< Zaburi 71 >

1 Ee Bwana, nimekukimbilia wewe, usiache nikaaibika kamwe.
На Тя, Господи, уповах, да не постыжуся в век.
2 Kwa haki yako uniponye na kuniokoa, unitegee sikio lako uniokoe.
Правдою Твоею избави мя и изми мя: приклони ко мне ухо Твое и спаси мя.
3 Uwe kwangu mwamba wa kimbilio, mahali nitakapokimbilia kila wakati; toa amri ya kuniokoa, kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu.
Буди ми в Бога защитителя и в место крепко спасти мя: яко утверждение мое и прибежище мое еси Ты.
4 Ee Mungu wangu uniokoe kutoka kwenye mkono wa mwovu, kutoka kwenye makucha ya watu wabaya na wakatili.
Боже мой, избави мя из руки грешнаго, из руки законопреступнаго и обидящаго:
5 Kwa kuwa umekuwa tumaini langu, Ee Bwana Mwenyezi, tegemeo langu tangu ujana wangu.
яко Ты еси терпение мое, Господи, Господи, упование мое от юности моея.
6 Tangu kuzaliwa nimekutegemea wewe, ulinitoa tumboni mwa mama yangu. Nitakusifu wewe daima.
В Тебе утвердихся от утробы, от чрева матере моея Ты еси мой покровитель: о Тебе пение мое выну.
7 Nimekuwa kama kioja kwa wengi, lakini wewe ni kimbilio langu imara.
Яко чудо бых многим: и Ты помощник мой крепок.
8 Kinywa changu kimejazwa sifa zako, nikitangaza utukufu wako mchana kutwa.
Да исполнятся уста моя хваления, яко да воспою славу Твою, весь день великолепие Твое.
9 Usinitupe wakati wa uzee, wala usiniache nguvu zangu zinapopungua.
Не отвержи мене во время старости: внегда оскудевати крепости моей, не остави мене.
10 Kwa maana adui zangu wananisengenya, wale wanaonivizia kuniua wafanya hila.
Яко реша врази мои мне, и стрегущии душу мою совещаша вкупе,
11 Wanasema, “Mungu amemwacha, mkimbilieni mkamkamate, kwani hakuna wa kumwokoa.”
глаголюще: Бог оставил есть его, пожените и имите его, яко несть избавляяй.
12 Ee Mungu, usiwe mbali nami, njoo haraka kunisaidia, Ee Mungu wangu.
Боже мой, не удалися от мене: Боже мой, в помощь мою вонми.
13 Washtaki wangu na waangamie kwa aibu, wale wanaotaka kunidhuru na wafunikwe kwa dharau na fedheha.
Да постыдятся и изчезнут оклеветающии душу мою, да облекутся в студ и срам ищущии злая мне.
14 Lakini mimi, nitatumaini siku zote, nitakusifu zaidi na zaidi.
Аз же всегда возуповаю на Тя, и приложу на всяку похвалу Твою.
15 Kinywa changu kitasimulia haki yako, wokovu wako mchana kutwa, ingawa sifahamu kipimo chake.
Уста моя возвестят правду Твою, весь день спасение Твое, яко не познах книжная.
16 Ee Bwana Mwenyezi, nitakuja na kutangaza matendo yako makuu, nitatangaza haki yako, yako peke yako.
Вниду в силе Господни: Господи, помяну правду Тебе единаго.
17 Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu, hadi leo ninatangaza matendo yako ya ajabu.
Боже мой, имже научил мя еси от юности моея, и доныне возвещу чудеса Твоя.
18 Ee Mungu, usiniache, hata niwapo mzee wa mvi, mpaka nitangaze uwezo wako kwa kizazi kijacho, nguvu zako kwa wote watakaokuja baadaye.
И даже до старости и престарения, Боже мой, не остави мене, дондеже возвещу мышцу Твою роду всему грядущему,
19 Ee Mungu, haki yako imefika juu katika mbingu, wewe ambaye umefanya mambo makuu. Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?
силу Твою и правду Твою, Боже, даже до вышних, яже сотворил ми еси величия: Боже, кто подобен Тебе?
20 Ingawa umenifanya nipate taabu, nyingi na chungu, utanihuisha tena, kutoka vilindi vya dunia utaniinua tena.
Елики явил ми еси скорби многи и злы? И обращься оживотворил мя еси и от бездн земли возвел мя еси.
21 Utaongeza heshima yangu na kunifariji tena.
Умножил еси на мне величествие твое, и обращься утешил мя еси, и от бездн земли паки возвел мя еси.
22 Ee Mungu wangu, nitakusifu kwa kinubi kwa ajili ya uaminifu wako; Ee Uliye Mtakatifu wa Israeli, nitakuimbia sifa kwa zeze.
Ибо аз исповемся Тебе в людех, Господи, в сосудех псаломских истину Твою, Боже: воспою Тебе в гуслех, Святый Израилев.
23 Midomo yangu itapaza sauti kwa furaha ninapokuimbia sifa, mimi, ambaye umenikomboa.
Возрадуетеся устне мои, егда воспою Тебе, и душа моя, юже еси избавил:
24 Ulimi wangu utasimulia matendo yako ya haki mchana kutwa, kwa maana wale waliotaka kunidhuru, wameaibishwa na kufadhaishwa.
еще же и язык мой весь день поучится правде Твоей, егда постыдятся и посрамятся ищущии злая мне.

< Zaburi 71 >