< Zaburi 96 >

1 Mwimbieni Bwana wimbo mpya; mwimbieni Bwana dunia yote.
Oh sing unto the Lord a new song: sing unto the Lord, all the lands.
2 Mwimbieni Bwana, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
Sing unto the Lord, bless his name: announce from day to day his salvation.
3 Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
Relate among the nations his honor, among all the people his wonders.
4 Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
For the Lord is great, and greatly praised: he is to be feared above all gods.
5 Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
For all the gods of the nations are idols; but the Lord hath made the heavens.
6 Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
Glory and majesty are before him: strength and beauty are in his sanctuary.
7 Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
Ascribe unto the Lord, O ye families of the people, ascribe unto the Lord honor and strength.
8 Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.
Ascribe unto the Lord the honor [due unto] his name: bear hither a present, and come unto his courts.
9 Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake; dunia yote na itetemeke mbele zake.
Bow down unto the Lord in the beauty of holiness: tremble before him, all ye lands.
10 Katikati ya mataifa semeni, “Bwana anatawala.” Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa; atawahukumu watu kwa uadilifu.
Say among the nations, “The Lord reigneth;” [therefore] also the world is ever firmly established that it shall hot be moved: he will judge the people in equity.
11 Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake;
Let the heavens rejoice, and let the earth be glad: let the sea roar, with all that filleth it.
12 mashamba na yashangilie, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;
Let the field exult, and all that is therein: then shall all the trees of the forest sing for joy,
13 itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja, anakuja kuihukumu dunia. Ataihukumu dunia kwa haki, na mataifa katika kweli yake.
Before the Lord; for he cometh, for he cometh to judge the earth: he will judge the world with righteousness, and people in his truth.

< Zaburi 96 >