< Hesabu 6 >

1 Bwana akamwambia Mose,
И рече Господь к Моисею, глаголя:
2 “Sema na Waisraeli na uwaambie: ‘Ikiwa mwanaume au mwanamke anataka kuweka nadhiri maalum, nadhiri ya kutengwa kwa ajili ya Bwana kama Mnadhiri,
глаголи сыном Израилевым и речеши к ним: муж или жена, иже аше обещается зело обетом, еже очиститися чистотою Господу,
3 ni lazima ajitenge na mvinyo na kinywaji kingine chochote chenye chachu, na kamwe asinywe siki itokanayo na mvinyo au itokanayo na kinywaji kingine chenye chachu. Kamwe asinywe maji ya zabibu wala kula zabibu mbichi au kavu.
да воздержится от вина и сикера, и оцта винна и оцта от сикера да не пиет: и, елика делаются от грозд винных, да не пиет, и гроздия свежаго и сухаго да не снест.
4 Kwa muda wote atakaokuwa Mnadhiri, kamwe hatakula chochote kitokanacho na mzabibu, sio mbegu wala maganda.
Во вся дни обета своего от всех, елика бывают от винничины вина, от кости и до скорлупы да не пиете, ниже ясте от всего.
5 “‘Kwa muda wote wa nadhiri yake ya kujitenga kwa ajili ya Bwana, wembe hautapita kichwani mwake. Ni lazima awe mtakatifu mpaka kipindi cha kujitenga kwake kwa ajili ya Bwana kiishe; ni lazima aache nywele za kichwa chake zirefuke.
Во вся дни обета очищения своего бритва да не взыдет на главу его, дондеже скончаются дние, елики обещал есть Господу: свят будет растяй власы главы своея.
6 Kwa kipindi chochote cha kujitenga kwa ajili ya Bwana hatakaribia maiti.
Во вся дни обета своего Господу, ко всякой душе скончавшейся да не внидет.
7 Hata kama baba yake mwenyewe au mama au kaka au dada akifa, hatajinajisi mwenyewe kwa taratibu za ibada kwa ajili yao, kwa sababu ishara ya kujiweka wakfu kwake kwa Mungu ipo katika kichwa chake.
Над отцем и над материю, и над братом и над сестрою, да не осквернится над ними, умершым им, яко обет Бога его на главе его.
8 Kwa kipindi chote cha kujitenga kwake yeye ni wakfu kwa Bwana.
Вся дни обета его свят будет Господу.
9 “‘Kama mtu yeyote akifa ghafula karibu naye, atakuwa ametiwa unajisi nywele zake alizoziweka wakfu, hivyo ni lazima anyoe nywele zake siku ya utakaso wake, yaani siku ya saba.
Аше же кто смертию внезапу умрет у него, абие осквернится глава обета его, и обриет главу свою, в оньже день очистится, в день седмый да обриется,
10 Kisha siku ya nane ni lazima alete hua wawili au makinda mawili ya njiwa kwa kuhani katika mlango wa Hema la Kukutania.
и в день осмый да принесет два горличища или два птенца голубина к жерцу пред двери скинии свидения:
11 Kuhani atatoa mmoja kama sadaka ya dhambi, na mwingine kama sadaka ya kuteketezwa ili kufanya upatanisho kwa ajili yake kwa sababu ametenda dhambi kwa kuwepo mbele ya maiti. Siku iyo hiyo atakiweka wakfu kichwa chake.
и да сотворит жрец едину греха ради, и другую во всесожжение, и да помолится о нем жрец, о нихже согреши, о души, и освятит главу свою в той день, в оньже освятися Господу, во дни обета своего.
12 Ni lazima ajitoe kabisa kwa Bwana kwa kipindi cha kujitenga kwake, na ni lazima atoe mwana-kondoo wa mwaka mmoja kama sadaka ya hatia. Siku zilizopita hazitahesabiwa kwa sababu alijitia unajisi katika siku zake za kujitenga.
И да приведет агнца единолетна в преступление, и дние прежнии да не будут ему в число, понеже осквернися глава обета его.
13 “‘Basi hii ndiyo sheria kwa ajili ya Mnadhiri baada ya kipindi chake cha kujitenga kupita. Ataletwa kwenye ingilio la Hema la Kukutania.
