< Warumi 13 >

1 Kila mtu na atii mamlaka inayotawala, kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu, nazo mamlaka zilizopo zimewekwa na Mungu.
Every soul to the authorities being above [him] should be subject. Not for there is authority only except (by *N(k)O*) God, those however existing (authorities *k*) by (*k*) God instituted are.
2 Kwa hiyo yeye anayeasi dhidi ya mamlaka inayotawala anaasi dhidi ya kile kilichowekwa na Mungu, nao wale wafanyao hivyo watajiletea hukumu juu yao wenyewe.
Therefore the [one] resisting the authority the of God ordinance has resisted; those now having resisted upon themselves judgment will bring.
3 Kwa kuwa watawala hawawatishi watu wale wanaotenda mema bali wale wanaotenda mabaya. Je, wataka usimwogope mwenye mamlaka? Basi tenda lile lililo jema naye atakusifu.
The for rulers not are a terror (to the good *N(k)O*) (work *N(K)O*) but (to the evil. *N(k)O*) Do you desire now not to fear the authority? The good do perform and you will have praise from him;
4 Kwa maana mwenye mamlaka ni mtumishi wa Mungu kwa ajili ya mema. Lakini kama ukitenda mabaya, basi ogopa, kwa kuwa hauinui upanga bila sababu. Yeye ni mtumishi wa Mungu, mjumbe wa Mungu wa kutekeleza adhabu juu ya watenda mabaya.
Of God for servant he is to you for good. If however evil you shall do, do be afraid; not for in vain the sword he bears. of God for a servant He is an avenger for wrath to the [one] evil doing.
5 Kwa hiyo ni lazima kutii wenye mamlaka, si kwa sababu ya kuogopa adhabu iwezayo kutolewa, bali pia kwa ajili ya dhamiri.
Therefore necessary [it is] to be subject, not only on account of the wrath but also on account of the conscience.
6 Kwa sababu hii mnalipa kodi, kwa maana watawala ni watumishi wa Mungu, ambao hutumia muda wao wote kutawala.
Because of this for also taxes pay you; servants for of God they are upon this very thing attending continually.
7 Mlipeni kila mtu kile mnachodaiwa. Kama mnadaiwa kodi lipeni kodi, kama ni ushuru, lipeni ushuru, astahiliye hofu, mhofu, astahiliye heshima, mheshimu.
do render (therefore *K*) to all their dues, to whom the tax the tax, to whom the revenue the revenue, to whom the respect the respect, to whom the honor the honor.
8 Msidaiwe kitu na mtu yeyote, isipokuwa kupendana, kwa maana yeye ampendaye mwenzake, ameitimiza sheria.
To no one nothing do owe only except one another to love; the [one] for loving the other [the] Law has fulfilled;
9 Kwa kuwa amri hizi zisemazo, “Usizini,” “Usiue,” “Usiibe,” “Usitamani,” na amri nyingine zote, zinajumlishwa katika amri hii moja: “Mpende jirani yako kama nafsi yako.”
For Not you will commit adultery, Not you will murder, Not you will steal (not will you bear false witness *K*) Not you will covet, and if any other commandment, in word this it is summed up, in the [saying] You will love the neighbour of you as (yourself. *NK(O)*)
10 Upendo haumfanyii jirani jambo baya. Kwa hiyo upendo ndio utimilifu wa sheria.
Love to the neighbour evil not does do; [the] fulfillment therefore of [the] law love [is].
11 Nanyi fanyeni hivi, mkiutambua wakati tulio nao. Saa ya kuamka kutoka usingizini imewadia, kwa maana sasa wokovu wetu umekaribia zaidi kuliko hapo kwanza tulipoamini.
And this knowing the time, that [it is the] hour already ([for] you *N(k)O*) out of sleep to awaken; now for nearer [is] of us the salvation than when first we believed;
12 Usiku umeendelea sana, mapambazuko yamekaribia. Kwa hiyo tuyaweke kando matendo ya giza na tuvae silaha za nuru.
The night is nearly over and the day has drawn near. (We may cast off *NK(o)*) therefore the works of darkness, (and *k*) we may put on (now *no*) the armor of light.
13 Basi na tuenende kwa adabu kama inavyopasa wakati wa mchana, si kwa kufanya karamu za ulafi na ulevi, si kwa ufisadi na uasherati, si kwa ugomvi na wivu.
As in daytime properly we may walk, not in reveling and in drinking, not in sexual immorality and in sensuality, not in dissension and in jealousy;
14 Bali jivikeni Bwana Yesu Kristo, wala msifikiri jinsi mtakavyotimiza tamaa za miili yenu yenye asili ya dhambi.
But do put on the Lord Jesus Christ and of the flesh provision not do make for desires.

< Warumi 13 >