< 1 Wafalme 20 >
1 Beni Hadadi mfalme wa Shamu akakusanya jeshi lake lote pamoja. Kulikuwa na wafalme thelathini na mbili wasaidizi pamoja naye, na magari na farasi. Akapanda, akaihusuru Samaria na kupigana nayo.
Then Ben-hadad the King of Aram assembled all his armie, and two and thirtie Kings with him, with horses, and charets, and went vp and besieged Samaria, and fought against it.
2 Akatuma wajumbe katika mji kwa Ahabu mfalme wa Israeli, akamwambia, “Beni Hadadi anasema hivi:
And he sent messengers to Ahab King of Israel, into the citie,
3 Fedha zako na dhahabu zako ni zangu. Pia wake zako na watoto, wale wazuri, sasa ni wangu.”
And sayd vnto him, Thus sayth Ben-hadad, Thy siluer and thy golde is mine: also thy women, and thy fayre children are mine.
4 Mfalme wa Israeli akajibu akasema, “Na iwe kama unavyosema, bwana wangu, mfalme. Mimi pamoja na vile nilivyo navyo ni mali yako.”
And the King of Israel answered, and sayd, My lord King, according to thy saying, I am thine, and all that I haue.
5 Wale wajumbe wakaja tena wakasema, “Beni Hadadi anasema hivi, 'Nilituma neno kwako nikisema kwamba lazima ukabidhi kwangu fedha zako, dhahabu zako, wake zako na watoto wako.
And when the messengers came againe, they said, Thus commandeth Ben-hadad, and saith, When I shall send vnto thee, and command, thou shalt deliuer me thy siluer and thy golde, and thy women, and thy children,
6 Lakini kesho nitatuma watumishi wangu kwako wakati kama huu, nao wataichunguza nyumba yako na nyumba za watumishi wako. Nao watatia mikononi mwao na kukichukua kila wakipendacho machoni mwao.'”
Or els I will sende my seruants vnto thee by to morow this time: and they shall search thine house, and the houses of thy seruants: and whatsoeuer is pleasant in thine eyes, they shall take it in their handes, and bring it away.
7 Ndipo mfalme wa Israeli akawaita wazee wote wa nchi pamoja akawaambia, ''Hebu angalieni jinsi huyu mtu anavyotafuta matatizo. Amenitumia ujumbe kwamba anataka kuchukua wake zangu, watoto wangu, fedha na dhahabu zangu, nami sijamkatalia.”
Then the King of Israel sent for all the Elders of the land, and sayd, Take heede, I pray you, and see how he seeketh mischiefe: for he sent vnto me for my wiues, and for my children, and for my siluer, and for my golde, and I denyed him not.
8 Wazee wote na watu wote wakamwambia Ahabu, “Usimsikilize wala kukubaliana na matakwa yake.”
And all the Elders, and all the people sayd to him, Hearken not vnto him, nor consent.
9 Ahabu akawaambia wajumbe wa Beni Hadadi, “Mwambieni bwana wangu mfalme kwamba, 'Ninakubaliana na kila kitu ambacho kwanza uliwatuma watumishi wako kufanya kwangu, lakini sikubaliani na matakwa yako haya ya pili.'” Wale watumishi wa Beni Hadadi wakaondoka wakampelekea mrejesho Beni Hadadi.
Wherefore hee sayde vnto the messengers of Ben-hadad, Tell my lorde the King, All that thou didddest sende for to thy seruant at the first time, that I will doe, but this thing I may not do. And the messengers departed, and brought him an answere.
10 Naye Beni Hadadi akatuma tena majibu yake kwa Ahabu, akaisema, “basi miungu inifanyie hivyo na zaidi, kama hata mavumbi ya Samaria yatawatosheleza watu watu wote wanaonifuata kuchukua kila mmoja angalau konzi mkononi mwake.”
And Ben-hadad sent vnto him, and sayde, The gods do so to me and more also, if the dust of Samaria be ynough to all the people that follow me, for euery man an handfull.
11 Naye mfalme wa Israeli akamjibu akisema, “Mwabieni Beni Hadadi, 'Hakuna abebaye silaha yake, atakayejivuna kama wakati wa kuishusha.”'
And the King of Israel answered, and sayd, Tell him, Let not him that girdeth his harneis, boast himselfe, as he that putteth it off.
