< Zaburi 33 >

1 Mwimbieni Bwana kwa furaha, enyi wenye haki; kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo.
Rejoice, O ye righteous, in the LORD! For praise becometh the upright.
2 Msifuni Bwana kwa kinubi, mwimbieni sifa kwa zeze la nyuzi kumi.
Praise the LORD with the harp; Sing to him with the ten-stringed psaltery!
3 Mwimbieni wimbo mpya; pigeni kwa ustadi, na mpaze sauti za shangwe.
Sing to him a new song; Play skilfully amid the sound of trumpets!
4 Maana neno la Bwana ni haki na kweli, ni mwaminifu kwa yote atendayo.
For the word of the LORD is right, And all his acts are faithful.
5 Bwana hupenda uadilifu na haki; dunia imejaa upendo wake usiokoma.
He loveth justice and equity; The earth is full of the goodness of the LORD.
6 Kwa neno la Bwana mbingu ziliumbwa, jeshi lao la angani kwa pumzi ya kinywa chake.
By the word of the LORD were the heavens made, And all the hosts of them by the breath of his mouth.
7 Ameyakusanya maji ya bahari kama kwenye chungu; vilindi vya bahari ameviweka katika ghala.
He gathereth the waters of the sea, as a heap; He layeth up the deep in storehouses.
8 Dunia yote na imwogope Bwana, watu wote wa dunia wamche.
Let all the earth fear the LORD; Let all the inhabitants of the world stand in awe of him!
9 Kwa maana Mungu alisema, na ikawa, aliamuru na ikasimama imara.
For he spake, and it was done; He commanded, and it stood fast.
10 Bwana huzuia mipango ya mataifa, hupinga makusudi ya mataifa.
The LORD bringeth the devices of the nations to nothing; He frustrateth the designs of kingdoms.
11 Lakini mipango ya Bwana inasimama imara milele, makusudi ya moyo wake kwa vizazi vyote.
The purposes of the LORD stand for ever; The designs of his heart, to all generations.
12 Heri taifa ambalo Bwana ni Mungu wao, watu ambao aliwachagua kuwa urithi wake.
Happy the nation whose God is Jehovah; The people whom he hath chosen for his inheritance.
13 Kutoka mbinguni Bwana hutazama chini na kuwaona wanadamu wote;
The LORD looketh down from heaven; He beholdeth all the children of men;
14 kutoka maskani mwake huwaangalia wote wakaao duniani:
From his dwelling-place he beholdeth all the inhabitants of the earth, —
15 yeye ambaye huumba mioyo yao wote, ambaye huangalia kila kitu wanachokitenda.
He that formed the hearts of all, And observeth all their works.
16 Hakuna mfalme aokokaye kwa ukubwa wa jeshi lake; hakuna shujaa aokokaye kwa wingi wa nguvu zake.
A king is not saved by the number of his forces, Nor a hero by the greatness of his strength.
17 Farasi ni tumaini la bure kwa wokovu, licha ya nguvu zake nyingi, hawezi kuokoa.
The horse is a vain thing for safety, Nor can he deliver his master by his great strength.
18 Lakini macho ya Bwana yako kwa wale wamchao, kwa wale tumaini lao liko katika upendo wake usio na kikomo,
Behold, the eye of the LORD is upon them that fear him, —Upon them that trust in his goodness;
19 ili awaokoe na mauti, na kuwahifadhi wakati wa njaa.
To save them from the power of death, And keep them alive in famine.
20 Sisi tunamngojea Bwana kwa matumaini, yeye ni msaada wetu na ngao yetu.
The hope of our souls is in the LORD; He is our help and our shield.
21 Mioyo yetu humshangilia, kwa maana tunalitumainia jina lake takatifu.
Yea, in him doth our heart rejoice; In his holy name we have confidence.
22 Upendo wako usio na mwisho ukae juu yetu, Ee Bwana, tunapoliweka tumaini letu kwako.
May thy goodness be upon us, O LORD! According as we trust in thee!

< Zaburi 33 >