< Zaburi 81 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Asafu. Mwimbieni kwa furaha, Mungu aliye nguvu yetu; mpigieni kelele za shangwe Mungu wa Yakobo!
To the Chief Musician. On "the Gittith." Asaph’s. Shout ye for joy, unto God our strength, Sound the note of triumph, to the God of Jacob;
2 Anzeni wimbo, pigeni matari, pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri.
Raise a melody, and strike the timbrel, The lyre so sweet, with the harp:
3 Pigeni baragumu za pembe za kondoo dume wakati wa Mwandamo wa Mwezi, na wakati wa mwezi mpevu, katika siku ya Sikukuu yetu;
Blow, at the new moon, the horn, At the full moon, for the day of our sacred festival:
4 hii ni amri kwa Israeli, agizo la Mungu wa Yakobo.
For, a statute to Israel, it is, A regulation, by the God of Jacob;
5 Aliiweka iwe kama sheria kwa Yosefu alipotoka dhidi ya Misri, huko tulikosikia lugha ambayo hatukuielewa.
A testimony in Joseph, he appointed it, When he went forth over the land of Egypt: A language I liked not, used I to hear;
6 Asema, “Nimeondoa mzigo mabegani mwao; mikono yao iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.
I took away, from the burden, his shoulder, his hands, from the clay, were set free.
7 Katika shida yako uliniita nami nikakuokoa, nilikujibu katika mawingu yenye ngurumo; nilikujaribu katika maji ya Meriba.
In distress, thou didst cry, and I delivered thee, —I answered thee, within a hiding-place of thunder, I proved thee by the waters of Meribah. (Selah)
8 “Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya: laiti kama mngenisikiliza, ee Israeli!
Hear, O my people, and I will adjure thee, O Israel, if thou wilt hearken unto me!
9 Hamtakuwa na mungu mgeni miongoni mwenu; msimsujudie mungu wa kigeni.
There shall not be, within thee, a foreign GOD, —Neither shalt thou bow down to a strange GOD:
10 Mimi ni Bwana Mungu wako, niliyekutoa nchi ya Misri. Panua sana kinywa chako nami nitakijaza.
I, Yahweh, am thy God, Who brought thee up out of the land of Egypt, —Open wide thy mouth, that I may fill it.
11 “Lakini watu wangu hawakutaka kunisikiliza; Israeli hakutaka kunitii.
But my people, hearkened not, unto my voice, Even, Israel, inclined not unto me.
12 Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao wafuate mashauri yao wenyewe.
So then I let them go on in the stubbornness of their own heart, They might walk in their own counsels!
13 “Laiti kama watu wangu wangalinisikiliza, kama Israeli wangalifuata njia zangu,
If, my people, were hearkening unto me, [If, ] Israel, in my ways, would walk,
14 ningaliwatiisha adui zao kwa haraka, na kuugeuza mkono wangu dhidi ya watesi wao!
Right soon, their foes, would I subdue, And, against their adversaries, would I turn my hand:
15 Wale wanaomchukia Bwana wangalinyenyekea mbele zake, na adhabu yao ingedumu milele.
The haters of Yahweh, should come cringing unto him, Then let their own good time be age-abiding!
16 Bali ninyi mngalilishwa ngano iliyo bora, na kuwatosheleza kwa asali itokayo kwenye mwamba.”
Then would he feed them from the marrow of the wheat, Yea, out of the rock—with honey, would I satisfy thee.

< Zaburi 81 >