< 1 Nyakati 11 >

1 Kisha Waisraeli wote walikuja Hebroni kwa Daudi na kusema, “Angalia, sisi ni nyama na mifupa yako.
ENTONCES todo Israel se juntó á David en Hebrón, diciendo: He aquí nosotros somos tu hueso y tu carne.
2 Katika wakati uliopita, Sauli alipoo kuwa mfalme juu yetu, ni wewe uliye ongoza jeshi la Israeli. Yahweh Mungu wako alisema kwako, 'utawachunga watu wangu wa Isaraeli, na utakuwa mtawala wa watu wangu wa Israeli”'.
Y además antes de ahora, aun mientras Saúl reinaba, tú sacabas y metías á Israel. También Jehová tu Dios te ha dicho: Tú apacentarás mi pueblo Israel, y tú serás príncipe sobre Israel mi pueblo.
3 Kwaiyo wazee wote wa Israeli wakamjia mfalme huko Hebroni, na Daudi akafanya agano nao mbele ya Yahweh. Wakampaka mafuta Daudi kuwa mfalme wa Israeli. Kwa namna hii, neno la Yahweh lilo nenwa na Samweli likawa kweli.
Y vinieron todos los ancianos de Israel al rey en Hebrón, y David hizo con ellos alianza delante de Jehová; y ungieron á David por rey sobre Israel, conforme á la palabra de Jehová por mano de Samuel.
4 Daudi na Israeli yote wakaenda Yerusalemu (yani, Yebusi). Sasa Wayebusi, wakazi wa nchi, walikuwa pale.
Entonces se fué David con todo Israel á Jerusalem, la cual es Jebus; y allí era el Jebuseo habitador de aquella tierra.
5 Wakazi wa yebusi wakamwabia Daudi, “Hautakuja humu.” Lakini Daudi alichukuwa ngome ya Sayuni, mji wa Daudi.
Y los moradores de Jebus dijeron á David: No entrarás acá. Mas David tomó la fortaleza de Sión, que es la ciudad de David.
6 Daudi alisema, “Yeyote atakaye washambulia Wayebusi wa kwanza atakuwa mkuu wa jeshi” kwaiyo Yoabu mwana wa Zeruia akashambulia wa kwanza, hivyo akafanywa mkuu wa jeshi.
Y David había dicho: El que primero hiriere al Jebuseo, será cabeza y jefe. Entonces Joab hijo de Sarvia subió el primero, y fué hecho jefe.
7 Daudi akaanza kuishi katika hiyo ngome. Kwaiyo wakaiita mji wa Daudi.
Y David habitó en la fortaleza, y por esto le llamaron la ciudad de David.
8 Akaimarisha mji kutoka Milo na hadi mpaka ukuta unao zunguka. Yoabu akaimairisha mji wote uliyo baki.
Y edificó la ciudad alrededor, desde Millo hasta la cerca: y Joab reparó el resto de la ciudad.
9 Daudi akawa mkuu na mkuu kwa sababu Yahweh wa Majeshi alikuwa naye.
Y David iba adelantando y creciendo, y Jehová de los ejércitos era con él.
10 Hawa walikuwa viongozi Daudi aliyo kuwa nao, waliyo jionyesha imara katika ufalme wake, pamoja na Israeli, kumfanya mfalme, kutii neno la Yahweh kuhusu Israeli.
Estos son los principales de los valientes que David tuvo, y los que le ayudaron en su reino, con todo Israel, para hacerle rey sobre Israel, conforme á la palabra de Jehová.
11 Hii ni orodha ya wanajeshi shupavu wa Daudi. Yashobeami, mwana wa Mhakimoni, alikuwa mkuu wa kikosi cha thelathini. Aliwaua wanaume mia tatu na mkuki wake katika sehemu moja.
Y este es el número de los valientes que David tuvo: Jasobam hijo de Hachmoni, caudillo de los treinta, el cual blandió su lanza una vez contra trescientos, á los cuales mató.
12 Baada ya yeye alikuwa Eleazari mwana wa Dodo, Mahohi, aliyekuwa mmoja wa wanaume watatu hodari.
Tras de éste fué Eleazar hijo de Dodo, Ahohita, el cual era de los tres valientes.
