< Zaburi 99 >

1 Bwana anatawala, mataifa na yatetemeke; anakalia kiti cha enzi katikati ya makerubi, dunia na itikisike.
Yahvé règne! Que les peuples tremblent. Il est assis sur un trône parmi les chérubins. Que la terre s'émeuve.
2 Bwana ni mkuu katika Sayuni; ametukuzwa juu ya mataifa yote.
Yahvé est grand en Sion. Il est élevé au-dessus de tous les peuples.
3 Wanalisifu jina lako ambalo ni kuu na la kuogopwa: yeye ni mtakatifu!
Qu'ils louent ton nom grand et redoutable. Il est saint!
4 Mfalme ni mwenye nguvu na hupenda haki, wewe umethibitisha adili; katika Yakobo umefanya yaliyo haki na sawa.
La force du roi aime aussi la justice. Vous établissez l'équité. Tu exécutes la justice et la droiture en Jacob.
5 Mtukuzeni Bwana Mungu wetu, na mkaabudu katika mahali pa kuwekea miguu yake; yeye ni mtakatifu.
Exaltez Yahvé notre Dieu. Se prosterner devant son marchepied. Il est saint!
6 Mose na Aroni walikuwa miongoni mwa makuhani wake, Samweli alikuwa miongoni mwa walioliitia jina lake; walimwita Bwana, naye aliwajibu.
Moïse et Aaron étaient parmi ses prêtres, Samuel était parmi ceux qui invoquent son nom. Ils invoquèrent Yahvé, et il leur répondit.
7 Alizungumza nao kutoka nguzo ya wingu; walizishika sheria zake na amri alizowapa.
Il leur parla dans la colonne de nuée. Ils ont gardé ses témoignages, le statut qu'il leur a donné.
8 Ee Bwana, wetu, ndiwe uliyewajibu, kwa Israeli ulikuwa Mungu mwenye kusamehe, ingawa uliadhibu matendo yao mabaya.
Tu leur as répondu: Yahvé, notre Dieu. Tu es un Dieu qui leur a pardonné, bien que vous vous soyez vengé de leurs actes.
9 Mtukuzeni Bwana Mungu wetu, mwabuduni kwenye mlima wake mtakatifu, kwa maana Bwana Mungu wetu ni mtakatifu.
Exaltez Yahvé, notre Dieu. Vénérer sur sa colline sacrée, car Yahvé, notre Dieu, est saint!

< Zaburi 99 >