< Hesabu 1 >

1 Bwana alisema na Mose katika Jangwa la Sinai, katika Hema la Kukutania, siku ya kwanza ya mwezi wa pili, katika mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Akamwambia,
And he spoke Yahweh to Moses in [the] wilderness of Sinai in [the] tent of meeting on [day] one of the month second in the year second of going out their from [the] land of Egypt saying.
2 “Hesabu watu wa jumuiya yote ya Waisraeli kwa kufuata koo zao na jamaa zao, ukiorodhesha kila mwanaume kwa jina lake, mmoja mmoja.
Lift up [the] head of all [the] congregation of [the] people of Israel to clans their to [the] house of ancestors their by [the] number of names of every male to heads their.
3 Wewe na Aroni mtawahesabu kwa migawanyo yao wanaume wote katika Israeli wenye miaka ishirini na kuendelea ambao wanaweza kutumika katika jeshi.
From a son of twenty year[s] and up-wards every [one who] goes forth warfare in Israel you will enroll them to military groups their you and Aaron.
4 Mwanaume mmoja kutoka kila kabila, kila aliye kiongozi wa jamaa yake, atawasaidia.
And with you they will be a man a man to the tribe a man [is the] head of [the] house of ancestors his he.
5 Haya ndiyo majina ya wanaume watakaowasaidia: “kutoka Reubeni, ni Elisuri mwana wa Shedeuri;
And these [are] [the] names of the men who they will stand with you for Reuben Elizur [the] son of Shedeur.
6 kutoka Simeoni, ni Shelumieli mwana wa Surishadai;
For Simeon Shelumiel [the] son of Zurishaddai.
7 kutoka Yuda, ni Nashoni mwana wa Aminadabu;
For Judah Nahshon [the] son of Amminadab.
8 kutoka Isakari, ni Nethaneli mwana wa Suari;
For Issachar Nethanel [the] son of Zuar.
9 kutoka Zabuloni, ni Eliabu mwana wa Heloni;
For Zebulun Eliab [the] son of Helon.
10 kutoka wana wa Yosefu: kutoka Efraimu, ni Elishama mwana wa Amihudi; kutoka Manase, ni Gamalieli mwana wa Pedasuri;
For [the] sons of Joseph for Ephraim Elishama [the] son of Ammihud for Manasseh Gamaliel [the] son of Pedahzur.
11 kutoka Benyamini, ni Abidani mwana wa Gideoni;
For Benjamin Abidan [the] son of Gideoni.
12 kutoka Dani, ni Ahiezeri mwana wa Amishadai;
For Dan Ahiezer [the] son of Ammishaddai.
13 kutoka Asheri, ni Pagieli mwana wa Okrani;
For Asher Pagiel [the] son of Ocran.
14 kutoka Gadi, ni Eliasafu mwana wa Deueli;
For Gad Eliasaph [the] son of Deuel.
15 kutoka Naftali, ni Ahira mwana wa Enani.”
For Naphtali Ahira [the] son of Enan.
16 Hawa walikuwa wanaume walioteuliwa kutoka jumuiya, viongozi wa makabila ya baba zao. Walikuwa wakuu wa koo za Israeli.
These ([were those] called *Q(K)*) [of] the congregation [the] leaders of [the] tribes of ancestors their [were] [the] heads of [the] families of Israel they.
17 Mose na Aroni wakawachukua wanaume hao waliokuwa wamepewa majina yao,
And he took Moses and Aaron the men these who they had been designated by names.
18 wakaita jumuiya yote pamoja katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Watu wakaonyesha nasaba zao kwa koo zao na jamaa zao, nao wanaume waliokuwa na miaka ishirini au zaidi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja,
And all the congregation they summoned on [day] one of the month second and they recorded their ancestry on clans their to [the] house of ancestors their by [the] number of names from a son of twenty year[s] and up-wards to heads their.
19 kama Bwana alivyomwagiza Mose. Hivyo aliwahesabu katika Jangwa la Sinai:
Just as he had commanded Yahweh Moses and he enrolled them in [the] wilderness of Sinai.
