< Zekaria 2 >
1 Kisha nikatazama juu: pale mbele yangu alikuwepo mtu mwenye kamba ya kupimia mkononi mwake!
Je levai les yeux, et je vis, et voici, un homme qui tenait un cordeau à mesurer dans sa main.
2 Nikamuuliza, “Unakwenda wapi?” Akanijibu, “Kupima Yerusalemu, kupata urefu na upana wake.”
Alors je demandai: « Où vas-tu? » Il m'a dit: « Pour mesurer Jérusalem, pour voir quelle est sa largeur et quelle est sa longueur. »
3 Kisha malaika aliyekuwa akizungumza nami akaondoka, malaika mwingine akaja kukutana naye
Voici que l'ange qui m'a parlé sort, et un autre ange va à sa rencontre,
4 na kumwambia: “Kimbia, umwambie yule kijana, ‘Yerusalemu utakuwa mji usio na kuta kwa sababu ya wingi wa watu na mifugo iliyomo.
et lui dit: « Cours, parle à ce jeune homme, en disant: 'Jérusalem sera habitée comme des villages sans murs, à cause de la multitude d'hommes et de bêtes qui s'y trouvent.
5 Mimi mwenyewe nitakuwa ukuta wa moto kuuzunguka,’ asema Bwana, ‘nami nitakuwa utukufu wake ndani yake.’
Car moi, dit Yahvé, je serai pour elle une muraille de feu tout autour, et je serai la gloire au milieu d'elle.
6 “Njooni! Njooni! Kimbieni mtoke katika nchi ya kaskazini,” asema Bwana, “Kwa kuwa nimewatawanya kwenye pande nne za mbingu,” asema Bwana.
Viens! Venez! Fuyez du pays du nord, dit Yahvé, car je vous ai dispersés comme les quatre vents du ciel, dit Yahvé.
7 “Njoo, ee Sayuni! Kimbia, wewe ukaaye ndani ya Binti Babeli!”
« Viens, Sion! Fuis, toi qui habites avec la fille de Babylone!
8 Kwa kuwa hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Baada ya yeye kuniheshimu na kunituma mimi dhidi ya mataifa yaliyokuteka nyara, kwa kuwa yeyote awagusaye ninyi, anaigusa mboni ya jicho lake,
Car Yahvé des armées dit: « C'est pour l'honneur qu'il m'a envoyé vers les nations qui t'ont pillée, car celui qui te touche touche la prunelle de ses yeux.
9 hakika nitauinua mkono wangu dhidi yao ili watumwa wao wawateke nyara. Ndipo mtakapojua ya kwamba Bwana Mwenye Nguvu Zote amenituma.
Car voici, j'agiterai ma main sur elles, et elles seront un butin pour ceux qui les ont servies; et vous saurez que l'Éternel des armées m'a envoyé.
10 “Piga kelele na ufurahie, ee Binti Sayuni, kwa maana ninakuja, nami nitaishi miongoni mwenu,” asema Bwana.
Chante et réjouis-toi, fille de Sion! Car voici, je viens et j'habiterai au milieu de toi, dit Yahvé.
11 “Mataifa mengi yataunganishwa na Bwana siku hiyo, nao watakuwa watu wangu. Nitaishi miongoni mwenu nanyi mtajua kwamba Bwana Mwenye Nguvu Zote amenituma kwenu.
En ce jour-là, des nations nombreuses se joindront à Yahvé et seront mon peuple; j'habiterai au milieu de vous, et vous saurez que Yahvé des armées m'a envoyé vers vous.
12 Bwana atairithi Yuda kama fungu lake katika nchi takatifu na atachagua tena Yerusalemu.
L'Éternel fera de Juda sa part dans la terre sainte, et il choisira de nouveau Jérusalem.
13 Tulieni mbele za Bwana, enyi watu wote, kwa sababu ameinuka kutoka makao yake matakatifu.”
Silence, toute chair, devant l'Éternel, car il s'est réveillé de sa demeure sainte! »