< Zaburi 114 >

1 Wakati Israeli walipotoka Misri, nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,
When went out Israel from Egypt [the] house of Jacob from a people speaking a foreign language.
2 Yuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu, Israeli akawa milki yake.
It became Judah sanctuary his Israel dominion his.
3 Bahari ilitazama ikakimbia, Yordani ulirudi nyuma,
The sea it saw and it fled the Jordan it turned around to backwards.
4 milima ilirukaruka kama kondoo dume, vilima kama wana-kondoo.
The mountains they skipped about like rams hills like young ones of sheep.
5 Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia, nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,
What? [is] to you O sea that you will flee O Jordan you will turn around to backwards.
6 enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume, enyi vilima, kama wana-kondoo?
O mountains you will skip about like rams O hills like young ones of sheep.
7 Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana, mbele za Mungu wa Yakobo,
From to before [the] lord tremble O earth from to before [the] God of Jacob.
8 aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji, mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.
Who turned the rock a pool of water flint into spring of his water.

< Zaburi 114 >