13 Alikuwa na Daudi huko Pasidamimu, na pale Wafilisti wakakusanyika pamoja kwa mapambano, ambapo palikuwa na uwanja wa ngano na jeshi liliwakimbia Wafilisti.
Este estuvo con David en Pasdammin, estando allí juntos en batalla los Filisteos: y había [allí] una suerte de tierra llena de cebada, y huyendo el pueblo delante de los Filisteos,
14 Walisimama katikati ya uwanja. Wakautetea na kuwakata Wafilisti na Yahweh akawaokoa na ushindi mkubwa.
Pusiéronse ellos en medio de la haza, y la defendieron, y vencieron á los Filisteos; y favoreciólos Jehová con grande salvamento.
15 Kisha watatu wa viongozi thelathini wakashuka chini kwenye mwamba wa Daudi, katika pango la Adulamu. Jeshi la Wafilisti walieka kambi katika bonde la Refaim.
Y tres de los treinta principales descendieron á la peña á David, á la cueva de Adullam, estando el campo de los Filisteos en el valle de Raphaim.
16 Kwa wakati huo Daudi alikuwa katika ngome yake, pangoni, Wafilisti walikita kambi yao Bethilehemu.
Y David estaba entonces en la fortaleza, y había á la sazón guarnición de Filisteos en Beth-lehem.
17 Daudi alikuwa na kiu ya maji na akasema, “Laiti mtu akanipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilicho Bethilehemu, kisima kilicho pembeni mwa lango!”
David deseó entonces, y dijo: ¡Quién me diera á beber de las aguas del pozo de Beth-lehem, que está á la puerta!
18 Hawa wanaume hodari watatu wakatoboa kupita jeshi la Wafilisti na kuchota maji kwenye kisima cha Bethilehemu, kisima pembeni mwa lango. Wakachukuwa maji na kumletea Daudi, lakini alikataa kunywa. Badala yake, akamwaga chini kwa Yahweh.
Y aquellos tres rompieron por el campo de los Filisteos, y sacaron agua del pozo de Beth-lehem, que está á la puerta, y tomaron y trajéronla á David: mas él no la quiso beber, sino que la derramó á Jehová, y dijo:
19 Kisha akasema, “Yahweh, iwe mbali na mimi, kwamba ni yanywe haya maji. Je ninywe damu ya wanaume walio hatarisha maisha yao?” Kwa sababu wameeka maisha ya hatarini, akakataa kunywa. Haya ni mambo wanaume hodari watatu walio fanya.
Guárdeme mi Dios de hacer esto: ¿había yo de beber la sangre de estos varones con sus vidas, que con [peligro de] sus vidas la han traído? Y no la quiso beber. Esto hicieron aquellos tres valientes.
20 Abishai kaka wa Yoabu, alikuwa kiongozi wa watatu. Alitumia mkuki wake dhidi ya watu mia tatu na kuwaua. Ametajwa pamoja na wale watatu.
Y Abisai, hermano de Joab, era cabeza de los tres, el cual blandió su lanza sobre trescientos, á los cuales hirió; y fué entre los tres nombrado.
21 Kati ya wale watatu, yeye alipewa heshima mara mbili na akawa kiongozi wao. Japo hakuwa mmoja wa miongoni mwao.
De los tres fué más ilustre que los [otros] dos, y fué el principal de ellos: mas no llegó á los tres [primeros].
22 Benaia mwana wa Yehoiada alikuwa mwanaume mwenye nguvu aliye fanya mambo makuu. Aliua wana wawili wa Arieli wa Moabu. Pia alishuka chini ya shimo na kumuua simba wakati theluji ikianguka.
Benaías hijo de Joiada, hijo de varón de esfuerzo, de grandes hechos, de Cabseel: él venció los dos leones de Moab: también descendió, é hirió un león en mitad de un foso en tiempo de nieve.
23 Alimua hadi Mmisri, mwanaume mwenye mita mbili na theluthi moja. Mmisri alikuwa na mkuki kama gongo la mshonaji, lakini alimfuata chini na fimbo tu. Akakamata mkuki katika mkono wa Mmisri na kumuua na mkuki wake.
El mismo venció á un Egipcio, hombre de cinco codos de estatura: y el Egipcio traía una lanza como un enjullo de tejedor; mas él descendió á él con un bastón, y arrebató al Egipcio la lanza de la mano, y matólo con su misma lanza.