20 Kutoka wazao wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
And they were [the] descendants of Reuben [the] firstborn of Israel genealogies their to clans their to [the] house of ancestors their by [the] number of names to heads their every male from a son of twenty year[s] and up-wards every [one who] goes forth warfare.
21 Idadi kutoka kabila la Reubeni ilikuwa watu 46,500.
Enrolled [men] their of [the] tribe of Reuben [were] six and forty thousand and five hundred.
22 Kutoka wazao wa Simeoni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi walihesabiwa na kuorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Of [the] descendants of Simeon genealogies their to clans their to [the] house of ancestors their enrolled [men] its by [the] number of names to heads their every male from a son of twenty year[s] and up-wards every [one who] goes forth warfare.
23 Idadi kutoka kabila la Simeoni walikuwa watu 59,300.
Enrolled [men] their of [the] tribe of Simeon [were] nine and fifty thousand and three hundred.
24 Kutoka wazao wa Gadi: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Of [the] descendants of Gad genealogies their to clans their to [the] house of ancestors their by [the] number of names from a son of twenty year[s] and up-wards every [one who] goes forth warfare.
25 Idadi kutoka kabila la Gadi walikuwa watu 45,650.
Enrolled [men] their of [the] tribe of Gad [were] five and forty thousand and six hundred and fifty.
26 Kutoka wazao wa Yuda: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Of [the] descendants of Judah genealogies their to clans their to [the] house of ancestors their by [the] number of names from a son of twenty year[s] and up-wards every [one who] goes forth warfare.
27 Idadi kutoka kabila la Yuda walikuwa watu 74,600.
Enrolled [men] their of [the] tribe of Judah [were] four and seventy thousand and six hundred.
28 Kutoka wazao wa Isakari: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Of [the] descendants of Issachar genealogies their to clans their to [the] house of ancestors their by [the] number of names from a son of twenty year[s] and up-wards every [one who] goes forth warfare.
29 Idadi kutoka kabila la Isakari walikuwa watu 54,400.
Enrolled [men] their of [the] tribe of Issachar [were] four and fifty thousand and four hundred.
30 Kutoka wazao wa Zabuloni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Of [the] descendants of Zebulun genealogies their to clans their to [the] house of ancestors their by [the] number of names from a son of twenty year[s] and up-wards every [one who] goes forth warfare.
31 Idadi kutoka kabila la Zabuloni walikuwa watu 57,400.
Enrolled [men] their of [the] tribe of Zebulun [were] seven and fifty thousand and four hundred.
32 Kutoka wana wa Yosefu: Kutoka wazao wa Efraimu: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Of [the] descendants of Joseph of [the] descendants of Ephraim genealogies their to clans their to [the] house of ancestors their by [the] number of names from a son of twenty year[s] and up-wards every [one who] goes forth warfare.
33 Idadi kutoka kabila la Efraimu walikuwa watu 40,500.
Enrolled [men] their of [the] tribe of Ephraim [were] forty thousand and five hundred.
34 Kutoka wazao wa Manase: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Of [the] descendants of Manasseh genealogies their to clans their to [the] house of ancestors their by [the] number of names from a son of twenty year[s] and up-wards every [one who] goes forth warfare.
35 Idadi kutoka kabila la Manase walikuwa watu 32,200.
Enrolled [men] their of [the] tribe of Manasseh [were] two and thirty thousand and two hundred.
36 Kutoka wazao wa Benyamini: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Of [the] descendants of Benjamin genealogies their to clans their to [the] house of ancestors their by [the] number of names from a son of twenty year[s] and up-wards every [one who] goes forth warfare.
37 Idadi kutoka kabila la Benyamini walikuwa watu 35,400.
Enrolled [men] their of [the] tribe of Benjamin [were] five and thirty thousand and four hundred.
38 Kutoka wazao wa Dani: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Of [the] descendants of Dan genealogies their to clans their to [the] house of ancestors their by [the] number of names from a son of twenty year[s] and up-wards every [one who] goes forth warfare.
