< Zaburi 68 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo. Mungu na ainuke, watesi wake watawanyike, adui zake na wakimbie mbele zake.
To the choirmaster of David a psalm a song. May he arise God may they be scattered enemies his and they may flee [those who] hate him from before him.
2 Kama vile moshi upeperushwavyo na upepo, vivyo hivyo uwapeperushe mbali, kama vile nta iyeyukavyo kwenye moto, vivyo hivyo waovu na waangamie mbele za Mungu.
As is driven about smoke may you drive [them] about as melts wax from before a fire may they perish wicked [people] from before God.
3 Bali wenye haki na wafurahi, washangilie mbele za Mungu, wafurahi na kushangilia.
And righteous [people] may they be glad may they exult before God and may they rejoice with gladness.
4 Mwimbieni Mungu, liimbieni sifa jina lake, mtukuzeni yeye aendeshwaye juu ya mawingu: jina lake ni Bwana, furahini mbele zake.
Sing - to God sing praises to name his lift up to the rider in the clouds [is] Yahweh name his and exult before him.
5 Baba wa yatima, mtetezi wa wajane, ni Mungu katika makao yake matakatifu.
[is] a father of Fatherless ones and a judge of widows God in [the] dwelling place of holiness his.
6 Mungu huwaweka wapweke katika jamaa, huwaongoza wafungwa wakiimba, bali waasi huishi katika nchi kame.
God - [is] causing to dwell solitary [people] - a household [he is] bringing out prisoners in prosperiti only rebellious [people] they dwell a parched land.
7 Ee Mungu, ulipowatangulia watu wako, ulipopita nyikani,
O God when going out you before people your when marching you in a desolate place (Selah)
8 dunia ilitikisika, mbingu zikanyesha mvua, mbele za Mungu, Yule wa Sinai, mbele za Mungu, Mungu wa Israeli.
[the] earth It quaked - also [the] heavens they dropped from before God this Sinai from before God [the] God of Israel.
9 Ee Mungu, ulinyesha mvua nyingi na kuiburudisha ardhi iliyokuwa imechoka.
Rain of voluntariness you spread abroad O God inheritance your weary you you established it.
10 Ee Mungu, watu wako waliishi huko, nawe kwa wingi wa utajiri wako uliwapa maskini mahitaji yao.
Community your they dwelt in it you prepared in goodness your for poor [person] O God.
11 Bwana alitangaza neno, waliolitangaza neno hilo walikuwa kundi kubwa:
[the] Lord He gives a word the [women who] bear news [are] a host great.
12 “Wafalme na majeshi walikimbia upesi, watu waliobaki kambini waligawana nyara.
Kings of armies they flee! they flee! and [the] beautiful woman of [the] house she divides [the] plunder.
13 Hata ulalapo katikati ya mioto ya kambini, mabawa ya njiwa wangu yamefunikwa kwa fedha, manyoya yake kwa dhahabu ingʼaayo.”
If you will lie down! between [two] saddlebags [the] wings of a dove [are] covered with silver and pinions its with greenish of gold.
14 Wakati Mwenyezi alipowatawanya wafalme katika nchi, ilikuwa kama theluji iliyoanguka juu ya Salmoni.
When scatters [the] Almighty kings in it let it snow on Zalmon.
15 Milima ya Bashani ni milima iliyotukuka, milima ya Bashani ina vilele vilivyochongoka.
O mountain of God O mountain of Bashan O mountain of peaks O mountain of Bashan.
16 Enyi milima yenye vilele vilivyochongoka, kwa nini mnakazia macho kwa wivu, katika mlima Mungu anaochagua kutawala, ambako Bwana mwenyewe ataishi milele?
Why? - do you watch with envy! O mountains peaks the mountain [which] he desired God to dwell in he also Yahweh he will dwell to perpetuity.
17 Magari ya Mungu ni makumi ya maelfu, na maelfu ya maelfu; Bwana amekuja kutoka Sinai hadi katika patakatifu pake.
[the] chariotry of God [is] twice ten thousand thousands of repetition[s] [the] Lord [is] among them Sinai [is] in holiness.
