< Mithali 9 >
1 Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo zake saba.
La sagesse a construit sa maison. Elle a défini ses sept piliers.
2 Ameandaa nyama na kuchanganya divai yake; pia ameandaa meza yake.
Elle a préparé sa viande. Elle a mélangé son vin. Elle a également mis sa table.
3 Amewatuma watumishi wake wa kike, naye huita kutoka mahali pa juu sana pa mji.
Elle a envoyé ses servantes. Elle crie depuis les plus hauts lieux de la ville:
4 Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa!
« Celui qui est simple, qu'il se tourne ici! » Quant à celui qui est dépourvu d'intelligence, elle lui dit,
5 Njooni, mle chakula changu na mnywe divai niliyoichanganya.
« Viens, mange un peu de mon pain, Buvez un peu du vin que j'ai mélangé!
6 Acheni njia zenu za ujinga nanyi mtaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
Abandonnez vos habitudes simples, et vivez. Marchez dans la voie de la compréhension. »
7 “Yeyote anayemkosoa mwenye mzaha hukaribisha matukano; yeyote anayekemea mtu mwovu hupatwa na matusi.
Celui qui corrige un moqueur s'expose à être insulté. Celui qui réprouve un homme méchant s'expose à des abus.
8 Usimkemee mwenye mzaha la sivyo atakuchukia; mkemee mwenye hekima naye atakupenda.
Ne réprimandez pas le moqueur, de peur qu'il ne vous haïsse. Réprimandez une personne sage, et elle vous aimera.
9 Mfundishe mtu mwenye hekima naye atakuwa na hekima zaidi; mfundishe mtu mwadilifu naye atazidi kufundishika.
Instruisez une personne sage, et elle sera encore plus sage. Enseignez à un juste, et il augmentera son savoir.
10 “Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, na kumjua Aliye Mtakatifu ni ufahamu.
La crainte de Yahvé est le commencement de la sagesse. La connaissance du Saint est la compréhension.
11 Kwa maana kwa msaada wangu siku zako zitakuwa nyingi, na miaka itaongezwa katika maisha yako.
Car par moi vos jours seront multipliés. Les années de votre vie seront augmentées.
12 Kama wewe una hekima, hekima yako itakupa tuzo; kama wewe ni mtu wa mzaha, wewe mwenyewe ndiwe utateseka.”
Si tu es sage, tu l'es pour toi-même. Si vous vous moquez, vous seul le supporterez.
13 Mwanamke aitwaye Mpumbavu ana kelele; hana adabu na hana maarifa.
La femme folle est bruyante, indiscipliné, et ne sait rien.
14 Huketi kwenye mlango wa nyumba yake, juu ya kiti katika mahali pa juu sana pa mji,
Elle est assise à la porte de sa maison, sur un siège dans les hauts lieux de la ville,
15 akiita wale wapitao karibu, waendao moja kwa moja kwenye njia yao.
pour appeler ceux qui passent, qui vont droit sur leur chemin,
16 Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa ndani!”
« Celui qui est simple, qu'il se rende ici. » Quant à celui qui est dépourvu d'intelligence, elle lui dit,
17 “Maji yaliyoibiwa ni matamu; chakula kinacholiwa sirini ni kitamu!”
« L'eau volée est douce. La nourriture mangée en secret est agréable. »
18 Lakini hawajui hata kidogo kuwa wafu wako humo, kwamba wageni wake huyo mwanamke wako katika vilindi vya kuzimu. (Sheol )
Mais il ne sait pas que les esprits des défunts sont là, que ses invités sont dans les profondeurs de Sheol. (Sheol )