39 Idadi kutoka kabila la Dani walikuwa watu 62,700.
Enrolled [men] their of [the] tribe of Dan [were] two and sixty thousand and seven hundred.
40 Kutoka wazao wa Asheri: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
Of [the] descendants of Asher genealogies their to clans their to [the] house of ancestors their by [the] number of names from a son of twenty year[s] and up-wards every [one who] goes forth warfare.
41 Idadi kutoka kabila la Asheri walikuwa watu 41,500.
Enrolled [men] their of [the] tribe of Asher [were] one and forty thousand and five hundred.
42 Kutoka wazao wa Naftali: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
[the] descendants of Naphtali genealogies their to clans their to [the] house of ancestors their by [the] number of names from a son of twenty year[s] and up-wards every [one who] goes forth warfare.
43 Idadi kutoka kabila la Naftali walikuwa watu 53,400.
Enrolled [men] their of [the] tribe of Naphtali [were] three and fifty thousand and four hundred.
44 Hawa walikuwa wanaume waliohesabiwa na Mose, Aroni na viongozi kumi na wawili wa Israeli, kila mmoja akiwakilisha jamaa yake.
These [were] the enrolled [men] whom he enrolled Moses and Aaron and [the] leaders of Israel two [plus] ten man a man one for [the] house of ancestors his they were.
45 Wanaume wote Waisraeli waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi la Israeli walihesabiwa kufuatana na jamaa zao.
And they were all [those] enrolled of [the] people of Israel to [the] house of ancestors their from a son of twenty year[s] and up-wards every [one who] goes forth warfare in Israel.
46 Jumla ya hesabu yao ilikuwa watu 603,550.
And they were all those enrolled six hundred thousand and three thousand and five hundred and fifty.
47 Hata hivyo, jamaa ya kabila la Lawi hawakuhesabiwa pamoja na wengine.
And the Levites to [the] tribe of ancestors their not they were enrolled in midst of them.
48 Bwana alikuwa amemwambia Mose:
And he had spoken Yahweh to Moses saying.
49 “Kamwe usihesabu kabila la Lawi wala kuwaweka pamoja katika hesabu ya Waisraeli wengine.
Only [the] tribe of Levi not you will enroll and head their not you will lift up in among [the] people of Israel.
50 Badala yake, waweke Walawi kuwa viongozi wa Maskani ya Ushuhuda, juu ya samani zake na kila kitu kilichomo ndani yake. Wao watabeba Maskani na samani zake zote; wataitunza na kupiga kambi kuizunguka.
And you appoint the Levites over [the] tabernacle of the testimony and over all articles its and over all that [belongs] to it they they will carry the tabernacle and all articles its and they they will serve it and around the tabernacle they will encamp.
51 Wakati wowote Maskani inapohamishwa, Walawi wataifungua, na wakati wowote maskani inapotakiwa kusimamishwa, Walawi watafanya kazi hiyo. Mtu yeyote mwingine ambaye atasogea karibu nayo atauawa.
And when sets out the tabernacle they will take down it the Levites and when encamps the tabernacle they will raise up it the Levites and the stranger approaching he will be put to death.
52 Waisraeli watapiga mahema yao kwa makundi makundi, kila mwanaume katika kambi yake mwenyewe chini ya bendera yake.
And they will encamp [the] people of Israel everyone at camp his and everyone at standard his to military groups their.
53 Hata hivyo, Walawi watapiga mahema yao kuzunguka Maskani ya Ushuhuda ili ghadhabu isiipate jumuiya ya Waisraeli. Walawi watawajibika kwa utunzaji wa Maskani ya Ushuhuda.”
And the Levites they will encamp around [the] tabernacle of the testimony and not it will be wrath towards [the] congregation of [the] people Israel and they will keep the Levites [the] duty of [the] tabernacle of the testimony.
54 Waisraeli walifanya yote haya sawasawa kama Bwana alivyomwamuru Mose.
And they did [the] people of Israel according to all that he had commanded Yahweh Moses so they did.

< Hesabu 1 >