< Zaburi 33 >

1 Mwimbieni Bwana kwa furaha, enyi wenye haki; kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo.
Радуйтеся, праведнии, о Господе: правым подобает похвала.
2 Msifuni Bwana kwa kinubi, mwimbieni sifa kwa zeze la nyuzi kumi.
Исповедайтеся Господеви в гуслех, во псалтири десятоструннем пойте Ему:
3 Mwimbieni wimbo mpya; pigeni kwa ustadi, na mpaze sauti za shangwe.
воспойте Ему песнь нову, добре пойте Ему со восклицанием:
4 Maana neno la Bwana ni haki na kweli, ni mwaminifu kwa yote atendayo.
яко право слово Господне, и вся дела Его в вере.
5 Bwana hupenda uadilifu na haki; dunia imejaa upendo wake usiokoma.
Любит милостыню и суд Господь, милости Господни исполнь земля.
6 Kwa neno la Bwana mbingu ziliumbwa, jeshi lao la angani kwa pumzi ya kinywa chake.
Словом Господним небеса утвердишася, и духом уст Его вся сила их:
7 Ameyakusanya maji ya bahari kama kwenye chungu; vilindi vya bahari ameviweka katika ghala.
собираяй яко мех воды морския, полагаяй в сокровищих бездны.
8 Dunia yote na imwogope Bwana, watu wote wa dunia wamche.
Да убоится Господа вся земля, от Негоже да подвижутся вси живущии по вселенней:
9 Kwa maana Mungu alisema, na ikawa, aliamuru na ikasimama imara.
яко Той рече, и быша: Той повеле, и создашася.
10 Bwana huzuia mipango ya mataifa, hupinga makusudi ya mataifa.
Господь разоряет советы языков, отметает же мысли людий и отметает советы князей.
11 Lakini mipango ya Bwana inasimama imara milele, makusudi ya moyo wake kwa vizazi vyote.
Совет же Господень во век пребывает, помышления сердца Его в род и род.
12 Heri taifa ambalo Bwana ni Mungu wao, watu ambao aliwachagua kuwa urithi wake.
Блажен язык, емуже есть Господь Бог Его, людие, яже избра в наследие Себе.
13 Kutoka mbinguni Bwana hutazama chini na kuwaona wanadamu wote;
С небесе призре Господь, виде вся сыны человеческия:
14 kutoka maskani mwake huwaangalia wote wakaao duniani:
от готоваго жилища Своего призре на вся живущыя на земли:
15 yeye ambaye huumba mioyo yao wote, ambaye huangalia kila kitu wanachokitenda.
создавый на едине сердца их, разумеваяй на вся дела их.
16 Hakuna mfalme aokokaye kwa ukubwa wa jeshi lake; hakuna shujaa aokokaye kwa wingi wa nguvu zake.
Не спасается царь многою силою, и исполин не спасется множеством крепости своея.
17 Farasi ni tumaini la bure kwa wokovu, licha ya nguvu zake nyingi, hawezi kuokoa.
Ложь конь во спасение, во множестве же силы своея не спасется.
18 Lakini macho ya Bwana yako kwa wale wamchao, kwa wale tumaini lao liko katika upendo wake usio na kikomo,
Се, очи Господни на боящыяся Его, уповающыя на милость Его:
19 ili awaokoe na mauti, na kuwahifadhi wakati wa njaa.
избавити от смерти душы их, и препитати я в глад.
20 Sisi tunamngojea Bwana kwa matumaini, yeye ni msaada wetu na ngao yetu.
Душа же наша чает Господа, яко помощник и защититель наш есть:
21 Mioyo yetu humshangilia, kwa maana tunalitumainia jina lake takatifu.
яко о Нем возвеселится сердце наше, и во имя святое Его уповахом.
22 Upendo wako usio na mwisho ukae juu yetu, Ee Bwana, tunapoliweka tumaini letu kwako.
Буди, Господи, милость Твоя на нас, якоже уповахом на Тя.

< Zaburi 33 >