23 Tena akafanya bahari ya kusubu ya, yenye mita 2. 3 kutoka ukingo hadi ukingo, kimo chake kilikuwa mita 4. 6, mziingo wake ulikuwa mita 13. 7.
And he made a great metal water-vessel ten cubits across from edge to edge, five cubits high and thirty cubits round.
24 Na chini ya ile bahari kulikuwa na vibuyu vilivyoizunguka, vilikuwa vibuyu kumi na nane katika kila mita, vilivyowekwa katika kila hicho kipande wakati bahari inapokuwa kalibu.
And under the edge of it, circling it all round for ten cubits, were two lines of flower buds, made together with it from liquid metal.
25 Bahari ikakaa juu ya makisai kumi na mbili, tatu, zilitazama kaskazini, tatu zikitazama magharibi, tatu zikitazama kusini na tatu zikitazama kaskazini. Ile bahari iliwekwa juu yao, na pande zao zote za nyuma zilikuwa ndani.
It was supported on twelve oxen, with their back parts turned to the middle of it, three of them facing to the north, three to the west, three to the south, and three to the east; the vessel was resting on top of them.
26 Bahari ilikuwa nene kama upana wa mkono, na ukingo wake ulikuwakama ukingo wa kikombe, kama ua la yungi huingia bathi elfu mbili za maji.
It was as thick as a man's open hand, and was curved like the edge of a cup, like the flower of a lily: it would take two thousand baths.
27 Huramu akatengeneza makalio kumi ya shaba. Kila kalio lilkuwa na urefu wa mita 1. 8, upana wa mita 1. 8, na kimo cha mita 1. 3.
And he made ten wheeled bases of brass; every one four cubits long, four cubits wide, and three cubits high.
28 Hivi ndivyo kazi za makalio zilivyofanywa. Yalikuwa na papi ambazo zilikaa kati kati ya vipandio,
And the bases were made in this way; their sides were square, fixed in a framework;
29 na juu ya papi na vipandio kulikuwa na simba, makisai, na makerubi. Chini na juu simba kulikuwa na masongo ya kazi ya kufuliwa.
And on the square sides between the frames were lions, oxen, and winged ones; and the same on the frame; and over and under the lions and the oxen and the winged ones were steps.
30 Kila kalio lilikuwa na magurudumu ya shaba na vipini, na pande zake nne na miguu yake minne ilikuwa na mataruma chini ya birika. Chini ya birika yalikuweko mataruma ya kusubu yenye masongo katika kila upande.
Every base had four wheels of brass, turning on brass rods, and their four angles had angle-plates under them; the angle-plates under the base were of metal, and there were ornaments at the side of every one.
31 Na kinywa chake kilikuwa cha kuviringana, chenye upana wa sentimita araobaini na sita, na ile taji ilikuwa na sentimita ishirini na tatu. Na kinywa chake kilikuwa na nakshi, na papi zake zilikuwa za mraba, na wala siyo za mvringo.
The mouth of it inside the angle-plate was one cubit across; it was round like a pillar, a cubit and a half across; it had designs cut on it; the sides were square, not round.
32 Yale magurudumu mawili yalikuwa chini ya papi, na mikono ya magurudumu yalikuwa ndani ya makalio. Kimo cha yale magurudumu kilikuwa sentimeta sitini na tisa.
The four wheels were under the frames, and the rods on which the wheels were fixed were in the base; the wheels were a cubit and a half high.
33 Yale magurudumu yalikuwa kama ya gari. Mikono yake, na maduara, matindi yake, na vipande vya ndani vyote vilikuwa vya kusubu.
The wheels were made like carriage-wheels, the rods on which they were fixed, the parts forming their edges, their rods and the middle points of them, were all formed out of liquid metal.
34 Kulikuwa na mataruma manne katika pande zake nne za makalio, yaliyokuwa yameshikamanishwa na kalio lenyewe.
And there were four angle-plates at the four angles of every base, forming part of the structure of the base.
35 Juu ya makalio kulikuwa na duara yenye kina cha sentimita ishirini na tatu, na juu ya makalio mashikio yake na papi zake zikiwa zimeshikamanishwa.
And at the top of the base there was a round vessel, half a cubit high;
36 Juu ya mabamba na papi zake Huramu akachora makerubi, simba, na mitende ambayo ilifunika nafasi ya juu, nayo ilikuwa imezungukwa na masongo.
In the spaces of the flat sides and on the frames of them, he made designs of winged ones, lions, and palm-trees, with ornamented edges all round.
37 Alitengeneza makalio kumi kwa jinsi hii. Yote yalikuwa yametengenezwa kwa kufanana, na yalikuwa ya vipimo sawa, na sura inayofanana.
All the ten bases were made in this way, after the same design, of the same size and form.
