< Zaburi 84 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya wana wa Kora. Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, makao yako yapendeza kama nini!
В конец, о точилех, сыном Кореовым, псалом. Коль возлюбленна селения Твоя, Господи сил.
2 Nafsi yangu inatamani sana, naam, hata kuona shauku, kwa ajili ya nyua za Bwana; moyo wangu na mwili wangu vinamlilia Mungu Aliye Hai.
Желает и скончавается душа моя во дворы Господни: сердце мое и плоть моя возрадовастася о Бозе живе.
3 Hata shomoro amejipatia makao, mbayuwayu amejipatia kiota mahali awezapo kuweka makinda yake: mahali karibu na madhabahu yako, Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mfalme wangu na Mungu wangu.
Ибо птица обрете себе храмину, и горлица гнездо себе, идеже положит птенцы своя, олтари Твоя, Господи сил, Царю мой и Боже мой.
4 Heri wale wanaokaa nyumbani mwako, wanaokusifu wewe daima.
Блажени живущии в дому Твоем: в веки веков восхвалят Тя.
5 Heri wale ambao nguvu zao ziko kwako, na njia ziendazo Sayuni zimo mioyoni mwao.
Блажен муж, емуже есть заступление его у Тебе: восхождения в сердцы своем положи,
6 Wanapopita katika Bonde la Baka, hulifanya mahali pa chemchemi, pia mvua za vuli hulijaza kwa madimbwi.
во юдоль плачевную, в место еже положи: ибо благословение даст законополагаяй.
7 Huendelea toka nguvu hadi nguvu, hadi kila mmoja afikapo mbele za Mungu huko Sayuni.
Пойдут от силы в силу: явится Бог богов в Сионе.
8 Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, sikia maombi yangu; nisikilize, Ee Mungu wa Yakobo.
Господи Боже сил, услыши молитву мою, внуши, Боже Иаковль.
9 Ee Mungu, uitazame ngao yetu, mtazame kwa wema mpakwa mafuta wako.
Защитниче наш, виждь, боже, и призри на лице христа Твоего.
10 Siku moja katika nyua zako ni bora kuliko siku elfu mahali pengine; afadhali ningekuwa bawabu katika nyumba ya Mungu wangu kuliko kukaa katika mahema ya waovu.
Яко лучше день един во дворех Твоих паче тысящ: изволих приметатися в дому Бога моего паче, неже жити ми в селениих грешничих.
11 Kwa kuwa Bwana ni jua na ngao, Bwana hutoa wema na heshima; hakuna kitu chema anachowanyima wale ambao hawana hatia.
Яко милость и истину любит Господь, Бог благодать и славу даст: Господь не лишит благих ходящих незлобием.
12 Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, heri ni mtu yule anayekutumaini wewe.
Господи Боже сил, блажен человек уповаяй на Тя.

< Zaburi 84 >