< Mithali 3 >

1 Mwanangu, usisahau mafundisho yangu, bali zitunze amri zangu moyoni mwako,
Oğlum, unutma öğrettiklerimi, Aklında tut buyruklarımı.
2 kwa kuwa zitakuongezea miaka mingi ya maisha yako na kukuletea mafanikio.
Çünkü bunlar ömrünü uzatacak, Yaşam yıllarını, esenliğini artıracaktır.
3 Usiache kamwe upendo na uaminifu vitengane nawe; vifunge shingoni mwako, viandike katika ubao wa moyo wako.
Sevgiyi, sadakati hiç yanından ayırma, Bağla onları boynuna, Yaz yüreğinin levhasına.
4 Ndipo utapata kibali na jina zuri mbele za Mungu na mwanadamu.
Böylece Tanrı'nın ve insanların gözünde Beğeni ve saygınlık kazanacaksın.
5 Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote wala usizitegemee akili zako mwenyewe;
RAB'be güven bütün yüreğinle, Kendi aklına bel bağlama.
6 katika njia zako zote mkiri yeye, naye atayanyoosha mapito yako.
Yaptığın her işte RAB'bi an, O senin yolunu düze çıkarır.
7 Usiwe mwenye hekima machoni pako mwenyewe; mche Bwana ukajiepushe na uovu.
Kendini bilge biri olarak görme, RAB'den kork, kötülükten uzak dur.
8 Hii itakuletea afya mwilini mwako, na mafuta kwenye mifupa yako.
Böylece bedenin sağlık Ve ferahlık bulur.
9 Mheshimu Bwana kwa mali zako na kwa malimbuko ya mazao yako yote;
Servetinle ve ürününün turfandasıyla RAB'bi onurlandır.
10 ndipo ghala zako zitakapojaa hadi kufurika, viriba vyako vitafurika kwa mvinyo mpya.
O zaman ambarların tıka basa dolar, Teknelerin yeni şarapla dolup taşar.
11 Mwanangu, usiidharau adhabu ya Bwana na usichukie kukaripiwa naye,
Oğlum, RAB'bin terbiye edişini hafife alma, O'nun azarlamasından usanma.
12 kwa sababu Bwana huwaadibisha wale awapendao, kama vile baba afanyavyo kwa mwana apendezwaye naye.
Çünkü RAB, oğlundan hoşnut bir baba gibi, Sevdiğini azarlar.
13 Heri mtu yule aonaye hekima, mtu yule apataye ufahamu,
Bilgeliğe erişene, Aklı bulana ne mutlu!
14 kwa maana hekima ana faida kuliko fedha na mapato yake ni bora kuliko ya dhahabu safi.
Gümüş kazanmaktansa onu kazanmak daha iyidir. Onun yararı altından daha çoktur.
15 Hekima ana thamani kuliko marijani; hakuna chochote unachokitamani kinachoweza kulinganishwa naye.
Daha değerlidir mücevherden, Dileyeceğin hiçbir şey onunla kıyaslanamaz.
16 Maisha marefu yako katika mkono wake wa kuume; katika mkono wake wa kushoto kuna utajiri na heshima.
Sağ elinde uzun ömür, Sol elinde zenginlik ve onur vardır.
17 Njia zake zinapendeza, mapito yake yote ni amani.
Yolları sevinç yollarıdır, Evet, bütün yolları esenliğe çıkarır.
18 Yeye ni mti wa uzima kwa wale wanaomkumbatia; wale wamshikao watabarikiwa.
Bilgelik yaşam ağacıdır ona sarılanlara, Ne mutlu ona sımsıkı tutunanlara!
19 Kwa hekima Bwana aliiweka misingi ya dunia, kwa ufahamu aliziweka mbingu mahali pake;
RAB dünyanın temelini bilgelikle attı, Gökleri akıllıca yerleştirdi.
20 kwa maarifa yake vilindi viligawanywa, nayo mawingu yanadondosha umande.
Bilgisiyle enginler yarıldı, Bulutlar suyunu verdi.
21 Mwanangu, hifadhi maamuzi mema na busara, usiache vitoke machoni pako;
Oğlum, sağlam öğüde, sağgörüye tutun. Sakın gözünü ayırma onlardan.
22 ndipo vitakapokuwa uzima nafsini mwako na pambo la neema shingoni mwako.
Onlar sana yaşam verecek Ve boynuna güzel bir süs olacak.
23 Kisha utaenda katika njia yako salama, wala mguu wako hautajikwaa;
O zaman güvenlik içinde yol alırsın, Sendelemeden.
24 ulalapo, hautaogopa; ulalapo usingizi wako utakuwa mtamu.
Korkusuzca yatar, Tatlı tatlı uyursun.
25 Usiogope maafa ya ghafula au maangamizi yanayowapata waovu,
Beklenmedik felaketten, Ya da kötülerin uğradığı yıkımdan korkma.
26 kwa kuwa Bwana atakuwa tumaini lako na kuepusha mguu wako kunaswa katika mtego.
Çünkü senin güvencen RAB'dir, Tuzağa düşmekten seni O koruyacaktır.
27 Usizuie wema kwa wale wanaostahili ikiwa katika uwezo wako kutenda.
Elinden geldikçe, İyiliğe hakkı olanlardan iyiliği esirgeme.
28 Usimwambie jirani yako, “Njoo baadaye, nitakupa kesho”: wakati wewe unacho kitu kile karibu nawe.
Elinde varken komşuna, “Bugün git, yarın gel, o zaman veririm” deme.
29 Usifanye hila ya kumdhuru jirani yako, ambaye anaishi karibu na wewe akikuamini.
Sana güvenerek yanında yaşayan komşuna Kötülük tasarlama.
30 Usimshtaki mtu bila sababu, wakati hajakutenda dhara lolote.
Sana kötülük etmemiş biriyle Yok yere çekişme.
31 Usimwonee wivu mtu mwenye jeuri wala kuchagua njia yake iwayo yote,
Zorba kişiye imrenme, Onun yollarından hiçbirini seçme.
32 kwa kuwa Bwana humchukia mtu mpotovu, lakini siri yake iko kwa mwenye haki.
Çünkü RAB sapkınlardan tiksinir, Ama doğruların candan dostudur.
33 Laana ya Bwana i juu ya nyumba ya mwovu, lakini yeye huibariki nyumba ya mwenye haki.
RAB kötülerin evini lanetler, Doğruların oturduğu yeriyse kutsar.
34 Huwadhihaki wale wanaodhihaki, lakini huwapa neema wale wanyenyekevu.
RAB alaycılarla alay eder, Ama alçakgönüllülere lütfeder.
35 Wenye hekima hurithi heshima, bali huwaaibisha wapumbavu.
Bilge kişiler onuru miras alacak, Akılsızlara yalnız utanç kalacak.

< Mithali 3 >