< Zaburi 46 >
1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora. Mtindo wa alamothi. Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.
Pour le chef musicien. Par les fils de Koré. D'après Alamoth. Dieu est notre refuge et notre force, une aide très présente dans les difficultés.
2 Kwa hiyo hatutaogopa, hata kama dunia ikiondolewa nayo milima ikiangukia moyoni mwa bahari.
C'est pourquoi nous n'aurons pas peur, même si la terre change, bien que les montagnes soient ébranlées au cœur des mers;
3 Hata kama maji yake yatanguruma na kuumuka, milima nayo ikitetemeka kwa mawimbi yake.
même si ses eaux mugissent et sont agitées, même si les montagnes tremblent de leur gonflement. (Selah)
4 Kuna mto ambao vijito vyake vinaufurahisha mji wa Mungu, mahali patakatifu ambako Aliye Juu Sana anaishi.
Il y a un fleuve dont les flots réjouissent la cité de Dieu, le lieu saint des tentes du Très-Haut.
5 Mungu yuko katikati yake, hautaanguka, Mungu atausaidia asubuhi na mapema.
Dieu est en elle. Elle ne sera pas déplacée. Dieu l'aidera à l'aube.
6 Mataifa yanafanya ghasia, falme zinaanguka, Yeye huinua sauti yake, dunia ikayeyuka.
Les nations étaient en colère. Les royaumes ont été bouleversés. Il a élevé la voix et la terre a fondu.
7 Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
Le Yahvé des armées est avec nous. Le Dieu de Jacob est notre refuge. (Selah)
8 Njooni mkaone kazi za Bwana jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi.
Venez, voyez les œuvres de l'Éternel, quelles désolations il a faites sur la terre.
9 Anakomesha vita hata miisho ya dunia, anakata upinde na kuvunjavunja mkuki, anateketeza ngao kwa moto.
Il fait cesser les guerres jusqu'à l'extrémité de la terre. Il casse l'arc, et brise la lance. Il brûle les chars dans le feu.
10 “Tulieni, mjue ya kwamba mimi ndimi Mungu; nitatukuzwa katikati ya mataifa, nitatukuzwa katika dunia.”
« Sois tranquille, et sache que je suis Dieu. Je serai exalté parmi les nations. Je serai exalté sur la terre. »
11 Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
Le Yahvédes armées est avec nous. Le Dieu de Jacob est notre refuge. (Selah)