38 Huramu akatengeneza birika kumi za shaba. Birika moja liliweza kubeba bathi arobaini za maji. Kila birika lilikuwa mita 1. 8 toka birika moja hadi jingine na kulikuwa na birika moja katika kila kalio kati ya yale kumi.
And he made ten brass washing-vessels, everyone taking forty baths, and measuring four cubits; one vessel was placed on every one of the ten bases.
39 Alitengeneza makalio tano upande wa kusini unaoelekea upande wa hekalu. Akatengeneza bahari katika upande wa mashariki, ukielekea upande wa kusini wa hekalu.
And he put the bases by the house, five on the right side and five on the left; and he put the great water-vessel on the right side of the house, to the east, facing south.
40 Huramu akatengeneza birika na koleo na besini la kunyunyizia. Kisha akamaliza kazi yote aliyofanya kwa mfalme Sulemani katika hekalu la BWANA:
And Hiram made the pots and spades and the basins. So Hiram came to the end of all the work he did for King Solomon in the house of the Lord:
41 Zile nguzo mbili, na lile besini lakawa kama taji ambalo lilikuwa juu ya zile nguzo, na nyavu mbili za mapambo za kufunika zile besini mbili za kuwa kama taji zilizokuwa juu ya nguzo.
The two pillars and the two cups of the crowns which were on the tops of the two pillars; and the network covering the two cups of the crowns on the tops of the pillars,
42 Kisha akatengeneza makomamanga mia nne kwa ajili ya zile nyavu mbili za mapambo: safu mbili za makomamamanga kwa kila kazi ya nyavu kwa ajili ya kufunikia zile besini mbili kama taji iliyo juu ya nguzo,
And the four hundred apples for the network, two lines of apples for every network, covering the two cups of the crowns on the pillars;
43 yale makalio kumi, na birika kumi kwenye makalio.
And the ten bases, with the ten washing-vessels on them;
44 Akatengeneza bahari na makisai kumi chini yake;
And the great water-vessel, with the twelve oxen under it;
45 na masufuria, koleo, birika na vyombo vingine vyote. Huramu akivitengeneza kwa shaba iliyosuguliwa, kwa ajili ya mfalme Sulemani, na kawa ajili ya hekalu la BWANA.
And the pots and the spades and the basins; all the vessels which Hiram made for King Solomon, for the house of the Lord, were of polished brass.
46 Mfalme alivisubu katika uwanda wa Yorodani, katika udongo mfinyanzi kati ya Sukoti na Zarethani.
He made them of liquid metal in the lowland of Jordan, at the way across the river, at Adama, between Succoth and Zarethan.
47 Sulemani hakuvipima vyombo vyote kwa sababu vilikuwa vingi mno kuvipima, na kwa sababu uzito wa shaba ulikuwa hauwezi kupimwa.
The weight of all these vessels was not measured, because there was such a number of them; it was not possible to get the weight of the brass.
48 Sulemani akatengeneza mapambo yote yaliyokuwa kwenye hekalu la BWANA kwa kutumia dhahabu: Ile madhabahu ya dhahabu na ile meza ambayo iliwekwa mikate ya wonyesho.
And Solomon had all the vessels made for use in the house of the Lord: the altar of gold and the gold table on which the holy bread was placed;
49 Vile vinara vya dhahabu, ambavyo vitano vilikuwa upande wa kulia na vitano mkono wa kushoto, mbele ya chumba cha ndani, vilikuwa vya dhahabu safi, na maua, na taa na koleo zilikuwa za dhahabu.
And the supports for the lights, five on the right side and five on the left before the inmost room, of clear gold; and the flowers and the lights and all the instruments of gold;
50 Vile vikombe, na makasi, mabakuri, na vijiko, na vyetezo vyote vilikuwa vimetengenezwa kwa dhahabu safi. na bawaba za dhahabu za milango ya ndani, ambazoo ndio mahali patakatifu sana, na milango ya ukumbi mkubwa, vyote vilitengenezwa kwa dhahabu.
And the cups and the scissors and the basins and the spoons and the fire-trays, all of gold; and the pins on which the doors were turned, the doors of the inner house, the most holy place, and the doors of the Temple, all of gold.
51 Kwa njia hii, kazi yote ambayo mfalme Sulemani alifanya kwa ajili ya hekalu ilimalizika. Kwa Sulemani akaviingiza ndani yake vitu vile vilivyokuwa vimewekwa wakfu na Daudi, baba yake, na fedha na dhahabu, na mapambo, na vile vya ndani ya hazina ya BWANA.
So all the work King Solomon had done in the house of the Lord was complete. Then Solomon took the holy things which David his father had given, the silver and the gold and all the vessels, and put them in the store-houses of the house of the Lord.