< Zaburi 104 >
1 Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, umejivika utukufu na enzi.
Blagoslivljaj Jahvu, dušo moja, Jahve, Bože moj, silno si velik! Odjeven veličanstvom i ljepotom,
2 Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, amezitandaza mbingu kama hema
svjetlošću ogrnut kao plaštem! Nebo si razapeo kao šator,
3 na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, na hupanda kwenye mbawa za upepo.
na vodama sagradio dvorove svoje. Od oblaka praviš kola svoja, na krilima vjetrova putuješ.
4 Huzifanya pepo kuwa wajumbe wake, miali ya moto watumishi wake.
Vjetrove uzimaš za glasnike, a žarki oganj za slugu svojega.
5 Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.
Zemlju si stavio na stupove njene: neće se poljuljati u vijeke vjekova,
6 Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.
pokrio si je vodama bezdanim k'o haljinom, iznad bregova stajahu vode;
7 Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
na tvoju se prijetnju povukoše, od tvoje grmljavine zadrhtaše.
8 yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
Bregovi se digoše, doline spustiše na mjesto koje si im odredio.
9 Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.
Odredio si granicu koju ne smiju prijeći, da opet ne pokriju zemlju.
10 Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.
Izvore svraćaš u potoke što žubore među brdima.
11 Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.
Oni poje sve živine poljske, divlji magarci žeđ gase u njima.
12 Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.
Uz njih se gnijezde ptice nebeske i pjevaju među granama.
13 Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
Ti natapaš bregove iz dvorova svojih, zemlja se nasićuje plodom tvojih ruku.
14 Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
Ti daješ te niče trava za stoku i bilje na korist čovjeku da izvede kruh iz zemlje
15 divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, na mkate wa kutia mwili nguvu.
i vino što razvedruje srce čovječje; da uljem lice osvježi i da kruh okrijepi srce čovjeku.
16 Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
Stabla se Jahvina napajaju hranom, cedri libanonski koje on zasadi.
17 Humo ndege hufanya viota vyao, korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.
Ondje se ptice gnijezde, u čempresu dom je rodin.
18 Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, majabali ni kimbilio la pelele.
Visoki bregovi daju kozorogu a pećine jazavcu sklonište.
19 Mwezi hugawanya majira, na jua hutambua wakati wake wa kutua.
Ti si stvorio mjesec da označuje vremena i sunce znade kada ima zaći.
20 Unaleta giza, kunakuwa usiku, wanyama wote wa mwituni huzurura.
Kad razastreš tmine i noć se spusti, tad se šuljaju u njoj životinje šumske.
21 Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
Lavići riču za plijenom i od Boga hranu traže.
22 Jua huchomoza, nao huondoka, hurudi na kulala katika mapango yao.
Kad sunce ograne, nestaju i liježu na ležaje.
23 Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, katika kazi yake mpaka jioni.
Tad čovjek izlazi na dnevni posao i na rad do večeri.
24 Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
Kako su brojna tvoja djela, o Jahve! Sve si to mudro učinio: puna je zemlja stvorenja tvojih.
25 Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, imejaa viumbe visivyo na idadi, vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
Eno mora, velika i široka, u njemu vrve gmazovi bez broja, životinje male i velike.
26 Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
Onud prolaze nemani, Levijatan kojeg stvori da se igra u njemu.
27 Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
I sva ova bića željno čekaju da ih nahraniš na vrijeme.
28 Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
Daješ li im, tada sabiru: otvaraš li ruku, nasite se dobrima.
29 Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
Sakriješ li lice svoje, tad se rastuže; ako dah im oduzmeš, ugibaju i opet se u prah vraćaju.
30 Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
Pošalješ li dah svoj, opet nastaju, i tako obnavljaš lice zemlje.
31 Utukufu wa Bwana na udumu milele, Bwana na azifurahie kazi zake:
Neka dovijeka traje slava Jahvina: nek' se raduje Jahve u djelima svojim!
32 yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.
On pogleda zemlju i ona se potrese, dotakne bregove, oni se zadime.
33 Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
Pjevat ću Jahvi dokle god živim, svirat ću Bogu svome dokle god me bude.
34 Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
Bilo mu milo pjevanje moje! Ja ću se radovati u Jahvi.
35 Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.
Nek' zločinci sa zemlje nestanu i bezbožnika nek' više ne bude! Blagoslivljaj Jahvu, dušo moja! Aleluja!