24 Benaia mwana wa Yehoiada alifanya haya matukio, na akatajwa miongoni mwa wale wanaume hodari watatu.
Esto hizo Benaías hijo de Joiada, y fué nombrado entre los tres valientes.
25 Alisifika zaidi ya wale wanajeshi thelathini kwa ujumla, lakini hakuwa pewa hadhi ya wale wanajeshi watatu hodari. Daudi alimueka kiongozi wa walinzi wake.
Y fué el más honrado de los treinta, mas no llegó á los tres [primeros]. A éste puso David en su consejo.
26 Wanaume hodari walikuwa Asaheli kaka wa Yoabu, Elhanani mwana wa Dodo wa Bethilehemu,
Y los valientes de los ejércitos: Asael hermano de Joab, y Elchânan hijo de Dodo de Beth-lehem;
27 Shamothi Mherori, Helezi Mpeloni,
Samoth de Arori, Helles Pelonita;
28 Ira mwana wa Ikeshi Mtekoi, Abi Eza Manathothi,
Ira hijo de Acces Tecoita, Abiezer Anathothita;
29 Sibekai Mhushathite, Ilai Mahohite,
Sibbecai Husatita, Ilai Ahohita;
30 Maharai Mnetofathi, Heledi mwana wa Baana Mnetofathite,
Maharai Nethophathita, Heled hijo de Baana Nethophathita;
31 Itai mwana wa Ribai wa Gibea uzao wa Benjamini, Benaia Mpirathoni,
Ithai hijo de Ribai de Gabaath de los hijos de Benjamín, Benaías Phirathita;
32 Hurai wa mabonde ya Gaashi, Abieli Marbathi,
Hurai del río Gaas, Abiel Arbathonita;
33 Azmavethi Mbaharumi, Eliaba Mshaalboni,
Azmaveth Baharumita, Eliaba Saalbonita;
34 Mwana wa Hashemu Mgizoni, Yonathani mwana wa Shagee Mhararite,
Los hijos de Asem Gizonita, Jonathán hijo de Sajé Hararita;
35 Ahiamu mwana wa Sacari Mhararite, Elifali mwana wa Uri,
Ahiam hijo de Sachâr Ararita, Eliphal hijo de Ur;
36 Hefa Mmekarathi, Ahija Mpeloni,
Hepher Mechêrathita, Ahía Phelonita;
37 Hezro Mcarmeli, Maarai mwana wa Ezibai,
Hesro Carmelita, Nahari hijo de Ezbai;
38 Yoeli kaka wa Nathani, Mibhari mwana wa Hagiri,
Joel hermano de Nathán, Mibhar hijo de Agrai;
39 Zeleki Mamoni, Naharai Mberothi ( mbeba ngao ya Yoabu mwana wa Zeruia),
Selec Ammonita, Naarai Berothita, escudero de Joab hijo de Sarvia;
40 Ira Mithire, Garebu Mithire,
Ira Ithreo, Yared Ithreo;
41 Uria Mhiti, Zabadi mwana wa Ahlai,
Uría Hetheo, Zabad hijo de Ahli;
42 Adina mwana wa Shiza Mreubeni ( kiongozi wa Wareubeni) na thelathini pamoja nae,
Adina hijo de Siza Rubenita, príncipe de los Rubenitas, y con él treinta;
43 Hanani mwana wa Maaka, na Yoshafati Mmithini,
Hanán hijo de Maachâ, y Josaphat Mithnita;
44 Uzia Mashiterathi, Shama na Yeieli wana wa Hothamu Waaroeri,
Uzzías Astarothita, Samma y Jehiel hijos de Hotham Arorita;
45 Jediaeli mwana wa Shimri, Joha ( kaka yake Mtize),
Jediael hijo de Simri, y Joha su hermano, Thisaita;
46 Elieli Mmahavi, Yeribai na Yoshavia mwana wa Elnaamu, Ithima Mmoabi,
Eliel de Mahaví, Jeribai y Josabia hijos de Elnaam, é Ithma Moabita;
47 Elieli, Obedi, na Yaasieli Wamezobai.
Eliel, y Obed, y Jaasiel de Mesobia.

< 1 Nyakati 11 >