И сей закон обещавшагося, в оньже день скончает дни обета своего, да принесет сам к дверем скинии свидения:
14 Hapo atatoa sadaka zake kwa Bwana: yaani, mwana-kondoo wa mwaka mmoja asiye na waa kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, kondoo mke wa mwaka mmoja asiye na waa kwa ajili ya sadaka ya dhambi, kondoo dume asiye na waa kwa ajili ya sadaka ya amani,
и да приведет дар свой Господу агнца единолетна непорочна единаго во всесожжение, и агницу единолетну едину непорочну греха ради, и овна единаго непорочна во спасение,
15 pamoja na sadaka zake za nafaka na za vinywaji, na kikapu cha mikate isiyotiwa chachu, yaani maandazi yaliyotengenezwa kwa unga laini uliochanganywa na mafuta, na mikate myembamba iliyopakwa mafuta.
и кош опресноков от муки пшеничны, хлебы смешаны с елеем, и опресноки помазаны елеем, и жертву их и возлияние их.
16 “‘Kuhani atavileta vitu hivyo mbele za Bwana na kufanya sadaka ya dhambi na sadaka ya kuteketezwa.
И да принесет жрец пред Господа, и да сотворит еже греха ради его, и всесожжение его,
17 Ataleta pia kikapu cha mikate isiyotiwa chachu, na atatoa dhabihu kondoo dume kama sadaka ya amani kwa Bwana, pamoja na sadaka yake ya nafaka na sadaka ya kinywaji.
и овна сотворит жертву спасения Господу на кошнице опресноков, и да сотворит жрец жертву его и возлияние его.
18 “‘Kisha kwenye ingilio la Hema la Kukutania, Mnadhiri ni lazima anyoe nywele zake ambazo alikuwa ameziweka wakfu. Atazichukua hizo nywele na kuziweka ndani ya moto ulio chini ya dhabihu ya sadaka ya amani.
И да обриет обещавый пред дверми скинии свидения главу обета своего, и да возложит власы на огнь, иже есть под жертвою спасения:
19 “‘Baada ya Mnadhiri kunyoa hizo nywele zake za kujitenga kwake, kuhani atampa mikononi mwake bega la kondoo dume lililochemshwa, na pia andazi na mkate mwembamba kutoka kwenye kikapu, vyote vikiwa vimetengenezwa bila kuwekwa chachu.
и да возмет жрец рамо варено от овна, и хлеб един опресночный от кошницы, и опреснок един, и да возложит на руки обещавшемуся, по обритии главы его,
20 Kisha kuhani ataviinua mbele za Bwana kama sadaka ya kuinua; ni vitakatifu na ni mali ya kuhani, pamoja na kile kidari kilichoinuliwa na lile paja lililotolewa. Baada ya hayo, Mnadhiri anaweza kunywa divai.
и да принесет я жрец возложение пред Господа: свято да будет жерцу на грудех возложения и на раме участия: и по сих обещавыйся да пиет вино.
21 “‘Hii ndiyo sheria ya Mnadhiri ambaye anaweka nadhiri kwa matoleo yake kwa Bwana kufuatana na kujitenga kwake, zaidi ya chochote kile anachoweza kupata. Ni lazima atimize nadhiri aliyoiweka kufuatana na sheria ya Mnadhiri.’”
Сей закон обещавшагося, иже аще обещает дар Господу о обете, кроме сих яже обрящет рука его: по силе обета его, егоже аще обещает, по закону очищения.
22 Bwana akamwambia Mose,
И рече Господь к Моисею, глаголя.
23 “Mwambie Aroni na wanawe, ‘Hivi ndivyo mtakavyowabariki Waisraeli. Waambieni:
Рцы Аарону и сыном его, глаголя: сице благословите сыны Израилевы, глаголюще им:
24 “‘“Bwana akubariki na kukulinda;
да благословит тя Господь и сохранит тя:
25 Bwana akuangazie nuru ya uso wake na kukufadhili;
да просветит Господь лице Свое на тя и помилует тя:
26 Bwana akugeuzie uso wake na kukupa amani.”’
да воздвигнет Господь лице Свое на тя и даст ти мир:
27 “Hivyo wataliweka Jina langu juu ya Waisraeli, nami nitawabariki.”
и да возложат имя Мое на сыны Израилевы, и Аз Господь благословлю я.

< Hesabu 6 >