18 Ulipopanda juu, uliteka mateka, ukapokea vipawa kutoka kwa wanadamu, hata kutoka kwa wale walioasi, ili wewe, Ee Bwana Mungu, upate kuishi huko.
You went up to the height - you took captive captive[s] you took gifts among humankind and even rebellious [people] to dwell - Yahweh God.
19 Sifa apewe Bwana, Mungu Mwokozi wetu, ambaye siku kwa siku hutuchukulia mizigo yetu.
[be] blessed [the] Lord Day - day he carries a load for us God salvation our (Selah)
20 Mungu wetu ni Mungu aokoaye, Bwana Mwenyezi hutuokoa na kifo.
God - of us [is] a God of saving acts and [belong] to Yahweh [the] Lord to death escapes.
21 Hakika Mungu ataponda vichwa vya adui zake, vichwa vya hao waendao katika njia za dhambi.
Surely God he will shatter [the] head of enemies his scalp of hair [one who] goes about in guilt his.
22 Bwana alisema, “Nitawarudisha kutoka Bashani; nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari,
He has said [the] Lord from Bashan I will bring back I will bring back from [the] depths of [the] sea.
23 ili uweze kuchovya miguu yako katika damu ya adui zako, huku ndimi za mbwa wako zikiwa na fungu lake.”
So that - it may smash foot your in blood [the] tongue of dogs your [will be] from [the] enemies portion its.
24 Ee Mungu, maandamano yako yameonekana, maandamano ya Mungu wangu, Mfalme wangu, yakielekea patakatifu pake.
People have seen processions your O God [the] processions of God my king my in the holy place.
25 Mbele wako waimbaji, baada yao wapiga vinanda, pamoja nao wako wanawali wakipiga matari.
They went in front singers ([were] behind *L(S)*) musicians in among young women playing tambourines.
26 Msifuni Mungu katika kusanyiko kubwa, msifuni Bwana katika kusanyiko la Israeli.
In assemblies bless God Yahweh from [the] fountain of Israel.
27 Liko kabila dogo la Benyamini likiwaongoza, wakifuatwa na kundi kubwa la watawala wa Yuda, hatimaye watawala wa Zabuloni na Naftali.
There Benjamin - insignificant [is] ruling them [the] princes of Judah heaps of stones their [the] princes of Zebulun [the] princes of Naphtali.
28 Ee Mungu, amuru uwezo wako, Ee Mungu tuonyeshe nguvu zako, kama ulivyofanya hapo awali.
He has ordained God your strength your be strong! O God who you have acted for us.
29 Kwa sababu ya Hekalu lako Yerusalemu wafalme watakuletea zawadi.
From temple your at Jerusalem to you they will bring kings a gift.
30 Mkemee mnyama aliyeko kwenye manyasi, kundi la mafahali katikati ya ndama za mataifa. Na walete minara ya madini ya fedha wakinyenyekea. Tawanya mataifa yapendayo vita.
Rebuke [the] animal[s] of [the] reed[s] a herd of mighty [bulls] - with calves of peoples trampling on pieces of silver he has scattered peoples [which] wars they delight in.
31 Wajumbe watakuja kutoka Misri, Kushi atajisalimisha kwa Mungu.
They will come envoys from Egypt Cush it will cause to run hands its to God.
32 Mwimbieni Mungu, enyi falme za dunia, mwimbieni Bwana sifa,
O kingdoms of the earth sing to God sing praises to [the] Lord (Selah)
33 mwimbieni sifa yeye apandaye mbingu za kale zilizo juu, yeye angurumaye kwa sauti kuu.
To the rider in [the] heavens of heavens of ancient time there! he gives with voice his a voice of strength.
34 Tangazeni uwezo wa Mungu, ambaye fahari yake iko juu ya Israeli, ambaye uwezo wake uko katika anga.
Ascribe strength to God [is] over Israel majesty his and strength his [is] in the clouds.
35 Ee Mungu, wewe unatisha katika mahali patakatifu pako, Mungu wa Israeli huwapa watu wake uwezo na nguvu. Mungu Asifiwe!
[is] to be feared God from sanctuari your [the] God of Israel he [is] giving - strength and power to the people [be] blessed God.

< Zaburi 68 >