< Zaburi 114 >

1 Wakati Israeli walipotoka Misri, nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,
Halleluja! Als Israel aus Ägypten auszog, Jakobs Haus aus dem Volk fremder Sprache,
2 Yuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu, Israeli akawa milki yake.
da ward Juda sein Heiligtum, Israel sein Herrschaftsgebiet.
3 Bahari ilitazama ikakimbia, Yordani ulirudi nyuma,
Das Meer sah es und floh, der Jordan wandte sich rückwärts,
4 milima ilirukaruka kama kondoo dume, vilima kama wana-kondoo.
die Berge hüpften wie Widder, die Hügel gleichwie Lämmer.
5 Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia, nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,
Was war dir, o Meer, daß du flohest, dir, Jordan, daß du dich rückwärts wandtest?
6 enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume, enyi vilima, kama wana-kondoo?
(Was war euch) ihr Berge, daß ihr hüpftet wie Widder, ihr Hügel gleichwie Lämmer?
7 Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana, mbele za Mungu wa Yakobo,
Vor dem Anblick des Herrn erbebe, du Erde, vor dem Anblick des Gottes Jakobs,
8 aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji, mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.
der Felsen wandelt zum Wasserteich, Kieselgestein zum sprudelnden Quell!

< Zaburi 114 >