12 Beni Hadadi aliusikia ujumbe huu wakati alipokuwa akinywa, yeye na wafalme walikuwa pamoja naye waliokuwa kwenye mahema yao. Beni Hadadi akayaamuru majaeshi yake, “Jipangeni katika sehemu zenu kwa ajili ya vita.” Kwa hiyo wakajiandaa kivita ili kuuvamia mji.
And when he heard that tidings, as he was with the Kings drinking in the pauilions, he sayd vnto his seruants, Bring forth your engines, and they set them against the citie.
13 Tazama, nabii akaja kwa Ahabu mfalme wa Israeli akasema, “BWANA asema, 'Je umeliona hili jeshi kubwa? Tazama, nitaliweka katika mkono wako leo, nawe utatambua kuwa mimi ni BWANA.'”
And beholde, there came a Prophet vnto Ahab King of Israel, saying, Thus sayeth the Lord, Hast thou seene all this great multitude? beholde, I will deliuer it into thine hande this day, that thou mayest knowe, that I am the Lord.
14 Naye Ahabu akajibu, ''kwa nani? BWANA akamjibu akasema, “kwa kuwatumia viijana wanaotumikia maliwali wa wilaya.” kisha Ahabu akasema, “Ni nani atakayepewa hiyo vita?' BWANA akamwambia, “wewe.”
And Ahab sayd, By whome? And he sayde, Thus sayth the Lord, By the seruants of the princes of the prouinces. He sayde againe, Who shall order the battel? And he answered, Thou.
15 Ndipo Ahabu alipowataarifu wale vijna wanaowatumikia maliwali wa wilaya. Idadi yao ilikuwa 232. Baada yao aliwahesabu wanajeshi wote, jeshi lote la Israeli; idadi yao ilikuwa elfu saba.
Then he nombred the seruantes of the princes of the prouinces, and they were two hundreth, two and thirtie: and after them he nombred the whole people of all the children of Israel, euen seuen thousand.
16 Nao wakatoka wakati wa adhuhuri. Naye Beni Hadadi alikuwa akinywa na kulewa hemani mwake, yeye na wale wafalme wadogo thelathini na mbili waliokuwa wakimsaidia.
And they went out at noone: but Ben-hadad did drinke till he was drunken in the tentes, both he and the Kings: for two and thirtie Kings helped him.
17 Wale maakida vijana waliokuwa wakiwasaidia maliwali wa wilaya walitangulia kwanza. Kisha Beni Hadadi alitaarifiwa na wanaskauti aliokuwa amewatuma kwamaba, “kuna watu wanakuja kutoka Samaria.”
So the seruants of the princes of the prouinces went out first: and Ben-hadad sent out, and they shewed him, saying, There are men come out of Samaria.
18 Beni Hadadi akasema, “wawe wamekuja kwa amani au kwa vita, wakamteni wakiwa hai.”
And he sayde, Whether they be come out for peace, take them aliue: or whether they bee come out to fight, take them yet aliue.
19 Kwa hiyo wale vijvana wanaowatumikia maliwali wa wilaya wakaenda mjini na jeshi likawafuata kwa nyuma.
So they came out of the citie, to wit, the seruants of the princes of the prouinces, and the hoste which followed them.
20 Kila mmoja akaua adui wake na wale washami wakakimbia. Israeli ikawashinda. Beni Hadadi mfalme wa Shamu akatoroka kwa farasi pamoja na wapanda farasi.
And they slew euery one his enemie: and the Aramites fled, and Israel pursued them: but Ben-hadad ye King of Aram escaped on an horse with his horsemen.
21 Kisha mfalme wa Israeli akaenda akawashambulia farasi na magari, na kuwaua washami kwa mauaji makubwa.
And the King of Israel went out, and smote the horses and charets, and with a great slaughter slew he the Aramites.
22 Yule nabii akaja kwa mfalme wa Israeli akamwambia, “Nenda, ukajiimarishe mwenyewe, uelewa na kupanga kile unachofanya, kwa sababu mwakani mfalme wa Shamu atapanda dhidi yako tena.”
(For there had come a Prophet to the King of Israel, and had sayd vnto him, Goe, be of good courage, and consider, and take heede what thou doest: for when the yeere is gone about, the King of Aram wil come vp against thee)
23 Wale watumishi wa mfalme wa Shamu wakamwambia, “Mungu wao ni mungu wa milimani. Hiyo ndiyo sababu walikuwa na nguvu kuliko tulivyokuwa. Lakini sasa hebu tupigane nao katika nchi tambarare, na kwa hakika tutakuwa na nguvu kuliko wao.
