< Zaburi 22 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Kulungu wa Alfajiri.” Zaburi ya Daudi. Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali hivyo kuniokoa? Mbali hivyo na maneno ya kuugua kwangu?
Au chef de musique. Sur Ajéleth-Hashakhar. Psaume de David. Mon Dieu! mon Dieu! pourquoi m’as-tu abandonné, [te tenant] loin de mon salut, – des paroles de mon rugissement?
2 Ee Mungu wangu, ninalia mchana, lakini hunijibu, hata usiku, sinyamazi.
Mon Dieu! je crie de jour, mais tu ne réponds point; et de nuit, et il n’y a point de repos pour moi.
3 Hata hivyo umesimikwa katika kiti cha enzi kama Uliye Mtakatifu; wewe ni sifa ya Israeli.
Et toi, tu es saint, toi qui habites [au milieu des] louanges d’Israël.
4 Kwako wewe baba zetu waliweka tumaini lao, walikutumaini nawe ukawaokoa.
Nos pères se sont confiés en toi; ils se sont confiés, et tu les as délivrés.
5 Walikulilia wewe na ukawaokoa, walikutegemea wewe nao hawakuaibika.
Ils ont crié vers toi, et ils ont été sauvés; ils se sont confiés en toi, et ils n’ont point été confus.
6 Mimi ni mnyoo wala si mwanadamu, wanaume wamenibeza, na watu wamenidharau.
Mais moi, je suis un ver, et non point un homme; l’opprobre des hommes, et le méprisé du peuple.
7 Wote wanionao hunidhihaki, hunivurumishia matusi, wakitikisa vichwa vyao:
Tous ceux qui me voient se moquent de moi; ils ouvrent la bouche, ils hochent la tête:
8 Husema, “Anamtegemea Bwana, basi Bwana na amwokoe. Amkomboe basi, kwa maana anapendezwa naye.”
Il se confie à l’Éternel: qu’il le fasse échapper, qu’il le délivre, car il prend son plaisir en lui!
9 Hata hivyo ulinitoa tumboni, ukanifanya nikutegemee, hata nilipokuwa ninanyonya matiti ya mama yangu.
Mais c’est toi qui m’as tiré du sein [qui m’a porté]; tu m’as donné confiance sur les mamelles de ma mère.
10 Nimekabidhiwa kwako tangu kuzaliwa, toka tumboni mwa mama yangu umekuwa Mungu wangu.
C’est à toi que je fus remis dès la matrice; tu es mon Dieu dès le ventre de ma mère.
11 Usiwe mbali nami, kwa maana shida iko karibu na hakuna wa kunisaidia.
Ne te tiens pas loin de moi, car la détresse est proche, car il n’y a personne qui secoure.
12 Mafahali wengi wamenizunguka, mafahali wa Bashani wenye nguvu wamenizingira.
Beaucoup de taureaux m’ont environné, des puissants de Basan m’ont entouré;
13 Simba wangurumao wanaorarua mawindo yao hupanua vinywa vyao dhidi yangu.
Ils ouvrent leur gueule contre moi, comme un lion déchirant et rugissant.
14 Nimemiminwa kama maji, mifupa yangu yote imetoka katika viungo vyake. Moyo wangu umegeuka kuwa nta, umeyeyuka ndani yangu.
Je suis répandu comme de l’eau, et tous mes os se déjoignent; mon cœur est comme de la cire, il est fondu au-dedans de mes entrailles.
15 Nguvu zangu zimekauka kama kigae, ulimi wangu umegandamana na kaakaa la kinywa changu, kwa sababu umenilaza katika mavumbi ya kifo.
Ma vigueur est desséchée comme un têt, et ma langue est attachée à mon palais; et tu m’as mis dans la poussière de la mort.
16 Mbwa wamenizunguka, kundi la watu waovu limenizingira, wametoboa mikono yangu na miguu yangu.
Car des chiens m’ont environné, une assemblée de méchants m’a entouré; ils ont percé mes mains et mes pieds;
17 Naweza kuhesabu mifupa yangu yote, watu wananikodolea macho na kunisimanga.
Je compterais tous mes os. Ils me contemplent, ils me regardent;
18 Wanagawana nguo zangu wao kwa wao, na vazi langu wanalipigia kura.
Ils partagent entre eux mes vêtements, et sur ma robe ils jettent le sort.
19 Lakini wewe, Ee Bwana, usiwe mbali. Ee Nguvu yangu, uje haraka unisaidie.
Et toi, Éternel! ne te tiens pas loin; ma Force! hâte-toi de me secourir.
20 Okoa maisha yangu na upanga, uhai wangu wa thamani kutoka nguvu za mbwa.
Délivre mon âme de l’épée, mon unique de la patte du chien.
21 Niokoe kutoka kinywani mwa simba, niokoe kutoka pembe za mafahali mwitu.
Sauve-moi de la gueule du lion. Tu m’as répondu d’entre les cornes des buffles.
22 Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu, katika kusanyiko nitakusifu wewe.
J’annoncerai ton nom à mes frères, je te louerai au milieu de la congrégation.
23 Ninyi ambao mnamcha Bwana, msifuni! Ninyi nyote wazao wote wa Yakobo, mheshimuni yeye! Mcheni yeye, ninyi wazao wote wa Israeli!
Vous qui craignez l’Éternel, louez-le; toute la semence de Jacob, glorifiez-le; et révérez-le, vous, toute la semence d’Israël;
24 Kwa maana hakupuuza wala kudharau mateso ya aliyeonewa; hakumficha uso wake bali alisikiliza kilio chake ili amsaidie.
Car il n’a pas méprisé ni rejeté l’affliction de l’affligé, et n’a point caché sa face de lui; mais, quand il a crié vers lui, il l’a écouté.
25 Kwako wewe hutoka kiini cha sifa zangu katika kusanyiko kubwa, nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wakuchao wewe.
De toi [vient] ma louange dans la grande congrégation. Je paierai mes vœux devant ceux qui le craignent.
26 Maskini watakula na kushiba, wale wamtafutao Bwana watamsifu: mioyo yenu na iishi milele!
Les débonnaires mangeront et seront rassasiés; ceux qui cherchent l’Éternel le loueront; votre cœur vivra à toujours.
27 Miisho yote ya dunia itakumbuka na kumgeukia Bwana, nazo jamaa zote za mataifa watasujudu mbele zake,
Tous les bouts de la terre se souviendront, et ils se tourneront vers l’Éternel, et toutes les familles des nations se prosterneront devant toi.
28 kwa maana ufalme ni wa Bwana naye hutawala juu ya mataifa.
Car le royaume est à l’Éternel, et il domine au milieu des nations.
29 Matajiri wote wa dunia watasherehekea na kuabudu. Wote waendao mavumbini watapiga magoti mbele yake, wote ambao hawawezi kudumisha uhai wao.
Tous les gras de la terre mangeront et se prosterneront: devant lui se courberont tous ceux qui descendent dans la poussière, et celui qui ne peut faire vivre son âme.
30 Wazao wa baadaye watamtumikia yeye; vizazi vijavyo vitajulishwa habari za Bwana.
Une semence le servira; elle sera comptée au Seigneur comme une génération.
31 Watatangaza haki yake kwa watu ambao hawajazaliwa bado, kwa maana yeye ametenda hili.
Ils viendront et raconteront sa justice à un peuple qui naîtra, … qu’il a fait [ces choses].

< Zaburi 22 >