Then the seruants of the King of Aram said vnto him, Their gods are gods of the moutaines, and therefore they ouercame vs: but let vs fight against them in the playne, and doubtlesse we shall ouercome them.
24 Na ufanye hivi: waondoe wafalme; mwondoe kila mmoja mahali pake ukaweke majemedari mahali pao.
And this doe, Take the Kings away, euery one out of his place, and place captaines for them.
25 Kisha ujihesabie jeshi kama lile jeshi ulilopoteza, farasi kwa farasi na gari kwa gari, nasi tutapigana nao katika nchi tambarare. Kwa hakika tutakuwa na nguvu kuliko walivyo.” Kwa hiyo Beni Hadadi akausikiliza ushauri huo naye akafanya kama alivyoshauriwa.
And nomber thy selfe an armie, like the armie that thou hast lost, with such horses, and such charets, and we wil fight against them in the plaine, and doubtlesse we shall ouercome them: and he hearkened vnto their voyce, and did so.
26 Baada ya mwanzo wa mwaka mpya, Beni Hadadi akawahesabu Washami na akapanda Afeki kupigana na Israeli.
And after the yeere was gone about, Ben-hadad nombred the Aramites, and went vp to Aphek to fight against Israel.
27 Watu wa Israeli walikuwa wamehesabiwa na walikuwa wamejipanga kupigana nao. Watu wa Israeli wakafanya kambi mbele yao kama makundi mawili madogo ya mbuzi, lakini Washami wakaujaza upande wa nchi.
And the children of Israel were nombred, and were all assembled and went against them, and the children of Israel pitched before them, like two litle flockes of kiddes: but the Aramites filled the countrey.
28 Ndipo mtu wa Mungu akaja karibu akaongea mfalme wa Israeli akamwambia, “BWANA anasema: 'Kwa kuwa Washami wamesema kuwa BWANA ni mungu wa milima, na wala si mungu wa mabondeni, nitaliweka hili jeshi kubwa mkononi mwako, nawe utajua kuwa mimi ni BWANA.'”
And there came a man of God, and spake vnto the King of Israel, saying, Thus sayeth the Lord, Because the Aramites haue sayd, The Lord is the God of the mountaines, and not God of the valleis, therefore will I deliuer all this great multitude into thine hand, and ye shall know that I am the Lord.
29 Kwa hiyo majeshi yakaweka kambi yakikabiliana kwa muda wa siku saba. Kisha siku ya saba vita vikaanza. Watu wa Israeli wakawaua Washami 100, 000 wanajeshi wa ardhini kwa siku moja.
And they pitched one ouer against the other seuen dayes, and in the seuenth day the battel was ioyned: and the children of Israel slew of the Aramites an hundreth thousand footemen in one day.
30 Waliobaki wakakimbilia Afeki, mjini, na ule ukuta ukaanguka juu ya watu ishiriinina saba elfu waliobaki. Naye Beni Hadadi akakimbilia mjini. akaingia kwenye chumba cha ndani.
But the rest fled to Aphek into the citie: and there fel a wall vpon seuen and twentie thousand men that were left: and Ben-hadad fled into the citie, and came into a secret chamber.
31 Wale watumishi wa Beni Hadadi wakamwambia, “Tazama sasa, tumesikia kwamba wale wafalme wa nyumba ya Israeli ni wenye rehema. Tafadhali hebu tuvaeni magaunia viunoni mwetu na kamba vichwani mwetu, na twendeni kwa mfalme wa Israeli. Labda atakuokoa roho yako.”
And his seruants sayd vnto him, Beholde nowe, we haue heard say that the Kings of the house of Israel are mercifull Kings: we pray thee, let vs put sacke cloth about our loynes, and ropes about our heads, and goe out to the King of Israel: it may be that he will saue thy life.
32 Kwa hiyo wakavaa magunia viunoni mwao na kujifunga kamba vichwani mwao na kisha wakaenda kwa mfalme wa Israeli wakamwambia, “Mtumishi wako Beni Hadadi, anasema, 'tafadhali niachie uhai wangu.” Ahabu akawaambia, “Je, bado yuko hai? Yeye ni ndugu yangu.”
Then they gyrded sackecloth about their loynes, and put ropes about their heads, and came to the King of Israel, and sayd, Thy seruant Ben-hadad sayth, I pray thee, let me liue: and he sayd, Is he yet aliue? he is my brother.
33 Sasa wale watu walikuwa wakisikiliza ishara yeyote kutoka kwa Ahabu, kwa hiyo wakamjibu haraka, “Ndiyo ndugu yako Beni Hadadi bado yuko hai.” Ahabu akawaambia, “Nendeni mkamlete.” Ndipo Beni Hadadi alipokuja kwake, na Ahabu akamwacha aje kwenye gari lake.
Now the men tooke diliget heede, if they could catch any thing of him, and made haste, and sayd, Thy brother Ben-hadad. And he sayd, Go, bring him. So Ben-hadad came out vnto him, and he caused him to come vp vnto the chariot.
34 Beni Hadadi akamwambia Ahabu, “Nitakurudishia miji yako ambayo baba yangu alichukua toka kwa baba yako, na unaweza kutengeneza masoko kwa ajili yako Dameski, kama baba yangu alivyofanya kule Samaria.” Ahabu akajibu, “Nitakuacha uende kwa agano hili.” Kwa hiyo Ahabu akafanya agano naye kisha akamwacha aende.
And Ben-hadad sayd vnto him, The cities, which my father tooke from thy father, I wil restore, and thou shalt make streetes for thee in Damascus, as my father did in Samaria. Then said Ahab, I will let thee goe with this couenant. So he made a couenant with him, and let him goe.
35 Mtu mmoja, mmoja wana wa wana wa manabii, akamwambia mmoja wa wale manabii wenzake kwa neno la BWANA, “Tafadhali nipige.” Lakini yule mtu akakataa kumpiga.
Then a certaine man of the children of the Prophets sayd vnto his neighbour by the comandement of the Lord, Smite me, I pray thee. But the man refused to smite him.
36 Kisha yule nabii akamwambia nabii mwenzake, “Kwa sababu umekataa kutii sauti ya BWANA, mara tu utakaponiacha, simba atakuua.” na mara tu baad ya yule mtu kumwacha, simba akamkuta na kumwua.
Then sayd he vnto him, Because thou hast not obeyed the voyce of the Lord, beholde, as soone as thou art departed from me, a lyon shall slay thee. So when he was departed from him, a lyon found him and slew him.
37 Kisha yule nabii akamkuta mtu mwingine akamwambia, “Tafadhali nipige.”Yule mtu akampiga na kumwumiza.
Then he founde another man, and sayde, Smite mee, I pray thee. And the man smote him, and in smiting wounded him.
38 Kisha yule nabii akaondoka akaenda kumsubiri yule mfalme barabarani; naye alikuwa amejibadilisha kwa kilemba machoni pake.
So the Prophet departed, and wayted for the King by the way, and disguised himselfe with ashes vpon his face.
39 Ikawa mfalme alipokuwa akipita, Yule nabii akamwita mfalme na kumwambia, “Mtumishi wako alienda katikati ya pigano, na askari akasimama akamleta adui kwangu akasema, 'Mwangalie mtu huyu. Na ikiwa kwa vyovyote atatoroka, basi maisha yako yatatolewa kwa ajili ya maisha yake vinginevyo utalipa kilo thelathini za fedha.
And when the King came by, he cried vnto the King, and said, Thy seruant went into the middes of the battel: and beholde, there went away a man, whom another man brought vnto me, and sayd, Keepe this man: if he be lost, and want, thy life shall go for his life, or els thou shalt pay a talent of siluer.
40 Lakini kwa kuwa mtumishi wako alikuwa na mambo mengi akienda huku na kule, yule askari adui akatoroka.” Basi mfalme wa Israeli akamwambia, Hivyo ndivyo itakavyokuwa hukukmu yako - umejihukumu mwenyewe.”
And as thy seruant had here and there to do, he was gone: And the King of Israel said vnto him, So shall thy iudgement be: thou hast giuen sentence.
41 Ndipo yule nabii alipoondoa haraka kile kilemba machoni pake, na mfalme wa Israeli alipotambua kuwa huyo alikuwa mmoja wa manabii.
And hee hasted, and tooke the ashes away from his face: and the King of Israel knewe him that he was of the Prophets:
42 Yule nabii akamwambia mfalme, “BWANA anasema, 'Kwa sababu umemwachia aende mtu yule niliyekuwa nimemhukumu kifo, maisha yako yatachukua nafasi ya maisha yake.'”
And he said vnto him, Thus saith the Lord, Because thou hast let goe out of thine handes a man whom I appoynted to dye, thy life shall goe for his life, and thy people for his people.
43 Kwa hiyo mfalme wa Israeli akaenda nyumbani kwake akiwa na moyo mzito na mwenye hasira, akafika Samaria.
And the King of Israel went to his house heauie and in displeasure, and came to Samaria.